hatimaye boti iendayo kasi ya mv seagull ya kampuni ya wazalendo wa zenj ya seagull sea transport imeanza safari zake za dar/znz/pemba na leo imetia nanga kwa mara ya kwanza dar. boti hii yenye uwezo wa kubeba abiria 410 itaondoka ijumaa hii kuelekea visiwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Banu kubwa washikaji hii ndio tunataka lakini cha muhim ni kuwa amani idumishwe kama mnavyotengeneza pesa nilifikili michuzi hato toa nilichoandika lakini katoa. Kama mnavyofanya usafiri uwe rahisi na amani pia iwe rahisi tunahitajiana sio sababu mwarab kakaa muda mrefu pemba then atuletee baraa bara na pemba na unguja ni kitu kimoja watake wasitake mimi nipo newara lakini mshikaji aliyenisaidia ktk mambo mengi ni mpemba na mimi ni mtu wa bara jamani tuulinde umoja wa baba zetu na babu zetu sasa cha ajabu nimeoa mpemba pia mtake msitake mimi ni shemeji yenu nilitaka kulipa fadhila kwa mshikaji wangu!

    ReplyDelete
  2. darasa la tatu nilifundishwa zanzibar=unguja na pemba.Kila wanaposema zanzibar na pemba ina maana zanzibar ni unguja pekee yake ama?

    ReplyDelete
  3. inapendeza kuona usafiri wa bahari unakuwa bora ila mi dukuduku langu ni usafiri wa kwenda kule mtwara,kkuna port kubwa lakini usafiri wa majini ni headache,kwann sirikali isifikirie na kule????hali inakuwa mbaya sana kipindi cha mvua,manake njia zote zinafunga...kunani kuleeeee???????

    ReplyDelete
  4. Kwa Anonymous wa kwanza juu hapo:
    kwani cha ajabu ni nini wewe kuoa Mzanzibar?mbona mie nimetulia tu na mke wangu wa kibara?kwanza unakosea kuita Wazanzibar wote wapemba kwani kama anonymous wa pili alivosema Zanzibar = Unguja + Pemba.
    wanaoita Zanzibar ni unguja peke yake hua wanakosea bila shaka!
    tena hili halina mjadala kabisa.

    ReplyDelete
  5. Jamani ee!!

    Hivi ni nini manufaa ya kuwa na vyombo vya kusafiria majini ambavyo vinaua watanzania kila kukicha? Tulianza na MV Bukoba, ikafuatia MV Spice Islander na Sasa leo hii ni SkyGate. Hivi, kuna uhaba wa usafiri kiasi hichi hadi watu kujazana kwenye meli moja ikazidiwa uwezo? Tafadhali tuerevuke, usalama huanza na wewe unayekimbilia kupanda chombo ambacho umeshakiona kimejaa pamoja na wengineo ambao wameshaingia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...