sehemu za uani (juu) na barazani pa iliyokuwa klabu ya relwe gerezani inavyoonekana leo. itapokamilika na kufunguliwa itajulikana kama city garden club mmiliki akiwa mdau yule yule wa paradise beach resort ya bagtamoyo, city garden na dar es salaam international conference centre na pia city garden restaurant ambayo zamani ni cosy cafe usoni pa mbowe hotel ama billicanas kwa sasa


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 27, 2008

    Sasa hivyo vijisenti vya kujenga majumba hayo ya anasa wanayapatia kutoka wapi?manaake mie mnyonge mtanzania hata tofali mmoja naona vigumu kujipatia!!!

    ReplyDelete
  2. akumbuka enzi za Stanley Mabesi "Ninja" na kina Charles Libondo wa Zambia wanapigana ndondi Gerezani

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 28, 2008

    SASA BWANA MICHUZI NAOMBA UIFIKISHE HII MBELE KWA MBELE KWA WAHUSIKA WAKUU, KWA NINI HIZI SEHEMU MUHIMU ZA NCHI YETU WATU WANAZIKARABATI NA KUZIPA MAJINA YA KIINGEREZA???. KUTOKA RELWE GEREZANI MPAKA CITY GARDEN WAPI NA WAPI, HATA WAZUNGU WATATUSHANGAA JAMANI, HUWEZI KUBUNI JINA KAMA VILE, NDEVU ZA MBUZI, AU, STAREHE JELA, KWA SABABU NI GEREZANI. HEBU WAAMBIE HAO WAKUJA WAACHE USHAMBA.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 28, 2008

    KWA KIFUPI THE OLD RAILWAY GEREZANI CLUB, PALE KWA MZEE WA KIDEVU (SALVADOR), KISA CHA MPEMBA CHA KUTWANGA NA KUPEPETA, KISIKI CHA MPINGO NA KIPEPEO, NYUMBANI KWA SINGA SINGA CLUB........IS NOW NO MORE!!! EH MUNGU TUSAIDIE WANYONGE MAANA NEXT NI LEADERS CLUB.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 28, 2008

    wanapata wapi pesa. benki zinafanya nini?? acha ushamba kama kwenu hakuna cha kuwekea rehani usifikiri kila mtu mwizi wa pesa za serikali. watu wanajua kucheza na mikopo ya benki bwana achane majungu ulizeni mfafanuliwe acheni hizooooooooooooo

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 30, 2008

    Hivi hapo si ndio mechi za netball zilikuwa zinafanyika au nimeconfuse!du Kasheshe

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 01, 2008

    Jamani hawa wasomali wa city garden na holiday inn resort wametubadilishia kiwanja chetu cha netball na sasa wameweka bwawa la kuogelea. kama Serikali yetu ingekuwa macho hasa wizara ya habari, utamaduni na michezo ingewapa masharti hawa wawekezaji, wawekeze lakini wasiubadili uwanja huu wa mpira wa pete, ila wameachiwa wafanye wanavyotaka. sasa viwanja vya netball vinapungua kweli tutafika?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...