Wenyeviti wa Jumuiya za Japani na Italy wakijadili mada katika hoteli Universo mjini Roma jana.
Mwenyekiti wa Japan, Dr Simba akimkabidhi katiba ya Jumuiya ya watanzania Japani mwenyekiti mwenzanke wa Italy Bw. Abdulrahaman
Picha ya pamoja baada ya mazungumzo, kutoka kushoto (asiyevaa koti)ni Mwenyekiti wa watanzania wa Japani Dr Simba, Mwenyekiti wa watanzania wa Italy Bw. Abdulrahaman na katibu mkuu wake Bw. Kagguta. N.M
Mwenyekiti Dr Simba katika picha na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya watanzania Italy Bw Kagguta N. M ambaye alifuatana na mwenyekiti wake katika mazungumzo hayo hapo Jana.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Wanaoishi Nchini Japani Dr Ally Y. Simba, Jana(27/9/2008) alikutana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wa Italy Bw. Abdulrahaman A. Alli katika hotel ya Universo ya Mjini Roma, Italy.

Katika mkutano huo Mwenyekiti huyo wa Italy alifuatana na Katibu Mkuu wake Bw. Kagguta N. M. Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walijadiri kwa kirefu mifumo ya Jumuiya za Watanzania ughaibuni pamoja na matatizo wanayokabiliana nayo katika kufanikisha malengo ya Jumuiya hizo.

Kama ishara ya kuziweka Jumuiya hizi karibu zaidi, Dr Simba alimkabidhi Bw. Abdulrahaman katiba ya Jumuiya ya watanzania wa Japan.

Viongozi hao walikubaliana kundelea kuwasilina na kubadirishana habari za Jumuiya zao.

Mwisho kwa niaba ya vinogizi na wanajumiya wa Japani, Dr Simba alitoa shukurani zake za dhati kwa Viongozi hao wa Italy kwa kukubali kukutana naye. Dr Simba aliondoka Jana Jioni kuelekea Palermo kikazi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Jamani huyo ni mwenyekiti wa Watanzania Napoli..Mbona sisi watu Wa Roma hatumjui??Anaitwa mwenyekiti wa Watanzania Italia kwa kuchaguliwa na watu gani na waishio wapi??? Jamani naomba tuandike vitu vya ukweli..

    ReplyDelete
  2. dada wamekosea kuandika...huyo ni mwenyekiti wa pili wa watanzania wa Napoli, wa kwanza alikuwa Prof. Tandika.

    ReplyDelete
  3. dada wamekosea kuandika...huyo ni mwenyekiti wa pili wa watanzania wa Napoli, wa kwanza alikuwa Prof. Tandika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...