wadau wa ukerewe kaeni mkao wa kula. mambo ya mugongomugongo yanakuja kwenu wiki ijayo. yaani trupu zima la twanga pepeta linatarajiwa kuzuru london kwa shoo kibao. ratiba kamili subirini kesho

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Waaaaaaaaaaaa wa wa wa waaaaaaaaaaaaaaaaa!
    Mimi nafagilia kihaya.Yani mkubwa mimi nimefurahi sana kwa ziara hiyo.Mambo ya mgongo mgongo.ACHANA NA HUYO SIJUI ray cd, MIMACHO UTAFIKIRI ANAPIGA CHABO.sasa kaka misoup tupe mipicha ya kumwaga na habari kemkem ya ziara hiyo.Naamini wadau watasubiri kwa hamu ujio huo.Nashauri kama kuna mtu alitaka kwenda au kusafiri kumuona ray cd aache na aachane nae kwani hao twanga niliwaona majuzi sigara tcc wanatisha.
    Lakini wakubwa mimi swali langu ni moja tu,hao twanga watavuka maji toka ukerewe na kuja huku Majita Bugunda??Yarabi toba,ikitokea hii ndoto ikatimia,mwanangu ntalazwa kwa maumivu ya mgongo. kwani ntacheza non stop.
    wa Majita Bugunda

    ReplyDelete
  2. Kudadadeki mtoto Aisha Madinda kawape raha wadau huko Ukerewe.Kwa kweli mugongomugongo naukubali kwa kiasi kikubwa mno.Wanatwanga kadhihirisheni kuwa ninyini bora hata huko Ughaibuni.

    ReplyDelete
  3. Kaka michuzi na wewe unapenda mgongo mgongo kazi kweli kweli.

    ReplyDelete
  4. Haya kaka michuzi Je stokhomu watafika??? Duh waje basi na huku japo siku 1 tu waone na style yao mpya... tunawakumbuka safari 2005
    Tunawasubiri

    ReplyDelete
  5. Mgongo mgongo wanatisha, sasa huyu aliyevaa cream mbona pa matako pamevimba kitofauti kuna usalama?.

    ReplyDelete
  6. London pekee haitoshi, waje pia Reading kuna washabiki kibao!

    ReplyDelete
  7. Kaka Michu , waambie kabisa siku hizi kujilipua noma wazungu wameshtuka, hivyo .....!

    ReplyDelete
  8. holland walikimbia wawili sasa sijui huko uk watakimbia wangapi msitutie aibu mludi jamani mkikimbia mnawanyima nafasi wasanii wengine.

    ReplyDelete
  9. Mambo si hayo twanga tafadharini msikose kuja holland japo utusahaulishe maudhi aliotuachia rehema charamila na ole wake akija tena holland tutamtoa nishai.

    ReplyDelete
  10. hello, anon wa 11:36 Twanga pepeta wataishia London, usiwashushe hadhi, hawawezi kuja Reading, huko ni Uswahilini sana,,nasikia kuko kama Manzese tu, umbea, udaku, kusutana, kuibiana mabwana na mabibi n.k nasikia mpaka kurogana pia,shuti kwa waganga wa kigambia eti,,mmh,,kila la kheri na hivi ticket za bongo sikuhizi bei chee, Qatar airways..mh mtakuwa mnawafuata waganga wa jadi , kama walioko Reading hawawatoshi.

    ReplyDelete
  11. Reading ndio nini? aah, kule Manzese kwa mfuga mbwa eeh, ooh kweli lazima washabiki muWe wengi, kwa maana wote waswahili tu, shule hammalizi, nyumbani hamuwezi kurudi kuwasabahi ndugu zenu,,mmeshakuwa Big brother Reading, mikoba mmeichoma moto, MMEJILIPUA,,Ufuateni Mugongomgongo London, KAMA MNAYO NAULI....

    ReplyDelete
  12. kama unakusikia tu Reading una sababu gani ya kukupondea ?

    ...Unakufananisha na Manzese, kwani kuisihi manzese kuna tatizo gani, au huko manzese wanaishi punda ???

    ...Jiheshimu bana.

    ReplyDelete
  13. we anon hapo juu, Mwegelembwegele,,nadhani we ndo ungejiheshimu kwa kufunga virago vyako na kurUdi kwenu bongo, ukarelax,inaonekana uko Reading wewe, umeshazowea kusafisha vyoo vya wazungu, wacha bwana, rudi africa, kazi zipo( kama una cheti)...maana iliposagiwa Reading hasira imekupanda, yaonekana uko Reading na cheti huna kwa kifupi, UMELOST..mnapenda status tu kuonekana mwakaa Ulaya, je mnafanya nini huko, SWALI?? halohalo ya walioLOST....sijui mvi zitawaota mkiwa huko,,mmh mie simo mchanga pwani huo,,,hahaaaa, kufikia mwaka 2037 CCM itabidi watume ndege UK na US, kuwarudisha WANA WAPOTEVU, FOR FREE MAANA HATA NAULI MTAKUWA MMEISHIWA..MMEZEEKA..

    ReplyDelete
  14. CCM haitakuwa na ubavu wa kukodi ndege kuturudisha, pesa ya CCM inaliwa na vigogo, hata hivyo nyumba za kulea wazee ni chache bongo, huku tumeshaweka majina kwenye nyumba za kutulea tukizeheka. Kikwete aongeze nyumba za wazee, yatima, na watoto wa mitaani

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 10, 2010

    Wazee, ishu za wafanyakazi wa kima cha chini na mishahara ya kiulaya ulaya mbona hamuongelei? au kama kawaida hamtaki na siye wa kima cha chini tunenepe? kwenu wachumi, tuendelee kuikomalia serikali au kuna athari za kiuchumi tuiachie mada tuendelee kula sembe mchicha?

    anonimous

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...