joti 'mdebwedo' (kulia) na mpoki 'wakora waito'
masanja mkandamizaji
wadau mlio ughaibuni kwa taarifa yenu kwa sasa hapa bongo kuna kipindi cha luninga kinachotamba kuliko vyote kwenye eatv kiitwacho 'ze comedy' kinachorushwa kila siku ya alhamisi jioni na kurudiwa jumapili. kuna wabunifu wamekaa na kuja na uigizaji wa kutangaza taarifa ya habari kwa namna ya kuchekesha sana kiasi wengi huwaga wanawahi nyumbani siku hiyo kujionea vioja kwa lisaa lizima. stelingi ni huyu masanja mkandamizaji ambaye pamoja na mwenzie joti mdebwedo hurusha nyuuzi kwa namna isiyo mfano kiasi hata nahau za 'kandamiza' na 'mdebwedo' zimeshika nafasi kila kona. aidha, mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni - hawa jamaa wamewini...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 11, 2007

    jamaa wamewini, si mchezo. Lakini mwandishi mbona unaandika huku unanung`unika ? ... kwa nini unamwita Masanja eti mnyonge ? kanyongwa na nani ??

    kitu muhimu ni kuhakikisha umeme wa uhakika, ikiwezekana televisheni za vijiji ili watu wengi zaidi waweze kufaidi uhondo huu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 11, 2007

    Jamaa wako juuuuuuu!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 11, 2007

    Hasa viongozi na wasanii uchwara wanawakandamiza ile mbayaaa. Safi sana lakini siku moja utasikia kauli kutoka kwa wale jamaa kule Dodoma "Hawa comedy wafungiwe wanapotosha jamii" si mnakumbuka haki elimu?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 11, 2007

    Ahaaa,
    basi hiyo nadhani ni poa sana. Ni kama kipindi huku USA cha saturday night live cha jumamosi usiku, huwa kuna taarifa ya habari moja hivi ya kuchekesha sana. Mimi huwa siikosi,
    Labda wangeongezea na kuwaakti baadhi wanasiasa na watu maarufu, hawa wa huku huwa wanaakti prez bush na dik cheney basi ni vichekesho vitupu, kondoleza raisi ndo kabisaaaa, wanampatia mpaka mwanya,
    Keep up good stuff Bongo,
    grace.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 12, 2007

    Joti alivyo-pose utadhani Marehemu Tupac Shakur....

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 12, 2007

    Kaka Michuzi hawa Jamaa wanajitahidi sana kukosoa Jamii. Mi at least mpaka sasa so far nawafagilia sana.
    Kama kwenye show ya wiki iliyopita ile Stori ya WANAOJIDAI MASTAR kwenda kwenye misiba ya watu maarufu kwa lengo la KUJIBIISHOLISHA na "kusafisha nyota" ile ni kweli kabisa.
    Kuna WASHAMBA fulani ambao huwa kweli wanapendaga kufanya hivyo kwenye misiba. Sijui upungufu wa elimu! Mheeh!
    Eee bwana naomba unifikishie ombi langu kwao kwamba wiki hii WARUDIE TENA ile stori ya WANAOJIBIISHOLOLOLISHA kwenye misiba ili TUKOMESHE kabisa tabia hiyo mbovu!
    Big up!
    Ila sasa tatizo la Mastaa wa Bongo wakishaanza kupanda chati si unawajua Kaka Michuzi? Wataanza KUPOMBEKA kwa sanaaa, na MABIBI kwa wingiii!
    Noma hiyo jamani wWasanii wetu. Ninyi msiwe hivyo

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 12, 2007

    dada Grace (wa july 11,11:32:00),hawa jamaa wa ze comedy si mchezo. juzi wamemuonyesha Kikwete kahonga sh 25,000.-kapewa kitanda na nesi hospital,baada ya muda kaingia kibopa anatembeza mkwanja kiroho mbaya akamwambia nesi'kamati hii minoti toa hiyo taka taka hapo kitandani nilale mimi',kumbe kitandani kalala Kikwete amejifunika,kumfunua tu ili amtoe mkuku,lo! balaaa ni mwenye nchi!you can imagine. ukiona wanavyomuigiza Lowassa utacheka mbavu ziume.hawa jamaa majiniasi.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 12, 2007

    hao ndo macelebrity wa bongo kiukweli maana kila kona watayopita watu wanawashangaa kiukweli ukweli..

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 12, 2007

    The are true Tanzanian talent...

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 12, 2007

    mie nilikuwa najiuliza hii blog yako inabeef na ze comed nini mbona ulikuwa ujawarusha mda wote huo lkn nimefurahi sana yani hawa jamaa uspime kabisa ktk fani ya vichekesho kwa sasa yani wanatisha ile baraa

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 12, 2007

    Perez hao vijana especially mpoki na mwenzake nadhani wanajiheshimu manake wameshakuwa kwenye umaarufu kwa muda mwingi sana sasa... so nategemea wataendeleza kujiheshimu kule kule. Lakini kama usemavyo kama chati inapanda kwa spindi inaweza walewesha psychologically alafu ikazua mambo mengine!

    Michuzi tutafutie basi some video clips na sisi tufaidi manake kila mtu akitoka bongo ni kipimabaridi kipimabaridi sasa naachwa hoi tuu.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 12, 2007

    MICHUZI UMECHELEWA NA ZE COMEDY. TUMESHAONA VIMBWANGA VYAO SIKU NYINGI KATIKA TOVUTI NYINGINE. WALICHOANZISHA WENZIO HUJIFANYA HUKIANDIKI VIPI HIKI CHA ZE KOMEDY AU KWA SABABU NI MAARUFU SANA TENA SIYO KUPITIA KWENYE BLOG YAKO? UNAPENDA SANA MDEBWEDO WEWE...UTAKULA UROJO. SHAURI YAKO.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 12, 2007

    MBONA MICHUZI HUJAWEKA PICHA YA 'LOWASSA'??

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 13, 2007

    michuzi fanya basi siku moja tuwekee hao wakandamizaji tusikie. asante.

    ReplyDelete
  15. hehehe hawa jamaa jamani wanaburudisha sana! Mie ule muondoka wa joti tu hoi babake!! na msemo wake wa kudadadeki!! hehehehe very funny yakhe!! masanja yeye huwa anakandamiza kibara tu high speed!! hehehe!! i like that! mambo ya kubonyeza kizenji! Mdebwedo!! hehehe hawa jamaa ni mwisho wallahi yaani ukiwa na kisirani basi ikifika alhamisi jioni chaisha!!

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 13, 2007

    hehehe hawa jamaa jamani wanaburudisha sana! Mie ule muondoka wa joti tu hoi babake!! na msemo wake wa kudadadeki!! hehehehe very funny yakhe!! masanja yeye huwa anakandamiza kibara tu high speed!! hehehe!! i like that! mambo ya kubonyeza kizenji! Mdebwedo!! hehehe hawa jamaa ni mwisho wallahi yaani ukiwa na kisirani basi ikifika alhamisi jioni chaisha!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...