Na Mwandishi Wetu
WAHITIMU wa Shule ya Msingi na awali ya Pius Pre and Primary school wametakiwa kuendelea kuwa na tabia njema baada ya kupatiwa malezi mazuri Shuleni hapo.

Akizungumza jana katika mahafali yaliyofanyika shuleni hapo Mwalimu Mkuu Sospeter Simon Mabanga amesema Mabanga nendeni mkawe chachu ya maendeleo katika jamii zenu kwani elimu mlizopewa hapa shuleni ni hazina katika familia na taifa kwa ujumla.

Aidha Mabanga ametoa shukrani kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuruhususekta binafsi kutoa elimu hapa nchini.

Katika mahafali hayo mgeni rasmi alikuwa Dkt. Mwamba Ally Jingu ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Uhasibu (IFM) ambaye ametoa pongezi kwa uongozi pamoja wa wafanyakazi wote kwa kuwasiamia vema wanafunzi hao

Wakati huohuo zawadi za fedha zimetolewa kwa waalimu ikiwa ni mikakati ya kuinua taaluma na utoaji motisha kwa waalimu kutokana na namna walivyofaulisha kwenye mitihani yao ya taifa.
Shule hiyo ya Pius Pre and Primary iko Kongowe Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...