baada ya muda si mrefu mbavu za mbwa zitatoweka kariakoo. hiyo mbele ni shule ya msingi mnazi mmoja ambapo rais joseph kabila alipata kusoma masomo ya sekondari ya jioni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Wanapojenga kwenda juu(magorofa) wakumbuke na kuchimba chini(mfumo wa maji taka). Naamini mpaka sasa kariakoo inatumia drainage system iliyojengwa na wakoloni.Wahusika wasipokodelea macho hili tatizo, siku za mbele kariakoo patakua hawapitiki.

    ReplyDelete
  2. Nimeamini elimu ya Tanzania iko juu.Kama shule ya jioni ya vichochoroni uswahilini inaweza toa Rais wa nchi kubwa ya KONGO kama Raisi Kabila ni uthibitisho tosha kuwa elimu yetu iko juu zaidi ya ile ya degree za Malekani ambako msomi wa Tanzania akienda huko kusomea anaishia kusafisha matako ya Wazungu na kubeba mabox kwenye maduka! Elimu ya Tanzania hoyee!!

    ReplyDelete
  3. Jamani,

    Kariakoo pandeni miti. Magorofa bila kupanda miti hiyo Kariakoo itakuwa bomu.

    Jitahidini kufanya kama maeneo ya huku posta mpya.

    ReplyDelete
  4. Anony wa 27, 8:33 umechemsha. Kwanza, Suala la uraisi halina uhusiano na ubora wa elimu, kuna maraisi duniani elimu yao ni ya chini.Kilichomsaidia Kabila, baba yake alikuwa raisi na yeye ni mwanajeshi,na wala si elimu yake. Pili, tusijidanganye kuwa elimu ya Tanzania ni bora kuliko USA,U.K,n.k. Hizo ni ndoto. Tujilinganishe kwanza na Kenya au Uganda. Elimu bora wakati hata vitabu vinatushinda. Tatu,kutumwa na wazungu hakuna uhusiano na ubora wa elimu,kwani hata baadhi ya viongozi wa nchi walishawahi kufanya kazi hizi wakati wanasoma kwa hao wazungu. Watu wanajisomesha mpaka elimu za juu kwa kufanya kazi hizi. Inaonekana Anony hujatembea Duniani. Toka ujifunze, usikae mtungini siku zote,ungesoma au kuishi nje usingetoa maoni hayo. Tafadhali usiipotoshe jamii. Nchi zote Duniani wanajua elimu bora ipo U.K na U.S. ndio maana wanawaleta watu wao kusoma kwa gharama kubwa.

    ReplyDelete
  5. Tanzania tumesomesha wengi kuanzia Rais Museveni wa Uganda,Paul Kagame wa Rwanda,Marehemu John Garang wa Sudan,Kabila wa Kongo,Oginga Odinga wa Kenya,Chisano wa Msumbiji,Raisi mstaafu Chiluba wa Zambia,na wengine kibao wanaoshika nafasi za juu katika nchi za Afrika mashariki,kati kusini hadi Africa magharibi.Wamesomea hapa hapa ambapo wengi wanaiponda elimu ya hapa na kwenda Ulaya au marekani ambako wanaishia tu kurudi na utamaduni wa huko na vimini skirt na blouse,makaptula na matisheti na vikofia vya kihuni au Rasta vichwani na kiingereza cha wahuni wa huko hivyo ndivyo hasa wanavyorudi navyo wanavyoweza kujidai navyo wakitua airport.Lakini wengi wao hawaendi zaidi ya hapo wakitokea ulaya au marekani.

    ReplyDelete
  6. Jamani Anony wa Monday, November 27, 2006 8:33:03 AM umenichekesha sana jamani. Kweli vituko havitakaa viishe.

    ReplyDelete
  7. Hao annoy wawili inaelekea wanamachungu sana rohoni... Vipi!!!! Hebu tueleze...unataka msaada....wewe unasema tukirudi hatuendi zaidi ya hapo....According to your tone nimeshafuatilia nakuona ni nani wewe...nafanya PHD ya speech psychology kwa hiyo natafuta mkali wa technology aku ping nikufahamu kabisa inaelekea unamengi rohoni yanayohitaji msaada. Nchi yetu inaelimu natunamshukuru mola kwa hilo lakini kusomesha maraisi sijui wangapi sio kuona kuwa you have all that....challenge ni kitu muhimu duniani. Basi hao uliowaona marahisi wametoka hapo ..umeshasettle na kuona nchi ina the best education. Pole....Don't settle for less

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...