Kaka Michuzi,
Yaani inashangaza kweli. Nimepokea emails 654, kutoka kwa watanzania wenzangu. kati ya hizo zote, nimepitia karibia 350, lakini yote ni matusi na ya udhalilishaji, nimelia lakini sikati tamaa.

Akhsante
Jovi


WADAU KUNRADHI,
NIMEPOKEA UJUMBE WA MDAU JOVINATA KWA MASIKITIKO MAKUBWA, KWANI SIJAONA KOSA LAKE NI NINI KIASI CHA KUCHAFULIWA HALI YAKE YA HEWA KAMA KWAMBA YEYE NI MHALIFU SABABU TU IKIWA KATUMA WARAKA WA KUTAFUTA MCHUMBA HUMU.
INGAWA NI KWELI SINA NIA WALA MAMLAKA YA KUWAPANGIA WADAU MCHANGIE VIPI MAONI YENU LAKINI SI UWONGO KWAMBA INAKERA KUONA BAADHI (NASEMA KWA MSISITIZO, BAADHI NA NI KUNDI DOGO SANA!) YA WADAU HAWANA KAZI ILA KUSAGIA KILA KINACHOWEKWA HUMU. HAWANA JEMA, HAWANA DOGO, HAWANA SIMILE, HAWANA HATA MAWAZO MBADALA KWA WANALOPINGA, ILIMRADI WAMEPINGA.
KAMA MJUAVYO MIE SINA KAWAIDA KABISA KUINGILIA UHURU WA MAONI, KWANI KAMA MAONI HAYACHAFUI HALI YA HEWA SINA SABABU YA KUBANA, ILA KWA MDAU JOVINATA NIMEZUIA MENGI SANA AMBAYO YANAONEKANA YANATOKA KWA WATU WALE WALE WACHACHE WAISOPENDA MAENDELEO YAO AMA YA WENGINE.
HUKO NYUMA NILIWAHI KUFANANISHA BAADHI YA WADAU WA AINA HIYO KAMA SENENE. KWANI SENENE WAKIWEKWA KIKAPUNI, HUWA HAWAWEZI KUTOROKA SI KWA KURUKA AMA KUTAMBAA - JAPOKUWA KIKAPU HAKIJAFUNIKWA - KUTOKANA NA KUKABWA NA WENZIE. KWA LUGHA INGINE SENENE HAPENDI MAENDELEO YAKE WALA YA MWENZIE...
KWA HESHIMA NA TAADHIMA NAOMBA SANA WADAU TUWE WASTAARABU KWA KUTOA MAONI YA KUKOSOA AMA KUELEKEZA BILA KUCHAFUA HALI YA HEWA. KILA MMOJA WETU ANA FRASTRESHENI ZAKE NA HATA UANDIKE AMA UCHAFUE HALI YA HEWA NAMNA GANI HAZITOISHA KAMA HUCHUKUI HATUA ZINAZOSTAHILI. NA KAMWE HATUA ZA KUONDOLEA FRASTRESHENI ZAKO SI ZA KUMALIZIA HASIRA KWA WADAU WENZIO
VILE VILE KUTAFUTA WACHUMBA SI JAMBO GENI DUNIANI, LABDA HAPA BONGO AMBAKO TUNA MATATIZO YA KUCHELEWA KUPATA VITU NA VIKIJA VINAELEWEKA BAADA YA MUDA MREEEEFUU, NA SAA INGINE BAADA YA UCHAFUZI WA HALI YA HEWA.
SINA UHAKIKA NI KWA SABABU GANI KWANI UTAFITI WA KISAYANSI HAUJAFANYIKA KUGUNDUA SABABU YA BAADHI YA WADAU WACHACHE KUWA KAMA SENENE. NA KWA MDAU NINAYEPOKEA EMAIL ZAIDI YA 2000 KWA SIKU NAJUA NIKISEMACHO, NA KINASIKITISHA NA KUKATISHA TAMAA. YAANI NINGEKUWA NA ROHO NDOGO SIJUI INGEKUWAJE, MAANA NYIE WENYEWE MMESHUHUDIA HALI YANGU YA HEWA IKICHAFULIWA MARA KWA MARA.
KWA MDAU JOVINATA NAKUPA POLE KWA MASWAHIBA HAYO, NA NAKUOMBA WEWE NA WENGINE KAMA WEWE MSIKWAZWE NA WADAU WALIO KAMA SENENE. NA MOLA AKIPENDA UTAMPATA UMPENDAYE NA NITAFURAHI SANA KAMA UTAELEWA NA KUFUTA CHOZI UKIELEWA KWAMBA WENGI WANAKUSAPOTI.
-MICHUZI
Habari Kaka Misupu.

Kwanza nataka kuwapa pole Manka na Jovinata kwa kutusiwa bila sababu. Hakuna kitu kinacho nisikitisha kama kuona watu wanawatukana wenzao bila sababu maalumu kwani mtu huwezi kumwambia mtu kitu adi umtusi? Hivi kwa nini tunakua na tabia mbaya ambazo haziendani na mila zetu? Sema kweli mie sioni makosa ya kina dada hawa. Wamekuandikia kutafuta wachumba, hawajakuandikia kutaka matusi machafu kutoka kwa watu sasa kwa nini wengine waendee kinyume na kuanza kuwatusi na kuwatumia email zisizokua na kichwa wala miguu? Kwani kina dada hawa hawajaomba chumvi wala sukari kwao, kwa lipi washambuliwe kwa matusi?

Why cant we think before we write? Why dont we encourage one another?. Siku ya Manka alivyotuma maoni ya kutafuta mchumba nilisoma comments nyingi sana ambazo wengi walimwita majina ambayo sio mazuri kwa kitu kimoja tuu alicho fanya basi waungwana wakamtupia maneno yasokua na maana. Juzi Jovi anatuma maoni anatafuta mchumba basi yale yale yanatokea tena, hivi kwa nini watanzania tusiwe na akili kichwani, tuache mambo ya ubaladhuli. Mie binafsi nina hakika kwamba wengi wao wanao tukana madada hawa hawajasoma na hawana kazi za kufanya kwani mtu ukiwa na akili zako kamili hata siku moja huwezi kukaa kwenye computer kumtusi mtu usomjua kwa njeo wala sio.

Watanzania tunapenda sana kutupana chini, hata siku moja hatuwezi kufanya mtu apate moyo aendee na mambo afanyayo. Wengi sana wame mjudge Jovi kwa kwenda kwa mganga, lakini sutisahau kwamba 90% ya watanzania wanamini waganga, sasa leo hii iweje kumshambulia dada wa watu bila kosa? Kwani kama hamuwezi kumwambia mtu maneno ya maana kwa nini msikae kimya na kuendelea na shughuli zenu sio kama hawa madada wamewalazimisha au wamewataka nyie, wamekuja kwa misupu kutafuta SOULMATE sio MATUSI. Hii ni karne ya 21 husubiri mwanamme akutafute siku hizi unatafuta na mwanamke kumtafuta mwanamme si umalaya wala si ufuska. Asilimia kubwa wanao tukana kina dada hawa ni watu walokua majuu (US,CANADA,UK n So on). wadau wengi sana wakifika huko wanajiona wamefika na wao ndo wao, Dharau nyingi sana tena lakii sio vizuri hivyo. Mara nyingi watu wanasema "If you dont have anything nice to say dont say at all" this sentence applies to all people who have little brain.

Kinacho nishangaza wenzetu wengi sana wamepata chance ya kwenda nchi za watu basi wanakua na dharau sana wanasahau walipotoka. Yes sio mila zetu kutafuta wanaume lakini pia sio mila zetu kutukanana hadharani kuitana majina. Ni kwa nini watu hawa wanapata matusi bila sababu kwani tukiangalia hawajasema wanatafuta "Mabwana" wamesema "Mume' , na asilimia kubwa wanao wajibu madada hawa basi washafanya ufuska na wanazidi kufanya lakini hawayaoni yao ila wakitenda wenzao ndo uonekana. Kwa nini watanzania tunakua na roho za KWA NINI? Kwa nini hatupendi wenzetu wapate, kwa nini tunapenda kufanya wenzetu warudi nyuma ili sisi tuende mbele? Chuki binafsi si nzuri. Matusi si mazuri. Kwani mkija kwa misupu mkiona mtu anasema anatafuta mchumba basi lile neno la " Nakutakia la kheri" litawaumiza? Kwani lazima muwatusi watu adi nguoni? Kwa nini mnaacha ya kwenu mnafuata ya wenzenu? Unambiwa nyani huoni kundule na kwa maneno ya wadau na watanzania wengine basi nimeamini leo hii. Yani mtu unaacha kazi yako na kumuandikia Jovi email ya matusi kisa anataka mchumba? Kweli mlofanya mambo hayo meishiwa tena saaaaaaaaana. Mwenyezi mungu hapendi watu tutukanane bila sababu, hapendi tuwe na vijicho vya kwanini, Unambiwa nawatende wao ati uwa mwao kitenda wenzao. Basi msemo huu unawaendea woote walowatusi Manka na Jovi. Lakini maneno ya mkosaji yasiwanyime raha ya kunywa maji Manka na Jovi. Unambiwa Usisafirie Nyota Ya Mwenzio.

Haya Wantanzania mkitaka kunitusi mie kwa sababu ya maneno haya basi nawambia hewalwa, lakini ukweli ni kwamba watanzania tuache mambo ya kishenzi, kwani viji mambo vidogo tunafanya yawe makubwa mno.

Kila la kheri Manka na Jovi
Mdau Samira

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 82 mpaka sasa

  1. "Usigemee hata siku moja watu au binadamu watakuwa na namna moja ya kufikiri.Kufikiri tofauti na kutoa maoni tofauti ndio maana ya binadamu.Unachokiona wewe kinafaa kwa mwingine hakifai."

    ReplyDelete
  2. Uncle MICHUZI,
    mimi nilifikiri "KUCHAFUA HEWA" maana yake ni kujamba, sasa ina maana watu wamejamba humu ndani au labda mimi ni wa zamani sana, lugha mpya siijui. anyway, usishangae sana kawaida yetu wabongo ni kubomoa, hata ngudu zetu wakenya huwa wanatucheka. labda ipo siku tutakuwa.

    ReplyDelete
  3. Michuzi mie nakushauri uwe pia unawashauri wasomaji wako wanaokutumia barua za kutafuta wachumba wachague kwa makini maneno ya kujieleza mbele za watu, maana ni maneno yao wenyewe ndio yanayowachokoza watu wawasemee mbovu. Ingawa busara ya kawaida ingekuwa kwamba wanaume wasiomtaka huyo mwanamke basi wanyamaze, lakini wengine wanawashwa kutoa kero wanayojihisi kuipata kutokana na maelezo ya mhusika. Kwa mfano mtu anapotoa maelezo yanayoonekana wazi kuwabagua au kuwabeza watu wengine, basi wale waliojisikia kubezwa wanajibu, wanajitetea ili kuridhisha nafsi zao wasijisikie kuumia sana. Kwa hiyo bwana Michuzi ukishapata tangazo la anayesaka mchumba, hebu lipitie kwa makini kwa busara yako, kisha wasiliana na mhusika ushauriane naye kwanza kabla hujalibandika hapa. Ninaamini wewe binafsi una uzoefu wa kutosha tu hata kabla hujaanza haya mambo ya blogging, tumia uzoefu huo kumshauri mhusika kuhusu jinsi jamii inavyoweza kuyachukulia baadhi ya maneno atakayokuwa ameyaweka kwenye tangazo lake, alirekebishe ipasavyo ndipo ulibandike.

    ReplyDelete
  4. Mkuu Michuzi,
    Ujumbe wako ni mzito na ninakubaliana nawe mia kwa mia.
    Kuna wadau wengi katika blog yako wenye "negativism mind".
    Tungependa watu wawe na uhuru wa kutoa maoni, lakini kama uhuru unapitiliza, basi inabidi uweke "censorship" ya comments, ni kazi ya ziada, lakini inahitajika ikibidi.
    Mdau

    ReplyDelete
  5. Tatizo la wabongo upeo wetu ni mdogo sana kutafuta wachumba ni jambo la kawaida sana katika nchi zilizoendelea ila wabongo akili na upeo ni mdogo sana wa kung'amua mambo jamani tuelimike !!

    ReplyDelete
  6. Wheeeew.. What a speech! U said it all Michuzi!

    ReplyDelete
  7. Nimesoma malalamiko yako, pia baadhi ya maoni yaliyowekwa... hata mimi nimesikitika sana. Nikweli tusitegemee kupata maoni mazuri au ya aina moja wakati wote. Tunaheshimu uhuru wa kuchangia maoni, lakini pia sio kuvuka mipaka.

    Nakuomba uwe mvumilivu kwa ndugu zetu wasioelewa kabisa haya mambo, kwa Tanzania tunakubali bado mambo haya ni mageni hasa kwa baadhi yetu ambao hatujatembea nje ya Tanzania (lack of exposure), ingawa kimsingi kutokujua mengi hakufuti yale machache na ya msingi unayojua, sana sana ni ulimbukeni uliokithiri na wa kuendekeza ndio utakupotezea sifa na heshima yote ya ustaarabu kwa hawa wenzetu wasioelewa na kuamua kuchafua hali ya hewa.

    Zaidi ya hapo sina mengi, ila pamoja na kuchafuliwa hali ya hewa ningekusihi uchukulie jambo hilo kama uelewa wa baadhi yetu ambao kama Bro Michu alivyosema nanukuu "INAKERA KUONA BAADHI (NASEMA KWA MSISITIZO, BAADHI NA NI KUNDI DOGO SANA!) YA WADAU HAWANA KAZI ILA KUSAGIA KILA KINACHOWEKWA HUMU. HAWANA JEMA, HAWANA DOGO, HAWANA SIMILE, HAWANA HATA MAWAZO MBADALA KWA WANALOPINGA, ILIMRADI WAMEPINGA." mwisho wa kunukuu.

    Hapa inaonyesha jinsi gani ndugu zetu hawa wanavyohitaji kuelimishwa na kufahamishwa.

    Nakutakia kila la kheri kwenye shughuli zako hasa hili la kutafuta mchumba.

    ReplyDelete
  8. HIVI SISI WATANZANIA TUNA MATATAIZO GANI? MWANZO WATU WALIKUWA WANATAFUTA WACHAMBU BILA PICHA,KAKA MIUCHUZI AKASEMA WATU WAWEKA PICHA SASA DADA MZURI HUYO JUU NA KATAJA SIFA ZA MTU ANAYEMTAKA KAMA HAMNA MTU HUYO SIMUACHE TU MPAKA ATAKAPO PATA BAHATI HIO? MIE DADA KANIVUTIA KWELI KUSEMA KWELI SEMA DINI YANGU NDIO INANIKWAMISHA TU.WADAU WAKIKRISTO KAMA UNA MASTERS MTOTO HUYO YUKO SERIOUS NA KAMA UNAONA HUNA VIGEZO ALIVYOTAKA BASI MUACHE HAINA HAJA YA KUMTUPIA MATUSI.MATUSI NI HASIRA NA WIVU NDIO HUO UNASABABISHA MATUSI.NA NDIO MAANA WATU WAKIONA MATUSI NA WIVU HUTOSHI WANAKIMBILIA UCHAWI.NYIE WATOTO WADOGO SANA KUWA NA ROHO ZA KOROSHO.DADA NI MREMBO MPENI HONGERA ZAKE SIO WIVU NA MATUSI YA KUMKATISHA TAMAA.

    ReplyDelete
  9. Well said Michuzi.

    Umesomeka sawa sawia; ndio hivyo tena binadamu tumetofautiana, tuvumiliane ili tuendeleze libeneke!!

    Soames.

    ReplyDelete
  10. WABEBA BOX HAO WANA HASIRA KINOMA WANAJUA NGOMA ZAO NGUMU SANA HAWAWEZI KUPATA MTOTO KAMA HUYO SASA WANAONA BORA WATUPE MATUSI.KAKA MICHUZI UNAFIKIRI MTU UMETOKA KUPIGA BOX MGONGO WOTE UNAUMA ALAFU UNAFIKA NYUMBANI UNAKUTANA NA MTOTO MZURI KAMA HUYU ANATAFUTA MCHUMBA AKATI WEWE MWENYE HUJUI WAPI UTAPONA USIKU WA LEO HA HA HA HA.DADA KILEO USIJALI MATUSI HAYO WATU WAMEPIGIKA .ALAFU UMEWAMALIZA ZAIDI KUITAJI MASTERS MANAKE HILO NI TUSI KUBWA UMEWATUKANA WAO KULIKO WEWE MATUSI 350 WALIOKUTUMIA.KWAHIO WEWE WDELETE TU EMAILS HIZO USIUMIE SANA.

    ReplyDelete
  11. Kwa jinsi ulivyotiririka kwa ufasaha na kwa msisitizo natumai umeeleweka.Kweli muandishi ni muandishi tu.Hali hii inakera kwani wanakijiji wanapotuamini na kutushirikisha ndoto zao za kutafuta uchumba ni heshima kubwa.Ni jukumu letu wadau wote kuheshima hadhi hii tuliyopewa na kama hatuna cha kusaidia ni vema kuuchuna na sio kudhihaki.Pole Jovinata...we achana nao.by Jean Pierre Akayesu

    ReplyDelete
  12. Ohooo!!!!!!!!! This is too bad. Lakini na yeye mbona hakujibu yangu na nimemtumia nzuri tu? Na nilimuahidi kuwa atakaponijibu nami nitamtumia picha zangu? Shauri lake na yeye hajatulia.

    ReplyDelete
  13. Jovinatha, usikate tamaa, whoever did that to you has his/her own frustration kama alivyoainisha michuzi, mimi haiingi akilini kwa mtu mzima kutukana au kudhalilisha mtu kwa kujitosa kutafuta mchumba, manka mlimwomba picha, huyu kawa jasiri kaweka hapo... still..., there are people who come in to correct english, i call them unauthorised english teachers ( and there are people who correct those who are teachers !! ), there are those who critisize even a genuine thing, those are failures, and there are those who comments away without knowing what is it they are commenting about...aaaaaaaaaah lakini ndio hivyo mambo ya blog kila mtu anamwaga lake akiingia ki anony.. kama wewe jasiri, weka jina na picha... hata mie sithubutu..so mwacheni jasiri mpeni haki yake

    ReplyDelete
  14. Bwana Michuzi, Naomba unipe wasaa niseme kidogo. Nitaumia sana kama utanibania. Nimesoma ujumbe wa Jovinata na roho yangu imeuma sana kuona binti amelia kwa matusi na udhalilishaji ya vijana wasiopenda maendeleo ya wengine. Baadhi yetu sisi watanzania ni viumbe wa ajabu sana. Kwani mtu kuweka mambo hadharani ni kosa?? Kwa utafiti wangu asilimia kubwa ya watanzania wanaoa kwa kulazimishwa direct or indirect..wakati nasoma sikuwa na mpango na mademu.. ni kwa muda mrefu..kilichotokea nilisakamwa kuanzia dada zangu hadi wazazi..wote wakadhani mimi ni mwanaume hasara..nilisakamwa sana kisaikolojia hadi wakaniletea demu ili waone..any way..It is sad story..Mambo ya huyu binti yamenikumbusha jinsi watu wengine wanvyoweza kuingilia uhuru wa mtu mwengine.. Nimechoka sana kuona kuna viumbe wengine wanakaa na kufuatilia maisha ya wengine, wengi wao wameoa changudoa waliowapata kwenye ulabu, wengine wameoa wasichana wa kazi waliowapa mimba, wengine wameoa wanawake walisakikiziwa na ndugu zao kwa ajili ya dhiki na uwezo.. Tanzania yetu ni nchi masikini sana, Matatizo ya uchumi wetu yanaingia mpaka vichwani mwetu, hadi tunakosa uwezo wa kufikiri. Hebu niambie Brother Michuzi..kila mtu aliyemsakama huyo binti ajichunguze yeye mwenyewe kama yuko thabiti.. wenzetu wanaendelea.. mambo ya uwazi.. wanaongea mambo ya maana..Mimi napenda sana kupitia hii blogu yako kila siku.. lakini kuna watu humu wana roho za korosho na vichwa vilivyojaa virusi vya kutotaka maendeleo.. Kadiri navyotembea kwenye nchi za wenzetu ndivyo navyopata hasira kuona vijana wa nyumbani wasivyopenda kujishughulisha..na wasivyopenda kupanga maisha yao..wanakaa kuchafua hali ya hewa kwenye blogu yako..Ningependa kumpa pole Jovita..Najua wako wengi wenye negative thinking humu ndani lakini wapo wachache wenye positive thinking..huyu dada anatafuta mmoja wao..She has to remember.."To succeed, you must first believe that you can"

    ReplyDelete
  15. shame on all narrow minded people,yani hata sielewi watz kwanini tuna roho ya kwanini sana.mambo ya kutafuta wachumba kwenye internet ni kawaida sana,hata mimi nilipata mume kwenye internet and im happy married ila watu wanaponda mara utakuwa una kasoro ooh mara sijui nini.jovinata nenda kwenye dating site za waafrika weka profile yako na picha na sifa uzitakazo kwa huyo mume watakuja tu wenyewe hata watz ambao wanatafuta wapo kibao huko.all the luck
    Mrs Ben

    ReplyDelete
  16. pole jovinata,
    hivi sisi wabongo tukoje?
    binafsi sioni sababu hata ya kumtumia mail binafsi huyo mdada,kama huna interest naye.maana yeye ametoa email kwa wale ambao wanataka mahusiano naye,achambue kwa muda wake nani wa kuchukua na wa kumwacha.
    tena utashangaa sana bwana michuzi ukiambiwa hao waliotuma mails za kumtusi dada jovi frastresheni zao ni kuwa hawajafanikiwa kupata wapenzi,au ndo wale wanaotafuta bila mafanikio...au hata akimwimbisha mrembo anaishiwa kukataliwa kila leo..
    haters mtaishia tu kubwabwaja.
    maana huo ni wivu.......
    mwaya jovinata ukipata mchumba pia usisite kutuinform..tucelebrate..pole again.
    wish u lucky..
    mdau
    chema

    ReplyDelete
  17. Bro michu mimi si mchangiaji sana ila kwa kweli leo nimeguswa kusema huyu binti nilivyosoma habari yake juzi asubuhi sikutegemea watu wangesema maneno ya ajabu hivyo kwani nilitamani ningekuwa na vigezo nisingesita kumjibu na mwisho kuwa mke wangu. ila nimeshangaa kuona watu wamejibu kwa kejeli na matusi kweli kuna mambo mengi ambayo kutumia blog hii tungeweza kufaidika lakini unaposoma maoni ya watu unasita kubandika mawazo yako hapa. Naomba wadau tuwe wastaarabu jamani sio lazima uchezee keyboard if you have nothing good to comment, comment nothing. Nadhani wenye nia watajibu kwa ufasaha. NADHANI MTU kama manka hatathubutu tena kuandika kitu humu. ila kiboko ya waosha vinywa ni chibiliti!!!

    ReplyDelete
  18. Ano. April 4, 2008 3:16:00 PM EAT,
    Acha ujinga, Kama ulishidwa kupata visa kwa matatizo yako ya kushidwa kupima TB au ngoma nyamaza. It has nuthing to do na tuliokuwa half paradise. Atii wabebab box, Masters is a normal thing hapa si dili na we go further baada ya hizo Masters. Chunga kinywa chako maan ndio kinakuongoza.
    Londoner

    ReplyDelete
  19. Michuzi lazma umtetee huyu ms kalumanzila kwa nguvu zooote.
    Hamna cha senene au kuchafua upepo (hata mi hii maana yake siielewi!) sema demu anaibua mjadala na kukufanya upate hits nyingi na watu wengi sana watume comments therefore kiaina anakutuoa.

    Sasa braza mithupu mi nakushangaa sana unavyomtetea huyu demu wakati email katumiwa kwenye inbox yake so it is her won private affair na wewe ulitakiwa umpe pole tu lakini si kuja kuwakoromea wana blog. hapa mi naona conflict ya interest kubwa.

    Jovini, alitegemea email zote zimsifie tuu? Ndo maisha hayo dada, you need to grow up

    ReplyDelete
  20. Afadhali umesema Michuzi, hebu waambie hao BAADHI ya wanaume wanaopenda kuponda wasichana, waache hizo tabia, hawa ndio wale wanapokataliwa na wapenzi basi huanza kumwaga matusi na kashfa kibao, mara oo yule mwanamke malaya, ana dharau na mengine ya ndani ambayo ni ya aibu:si vizuri kumtangaza mwenzio vibaya na kumpakazia kisa kakunyima penzi au kakupiga kibuti.

    Yaani imekuwa kama vile wanaume ndio wanajua kupenda tu na wao ndio watoe vigezo, akitoa mwanamke dhambi, tujaribu kubadilika jamani.

    Kuwa na mawazo m-badala sio jambo baya..lakini kwani ukitofautiana na mtu ni lazima umtukane?! mwambie wapi amekosea na ajirekebishe vipi si kumtusi.

    Mimi ni mwanamke wa miaka 35, nina elimu zaidi ya mume wangu na mie ndie niliyemt*ngoza, tena nilimbembeleza kweli na kukomba kwa kila hali ambayo kufukuzia penzi inavyokuwa. Alinikubalia,nilimpa pesa za mahari na za kufanyia harusi, tukaoana, na tunaishi raha mustarehe na watoto wetu watatu sasa. Sijawahi mdharau hata siku moja though huwa tunatofautiana kama binadamu.

    Hivyo chonde kina dada wenye msimamo mnaotaka kutafuta wachumba wa type yenu tafuteni, msichoke wala msiogope, yatakwisha tu haya kwani hiki ni kipindi cha mpito.

    Mamdogo

    ReplyDelete
  21. POLE SANA JOVINATA,
    UNAJUA WASWAHILI SIKU ZOTE HAWANA DOGO, KWANI LIPI JIPYA NA GENI KAMA MSICHANA HAJAPATA MWANAUME KTK UMRI KAMA HUO?JAMANI TUWENI WASTAARABU TUNAPOCHANGIA WALA HULAZIMISHWI KUTOA MAONI.
    MANKA ALIPOSEMA ANATAKA MWANAUME WATU WALICHONGA SANA OHHH EHHHE KWANI JIPYA NI LIPI MIMI NASHINDWA KUELEWA KABISA.
    SASA JOVINATA WAPO WANAUME WENYE BUSARA NA AKILI TIMAMU WAMEKUONA NA KUKUPENDA WATAKUTAKA TU I BELIEVE.
    MUNGU YUPO NA ATAKUSAIDIA TU USIJALI.
    BE BLESSED.

    ReplyDelete
  22. pole sana dada. ni kweli inauma. ila lazima ukubali kuwa watu wapo wa aina tofauti sana. hata hivyo naamini wapo wachache waliokuwa serious. wajibu tu hao. naamini watanzania watabadilika taratibu. kumbuka mwanzo mgumu sana.

    hili lilianzishwa na Manka nadhani litabdilisha mitazamo ya wadau taratibu.

    mdau wa uholanzi

    ReplyDelete
  23. Ili kuondokana na hili zengwe Michuz haya masuala ya Uchumba na Kupotelewa na Pikipiki yatafutie Column yake.This is SERIOUS BUSINESS!Wengine hapa wanachukulia utani lakini kwa wengine kutafuta mchumba kupitia Internet si masuala ya utani.Wenzetu Ulaya kwa hili wamefika mbali sana.Watu hawana TIME ya kuzurura huku na kule ukifanya SAMPLING YA WASICHANA!Uonje kila ukionacho,Bulls*&%!They have more serious business to do than just shitting around politicking like we do most of the days!Ikiwepo Column maalum kwa ajili yao atakaye kwenda kutembelea pages za kule basi atakuwa amedhamiria.Ambao kwao ukiwatajia mambo ya uchumba umewatonesha machungu kibao ya kuachwa,kutelekezwa au hata kuingizwa mjini watazua sokomoko balaa kama ambalo umekuwa ukikabiliana nalo.Siyo kwamba watu siyo wastaarabu.Bali hizo ni dalili za mfadhaiko wa akili.Na tiba yake ni kuyatenganisha masuala hayo mawili,General News of Contemporary Interest na Masuala ya Funuafunua na kupotelewa!Ndio Ukubwa huo Michuz.Tuletee Konoooooooooooooooz!

    ReplyDelete
  24. Kaka Michu naomba nisiusemee moyo ila jamani imeniuma sana kuona watanzania tusivyokuwa hata na roho ya kimaendeleo mi sioni kwa nini wamtukane huyu dada, najua binadamu wote ni sawa na wana uhuru wa kuchagua na kusema yale ambayo wanayatarajia Jovita ana haki ya kusema anataka mchumba wa aina gani... ila nimkumbushe tuu amesahau kuweka point ya kuwa huyu mchumba atakayekubaliana naye lazima wakapime ukimwi dada yangu hiyo usije isahau maana nadhani nayo hii itazua mjadala kwa wale wanaorukaruka hapa na pale..sasa basi dada naomba usife moyo...kwani hata maandiko yanasema jicho lako la kushoto likikukosea ni heri ulingoe ubakie na jicho moja...kwa maan hii ni kwamba una uhuru wa kuchagua kipi kizuri kipi kibaya..you are free to live the life you want..mimi nawashangaa hao ambao wanakutukana kwanza vigezo hawana pili wanakutamani tuu na wanashindwa ni jinsi gani wakuingie kwani wanajua utawamwaga...lakini kumbuka Mchumba mwema kama kweli anasoma hii hoja atakutafuta tuu kwa muda wake anaoujua yeye...ila Mungu ndie anayepanga lakini bila sisi wenyewe kuangalia tutapataje..huwezi kunaiambia unatafuta kazi eti mungu atakupa na wakati ukiona tangazo gazetini hata hutumi applications how mtu aje akuambie njoo kuna kazi hiyo haipo kwa hiyo dada mi nazidi kukupa moyo usiumie na hayo walioandika hao watu tena naomba niwaite Mafisadi wa kutokutaka maendeleo ya mtanzania mwenzao,
    Ombi lako limeonekana na watu mbalimbali I'm sure you will get your soul mate soon. naomba kwa ushauri zaidi niandikie bethmsk@yahoo.com nimeshawasaidia wengi sana kwa ushauri wa issue kama zako.Kaka michu asante wa kutuelemisha na ushauri wako...Stay blessed kaka........Mdau

    ReplyDelete
  25. kuna mijitu sijui ina matatizo gani!! yani mtu kama hujapendezwa na kitu kwanini usiache wengine wenye interest zao ku-comment!! si lazma uchangie.niliona kwenye blog ya mjengwa alipiga picha akiwa shuleni aliposoma tambaza na akaelezea mambo yalivyokua kipindi hicho, kilichonishangaza mimi, kuna mtu ali-comment eti kichwa cha mjengwa kilikua kikubwa wakati ule kuliko sasa, IMAGINE!!!yani huyo alichoona kwenye picha ni kasoro na si kitu positive!!

    ReplyDelete
  26. Polei sana Jovinata kileo, hichi ndicho wengine wanakiita kijiwe, kwasababu kila jambo liwekwalo hapa kwa nia njema kwa minajili ya mjadala,na hasa likiwa linamgusa mtu hugeuzwa kinamna yake, kwasababu watu wanatofautiana kifikira na kiuoni.
    Lakini kumbuka kuwa kila jambo linalotokea linakuja kwasababu maalumu. Hii ni kwa ajili yetu wanadamu kujifunza, ili kila mtu aingie kwenye mitihani fulani kabla ya uamuzi wa busara, na kutokana na mitihani hiyo anaweza akajifunza baadaye kama ni mwingi wa kuelewa.
    Kama ulivyosema umepokea e-mail nyingi na wengi wao wameishia kukutusi, hiyo kwa namna moja ni heri kwako, ingawaje kwa namna nyingine inauma.
    Ni heri kwako kwasababu wote hawo waliokutusi unawabwaga chini (wamekurahisishia), kwani `tabia yao sio nzuri' kama walivyojionyesha. Huoni hapo wamekurahisishia kazi kama kweli ulikuwa na nia ya kutafuta mchumba kwa njia hii. Narudia tena, kama kweli ulikuwa na nia hiyo.
    Waliobakia ambao wamekujibu kwa busara, ndio unatakiwa uwafanyie kazi!(kazi kwako)!
    Kwa mfano wote wangekujibu unavyotaka wewe, huoni kama ungeingia mkenge? Sio kwamba nakubaliana na walivyokujibu kwa matusi, la hasha, ila wao walivyoona kuwa wamekukomoa kwa matusi, hawakujua kuwa nawewe umewagundua udhaifu wao, kuwa wao hawana busara. Kwani wewe ulipenda umpate mume muongo, ambaye angekudanganya kuwa yeye ni mwema mzuri ana elimu ana mali nk?
    Kwahiyo kila jambo likikukuta jaribu kutafakari kabla hujachukua hatua, kwani huenda ni taswira ya tukio jema au baya! Ingawaje kweli inauma, lakini ndio kidunia.
    Kama nilivyokushauri mwanzoni katika maoni yangu niliyotuma awali, inabidi `issue' kama hii uichukulie kwa hekima na busara, halafu uwe na subira. Mume/mke bora hachaguliwi kama nguo dukani, hapimwi kwa kipato au elimu pekee. Inawezekana ukampata kwa njia hiyo, lakini sio lazima, ndio maana unahitajiwa kuwa na subira. Mume/mke bora ni jinsi gani mtakavyopendana hata kama hana hela, hana elimu uitakayo au umbile fulani. Upendo, kuvumiliana na amani ndio ngao ya ubora wa wana ndoa.
    Pia na wewe ujaribu kuziondoa kasoro za kitabia ambazo unaziona, hazipendwi na wanaume, kama una tabia ya majivuno kupita kiasi, jirekebishe, kama una dharau jaribu kuiondoa. Ni vyema ukajenga tabia ya heshima kwa mkubwa hata mdogo,pia uvwaaji wa heshima ni kigezo muhimu na kumbuka kuwa dini ni ngao muhimu, muombe mola wako kwa usiku na mchana utaona tija yake baadaye.
    Samahani kama na mimi nitakuwa nimetumia lugha kali
    bye
    emu-three

    ReplyDelete
  27. Pole dada J-mie ningekuwa wewe ningeendelea kusoma message zote kuona kama angalau nitapata message 1 au mbili ya maana-naweza kufananisha hii kama job interview, watu wengi wana-aply-wachache wanachukuliwa.

    Kuwaziba midomo watu sio rahisi. Kaza roho dada, kupata mchumba sio mchezo. Tumia huu msemo "glass is half empty rather than half full"-angalia yale mazuri tu.

    ReplyDelete
  28. As a professional person( assumed), unapaswa kuelewa mazingira ya kazi zako. kumbuka hizi ni comments za watu. watu tunatofautiana sana (everyone is unique in every sense).
    Pia kumbuka you are the admin. of this blog, unazichuja comments before you release them for the public. Kimsing kwa utandawazi huu pengine usipaswa kuchuja bcoz u may b biased. ur a human being.
    Utakubaliana nami kuwa wewe naye una nyongo that is why u always react that way. kwa mtu mwingine maoni hayo yote yangekuwa ruksa kwa wasomaji wote. Nakumbuka una kesi nyingi sana za kutia kapuni comments za watu, kisa unatafsiri na kuzichambua mbovu na mbivu. je ni kwa manufaa ya nani? bila shaka ni kwa manufaa yako wewe uliye admin!!.
    Tujifunze toka kwa wenzetu na nadhani huu ni mwanzo mzuri tunavyokosoana sasa.
    Ukiangalia mazingira ya utandawazi, internet is the best source of information, equally the worst source as well.acheni taarifa zote ziwepo kwa watumiaji mbalimbali. Bila shaka tutafika tu!!!

    ReplyDelete
  29. BAADHI YA WATANZANIA KWELI WANATIA AIBU KIASI KWAMBA SINA HATA CLASS YA KUWAWEKA. KILA MTU ANAYETOA PICHA AU MAONI YANAYOHUSU PERSONAL LIFE ATASAKAMWA. WATATAFUTA KASORO YOYOTE MPAKA WAAZE KUWACHAMBUA WATU BILA SABABU. MIMI NILISHAREACT MUDA MREFU MFANO NI LADY JAY NA NYUMBA YAKE, CHIBIRITI, FLAVIANA NA WENGINE WENGI.

    HIVI MNATAKA NINI? HAWA WATU WANATAFUTA USHAURI NA KAMA HAMNA NI VYEMA KUNYAMAZA KULIKO KUCHAFULIA SIFA WATANZANIA WOTE. MIMI NAONA NI WIVU UNAOTUSUMBUA. WENGI WENU MNA FRUSTRATIONS ZENU MAISHA YAMEWASHINDA HASIRA MANAZIMALIZIA KWA WATU WASIO NA MAKOSA NA WALA HAWAHUSIKI NA FAILIER ZENU ZA KIMAISHA.
    POLE SANA MDOGO WANGU.

    ReplyDelete
  30. Acha uongo Michuzi.

    Kilichomliza siyo kutukanwa na bloggers bali ni kuona katika bloggers wote 654 waliomwandikia E-mail hajapata mume wa kumuoa.Inatisha.Ningekuwa mimi break ya kwanza bagamoyo kwa kupiga ramli kwa matapeli wa Bagamoyo kujua nina nuksi gani.

    Ana haki ya kulia.

    ReplyDelete
  31. Brother Michuzi,
    Umeongea vizuri sana. Kuna watu siku zote wako negative, na wana wivu wa ajabu, wanashindwa kuelewa kuwa watu hawalingani na kila mtu ana mapendeleo yake binafsi (personal preference). Huyu dada kasema hataki ku date mzungu, na pia mchanganyingo. Watu ooh..m-baguzi..ooh kaburu wa kike..whats all that about? Hii dunia tunayoishi wote tungekuwa tunapenda lets say rangi moja, hebu fikiria how boring that would have been. Tuko tofauti katika kufikiria, tuko tofauti katika kufanya uchaguzi, ndio maana ukienda dukani wana bidhaa mbalimbali na pia kuna wide selection kulingana na preference ya wateja.
    Sio kosa kuweka vigezo vya mtu unayetaka kuishi naye kindoa. Hii ndiyo dunia ya leo. Baadhi ya haya mambo (mageuzi) yanaweza yakawa yalizimwa na mila za makabila nyumbani Tanzania. Sisemi kwamba mila za makabila yetu hazifai, hapana. Ninachotaka kuonyesha hapa ni kwamba kuna mila chache ambazo zinatunyima uhuru na kuna nyingi ambazo zimetu shape kuwa who we are today. Ndio maana kuna baadhi ya mama zetu waliingia kwenye ndoa na baba zetu kwa kulazimishwa, halafu 10 years later wakaanza kuzoeana as spouses na ku fall in love. Tukirudi kwenye vigezo, kama mimi nimepiga piga shule kwa nini nisimtafute mwenzi ambaye na yeye kidogo “ka-kanyaga kanyaga umande” mtu ambaye atakuwa anani challenge intellectually kwenye mambo mengi tu. Mtu ambaye hata mkiwa na wageni wenu kunakuwa hakuna shortage ya points za maongezi kwa sababu atleast kuna enough knowledge on variety of subjects iwe katika siasa, michezo, uchumi, historia, biashara, teknolojia, fashion, geografia, na kadhalika. Ni nature yetu binadamu kupendelea perfection. Kama tungekuwa na ways tungependa tuwe na kila kitu top notch kuanzia usafiri, nyumba, kazi, bank accounts, spouses, watoto, etc., lakini sio vyote tuombavyo au tunavyo desire tuvipate. Lakini its okay to dream big...so long as we are not day dreaming. Ku day dream ni kufikiria vitu ambavyo havitakaa viwezekane. Ni kama mimi nianze kufikiria kuwa siku moja nitashindana kwenye Olympic kuogelea wakati swimming pool kwangu ni no no. Huyu binti ana dream na vitu ambayo viko within her reach. Ana drem reality. Hajasema anataka ku date mtu wa caliber ya akina Kennedy family, ama anamtaka Reggie Bush..huko kungekuwa ni ku day dream, lakini kasema anataka msomi wa kiwango cha Masters, mcha Mungu, asiyetumia kileo, nk. All those attributes ziko na kuna vijana wengi tu wanazo, whats the problem? Kila mtu ana ndoto zake zangu sitazitoa naziacha nikae nazo mie pekee.
    Ninawaomba watanzania wenzangu, tupunguze kupakana matope. Tuache kuwa bitter. Kuna wadau huwa wanabandika picha zao hapa....basi ni negativity na kupakana kwenda mbele. Kama mtu amesota shule na finally ka gradute na kaona kwamba sasa yuko on the mountain top, na akapendelea kuleta picha zake za tukio kama hilo...whats the problem? Kila mara hapa huwa na post maoni yangu na nimekuwa nikiwakemea watu ambao kazi yao ni kuwaambia wengine “YOU CAN NOT”, You are this, you are that. No we have to change this mentality. Tunaua vipaji vingi sana kwa sababu ya negativity zetu. Tanzania ukimuona mtoto wa mwenzako anafanya vizuri kwenye fani yeyote ile unamtakia mabaya...Marekani wanatafuta namna ya kuinua ile talent kwa sababu akifanikiwa mtu mmoja matunda hayo mafanikio yataenea na ku effect watu wengine. Kwa nini tusipeane moyo? Kwa nini tusianze kujenga tamaduni za kusifiana badala ya kupelekana kwa waganga wa kienyeji? Mambo mengi mazuri yanafunguka tukiwa kwenye positive mindset then tukifanya kazi sio kwa nguvu pekee, but also smartly.
    Finally, nampa Jovinata hongera kwa ujasiri aliokuwa nao wa kuweka hisia zake wazi. Hii confidence itakupa kazi popote pale dunia.

    ReplyDelete
  32. Sheeeeeeeeeeeeeeeeeee! naomba niseme!
    Wadau wote waliochangia wako sahihi, waliochafua hali ya hewa, waliopinga kistaarabu na waliounga mkono, wote hawajakosea. Kama mhe mbunge Mishusi alivyosema haujafanyika utafiti wa kisayansi wa kuelewa kwa nini wanachafua hali ya hewa, so hatujui sababu hivyo watu wote wako sahihi.
    Sisi wote ni watanzaniawengi wetu tumezaliwa tanzania na kukulia tanzania tujiulize mila zetu tulizokulia zilikuwaje? Je ilikuwa ni kawaida kuona msichana/mwanamke anatafuta mchumba? Je ilikuwa kawaida kusikia mwanamke anataka mume wake afanye kitu fulani? Nafikiri jibu ni hapana.

    Hivyo kutokana na jinsi tulivyokuwa na mila zetu zilivyokuwa ndio maana tunatoa maoni kama hayo mimi ninaamini zaidi ya 90% ya watanzania halisi wataona huyu binti amefanya kosa kupanga kuwa mchumba anayemtaka awe na elimu nzuri ya "juu" huko ni kujitafutia makuu. Na kueleza kuwa amempenda John Mashaka "sorry John" then atakubali tu kuwa na mtu mwingine endapo John atakuwa na mwenza au hatompenda, wengi wetu tunaona kuwa hatafuti mume bali anajitangaza na kutaka makuu ndio saababu ya kujibu vile watu wanajibu.

    Last but not least Jovi "ili uendelee unahitaji marafiki na ili uendelee zaidi unahitaji maadui" (HAPO VIPI Prof JIZZO) . Je we ulitegemea kuungwa mkono moja kwa moja?

    ReplyDelete
  33. Nami naungana na wadau wote kupinga lugha ya matusi baina yetu.

    Napenda kutoa ushauri kidogo kwa wale ambao wanadhani wanapaswa kutoa maoni, kuuliza swali au kukosoa baada ya kuhisi wamekwazwa au kuhisi mapungufu katika maelezo ya mtu.

    Kwa kua ni muhimu kutoa dukuduku la mtu na pia kwa kua hatuwezi kukwepa kutoa maoni kwani kila binadamu anao uwezo wake wa kufikiri inatupasa tujifunzi ni jinsi gani tunaweza kuyatoa mawazo yetu bila kukwaza wengine.

    Nadhani wadau tunapaswa kufahamu na kutumia kitu kinaitwa "positive criticism" (naomba msaada wa kimatumbi hapa). Kwa lugha rahisi, hii inahusisha kutafuta "positive" side ya kile unachodhani kukukwaza na kukitolea maelezo ukijaribu kuweka maelezo yako kwa kutumia nafsi ya kwanza (mimi).

    Mfano: Badala ya kumwambia mtu kua "Unakula vibaya au unachukiza kwa kutoa sauti wakati wa kula chakula" unajimilikisha hali na kutoa sentensi ifuatayo "Nimeweza kusikia sauti ya jinsi unavyotafuna tokea nikiwa chumba cha pili, tafadhali jaribu kufunga mdomo wakati wa kutafuna"

    Nitazungumzia hili suala mahala fulani ambayo naindaa

    Ignorant
    Jeremani

    ReplyDelete
  34. Jovi should not cry but simply ignore those idiots. Kama alivyosema mmoja hapo juu ni busara kama humtaki unyamaze. Hujawahi kupita njiani ukaona mtu kachora au kaandika matusi? Jiulize ni nini kinakuwa kinaendelea akilini mwake. It is ridiculous. I can understand how Jovi is feeling - dawa ni ku-ignore. Wanaocheza mpira wa kulipwa huku weusi wakati mwingine hutukanwa - lakini kuwanyamazisha watu kama hao ni kuonesha kuwa you can deliver.

    ReplyDelete
  35. Nimesoma kwa makini yaliyoandikwa na Michuzi na dada jovinatha.Mimi nina maoni tofauti.Kila kitu kina ugumu wake na mtu asitugemee kutokukumbana na changamoto yoyote maishani.Kwa hapa hata iweje wenye akili za uwendawazimu hawakosekani kutokana na maendeleo yetu kuwa nyuma.Ninachoweza kusema ukiwa mpiganaji usiogope ngumi za usoni.Dada amekerwa lakini naamini atafanikiwa na kero zote zitaisha na kusahau.Awaone wanaompa maneno ambayo hayafai kama ni wendawazimu na asiwasukilize ila ashike lake.
    POLE SANA DADA JOVINATHA NA ALUTA KONTINUA

    ReplyDelete
  36. pole dadaa ndiyo hivyo mawazo sikuzote yanatofautina na hasa pale mtu anapopokea ujumbe,usikate tamaa sana kawaida ya binadamu,sife moyo utampata unayempenda naamini hvyo

    ReplyDelete
  37. Pole sana kaka michuzi, yaani nimesoma ulichoandika na kama mwenye kutambua falsafa ya watu na jamii zao nimekusoma vizuri sana kwamba umeandika ujumbe huu kutoka moyoni.. umekerwa na kukereka ipasavyo,umeshindwa kuliweka moyoni ukaamua kulaindika tena kwa wino mwekundu.. nimesikitika sana na kufurahi kwa upande mungine uliposema unapata emailz zaid ya 2000 kwa siku.. Man that's awesome. HOW DO U MANAGE READING THEM NA VITU VINGINE UNAFANYA!!
    BIG UP SANA KAKA MICHUZI. mwisho napenda sana kutoa ushauri wa wazi kwa dada binti kileo, kwa mwanaume mwenye kujiamini na nia thabiti ya kuwa na mwanamke kama wewe (i'm not interested thou..) ningeweka pending maombi yako nikasubiri na kutafuta muda ambao utakuwa muafaka kwa kuanza mawasiliano nawe.. Sasa kama kweli unataka mume wa maana.. nakusihi futa email zote ulizotumiwa bila kusoma kwani wengi waliotuma kwasasa hawajui wanafanya nini kwasababu wamefanya maamuzi haraka mno. kwa mwanaume mwenye kujua anafanya nini na baada ya kashazingatia kila kigezo na sifa za kuwa nawe atakutafuta baada ya michakato mizima iliyokukuta kuisha na kukupoza moyo ili mfikie muafaka na pengine ndoa kama navyotamani iwe.

    Kwa sasa hutopata mkweli.. wengi ni walagai na wasiojua wanafanya nini.. huwezi kuona mwanamke leo kwenye blog tena kesho ukatangaza ndoa.. u need to spend time on u r own kutafakari na kumpa mwenzio muda wa kukupa nafasi moyoni.. mi sidhani kama kweli kwakuwa unahitaji mwenza basi uko tayari hata leo.. hata kaka mashaka uliyevutiwa nae na kueleza hisia zako hadharani angkujibu na kukwambia anakubali maombi yako ungechukua muda kufanya maamuzi pia.

    SO WAIT. WANAUME TUMESHAKUONA NA ALIYE MAKINI NA ANACHOFANYA ATAKUTAFUTA BAADA YA MUDA HII KUISHA.

    Mwisho pole kwa yote na hongera kwa ulipofikia..

    Michuzi dunia ina watu wa aina nyingi sana. wengine tuwazoee na wengine tuwadharau .. wanaostahili tuwaelimishe.

    Ndimi,

    Abu' l faadhil. UK

    ReplyDelete
  38. watu wengine sio wastaarabu usiwajali dada yangu

    ReplyDelete
  39. Michuzi,

    Kwani hii Imekuwa MATCH.COM au eHARMONY.COM!?. Hiz ni fiksi kama zile fiksi za kuchaguliwa Mkuu wa wilaya...au labda mi sielewi. Ila mi namshauri huyu mwanamke, a slow down kwani haya mambo hayahitaji haraka...amuombe mungu wake ili amsaidia kwenye maamuzi yake "Esp amesema yeye ni Mcha Mungu", na sio Kuanza kutafuta mtu wa kuishi/baba watoto kwani hizi ni dalili za kukata tamaa na maisha au stress, which can/may lead to absurd behavior(s). Kama hayo yote yakishindikana Basi Akaonane na Psychiatric "sijui kiswahili anaitwaje", Kwani MUME/MKE hatafutwi na hivi vitu huwa vinakuja vyenyewe (you cant grow chemistry within individuals, it grows itself) if it made sence. Kama Huu ushauri wangu hauja-fahamika basi..mwambie akaweke profile yake online... GooDLuck....mwambie aongeze picha, apiga picha akiwa ameshika Karatasi inasema MICHUZI-KWA-WOTE, ila ma-bloggers waprove kma ni kweli au la, ili kama kuna mtu mwenye msaada zaidi ya huu ameweze kuwa serious KIDOGO, kwani matusi aliyo receive ni kwa sababu watu hawaamini haya mambo ya ONLINE, wamekuwa Spoofed sana!...its hard to blv....kwa Leo Acha nichechemee!!....

    -BooSt3D.

    ReplyDelete
  40. we anany wa hapo juu Friday 4th saa 3:16:00 umechemsha umesema WACHAMBU !! sio wachambu ni WACHUMBA ! mpaka na kiswahili lugha tuwafundishe jamani? Speaking of which jamani nyie wadau mliopo bongo lile gazeti la sani bado lipo ? na yule Mzee Kifimbo Cheza je amefwariki ama yu hai ? nataka nijue mana kama alidedi hilo pati alilofanya Madenge na washkaji zake inaelekea lilikuwa la shoka.
    Anyway back to the subject , Bi. Jovinata pole mimi ningekuwa na mdogo wa kiume au kaka alietulia na mwenye sifa ulizozitaka bila ya kujali udini (mana ni Muislamu)Wallah ningekutafuta mimi halafu nikawaunganisha tukakubadilisha wewe dini then kandoa ka mkeka kakapita nikajipatia kawifikenye sura nzuuuri but bahati mbaya ndio hivyo tena naona process yangu ni ndeefu na ina vikwazo kedekede...otherwise ungekuwa wifi yangu sema ndio hivyo. My advise to you girl is dont ever mind the haters coz u got guts and balls than any of them unlike many who are just easy to criticise but we dont see them taking any action to sort out their sorry and miserable lives !They haters and they will always be sad till they change their ways.
    Kwa Kaka Michuzi kwa kweli ndio mana ukachaguliwa Mkuu wa Wilaya ya Tegeta (kwa siku moja) mana great speech with full of emotion ama kweli kaka yetu ni Mtetezi wa Wanyonge, you really care !! keep up the good work bro....!!
    To all ya haters out there ya'll keep hating and ya faces will look like lemons or lime !!! trust me it shows in ya face !! ha ha ha

    ReplyDelete
  41. Michuzi,

    Na wewe unashauriwa uache usenene. Mara nyingi unaweka picha zenye matangazo ya bidhaa na maelezo ya chini yake unasema hizo bidhaa zinatoka USA. Watu wakiandika tena kwa lugha nzuri tu kwamba hivyo vitu si vya USA na kwamba wananchi wajiadhari navyo, wewe kaka michuzi huwa unabania hizo points. Kubania kwako points nziko kunawafanya hao watu wakuige wewe tabia yako ya usenene na wao wawe masenene kama wewe.

    Hivyo kaka Michuzi na wewe inabidi ubadilishe mwelekeo wako.

    Ninafahamu hutaiweka hii point kwa sababu imekugusa moja kwa moja. Kama ukiiweka nitakusifu sana. Na ukiweka matangazo ya bidhaa na ukasema wkamba zinatoka USA mimi nitaendelea kutoa maoni yangu. Usipoyaweka then nita-prove kwamba mhhh Kaka Michuzi hajaacha usenene. Sawa?

    ReplyDelete
  42. MICHUZI mimi sidhani kama hawa wanaotoa matangazo ya uchumba ni watu wa kweli [ i don't think they actualy exist, i think they are invented !]kuna mtu tu anatuchezea akili, ninasema hivyo kwa sababu sijaona hata mtu mmoja anasema mimi namjua huyu dada, nimesoma naye mahali fulani, au nimefanya naye kazi mahali fulani. MICHUZI TUTHIBITISHIE KWELI kama huyu dada yupo, na wachumba wa kweli tutajitokeza, SITANII, kwa sababu wengine pia tunatafuta. Na hata hiyo picha, hizo fenicha siyo za Bongo wala Juba,na kama ni Juba sudan basi ni 5 star hotel, ambayo bado haijajengwa kwa sababu bado hawajasimama vizuri after 22 yrs of war !!!

    ReplyDelete
  43. Wasiwasi wangu nyie mnaojidai kulaumu ndo nyie nyie mlotuma hizo mail.....

    Ni wangu mtazamo... lkn kwa hesabu ya chap chap kwa idadi alioitoa huyo mdada sidhani kama nyie mliokandya si kati ya waliotukana...

    ReplyDelete
  44. Too sad...yaani inasikitisha...email 600 za matusi...!!!! kweli watanzania tubadilike...hii ni generation mpya hivi nyie mnabakia kung'ang'ania miaka ya nyuma tuuu ...mwanamke ni kukaa kutafutwa tuuuuu!!!! No choices ...no saying....!!!!!....I wonder why mliomtukana msichana wa watu anayetafuta mchumba....ni kwa vile quality zenu hazikufikia au ni nini?

    It is so sad to read this....Labda bongo ndio mna matatizo hayo lakini mimi niko huku na kupost info kwenye match.com ni jambo la kawaida...Na hata bosi wangu ana Phd yake lakini mwaka jana ndio ameoa na mke wake wamekutana kwenye net...Na mwanamke ndio alipost information zake yeye akamcontact.....

    Haters mtakufa siku si zenu ...kwanza midomo wazi kwa vile maneno hayawaishi.....damn ass!!!!!....

    Inabidi tubadilike....Kaka Michuzi thanks ...Kila siku tukiwapa vipande vyao labda watabadilika....

    Mtu akiolewa na mzungu ...maneno...akioa mzungu ...maneno...sasa huyu mtoto wa watu kaweka info zake anatafuta kaka zake ...maneno...hivi unazania hawezi kupost kwenye mail oder bride site akapata mtu wa nje ya bongo....???? ..ni kwamba anatafuta mtu wa kitanzania sasa nyie maneno ya nini....?????

    Wabaongo wanakatisha tamaa sana...sijui hii culture ni ya wapi hatuna jema kila kitu ni negatives tu...

    ReplyDelete
  45. Well said Michuzi, wabongo wana wivu. Sioni kama Jovi ame commit any crime kutafuta mchumba, mie mwenyewe nilimtafuta mume wangu, kwa hali na mali, ila nilianza mapema...Watu wana wivu kweli ndo maana wanaishia kumtukana dada wa watu. Hey Jovi usilie, be strong, wale wenye wivu woote ndo wana muda wa kukutukana...keep your spirit up, and guess what, ukifanikiwa kumpata mchumba let us know, some of us are positive minded people, and we like to stay that way, achana na negative minded people, they will not help you in any way, besides, jua kwamba not every success you achieve kila mtu anafurahia, so washiti wale wanaokuonea wivu, bse not everyone is brave kutafuta mchumba online.....You go girl

    ReplyDelete
  46. YAH U RYT BROTHER..U KNW IT IS INSANE SEEING PPLE DOIND STUPIDITY STUFFS LIKE THESE N MOS OF EM R GROWNUP SO NASHANGAA WHATS WRONG WID 'EM,ITS FLABBERGASTING N DISSAPPOINTING 4 SURE,MAY B TATIZO NI UMASKINI WA FIKRA WALIONAO...BUT U GUYS U BETTER B CIVILIZED,WE HV TO B READY 2 ACCEPT CHANGES..THESE MAJUNGUS N KUKANDIANA WE BETTER PUT EM ASIDE,LETS MAKE DIS BLOG A BETTER SITE 2 VISIT..NI HAYO 2!! @ SHAMIEZO

    ReplyDelete
  47. KUNA WASICHANA WENGI SANA WANATAFUTA WENZA WAO SASA HIVI, NA KUNA WANAUME PIA WANATAFUTA WENZA WA KUISHI NAO, LAKINI WENGI HAWANA UJASIRI WA HUYO DADA JO'. WENGI HUISHIA KUSONONEKA AU KUOA AU KUOLEWA NA YEYOTE ATAKAYEKATIZA MBELE YA USO WAKE. UNGEKUWA MWISLAM NINGEKWAMBIA NENDA KWENYE MUSLIM WEBSITE HUKO WALA WATU WASINGEONA AJABU MTOTO WA KIKE KUTAFUTA MCHUMBA.

    NA MICHUZI UNAKOSEA KUSEMA HAYA NI MAGENI, SI MAGENI KWA KWELI NDIO MAANA KUNA NENO LA KISWAHILI LA KUWADI, HUYU AWEZA KUPELEKA UJUMBE KWA MWANAUME AU KWA MWANAMKE. NA SI LA KUKUWADIWA TU KUTANGAZA KUWA UNATAFUTA MCHUMBA KWA WAISLAM SI JAMBO LA AJABU, MAANA WENGI WAMETANGAZA NA WAMEPATA. VILE VILE KUWEKA VIGEZO KWENYE UISLAM VIKO VIGEZO VIMEWEKWA NA UNARUHUSIWA KUWEKA VIGEZO ILA UNASHAURIWA KIGEZO KIKUU KIWE UCHA MUNGU.!

    SASA NATAKA KUWALAMBA HAO WENYE MATUSI, NA WAMEMTUKANA DADA WA WATU KWA KUWA NI MWANAMKE (NAHAMA SASA NAHAMIA KWENYE USAWA WA KINJISIA). JAMII YETU INA UGONJWA WA MFUMO DUME! KITU AKIKIFANYA MWANAUME WATAKISIFIA LAKINI AKIKIFANYA MWANAMKE BASI UTAFIKIRI KAJINYEA ATAKAVYOCHAMBWA NA KUTUKANWA, HAYA NI MAPUNGUFU MAKUBWA YALIYO KATIKA JAMII YETU NA TUSIPOBADILIKA NA KUONDOKA NA HUU MFUMO WA KUMDHALILISHA MWANAMKE BASI HATA HAYO MAENDELELO TUTAYASIKIA REDIONI.

    MWISHO SUALA LA MATUSI SI FRUSTRATION WALA NINI NI SUALA LA MALEZI NA MAKUZI, KAMA UMETOKA KWENYE MIFUPA YA WATU, UMELELEWA NA UKAFUNZWA ADABU VYA KUTOSHA KUTOKA NYUMBANI KWENU, UKAMHESHIMU MKUBWA NA MDOGO MKONO WAKO AU MDOMO WAKO HAUTAWEZA KUTOA MATUSI HATA KAMA UMEKASIRISHWA VIPI. NA KILA UKIJARIBU UTAPATA KIGUGUMIZI.KWA HIYO MICHUZI HAPA HATA UKIKATAZA VIPI NI SAWA NA KUMPIGIA MBUZI GITAA. ILA WASWAHILI WANA MSEMO ASIYEFUNZWA NA MAMAYE HUFUNZWA NA ULIMWENGU, IKO SIKU ULIMWENGU UTAWAFUNZA!

    SIE WENYE WATOTO TUANZE SASA KUWALEA WATOTO WETU KWENYE MAADILI KAMA TULIKUWA HATUFANYI HIVYO, TUWALEE WATOTO WETU WAMHESHIMU KILA APITEAYE MBELE YA MACHO YAKE BILA KUJALI KAMA NI MWANAMKE AU MWANAUME, MKUBWA AU MDOGO ILI WAKIWA WAKUBWA WAWE WATU NA SI VIATU!

    ReplyDelete
  48. calm down bro punguza hasira maisha yenyewe mafupi haya unajikunjisha sura huh

    ReplyDelete
  49. Michuzi mimi niliogopa kidogo niliposoma kwamba Jovita katumiwa mesiji zaidi ya 600 na ilinibidi niende kuangalia meseji zilizomo chini ya tangazo lake na niliona meseji zilizozopo hazifiki 200 na hazikuwa na maneno mabaya mengi, watu wengi walimshauri na wengine walionyesha waswasi wao juu yake. Nahisi hizo meseji 600 alitumiwa kupitia email yake. Nadhani inabidi huyu dada na wanawake wengine wajifunze kwamba wanaotangaziwa wengi wao wanaona kwamba mke/mume mwema ni vigumu kumpata kwa matangazo ya namna hii. Mara nyingi watu wamezoea kuona matangazo ya namna hii kwa ajili ya kutafuta uhusiano wa muda mfupi. Nawashauri kwamba watafute wachumba nje blog kwani humu wanaweza kuangukia kwa vihiyo wa sifa na kujuta baade

    ReplyDelete
  50. kaka michuzi
    nampa pole sana huyo binti kwa ya liyomkuta kusema kweli wabongo siwaelewi hasa tuna asili gani kamwe hatunasifa ya kupendana kusifiana wala kutakiana heri sawa na mfano ulio utoa wa senene,ushauri wangu kunamsemo unasema uhuru bila mipaka ni uwendawazimu so you know what I mean cheki maoni yauchafuzi wa hali yahewa hayana haja ya kuwepo,mwenye fustration zake akatafute suluhisho kivyake.asante

    ReplyDelete
  51. kaka michu mimi sina usemi kwani wewe hunifanyia roho mbaya hutaki kuziweka ukweli wangu kisa nabeba boxi sawa nawaachia hao watu wa moshi na pia nakuomba waeleze kuwa hili block la mr michu ni la sani la pimbi na kadala sasa dada asikasirike amuulize manka mume kapata wapi hata hivyo wabongo tunapenda utani na kama anataka bwana huo ndio unyango wa wabongo sasa kapasi kesho anakuja bwana usilie mwanangu huo ndio ukubwa nyamaza kulia mwanangu ushapita mtihani wa mila na desturi wellcome bongo.

    ReplyDelete
  52. Kusema ukweli baadhi ya matukio na comments za watu kwenye blog hii - sio ishu hii ya dada Jovi, Manka, Chibiliti tu - imenifanya nianze 'kutengeneza' theory kwanini Wabongo na Waafrika kwa ujumla tuna kasumba kama hizi.

    Binafsi, nadhani malezi yetu nyumbani na siasa zetu (kabla ya Mzee Rukhsa) zinachangia kwa kiasi kikubwa ku-shape mindsets zetu. Wachache hubadilika baada ya kuwa exposed to other cultures kwa njia yeyote ile; kwa kusoma vitabu, kusafiri, kupata elimu ya juu n.k.

    Simaanishi kila mtu aliyesoma atakuwa open-minded. Ila kuwa tolerant panapotokea tofauti za mawazo na kukubali hizo tofauti na kuendelea na maisha kama kawaida ndio jambo muhimu hapa. Siasa za Ujamaa zimetuathiri kwa kiasi kikubwa sana. Conformity kwenye jamii yetu ndio way of life. Ukitoka nje ya mstari utakiona cha mtema kuni - umbeya, usengenyaji, matusi na mengine kama hayo. Hii yote ni kujaribu kumweka mtu 'anayekiuka' maadili yetu kwenye mstari. Na tunapata ahueni pale mtu huyo anaporudi kundini na kuwa mmoja wetu.

    Sasa, hii inatupofusha hata pale mtu anapofanya mambo mazuri, lakini yaliyo nje ya maadili yetu. Kama hutaki kuangalia Watanzania, basi fuatilia watu kutoka kwenye nchi zilizokuwa zinafuata Communisism.

    Aaaah, nimechoka ku-type! Ijumaa leo halafu najua haitaleta maendeleo yoyote kwenye jamii yetu. Inaboa sometimes! Aaaaaghhrrr!

    ReplyDelete
  53. we anon wa Friday, April 4, 2008 10:17:00 PM EAT,kwani ni formula kama ameandikiwa email 654 zote ziwe zimetoka kwa watu 654? mtu mmoja anaweza akakuandikia hata emails 20 za matusi kwa muda wa moja. Pole Jovi.

    Manka

    ReplyDelete
  54. Mie ningependa kukuoa, ila dini kikwazo. Lazima ukubali ni bahati mbaya ya huo muda wa mwaka uliyotuma hiyo barua; wengi watakuwa walidhani ni "April Fools Day-Joke" (watu watakuwa walishindwa kuamini mtoto mzuri, msomi na mchapakazi kushindwa kupata mchumba). Piga moyo konde, na Inshallah utampata umpendaye uishi naye milele. Ushauri: Jitahidi kukaa mbali na hao washirikina dada Jovi.
    Kwa mapenzi! Amani...

    ReplyDelete
  55. Mimi nilichogundua so far kuna vibaka wengi humu wasomi wachache.
    Hakuna ubaya wowote wa Bibie kujitafutia mchumba. Na hata akimtaka Jesus awe wake kwani taabu iko wapi? Na bibie usilie kubadilisha watu wa mwaka 47 inataka moyo.

    ReplyDelete
  56. kosa ni la huyo dada kuweka mail yake na kama alikuwa misupu uwe mshenga basi mail zingepitia kwako na wewe ndio uwape detail zake sasa kaanika kila kitu kwa machizi lazima wavunje vunje si wameona sio deal kwao maana alikuwa ana mtaka mashaka then mara amtaki so ni kigugu mizi tu

    ReplyDelete
  57. Huna lolote! Aliekupa kutwanga mwambie akakupe na chungio...! Eti analia lol, sasa kilichokuliza nini matusi au kukosa mchumba hapa michuzi.blogspot au wa mlilia Mashaka i.e. the man of your dream!

    We ukiona vipi mwambie Michuzi akuowe akustiri, michuzi anaruhusiwa kuongeza mke wa pili au sio Misupuzzz?! Uskonde dada, "Aso mtu ana mungu, utapata lako fungu" Lakini ndo ushalikoroga hilo lazima ulinywe!

    Bablii

    ReplyDelete
  58. Wewe mwenyewe Michuzi unachangia hali hiyo na ndio sababu kubwa watu hawatumi picha za hapa. Wewe unacontrol na hii blog yako, sasa inakuwaje hata jumbe za kumdhalilisha mtu huwa unaziweka hapa? Na za kumtusi Jovinata zilikuwa nyingi tu achilia mbali wale waliomwandikia binafsi. Kwa hiyo na wewe mwenyewe badala ya kutaka kuwalaumu walimtumia emails Jovinata za kumtukana na wewe inabidi uangalie wajibu wako.

    Hakuna cha ajabu yoyote mwanamke katika mwaka 2008 kujua anataka mume wake awe na kisomo cha level ipi na pia kutangaza kwenye mtandao nia ya kumpata mchumba hatimaye mume. Kuna washamba wanafikiri bado tuko mwaka 47. Watu wana mawazo finyu sana na wengine husubiri mahali pa kutolea matusi yao.

    Jovina ulichofanya hakina ajabu yoyote na wala si cha aibu. Mwanamke kamam hujui unataka mume mwenye sifa zipi katika mwaka 2008, basi kuna walakini fulani kichwani mwako. Usikate tamaa dada mchumba utapata tu wewe ni bomba ile mbaya, msomi na una kazi ya maana. Kuna wanaume wa Kitanzania pia wanatafuta wake wenye sifa kama yako kwa hiyo nakutaki kila heri. Kama ukifanikiwa kupata mume mtandaoni, watakaowauliza mlifahamiana vipi na mkiwaambia mlifahamiana mtandaoni hakuna cha ajabu na hata watoto wenu mkijaliwa kuwapata mkiwaeleza hivyo hakuna cha ajabu. Watu wenye mawazo finyu na uwezo mdogo wa kufikiri wasikukoseshe usingizi.

    ReplyDelete
  59. POLE KWA MASWAHIBU..HATUITAJI USHAHIDI KWAMBA E-MAIL ZAIDI YA 300 ZA "..WANAINCHI WA WATANZANIA.."..WACHNGIAJI.."..ZINA MATUSI MATUPU..LABDA KUNAUKWELI...KUMRADHI JAMANI.."..MUONJA TAMU ..HUONJA CHUNGU.." CHAGUA TAMU KATI YA HIZO E-MAIL BIBIE...

    ReplyDelete
  60. michuzi usiti-bore bwana...una uhakika gani kama huyo demu kapelekewa mails za matusi? au mlisoma pamoja hizo mails?
    kama katumiwa kwenye inbox yake, haikuwa na haja wewe kuja kukoromea wadau humu.
    yeye alipoweka msg yake alitegemea watu wamsifu tu??

    mie namuona mzushi tu, anasema analia anatafuta "sympathy votes" kama mrs clinton. tushashtuka zamaniiiii.

    ReplyDelete
  61. Chema chajiuza, Kibaya chajitembeza. Mtume Muhammad SAW alisema pale tutakapokaribia na kiama wanawake watakuwa wanajitembeza na kujiuza.Watu eti wanataka kuiga ya nchi za wazungu! Ufirauni na ubaradhuli ndio umejaa huku. Mtanzania jivunie mila na tamaduni zako.

    ReplyDelete
  62. michuzi,nakupongeza kwa maneno yako, watu wengi wana matatizo sana na hawapendi maendeloo ya watu wengine, bila sababu yoyote, mimi ni mwana dada from texas, ninaelewa sitution a liyonayo dada jovina, internet ni kitu kigeni kwa watanzania wengi ndio maana tuna fanya uchunguzi kuwaelewesha watu umuhimu wa internet, watu walioko kwenye nchi zilizoendelea wanajua kuwa kutukana na ubize na maisha kuna kuwa kugumu ndiomaana wanatumia sana internet to meet their loved ones, huyu dada ana hitaji msaada, kama mtu ahitaji mke akae kimya, na kama huna elimu, go to school, usitake ku toa comment zisizo na maana kwa sababu una ji feel inferior mbele ya huyu dada, dada kasoma kasoma tu, acheni roho mbaya, you go girl!!!!!
    Mdau H-Town(TX) mwanadada tena msomi

    ReplyDelete
  63. Kelele za mlango zisikushughulishe binti mrembo,
    Vijineno vidogo vidogo inabidi tuvimege , tuvichakue na kuvimeza ila vikitukwama kooni inabidi tucheuwe, na tukisha cheuwa ndio hapo sasa harufu inapoanza kukera wenzetu. Hivyo tujitahidi kuomba radhi baada ya kuchafua hali ya hewa kwa wenzetu ili amani na upendo uendelee.

    Mi nilivoona tu katoto chenyewe kazuri kazuri hako nilijua katauliwa tu kwa vile vizuri havidumu.
    Kipi kizuri kisicho ila?
    Ni hayo tu:-)

    KAMANDA MANYoTA

    ReplyDelete
  64. kwani hiyo ajabu? sie waukae tushazoea hata kura kwenye uchaguzi zinaharibika itakuwa hizo email? mbona kitu cha kawaida tu dada jovi elewa ulikuwa unatafuta ustaa sasa umeupata na hayo ndio malipo ya ustaa, na kwa taarifa hao waliokutumia hizo meseji watakuwa wasichana wenzio tu, sisi watoto wa kiumeni hatna muda wa kupoteza kila siku tunatongoza wazuri kuliko wewe mie kwa upande wangu nasema ktk emails hizo hakuna hata moja mwanaume wa kibongo labda wabeba box

    ReplyDelete
  65. kaka yangu michuzi unajua kwa Tanzania hatuna utamaduni ya kwamba mwanamke atafute mume wa kuoa mmm haipo ndiyo maana matusi yanakuwepo madai kuwa tunaiga wazungu haipo kabisa hata mi ni mwanamke huwa najisikia vibaya sana mwanamke anapojitokeza anatafuta mchumba very bad mume wa mtu ni Mungu mwenyewe anapanga iweje wewe unatafuta mume kwa michuzi kwani we upo kwaajili hiyo nakushauri futi hii mambo yakutafuta wachumba watachafuliwa sana hali ya hewa. pole dada kwakukosa amani nakushauri muombe sana Mungu wako atakupa kila kitu unachokitaka ukiwa na IMANI.

    ReplyDelete
  66. Unajua unapovua nguo zako hadharani halafu ukawauliza watu ni nani ameipenda chupi yangu? hayo ndio matokeo yake watu wameifanya hii blogu kama babu yao hawajui kama kuna masuala ya binafsi ambayo hayausiani kabisa sasa huyu dada Jov alijisahau akadhani kwamba kila mtu ana fikra kama ilivyo kwenye kichwa chake.
    Kila mtu ana uhuru wa kupenda ,kuchagua maisha ayatakayo lakini kuna namna,wakati na jinsi ya kufanya yote hayo kwa wakati.Namshauri Jov atafute mshauri nasaha ili ampe shule kutokana na nia yake nadhani atafanikiwa.

    ReplyDelete
  67. Sioni sababu za kuwalaumu wachangiaji kwani wamechangia kutokana na uhuru na uwezo wao wa kufikiri.

    Lakini ni lazima tujiulize kwanini watu wengi wamemponda sana Jovinita?

    Ni kwa sababu hakuwa anatafuta mume (Husband) bali anatafuta just a man. Kwa mwendo huo basi hawezi hata kupata NYUMBA (HOME) bali ataishia kupata MAKAZI (HOUSE). Katu hataweza kupata LOVE (MAPENZI) bali ataishia kupata RELATION (MAHUSIANO).

    Baada ya kusoma messages za watu wote jiulize wapi umekosea au nini ulikuwa unakitafuta.

    ReplyDelete
  68. UKIONA MKONO WAKO UNAKIMBILIA KUANDIKA MATUSI KUKOMENT CHOCHOTE HASA UKIONA PICHA YA MWANAMKE, AU MANENO YA MWANAMKE, BASI UJUE WEWE NI MGONJWA. NA UGONJWA WAKO NI KUPENDA KU-ABUSE WATU HASA WANAWAKE KWA SABABU UNAWAONA WANYONGE. ABUSERS TAFUTENI TIBA, UGINJWA MBAYA SANA HUO NA UNAWEZA KUENDELEA NAO HATA UKIWA NA FAMILIA YAKO.

    NYIE WOTE MLIOMTUKANA DADA WA WATU KWA KISINGIZIO CHOCHOTE NI ABUSERS HIVYO VISINGIZIO VINATUMIWA SANA NA ABUSERS KUJISTIFY THEIR ABUSIVE BEHAVIOURS HAIJILISHI UNAISHI WAPI TAFUTENI MSAADA KWA MAKANSELA AU KWA VIONGOZI WA DINI LABDA MNAWEZA PONA, ILA MNATISHA MWANAWANE!

    ReplyDelete
  69. Mambo VP wadau?
    Dada anatafuta mchumba, kajibiwazaidi ya email 650.
    Anabahati sana, wengine hawajibiwi hata moja, la msingi kapata alichoomba anachopaswa kufanya ni kuchambua apate mchumba anayemtaka humo kati ya watu 650 walomwasiliana naye. Kama amekosa arudi tena kuomba humu au apanue wigo kwa kwenda sehemu nyingine. Kimsingi hana sababu ya kulalama kwani dada si unajua kupika? USHACHAMBUA MCHELE? unapokwenda sokoni kununua kilo ya mchele sikuzote mawe huwemo, si ajabu, chambua mama.

    ReplyDelete
  70. HII YAKO KAKA MICHU.
    USILETE MAMBO YA ENZI ZA CHAMA KIMOJA HUMU INGAWA BLOGU YAKO.
    UKIOMBA MAONI HUMU KUBALI NA USIYOYATAKA KUYASIKIA, MAAN SISI NI TAIFA MOJA< MAKABILA MBALIMBALI, DINI NA TAMADUNI TOFAUTI. MITIZAMO PIA NI TOFAUTI. HIVI NIAMBIE MZAZI WA KAWAIDA WA MTOTO WA KIKE BONGO AKIONA MWANAE ANATAFUTA MCHUMBA KWENYE MTANDAO ATAMWELEWAJE?
    CHUKULIA HALI HALISI, TUSIZUGE KUWA TUPO MTONI, OOOH UKISASA, MUULIZE BABA KAUNDIME ATAKWAMBIA KITAKACHOMPATA BINTI YAKE AKIANIKA MASUALA HAYA KWENYE INTERNET.

    ReplyDelete
  71. Mimi nampinga dada Samira kwamba watu waliomtusi Jovi ni watu tulioko Ulaya. Hapa Ulaya hivi ni vitu vya kawaida kabisa kutafuta wachumba kwenye net ila Bongo ni kitu kigeni sana. Kwa hiyo mimi naamini asilimia kubwa ya matusi imetoka kwa WALA VUMBI! kwa sababu kubwa zifuatazo, either shule ndogo au exposure ndogo. Ukitaka kujua ukweli angalia hata wanasiasa wetu wanavyopakana matope, unategemea kitu tofauti kwa wananchi wa kawaida tena ambao shule na exposure ni tatizo kubwa kwao? Dada Samira please don't conclude things without proper analysis!

    ReplyDelete
  72. Pole sana mdogo wangu. Hao wote ni wale wasiopenda maendeleo ya wenzao. Sio kwa nini mtu akutukane, kama hafai hapasi kukuandika. Mie nilikutana na mume wangu miaka 1999 iliyopita kwenye internet, kipindi hicho Tanzania mambo haya yalikuwa bado. Nilitoa sifa za mume niliyekuwa namtaka na mungu akanijalia nikampata mume na hadi leo tunaishi raha na mstarehe na tuna watoto wawili.

    Hivyo usikate tamaa, mungu atakujalia tu.

    Siwa
    Arusha

    ReplyDelete
  73. Wewe Ngwengwe acha hizo ni mzazi gani anayetaka hii biashara ya nyanya nyumbani kwake? Ni mzazi gani anayefurahia binti yake kuganda nyumbani miaka yoote hiyo bila hata dalili ya kuletwa posa kwao.

    Nakumbuka zamani nilipokuwa bado mdogo bibi yangu mmoja alikuwa analalamika kuwa baba yao anawasakama kwanini mpaka wana umri huo (miaka 20+) na hawajapata waume wanakasoro gani. Basi huyo bibi yangu alivyomjeuri alikuwa anamwambia baba yake kama wenyewe hawaji je sie tukawashike mashati au tusimame barabarani tutangaze tunatafuta mchumba? That was 1980S sasa hivi msichana pia anaulizwa hivi wewe una matatizo gani hupati mchumba, hata humu kwenye blogu wameuliza, sasa badala ya huyu dada kusimama barabarani au kuwashika mashati ameoamua kuomba kiistarabu tu. Na kwa mzazi wa kiislam si ajabu binti anaruhusiwa kutafuta mchumba, haina noma wala nini. Ni nyie tu na visingizio vyenu vya kutukania watu. Hata mie nilimshika mtu shati ama sivyo na vidato vyangu vyoote hivi ningekuwa kama da Jo' nasubiri kufuatwa. Jo ukimpata mtu karibu yako unaona anakufaa mshike shati hata huyo Mashaka ukimtaka wewe mshike shati tuu. Mwenye kisu kikali ndiye atakayekula nyama. Hata hawa wanaomtukana Jo wengi wao wameshika sketi au shati ndio wakaoa haikuwa kirahisi (wamepora wachumba za watu). Kwani si rahisi kumpata mtu ambaye hayuko katika mahusiano kabisa yaani yuko yuko tu hana girlfriend wala boyfriend, shika shati mama livutie kwako jinyenyekeze upate mume!

    ReplyDelete
  74. haters haters haters .......Jovi I wish u all the best.

    Ila bi. Samira kunradhi si matusi acha kutupaka matope sisi wa Ulaya na kututupia hili chachu la kukosa uungwana tena tafadhali sana bi dada ,na mabox yetu tunayobeba sisi huku kuna Dating Agencies kila kona yaani its a proffesion ya watu hiyo na its a normal day to day service watu wanatafuta wachumba magazetini, online redioni ,kwenye TV yaani ni vitu vya kawaida kabisa havishitui wala havitukondeshi so hatuna ulimbukeni wa kiasi cha kumtukana mtu akitafuta uchumba hapa kwa bwana Michuu kwetu ni kitu cha kawaidaa saaaaaaaana tena innit ! Sie huku tumeshayaona ya Musa na Firauni hatuyashangai so ukitaka kushika wadau mashati washike wa huku huko bongoland tafadhali bi dada !!
    Mimi naona nikutumie invitation letter uje huko ujionee, tena mwambie hata Jovi akitaka aje kujiandikisha Dating Agency huku atapata kijana aachane na Wabongo nuksi na vikoroshooo.

    ReplyDelete
  75. wewe uliyejiita Mdau Samira shika adabu yako tena tuheshimiane,hivi umetumia Criteria gani kusema asilimia 90 ya watanzania wanaamini waganga wa kienyeji?umefanya lini hiyo research?au unaongea tu bila data?kwanza inaonyesha wewe ndio mshirikina namba moja kwahiyo unadhani kila mtu mshirikina,au ni mke wa mganga wewe huna akili,kumbuka kuna uhuru wa maoni na mitazamo tofauti.

    ReplyDelete
  76. SAMIRA!! SAMIRA!!! SAMIRA???!! MIMI SIKUTUSI WEWE KWA HAYO MATUSI YAKO ULIYOANDIKA HAPO, ILA NAKWAMBIA KUWA SIONI TOFAUTII KABISAAAAAA KATI YAKO WEWE NA HAO WALIOANDIKA EMAIL 650 ZA MATUSI. WEWE UMEPATA WAPI HIZO HISIA KAMA WALIOANDIKA HIZO EMAIL WANAKAA NJE YA TANZANIA?? YAANI WEWE NDIYO UMEJUA KWELI KUTUKANA WATU HUMU KWENYE BLOG, NINA WASIWASI NA HIZO EMAIL 650 ZA MATUSI LAZIMA NA WEWE UNAZO ZAKO HUMO, NA KWA VILE KIU YAKO YA KUTUKANA HAIJAKWISHA UKAAMUA KULETA MATUSI YAKO TENA HAPA, UNAPOSEMA ASILIMIA 90 YA WATANZANIA INAAMINI UCHAWI INA MAANA NA FAMILY YAKO PIA IMO HUMO??? WEEE MTOTO EHEE MBONA UNA FIKIRA POTOFU HIVYO?? JIFUNZE ADABU WEEE KUNA WAKUBWA ZAKO HUMU. POLE SANA JOVI MUNGU ATAKUSAIDIA,
    NI MIMI MCHA MUNGU.

    ReplyDelete
  77. duh ishakua tabuuu "wantanzania" halafu misupu kama utafuta mchapaji au seketari huyo samira ameonyesha ufundi kwenye kuandika sijui imemchukua muda gani hio miparagrafu?alioyandika kuhusu wa tukanaji wako nchi za uk, canada na usa ni facts au nayeye anaongea tu mradi asikike?

    ReplyDelete
  78. Kweli kabisa anon a mar 4, 7:55. Mtu agombe humuuuu kwenye kijiwe kisha atoke aende kwenye email ya Jovi akamwage upupuuuu ana maana gani? kama si machungu, hapo kaona hawezi kumpata ndo maana akaamua amwage upupu ili umuwashe Jovi KISEBUSEBU NA KIROHO PAPO. sasa ndugu zagu kuweni waungwana
    maneno matamu humtoa nyoka pangoni utakuta hata huyo qeen angepunguza vigezo, msitishwe na vigezo nyie jitoseni tu na kigezo cha nyama ya ulimi uone kama demu hajalegeza masharti hapo.

    ReplyDelete
  79. Mheshimiwa Michuzi, Mimi ningependa kusemea hali hii ya comments katika blog yako! kuna mambo mengi yanaandikwa kati blog hii. Mimi binafsi nachukulia blog hii kama chombo fulani cha kuelimishana, kufahamiana, kupashana habari na kuburudishana kwa habari mbalimbali za kufurahisha. yaani ninamaana ya habari zenye "Light touch"
    Kwahiyo mii ninaposoma habari katika blog hii na kuwa na mitazamo mbalimbali na tafsiri mbalimbali, kulingana na hayo niliyoyaeleza hapo juu.
    Habari za kama dada Jovi na chibiriti, mara nyingi huwa nazichukulia kama habari zinazotaka kutoa burudani ya aina fulani katika blog.
    Mfano suala la kutafuta mchumba katika blog hii ya Michuzi, siwezi kulipa kipa umbele kabisa kwani naona kuwa ni jambo ambalo linaweza kufanikiwa ndio lakini katika upeo usio kuwa wa mbali. Nina maana kuwa, kwetu watanzania, kitu hiki cha kutafuta wachumba katika blog bado hakijawa cha kawaida sana kwani watanzania, japo utandawazi unatuaffect, bado tunafuata sana mila na tamaduni zetu, hasa zinazohusu mambo ya uchumba. Reactions ambazo zimekuja kwa Dada Jovi, sio reactions ambazo zinapaswa kumuumiza sana Jovi, bali anapaswa kujua kuwa reactions za wengi zimekuja zikichukulia kuwa suala zima la Jovi ni suala lililoletwa kama "Light touch".

    Reaction nyingine, kama hii mimi ninayotaka kusemea ni "hii ya farrasi ya Generalization" yaani kujumuisha na kuwakashfu watanzania wote kwa suala hili la Jovita. Sio jambo la usomi vilevile kuwona watanzania wote ni bure, hawajaelimika, eti sababu tu ya reaction kwa Jovita. Hii inaonyesha kuwa hata anayereact hivi vilevile hajaelimika.

    Tuangalie reactions zetu, na tuepuke kuwakashfi watanzania wote kwa jambo linalohuwasu watu wachache tu!

    ReplyDelete
  80. Aniny hapo juu April 05, 2008 3:00 PM,
    Nakubaliana nawe kama huyo mwanamke ni kipori au hajiheshimu vizuri anaweza doda home, kwa kuwa sisi wanaume hupenda tunapokuja mtaani kwenu ijulikane kuwa wewe ni wangu na wangu tu, ikishakuwa, James, John, Hamis, Issa, nakadhalika wamepita ujue tunafanya kuuweka kiaina tu, kupunguza uzito wa bunduki. Halafu tunahamisha kiwanja tunapopata sehemu ya kujisitiri maisha.

    Sasa kama demu kicheche atakaa home, akiwa matawi ya juu kwa kila mtu pia atakaa home, kwani kila atakayemfuata atataka awe wa namna fulani anayotaka yeye mwanamke, halafu anaishia kutompata yeyote kwa kuwa wote anaona wanakasoro.

    Akishindwa kujichanganya napo ni shida kwa kuwa watu watashindwa kumtokea, mkali kama mbogo, huyo aficha uchi, hatozaa.

    La msingi, awe na msimamo, achague katika wanaomfuata ni yupi anampenda na hii si hoja sana bali yupi mwenye nia naye ya kweli. Akiambatana naye safi hawezi mtupa.
    Tatizo wanawake hasa wa kibongo, macho juu, tamaa mbele, kujidai kwingi, halafu majirani zao wanawadharau. Hata ukiwa mtoni, wanawake wa kibongo wanaongoza kujipeleka kwa wapopo na jamaa wengine wasowajua kabisa hata tabia zao, matokeo wabongo tunawatazama tu wakisha temwa huko. Na wapopo wankuja kuwaponda kwa wabongo, kuwa mademu wetu vicheche macho juu, maji mara moja. Hivi unadhani ikishakuwa hivyo, sisi tutaomba uchumba hapo? Au tutajisaidia tu siku mojamoja tukiwa na shida tu.

    Wanawake wa kibongo anzeni kuweka malengo kwa watu mnaohusiana nao na zaidi msikimbilie sura na sifa zingine zisizo za msingi na kudharau wanaume mnaotoka nao mtaa mmoja au kijijini kwenu.

    ReplyDelete
  81. Anony April 05, 2008 3:00 PM,
    bibi yako alikuwa na akili sana na mwenye kujiheshimu, ndo sababu hakutaka kujianika, kujitangaza kutafuta mchumba, halafu kipindi chao
    ilikuwa mpaka mtu aje home kuleta posa. Sasa mambo tofauti, mnatongozana popote halafu mnapelekana home, si mpaka waje wakufuate. Mwanamke anajitangaza kwa tabia yake na uzuri wake, huko shule, kazini, nakadhalika.

    Hii kesi ya kina Jovi ni tofauti kabisa na ya bibi yako. Hasa ukizingatia time, mazingira na exposure.

    ReplyDelete
  82. MICHUZI MIE NAMTAKA MASHAKA PEKE YAKE!!!!!KM UNA CONTACT ZAKE TUTOLEE SIE WADADA TUJARIBU BAHATI ZETU...

    SAA NYENGINE NATAMANI WANAUME WOTE WA KITANZANIA WANGEKUWA KM MASHAKA!!!!!!

    INGEKUWA TU NI KIJANA WA KAWAIDA NDIO KAFIKIA ALIPO MASHAKA BASI SI MASHAUZIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII!MBWEMBWE KIBAO ILA MUONENI MASHAKA..KILA SIKU ANAKUJA NA WAZO LA JINSI YA KUSAIDIA WATZ WENZAKE...JAMANI MASHAKA MIE NIKO TAYARI KUWA MKEO!!!KM UNA MKE BASI NIWE MKE WA PILI!!!!KM UNAO WAWILI TENA MNH!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!BASI NIWE HT MPANGUSA VIATU!LOL!,HOUSEMAID..NK..ON SERIOUS NOTE MASHAKA JAMANI I LOVE YOUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU!HOLLA AT ME!SILALI NAKONDA JUU YAKO...JUZI ETI NIMEOTA UNANINAHIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII...UKWELI VILE,

    NEY

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...