MIMI KAKERE JUNIOR PAMOJA NA RAFIKI ZANGU TUNATOA RAMBIRAMBI ZETU KWA NDUGU NA JAMAA WOTE WA MH SALOME MBATIA ALIYE FARIKI KWA AJALI YA GARI TUNA MUOMBA MWENYEZI MUNGU AIPOMZISHE ROHO YAKE PEMA PEPONI AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Samahani imebidi ni comment hii picha ya watoto. Inaonekana wazazi wengine wanwatumia watoto wao bila kufukiria. Kwanza huyu mtoto ni mdogo kufahamu kifo cha mama S.M. pili hao watoto wengine wazazi wao wametoa ruhusa ya kuwekwakweny picha? Tatu picha hii haifatani na tukio maana inaonekana wanasheherekea birthday! Ni bora huyo mzazi ange-tuma rambi rambi zake mwenyewe bila kwa expose watoto ambao hawajui kinachoendelea.

    ReplyDelete
  2. nakubaliana nawe anon wa sat 27,2007 11.22.00 am EAT
    huu ni upuuzi naofanya huyu mzazi!!tumeshaona picha za haka katoto mara nyingi tu humu!!sisemi kwa ubaya ila mzazi huyu naona anaona misifa kuweka picha za mwanawe humu kwa kila jambo hata lisohusu watoto!!Michuzi naomba usinibanie maoni yangu sijasema kwa ubaya ila mzazi ni vema akafikiria mara mbili!!

    ReplyDelete
  3. Si nia yangu kuchafua ama kukemea ila ninapenda kuzidisha wigo wa ufahamu.Mimi nami naishi nje ya nchi(UK),huwa nafanya kazi za kujitolea,nafundisha watoto wadogo,moja ya miiko niliyokutana nayo ni kutumia picha za watoto hao bila ruhusa ya wazazi wao ama shule kwa manufaa na malengo yako yanayoendana kinyume na taratibu hiyo.Hivyo basi nilikuwa napenda kuungana na hao juu kuwafahamisha wenzetu ambao labda kwa jinsi moja ama nyingine hawafahamu miiko hiyo.Kwa mzazi aliyefanya hivyo ni budi akaelewa na asiwe na mawazo hasi(negative impression) kwa watu ambao wameweza kuchangia ama kukosoa suala hili,mimi huamini ya kwamba si kila mtu anajua kila kitu,na si nia yake kuvunja sheria na miiko hii bali yachangiwa na kutokuelewa,sisi sote twatakiwa kuelekezana ama kukumbushana.Mwisho kabisa nilitaka pia kukuomba michuzi urekebishe maandishi yanayojitokeza hapo juu kwenye blogu hii:tujieshimu na akhasante nadhani lugha sahihi ni tujiheshimu na Akhsante.Nawasilisha Mkuu.

    Cheers

    ReplyDelete
  4. asante sana ma anon wa hapo juu, SEMENI NYIE VIAZI, NIKISEMA MIE MHONGO, WATASEMA MIE MGUMU!!!!!!!! nakubaliana nanyie, picha haihusiani na tukio kabisa..hapo ni sawa na kuwa anatoa pole huku ana advertise mengine, mwanae alibahatika kubebwa kwenye miguu ya mzungu....kitu ambacho sio dili wala issue, tunaombelezea mama yetu Salome, toeni pole zenu, na wala hatuhitaji picha za watoto,,,hata sie TUNAO.

    ReplyDelete
  5. mtajuaje wazazi wako ulaya jamani?
    kwa nini wasitume wao picha yao,wanaona ya mtoto na marafiki wazungu ndio ina maana zaidi.

    ReplyDelete
  6. Bad timing na huu ni ushamba. Watu wengine hata hawafikirii. Picha ya mtoto wako kwenye rambirambi. Ukiishi nje ya nchi sio kuwa unaelimika ...kuna wengine wanamind za kijinga bado...sasa hii ni big deal kwa mwanae kuwa kwenye picha ya wazungu sijui. What is the point?

    Lakini hii sio utani kuna mdada mmoja pia hataki mtoto wake acheze na watoto weusi. Kujidharau wenyewe...sasa huyu kashatuonyesha pich amara ya kwanza ...akaona we didn't get the point sasa hii tena...

    Ni wakati mgumu huu sana kwa ndugu, jamaa na marafiki wa watu waliofiwa Tanzania and we better keep that way kuwa nao pamoja.

    ReplyDelete
  7. Ndugu zangu nimewaelewa sitarudia, kusema ukweli nilikuwa sijuhi kuwa ni mwiko kuweka picha za watoto. Lakini at least mmeona niko ulaya na familia yangu inafahamiana na wazungu, mlie tu mie nadunda!

    ReplyDelete
  8. nyie wote mliotoa maoni juu ya hii picha mnachuki binafsi kwani mtoto anapo soma lisala mbele ya mkutano.kifo au sherehe ni yeye ndie alisema mbona picha ya wadau wa ukrein au ya huyo dada wa kimasai hazipo ktk huzuni yeyote ile hamkuiweke maoni yeyote wacheni chuki binafsi.

    ReplyDelete
  9. Nyie kina anon mnaoneka roho zimewauma sana kuona hiyo picha ya huyo mtoto kwanza hayupo ulaya hapo ni msimbazi center huyo mama wa kizungu na hao watoto wake walitembelea tu watoto yatima hapo msimbazi na huyo mtoto alipata tu picha ya ukumbusho kingine kama inawauma sana na nyie tumeni picha za watoto wenu ISSA MICHUZI yupo kwa ajili yetu na hii blog ni yetu sisi wadau ISSA MICHUZI ni mtendaji wetu hata mimi sasa nitaanza kutuma picha za mtoto wangu mrembo SHANI.

    ReplyDelete
  10. DUUH WABONGO KWA JEROUS TUMEZIDI HADI KATIKA BLOG HATUZIFICHI INGEKUWA MTOTO WA KIZUNGU KAPIGA PICHA NA WATOTO WEUSI WALA MSINGESEMA LOLOTE OOH MARA MTAJUAJE KAMA WAPO ULAYA! YOTE MNAMALIZA NYINYI ULAYA SIKU HIZI WATU WANAENDA NAKURUDI KAMA KARIAKOO TO MBAGARA HATA MICHU HAMMUONAGI MARA UK MARA SWEDEN WACHENI USHAMBA NA JEROUS NYIE KINA ANON TUMEMENI NA NYIE PICHA ZA WATOTO WENU NA NDUGU YANGU KAKERE USICHOKE. MIMI NAKUFAGILIA WAWAAA!

    ReplyDelete
  11. anony 27 hebu nyamaza. Hivi hiyo picha ya mama mwenye nguo ya kimasai umesoma au umekimbilia tu kuprtec ujinga wa watu. Huyo mwenye nguo ya kimasai ndio marehemu. Sasa soma kwanza ndio uongee. The point ni moja kama unataka kutuma rambirambi tuma picha yako. Picha za watoto wanajua nini?

    Tumeshamwona mwanae mara moja sasa hii ya nini tena.

    Na who cares kama yupo shule na watotot wakidhungu au la? mbona watoto wetu ndio shule hizo hizo wanasoma. Kila siku tukituma hizi picha itakua nini.

    ReplyDelete
  12. WE ANON OCTOBER 28 10:16 HEBU RUDI
    TENA CLASS AU KAMA HUKWENDA BASI
    NENDA SHULE SASA AU ONGEA TU KISWAHILI.JEROUS NDIO NINI? UMEJIFUNZIA KIJIWENI AMA? MUONE
    MACHO YAKE KAMA YA CHURA.HEBU
    NENDA SHULE.OTHERWISE MAONI YAKO
    MAZURI ILA UNAHITAJI SCHOOL KIDOGO
    REGARDS

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...