Bro Michuzi habari ya vakesheni? natumaini unaenjoy. Ktk pitapita yangu kwenye mitaa ya Sao Paulo nikakutana na fulanazz ambayo nilikua na wasiwasi kuwa ni ile yako iliyotoweka, but jamaa aliyevaa alikua baunsa nikashindwa kumuuliza.

Hebu icheki kama yenyewe niifuatilie.

Mdau Brasil.

------------------------------------
dah! mdau wa brasil umenirusha roho kweli. maana kuiona tu moyo ukafanya paa! hapana. sio hiyo mdau. nashukuru kwa juhudi zako zinazofaa kuigwa. pia nimeguswa sana kwa ujasiri wako, maana jamaa angekung'aa unamfotoa sijui ukijieleza nini.... ooohhh ze funalazzzzz iz ze jamiii... iz not richebo bongo kwa michuzizzzz.. mbona ingekuwa kazi....
asante mdau, pumzika, sio hio. asante sana
jameni eee funalazzzz bado haijulikani ilipo. ishukuriwe huu ni mwezi mtukufu, la sivyo ningenanihiii mtu. na kwa taarifa tu ni kwamba nimeshachukua RB polisi natembea nayo. yaani nikimbamba nayo mtu ama zake ama zangu....nshasema hivyo, ohoooo...
-michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. kwako broo michuzi nimetembelea blog yako nikakuta ina vitu vingi sana kutoka home (habari) ila kabla sijaingia kwenye blog nilishtuka kuona tahadhari kuhusu matusi na lugha chafu nilihisi ni blog ya wahuni na watu wasiostaarabika.

    lakini nikamuacha broo wangu ndo aliingia kwanza na akanijulisha hii blog ni nzuri sana na kweli ni nzuri hasa kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya broo nakupongeza sana .

    kutoka norwich uk

    ReplyDelete
  2. jamaa kisha ifukizia ubani na usipokwenda kwa fundi akuweke miunnda kuna risk uanaweza kuanza kutupa nguo.Mungu akusaidie

    ReplyDelete
  3. hahaahahah,kaka michuzi huijui fulana yako hio kwenye picha huyo jamaa kaivaa ndio ilile yako kweli nakwambia fanya uchuguzi.hahahahaaa fulanazzzz.

    ReplyDelete
  4. Hello Bro Michuzi,
    pole ya kupotelewa na kavazi ukapendako!
    Lakini jaribu kumuuliza Mamusapu iseje ikawa kachangana kwenye kabati la watoto..aka...serengeti boys!

    Ujumbe wa leo:
    "A man who loves his woman openly is a man indeed."

    ReplyDelete
  5. michuzi inabidi ukawaone viongozi wa simba, wao ni wataalamu wa mavituzi. kajikuku katachinjwa na mambo yote yatakuwa salama.
    Watu waliingia dau kwenye hiyo t-shirt ukatoa nje sasa unaona tumepata hasara mara mbili.

    ReplyDelete
  6. You guys are funny. Hiyo t-shirt imekuwa kama The sisterhood of the traveling pants.

    Hebu peleka nyingine bagamoyo ikafukiziwe tena. Au ni kuku wengi wanahitajika kwa hilo zoezi? Tutachanga ili blog yetu isije ikapata kwikwi

    ReplyDelete
  7. Misupu..usiwaliskize.. hivyo viti vya njano viko tanzania tu.. lazima tusake sehemu za viti vya njano..

    ReplyDelete
  8. SASA WE MICHUZI UNAIKANA FULANAZ AU UNAJUA ILIPO NINI, TUAMBIANE BASI!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  9. AISEE NIMETOKA KUANGALIA MECHI YA SIMBA NA MTIBWA KWENYE KARAI YA MTAALAMU WANGU SIMBA AMELALA TENA BAO MOJA ILA MTAALAMU AMESEMA MATOKEO YANAWEZA KUBADILIKA NA KUWA 1-1. KAMA HII ITAKUWA KWELI MICHUZI NITAFUTE MTAALAMU AMEDAI KUMVIMBISHA MTU TUMBO NA MA-T-SHIRT KWAKE NI JAMBO DOGO.

    ReplyDelete
  10. Au ni fulana aliyotinga nayo Spika akimfafanulia mama Wangwe jambo? Yaweza kuwa ameipiga mkorogo umma usiitambue.

    ReplyDelete
  11. ni EDO ! nini huyo aliyevaa ?

    ReplyDelete
  12. annon 2.01pm
    i think ichi ni jamii ya chimpanzee ivi asa ukitegemea ni kule Brazil mapori mazito,,,teh teh teh

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...