wadau mlioanza kubukua enzi hizo za naintini kweusi mnavikumbuka vitabu hivi ana stelingi wake bulicheka na lisabeta mai waifu wake?


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. kaka Michu, nimefurahia sana hivi vitabu......je, vinapatika bado madukani? safi sana.....

    ReplyDelete
  2. Bw. Issa Michuzi, nimefurahi sana kuona hiko kitabu cha bulucheka nakuomba kama utaweza kutupa link kitabu naweza kukipata wapi, Miaka kama 15 toka nisome hiko kitabu ni vizuri kama tutakuwa tunasomesha wenetu, mie kusoma nilikuwa sijui mpaka nilivyofundishwa na hicho kitabu fanya kweli kuhusu link ya kitabu.

    ReplyDelete
  3. Du Bwana misupu umeikumbusha mbali sana kitabu hiko kina stori za MAKALI HODARI ....

    ReplyDelete
  4. Duh Michuzi kweli leo umenivunja mbavu, yaani ni miaka zaidi ya 20 nimesema vitabu hivyo, kusema ukweli sikumbuki hata kuna nini humo ndani, duh PINOKYO ahaha...ila nakumbuka bulicheka alikuwa fara kweli, ila to be honest sikubuki vizuri......hii ndo blog babake,

    ReplyDelete
  5. Kaka Michuzi hivyo vitabu mi vinanikumbusha mbali sana hasa pale Mfalme Huihui alipokasirika alipoona Bulicheka ameingia mjini kwake, bila ruhusa yake na kujenga nyumba kwa kutumia meza kwenye minazi minne iliyokaa skwea.
    Huihui alivyokenua domo lake na kujishika mikono kiunoni iliyokaa kama Upinde. Tehe teh tee! We acha tu!
    Vinapatikana bukshop gani hivyo?

    ReplyDelete
  6. Michu, hebu tuace masihara....TUNAOMBA KAMA ATAJITOKEZA MDAU KUFUFUA VITABU HIVI KWA AJILI YA WANETU.....halafu pia kile kitabu cha ALF-LELA-U-LELA.....jamani hebu fikirieni wanetu wakiwa wanasoma na kujijengea mazingira ya kupenda kusoma vitabu...usomaji vitabu unapanua sana ubongo wa mtoto.

    ReplyDelete
  7. Michuzi,
    Ni aibu sana kuwa watanzania wengi hawapendi kusoma. Mimi nadhani hata watoto wetu wamekosa hamasa ya kusoma kwa vile hakuna vitabu kama hivyo tulivyosoma sisi, maana kila wakati mtu ulikuwa unataka uende shule ili ukasome hadithi za Bulicheka na Elizabeta!
    Ilikuwa inapendeza kwa kweli, maana pamoja na mimi kuzizoma hizo hadithi miaka ya 72 na 73 bado nakumbuka kwa mbali zilivyokuwa zinasisimua!

    ReplyDelete
  8. Haluu Bro Michu! Yaani umenikumbusha mbaaali kweli! Mwaka wa Arobaini na Sabaa!! Nilikuwa napenda sana kuvisoma hivi vitabu vya Bulicheka na Paulo Mchafu! Yaani ilikuwa mtu you are actually looking forward kuvisoma, na wakati unavisoma unakuwa veeere excited, na unajenga kabisa picha kichwani, yaani kama unawaona vile walivyokuwa wanafanya. Duh, imenikumbusha pia enzi za Mama na Mwana.

    Aisee kwa kweli tujulishe vyapatikana wapi.

    ReplyDelete
  9. BULICHEKA NA MKEWE ELIZA ELIZA...ISSA MIMI NITANUNUA HIVYO VITABU KAMA UTAWEKA LINKI HUMUNDANI.

    ReplyDelete
  10. Si utani Umetukumbusha mbali na vitabu hivi!

    ReplyDelete
  11. wewe muidini una lazi. Samahani sikutukani bali nakusifia. Kumpata bulicheka na demu wake elizabeti, wakati wakimtoa mfalume huihuihui, hii kiboko. Tunataka mavintuz kama haya babaake.

    ReplyDelete
  12. Kaka michuzi hivi vilikuwa vitabu vya maana sana. Kuna kitabu pia kiliitwa HEKAYA ZA ABUNUWASI. Kama kuna mdau anafahamu ni wapi vitabu hivi vinapatikana naomaba tafadhali anielekeze niende nikanunue. Kama haviuzwi nitalipia nipige photocopy au hata kunakili kwa mikono. Ninachotaka tu ni maandish yake.Jamani tusiwe wachoyo wa elimu. Kama kuna mdau anayeweza kuni-assist tafadhali nijulishe kupitia 0754711028. Iam very serious about this.Thanks in advance!

    ReplyDelete
  13. hehehehehe Bulicheka na Elisabeta, nilishasaha jina la huyu mama, hata story sikumbuki vizuri tena. Kama wadau walaivyopendekeza hapo juu, ingekuwa jambo la busara kama tutavipata tena. Looh! Si mchezo!

    ReplyDelete
  14. Nahitaji vitabu vifuavyo:

    BULICHEKA
    MASHIMO YA MFALME SULEMANI
    ALFU LELA ULELA
    MALIMWENGU
    HADITHI ZA ESOPO

    TAFADHALI NIPO TAYARI KUNUNUA
    CALL ME OR SMS AT 0713 650 469

    ReplyDelete
  15. Duh, yaani kitabu cha someni bila shida cha Bulicheka, Lizabeta na Wagagagigikoko nilisoma miaka ya 80... Itabidi nikitafute tena nikumbushie zile stories.

    ReplyDelete
  16. Michuzi hakujibu hata comment 1, ana hasira gani Michuzi?

    ReplyDelete
  17. Msimsahau Kalumekenge asietaka kwenda shule; Hanahela; pia Msimsahau shairi la mgeni siku ya kwanza.

    ReplyDelete
  18. 0678 683 278 anauza hivi vitabu, yuko pale Ubungo UBT

    ReplyDelete
  19. Jamani pia navihitaji vitabu hivyo lkn sioni mjumbe aliyejibiwa hata mmoja tafadhali tusaidieni tujue namna yakuvipata. Mawasiliano yangu 0758050374

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...