Na Mwandishi Wetu
VIONGOZI nane waliokuwa wakihusika na masuala ya ulinzi na usalama katika ngazi mbalimbali za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa viongozi hao ni aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Usalama ya CHADEMA Taifa, Prosper Makonya, ambaye anatajwa kushika nafasi hiyo baada ya kifo cha aliyekuwa Kiongozi wa Idara hiyo, Ali Kibao.
Wanachama hao wamepokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, ambaye aliwaongoza kula kiapo kwa kusoma ahadi za wanachama zilizowekwa katika Katiba ya CCM.
Wengine waliojiunga na CCM ni aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mwanza, Peter Mashauri; aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Jimbo la Kawe, Gibson Mwamaliga; na aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Mkoa wa Tanga, Simon Lukindo.
Wengine ni aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Jimbo la Korogwe, Sarafu Jengo; aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Lushoto, Samwel Sylvester; pamoja na viongozi wengine waliowahi kushika nafasi za ulinzi na usalama katika mikoa ya Simiyu na Morogoro.
Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Makonya, ambaye baada ya kuondoka CHADEMA alijiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), alisema ameamua kujiunga na CCM kwa sababu anaamini ni chama chenye uwezo wa kufanya maamuzi na kuyasimamia.
“Ndani ya CCM kuna kila aina ya watu, na ninaweza nikadiriki kusema Chama Cha Mapinduzi ni chama cha Watanzania. Ndani ya CCM kuna maamuzi, wengine wanafuata njia za watu,” alisema.
VIONGOZI nane waliokuwa wakihusika na masuala ya ulinzi na usalama katika ngazi mbalimbali za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa viongozi hao ni aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Usalama ya CHADEMA Taifa, Prosper Makonya, ambaye anatajwa kushika nafasi hiyo baada ya kifo cha aliyekuwa Kiongozi wa Idara hiyo, Ali Kibao.
Wanachama hao wamepokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, ambaye aliwaongoza kula kiapo kwa kusoma ahadi za wanachama zilizowekwa katika Katiba ya CCM.
Wengine waliojiunga na CCM ni aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mwanza, Peter Mashauri; aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Jimbo la Kawe, Gibson Mwamaliga; na aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Mkoa wa Tanga, Simon Lukindo.
Wengine ni aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Jimbo la Korogwe, Sarafu Jengo; aliyekuwa Mkuu wa Ulinzi na Usalama Lushoto, Samwel Sylvester; pamoja na viongozi wengine waliowahi kushika nafasi za ulinzi na usalama katika mikoa ya Simiyu na Morogoro.
Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Makonya, ambaye baada ya kuondoka CHADEMA alijiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), alisema ameamua kujiunga na CCM kwa sababu anaamini ni chama chenye uwezo wa kufanya maamuzi na kuyasimamia.
“Ndani ya CCM kuna kila aina ya watu, na ninaweza nikadiriki kusema Chama Cha Mapinduzi ni chama cha Watanzania. Ndani ya CCM kuna maamuzi, wengine wanafuata njia za watu,” alisema.


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...