Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Stephen Wasira, amewasili leo mkoani Iringa, ambapo amepokelewa na viongozi wa Chama na Serikali wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Komredi Daudi Yasin.
Ndugu Wasira amepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Nduli, mkoani Iringa, alipowasili kwa ajili ya shughuli mbalimbali za Chama.
Akiwa mkoani humo, pamoja na shughuli nyingine, Ndugu Wasira anatarajiwa kufungua Mafunzo ya Wakufunzi wa Chama yatakayofanyika katika Chuo cha Mafunzo cha Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).



.jpeg)

.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...