benki inayotembea ya crdb ikidunda kama kawa leo viwanja vya maonesho vya sabasaba. kuna mdau katuletea ufafanuzi kuhusu habari kwamba leo ni sikukuu ya mabenki na kwamba eti benki zitafungwa. soma kwa makini hapo chini

Kaka misupu,

naomba uwaweke watu sawa kuhusiana na hiyo bank holiday.
ukweli ni kwamba walengwa wa hiyo siku ni benki kuu kwa sababu leo ni tarehe yao ya mwanzo wa mwaka wao. Hivyo basi toka jana wako bize na kufunga mahesabu yao ya mwaka.

Kinachotokea kwenye mabenki mengine ni kwamba shughuli ambazo zina uhusiano wa moja kwa moja na bank kuu ndizo hazitokwepo ila mabenki hayatafungwa na shughuli nyingine zitaendelea kama kawa, kasoro Bank kuu tu ndio hakuna shughuli ya kibank itakayoendelea leo

Mdau mtaalamu wa vijisenti

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2008

    SI KWELI MTAALAM WA VIJISENTI.LEO NIMEKWENDA STANBIC NA HUDUMA KWA WATEJA ILIKUWA HAKUNA,HUO NDIO UKWELI.ULIZA MTU YEYOTE.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 01, 2008

    crdb hongereni kwa bank inayotembea. michuzi umebania mail yangu kuirusha hewanio poa nijibu basi wewe swali langu,
    sweet

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 01, 2008

    hii bank holiday CRDB Bank jikusanyeni upya muwape Wazalendo card zao kama ni hivyo basi ATM na hilo ligari la nini ni Show Off tuuu au maana hatuwaelewi kabisa Mr Kimei tunaomba ufafanuzi kwa hili tumechoka njoo kesho na kupanga foleni tujue moja bado tuko Zama zile za Mawe!!!!!!!

    Mtanzania aliyechoshwa na Nchi hiii maana watu wanaangalia kwenye 10% kam hilo ligari kuna mtu anacheka sasa

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 02, 2008

    Asante mtaaluma wa Vijisent kwani maalezo yako ni kamilifu na sahihi...
    Eti mahesabu ya nafungwa siku ya Mwaka mpya?????!!!!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 02, 2008

    Hakuna lolote.
    Benk zote zilifungwa na msela wangu anayefanya benki alikuwa maeneo ya saba saba akienjoy HOLIDAY !!!
    Nanilosoma waraka waliotoa BOT unasema ni HOLIDAY ya wafanyakazi wa BENKI.
    Labda ni mapumziko BAADA ya kufunga mahesabu na siyo WAKATI wanafunga mahesabu !!!
    Mbaya zaidi hawakutoa taarifa mapema !!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...