wadau kunaradhi. hicho kilio si cha bure. ile ze fulanazzz ya globu ya jamii imetoweka. juzi nilikuwa nimeifua na kuianika uani na nguzo zingine.
nguo zoooote zipo ila funalazzzz sikuikuta. yeyote atayeiona naomba tafadhali sana sana sana tena sana anijulishe kupitia
ni muhimu. msidhanie mzaha wajameni....
hivi nilipo naelekea polisi kutoa taarifa na kuchukua RB. kama kuna mtu kachapa tutawekana ubaya.
pia naandaa zawadi nono kwa atyeiona
uwwwiiiiiii.....nafwa!
-michuzi
------------------------------------------------------------------
Pole sana DC wangu wa wilaya yetu ya nanii na balozi wa Zain. Mimi nimehuzunishwa sana na kitendo chakuihamisha/kuianua/kuichuchukua fulana ya Mkuu wa wilaya bila ruhusa yake.
Natangaza dau la dola mia ($100) kwa yoyote yule atakayemrudishia Mhe. DC na Ambassador fulana yake.Iwe ile ile fulana yetu ya globu yetu ya jamii.
Roho yangu imeumia sana Mh. DC, kwani inanikumbusha nilishawahi kuibiwa pamba zangu zote pale sinzakaribu na ilipokuwa ikikaa bendi ta Extra bongo na ni kwa karibu Mzee Mwaibula.
Jamaa wali time ndani ya myumba yanguuani, yaani siku hiyo mai wife alinifua zile pamba zangu kali na mpya, zililambwa zote, Bullshit, nyamafuuuz. Hawa jamaa wajinga sana.
Hivyo basi natangaza waziwazi zawadi ya dola 100 (mia moja) kwa yoyote atakaileta fulana yetu.wadau kazi kwenu.
Mdau Alex
0716 310346

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 37 mpaka sasa

  1. Michuzi hiyo fulana kuna mdau anaona kuwa haiendani na ubunge na ubalozi wako hivyo hajaiiba ila ameinyakua ili akusaidie kwa hiyo usisikitike bali furahi.

    Kwa wadhifa wako inabidi ubadilishe image - (kaunda suti, mjusi, bazee etc) lakini siyo fulana

    Kila lakheri

    Mdau middle east

    ReplyDelete
  2. Bora :) Kalikuwa kananiudhi mno hako kafulana kako :(. Ukikavaa ulikuwa unaonekana kama vile ndiyo kwanza umeshuka toka Namtumbo.

    ReplyDelete
  3. Dah, afadhali mana kelele ziishe, kila siku fulanaaz fulanaaz.
    Mpaka inabadilika rangi! yani kama ni mtu alishakukimbia.

    ReplyDelete
  4. Braza michu hiyo sio gia ya kuombea fulana au vizawadi vya Idd? poa umeeleweka mwanawane.Karibu K'koo tukupe zawadi ya vifulana vya China. lakini vyenyewe ukufua mara tatu kanabadilka rangi.


    Mangi K'koo

    ReplyDelete
  5. KILIO CHA MTU MZIMA NOMA???jamani mrudishieni kauganga kake??sasa sijui picha tutazionaje?maana wamechukua jicho???pole sana mchu!!ndio matatizo ya kuishi sehemu isio kuwa na uwakika wa kiulizi??ujoo uku mamtoni,achana na hao mafisadi????

    ReplyDelete
  6. Samson na nywele zake
    Michuzi na fulana yake
    Pole hasa wakati huu wa kukaribia Eid, isiporudishwa itakubidi upige rakaa mbili kufua wazi
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  7. Kumbe kweli ile fulanaz ina yale mambo yetu!!! nilijua siyo bure...

    ReplyDelete
  8. kweli BANGI MBAYA!!
    WEE MICHUZI UNATAKA WAOSHAVINYWA WASEME...HAYA SASA SUBIRI KIDOOOGO WAJE.LEO UNAO!!!

    ReplyDelete
  9. kweli BANGI MBAYA!!
    WEE MICHUZI UNATAKA WAOSHAVINYWA WASEME...HAYA SASA SUBIRI KIDOOOGO WAJE.LEO UNAO!!!

    ReplyDelete
  10. Pole sana kaka michuzi.Kwa Dar kuipata tena itakuwa Kazi.Jiji la akili sana.

    ReplyDelete
  11. Ahidi hutoniripoti Polisi na kisha nihakikishie hiyo zawadi (kiasi gani) kisha tutawekana sawa. Kwa sasa hivi iko maeneo ya Gerezani na galoni la petroli na kiberiti viko tayari...

    ReplyDelete
  12. Michuzi, mganga wako alikwambia ikipotea basi mazali yataisha?
    Usiogope, imeshafanya kazi..upo juu. Mganga kaichukua ampe mwingine

    ReplyDelete
  13. MISHUZIIIIIIIIIIIIIIII HAHAHAHHA ITAZIDI KUKUTOKA NA MICHUZI IIIIIIIIIIII, THE FULANA NINA NITAFUTE KWA MUDA WAKO.

    ReplyDelete
  14. Hahahaaaa Wakuu wa Wilaya hawavaagi fulana. Wanavaaga Suti kwa kwenda mbele.

    Sema tu kuwa imezeeka/imechanika na huwezi kui-'update' tena.

    Kila la heri.

    ReplyDelete
  15. he, we michuzi,
    we acha utani, shauri yako...
    Hii tisheti ya blog haiwezi kupotea.

    utani mwingine mbaya, halafu mwezi wa ramadhani.

    Anyway kama ni kweli, Good ridance!!!
    japo tutaimiss. usijisumbue polisi,

    ReplyDelete
  16. Mpigie Kamanda Kova(Mkuu wa polisi Dar) kwenye hotline yake aliyoitangaza, pia mjulishe na Afande Mwema(mkuu wa polisi Tanzania),Masha(Waziri wa Mambo ya Ndani) na JK(Rais wa Tanzania), then wafahamishe Uhamiaji na customs waimarishe ulinzi mpakani kwa kila anayetoka nje ya Tanzania asachiwe the fulanaaaaaaaazzz! Uwwwiiiii the fulanaaaaaaaazz ya jamii!

    Mdau,
    Scandinavian countries.

    ReplyDelete
  17. May the Shirt rest in Peace.

    ReplyDelete
  18. Kila Mtu mzima!? JAMANI!!!!CHONDE
    CHONDE!! CHONDE!!!! FULANAZI LAZIMA ITAFUTWE! SISI WADAU BLOG HII YA JAMII! TUNAUNGANA NA Mheshimiwa mkuu wa wilaya ya Nanihii ambaye pia ni Balozi wa Nanihi! Hon.Michuzi wa jijini Dar!
    kuwa hile fulanazi ni muhim sana
    kwani ndio bendera na nembo yetu!
    Yeyote hatakayeiona tafadhali atoe taarifa kituo cha polisi

    ReplyDelete
  19. Mheshimiwa Balozi wa Zain, Mkuu wa Wilaya ya Nanihii, na Mzee wa Libenekezzz;

    Naomba nichukue fursa hii kwa heshima na taadhima kumshukuru My Wife wako kwa kuitikia wito wa wadau wa globu hii ya jamii.

    Mnamo Disemba mwaka 2007 viongozi wa wadau wa Globu ya Jamii tulifanya kikao cha siri na mpendwa my wife wako na tukamuomba atusaidia kuhusu hicho kifulana.

    Naona alikuwa anasitasita, lakini baada ya kuteuliwa hivi karibuni kuwa Balozi wa Nanihii imepidi my wife wako atekeleze yale maazimio ya kikao.

    Naomba pia nichukue fursa hii kukupa pole Mheshimiwa Balozi kwa usumbufu wowote utakaoupata katika kipindi cha mpito wa "kupotelewa" na za fulanazzzz.

    Hata hivyo sina wasiwasi kuwa libenekezzzz litaendelea kwa kasi mpya.

    Na ni matumaini yetu wadau wako wa globu ya jamii kwamba hatimaye Mzee mwenyewe wa Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya atakuona siku moja na kukuidhinisha rasmi kuwa Mkuu wa Wilaya yetu mpya ya nanihii.

    Alamsiki

    //Mdau

    ReplyDelete
  20. HAHAHA! MICHUZI mie nataka SH KAzaa Blog kama wanakupenda wachangishe pesa wanitilie mie, najuwa wapi ipo Fulana naku black mail kwakwakwa hahaah. jamani Fulanaz mrudishieni ile ndio inamuwekea mambo safi mh issa bin michuzi. from Zaramo.

    ReplyDelete
  21. Amechukua Michuzi Junior(Mzee wa Jiachie) anataka aanze kukurithi mapema

    ReplyDelete
  22. duuuuuuuuuuuuuu wameshakuliza? hiyo haina kurudi changa changa nunua mpya basi!

    ReplyDelete
  23. LOL!Aliyeichukua angekuwa sehemu sehemu angepiga mnada on ebay! Kamradi ka mtu hako.

    ReplyDelete
  24. nawashukuru wadau wote waliojitokeza kutaka kuchangia kupatikana kwa THE FULNAZZZ.....
    Bro Michuzi itabidi techonlogy ya FORENSIC itumike.
    Kwa hilo basi itabidi utoe damu au nywele za kwapani ili tuweze thibitsha DNA yako na ile itakayopatikana katika hiyo fulanazzzz...
    Vilevile lazima consent form ili usije ukawa sue watu kwani katika mchanganuo huo wanaweza pima ngoma vilevile.
    Ni hayo tuu bro

    ReplyDelete
  25. Napitiliza nyumbani kwangu nanihii kwenda Bagamoyo...haiwezekani wakaiba T-shirt ya Mkuu wangu wa wilaya..naona sasa wakuu wa wilaya wanaonewa sana!!! jana kule nanihii wamevamiwa na majambazi wakajificha chooni!! leo wanaiba T-shirt ya mkuu wetu wa wilaya!! Hapo wametushika pabaya....natoka kazini muda si mrefu na sishuki pale nanihii...moja kwa moja Bagamoyo!! hakuna kulala hadi t-shirt irudi!! na kama ilikuwa na mambo fulani itajulikana hukohuko bagamoyo!!

    ReplyDelete
  26. Nakuonea huruma,basi nitakusaidia, nitakupigia bao ujue fulana yako imefichwa wapi.Kwanza kuna miko yataka kuzinduliwa na kufanya maarifa hayo nahitaji vitu kidogo yaani nataka uniletee kuku na jogoo mwekundu,ratli mbili za sukari na kibaba cha mchele, ukikubali nijulishe nianze kazi
    Janja iko
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  27. MWENYE NAYO NAOMBA AIWEKE KWA EBAY TUIFANYIE MNADA KWA AJILI YA KUSAIDIA MAENDELEO YA WAKAZI WA NANIII!!!!
    AHHAAAHHHH

    ReplyDelete
  28. Dah kaka michuzi pole ina inabidi uende china ukakifate kingine maana ulikuwa unakipenda sana kwa sababu uliki nunua nje ya nchi na ukiangalia na gharama ya usafiri wa ndege kwa asira ulibidi ukivae kila siku. Mimi mdau wa Holand.

    ReplyDelete
  29. Pole sana Misupu, kwa vile wewe ni Mkuu wa wa Wilaya ya nanihiii, wewe ni celebrity jaribu kuiangalia ebay. Itakuwapo type Michuzi fulanas

    ReplyDelete
  30. Kaka Michuzi pole sana kwa kusaidiwa kuhifadhiwa flana yako. La maana take action si unazo picha ulizopiga umevaa hiyo fulana??? watumie wachina watakufyatulia nyingine kama hiyo hata 100 ukitaka wala usihofu, Yaani na mi nipo hapa nshafungua account ya SAIDIA MICHUZI APATE FULANA(SaMiAFu) kwa yoyote ambae anataka kudonate.

    Mdau Amsterdam

    ReplyDelete
  31. Habari zilizoingia sasa hivi ni kwamba hiyo fulana imeonekana jijini Mumbai,India na wataalamu wa interpol wanafuatilia kwa makini habari hiyo.

    ReplyDelete
  32. Kaka mimi naitwa Agwegwe najua hiyo fulana mara ya mwisho nilikusikia unasema utaipeleka kwa kufundi kwani imechanika kwapani. Sasa najua mkuu wa wilaya yetu ya nani hii, mshiko umepiga chenga na fundi hawezi kurudisha kwani msambaa naona naye anataka fweza yake akawanunulie watoto chochote kile kwa ajili ya kusherehekea Eid. Hivyo nipe account # yako nikutumie uchache au michuzi kama jina letu. Pole kaka ni imani yangu utaenda duka lile lile kama kweli imeibiwa ili upate toleo jipya. Jamaa yangu wa London wa pale Dwelle ameiona mtu anayo hivyo wanatoa taarifa kwa polisi wa hapa Cologne ili waikamate wailete fulana ya mkuu wa nani hii na Mheshimiwa sana Ambassador wa Zain.

    ReplyDelete
  33. WAPENDWA WADAU.

    FULANA YA MICHUZI NINAYO MIMI ILIKUWA INANIUMA SANA YEYE KUWA BALOZI WA ZAIN LAKINI BADO ANAVAA RANGI ZA TIGO SASA NIKAONA LABDA KUANZIA SASA ATAANZA KUWA NA FULANAZ YENYE RANGI ZA ZAIN KAMA ATAPENDA AJE MTAA WA MKUNGANI KARIAKOO NINAYO YENYE RANGI HIZO.

    MPENZI WA ZAIN

    ReplyDelete
  34. Bora jamani, ilikuwa kama Ngekewa??? nadhani ilikuwa ya dawa ya kutafutia picha za kwenye Blog. sasa imepotea je utasonga mbele na blog au uta LOOSE?? Rudi tena kwa KARUMANZIRAA.

    Sasa fanya Suprise ingia na mpyaaa balaa wadau wachoke, tafuta ya dizaini tucheke kaka.

    ReplyDelete
  35. pole kaka michuzi,ingawa nimefurahi hahahah,kafulana kimeibiwa hahahaha,sema huyo mwizi aliechukua yuko hatarini maana hatoweza kuiuza hata mitumbani wala kuivaa maana kila mtu anajua kafulana ya kaka michuzi,na hata aje kuivaa si basi atashabuliwa.
    nakusihi mwizi wa fulana ya kaka michuzi bora ujitokeze useme mimi ndio jambazi wa fulana lkn siitowi ng;oo.inaonesha huyo mwizi anajua kuwa fulana hii kaka michuzi anaipenda kwanini asichukue nguo nyengine abebe fulana tuu ni mtu wa karibu huyoo kwa hivyo jitokeze.

    ReplyDelete
  36. okey sikiliza kwa makini!!! fulana itafika london weekend hii. na itwekwa kwa ebay. from monday.nitawapa link jumatatu.thamani yake reserve price ni pound 99 kazi kwenu.ntaiweka kwa week moja tu. na michuzi atawapa update kila siku nani highest bider.

    ReplyDelete
  37. ZE FULANAZZZZZ,ZE FULANAZZZZ
    yani ndo ilinofanya nifall in luv with u michuzzzzzz

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...