Michuzi,

Nadhani utaendelea kunikumbuka mimi mdau mwingine na mchangiaji mkubwa wa globu hii ya jamii, lakin sio hai saaaaaaaaana. Labda kama mgonjwa yupo ICU.


Leo naomba wadau wasome hilo tangazo halafu wachangie Kuna haja ya kuwa na X-ray kama mionzi ya jua inaunga mifupa.


Na huyu Bwana kwa nini technology hii asiwahusishe wadau wengine??


Mdau Vingunguti

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Hii ya kutibu "fractures" kwa mionzi ya jua ndio nimesikia leo.
    Inasikitisha kuona kuna watu wanataka kujipatia pesa kwa njia za udanganyifu.
    Kweli Jua ni muhimu katika machakato wa mfupa kuunga au kukua. Lakini kuna taratibu nyingine za msingi lazima zifanyike kabla ya hii "natural process" kuendelea.

    Itakuwa vizuri huyu Mhe. akatafutwa na kuulizwa jinsi matibabu yake yanavyofanya kazi.Inawezekana amegundua njia mbadala za matibabu ya mifupa.

    Mdau
    http://drfaustine.blogspot.com/

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 14, 2008

    Nafikiri mzee umesahau jambo dogo hapa.X-ray haitibu kitu.ni kipimo tu.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 14, 2008

    nadhani haijawahi kuwakuta nyie ya kukatwa mguu.....utafanya kila njia mguu wako usikatwe.....

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 15, 2008

    Jengo la Mahakama ya Kawe linaogopesha

    2008-07-14 18:38:10
    Na Robert Temalilwa,Kawe


    Mahakama ya Mwanzo Kawe ipo hatarini kuanguka kutokana na kujaa nyufa karibu katika jengo zima. Mbali ya Mahakama hiyo kuwa katika hali mbaya ambayo inaweza kusababisha madhara kwa wafanyakazi wa Mahakama hiyo na watu wanaofika hapo kwa ajili ya kupata huduma za kimahakama, pia choo nacho kimefurika, hivyo kusababisha harufu kali kwa wapita njia na watu wanaofika mahakamani hapo.

    Mmoja wa wafanyakazi wa Mahakama hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina, amesema jengo hilo lipo katika hali hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu.

    Amesema hivi sasa, suala hilo lipo katika ngazi za juu za uongozi kwani ni zaidi ya mwaka sasa wamekuwa wakiambiwa kuwa itajengwa.

    ``Ni suala ambalo linajulikana. Tangu tulipoambiwa kuwa ingeweza kujengwa, sasa ni mwaka. Lakini hakuna kinachoendelea hadi sasa.

    Tunafanya kazi humu ndani lakini kwa mashaka maana wakati wowote jengo hili linaweza kuanguka kama unavyoliona jengo lenyewe na kutuletea madhara,`` amesema mfanyakazi huyo.

    Mfanyakazi mwingine wa mahakama hiyo amesema licha ya jengo hilo kuwa katika hali mbaya, pia choo nacho hakifai kutumiwa kwani kimefurika na kinatoa harufu kali.

    ``Kwakweli inasikitisha sana kwa kuona waheshimiwa Mahakimu na wafanyakazi wengine kukumbana na mazingira magumu kama haya.

    Jengo bovu... sasa linaonekana wazi kuwa linaweza kuanguka wakati wowote na kuleta maafa makubwa,`` mfanyakazi mwingine wa mahakama hiyo ameongeza.

    Alipoulizwa juu ya suala hilo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Sophia Mwaipopo, amesema tayari taarifa zipo katika ngazi za juu za uongozi wao na wanaamini kuwa litashughulikiwa kama walivyowahi kuahidiwa mara kadhaa.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 15, 2008

    Mwanzo wa nukuu,

    "Kuna haja ya kuwa na X-ray kama mionzi ya jua inaunga mifupa."

    Ni sawa na kusema,

    "kuna haja gani ya kuwa na OPEC kama mionzi ya jua inaweza kuendesha gari"

    I. Kauli au maswali hayo yote mawili yana kasoro kubwa sana ya ama kutoelewa matumizi au faida ya kilichozoeleka (X-ray / OPEC) na pia mahusiano yake na kile kinachoonekana kigeni (Matumizi ya mionzi ya jua)!

    II. Pamoja na kwamba ni bayana kuwa Tiba asilia / Mbadala inakabiliwa na changamoto kibao, Mdau mwenzangu, pengine ni vema tukatoa pia changamoto kwa Serikali yetu na jamii kwa ujumla ni kwa kiwango gani tumetekeleza na kutimiza yaliyomo katika sheria ya Tz ya 2002 inayohusu Tiba ya Jadi na Tiba Mbadala na kuwawezesha wWataalamu hao itakiwavyo kuendeleza ujuzi na teknolojia walizonazo kabla ya kusukuma lawama tu upande mmoja!

    ReplyDelete
  6. KWA NIABA YA FAMILIA YA MZEE MUHAMEDI KUMBEMA BABA BAHATI/HASINA/MWANAISHA/JAMILA/KHAMISA/AMINA/ABOU/LATIFA ZA RAHMA WA HAPO VINGUNGUTI. NATANGAZA KULIUNGA MKONO HILO TANGAZONIKIWA KAMA DR PROF ING TUMAINI GEOFREY TEMU/LIAMPAWE . NATURAL INTELGENCIA NAD MORDERN PHILOSOPHER

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 15, 2008

    we mdau unaejiita tumaini lazima unaumwa akiri.hovyooooooooo!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...