darasa la dansa
tizi la kuimba
shaggy hakuamini macho yake
Ruge akimpa maelezo shaggy huku vijana wake wakila tizi ya nyimbo za asili. chini akiangalia darasa la dansa
Nyumba ya Vipaji Tanzania au kwa kimombo Tanzania House of Talent (THT) ni kituo kilichoko maeneo ya Morocco,Kinondoni, jijini Dar kinacholea na kukuza vipaji mbalimbali miongoni mwa vijana.

Kituo hicho ambacho kilianzishwa January mwaka 2006 chini ya Mkuruigenzi wake mkuu Ruge Mutahaba, kinalea na kuibua vipaji katika maigizo, madansa wa muziki na ngoma za kisasa na kiasili pamoja na waimbaji.

Baadhi ya vipaji, kwa upande wa muziki, ambavyo vimeibuliwa kutoka katika kituo hicho ni wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Mwasiti Almasi na Hafsa Kazinja. Mwasiti alitamba na wimbo wake uitwao Niambie wakati Hafsa aliwagusa wengi na wimbo wake wa Pressure. aliomshirikisha Banana Zorro. Dada yake Banana, Maunda Zorro, pia ni mmoja wa vijana wanaolelewa kituoni hapo.

Msanii Shaggy alipotua bongo kwa maonesho kadhaa hakuamini macho yake pale alipokuta kambi hiyo yaa vijana wapatao 100 wakijifua katika kuimba, kucheza na kupiga ala. Alimwambia Ruge kwamba kabla ya miaka 5 Shaggy watano wataibuka toka THT.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...