Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Meja Jenerali Mstaafu, Said Kalembo, (kulia) akiagana na Jumanne Kimbeo, ( Babu wa Mizimu) , Mkazi wa Kijiji cha Kisaki Stesheni, mara baada ya viongozi wa Serikali ya Mkoa huo kulitembelea eneo la kihistoria la chemichemi ya maji ya moto katika Kijiji hicho hivi karibuni. picha na mdua john nditi wa mji kasoro bahari

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Mheshimiwa Michuzi Pole na kazi.
    Kwa kweli hiyo habari ya Babu wa mizimu imenikumbusha mbali sana.Nakumbuka wakati nasoma enzi hizo reli ya TAZARA ndiyo kwanza imefunguliwa tulikuwa tunapata huduma babu kubwa kwenye treni hiyo.Moja ya huduma ilikuwa tunawekewa miziki ile ya kizaire kama mikolo milekimingi,kamiki,kasongoyeye,andoya n.k.Kulikuwa na mtangazaji ambaye alikuwa anatangaza kila treni ilipokuwa inakaribia kufika stesheni fulani.Pia alikuwa akitutangazia tunapokaribia sehemu mbalimbali za kuvutia kama vile mbuga za wanyama, mahandaki n.k. Kwahiyo Treni ilipokuwa inakaribia Kisaki mtangazaji huyo (mara nyingi alikuwa mwanamke) alikuwa akitutangazia kuwa tunakaribia stesheni ya Kisaki,ambapo kabla ya kufika Kisaki mtaona upande wenu wa kuume/kushoto kuna kisima cha maajabu kinachotoa maji moto.Mtangazaji huyo alikuwa akitoa full story kuhusu Kisima hicho.Kwa kweli ilikuwa inafurahisha sana.Lakini siku hizi mambo hayo hakuna tena.TAZARA imeoza kabisa.Mheshimiwa enzi hizo TAZARA ilikuwa kweli reli ya uhuru. Kwahiyo Mheshimiwa Michuzi nafikiri itakuwa jambo la busara na faida kwa wengine kama ukaifuatilia habari hiyo kwa undani na kisha ukaturushia kwenye mtandao huu ili wadau wengine wa blog hii waweze kuipata story hiyo kwa undani ili Wajue maajabu ya Mkoa wa Morogoro.Hata kama utairusha kwenye daily news, yote sawa ili mradi utupatie link tuweze kuisoma
    Ni mimi Mdau wako wa Cardiff

    ReplyDelete
  2. Saidi kalembo as know Safi Sana Kalembo tulikuwa naye pale High Commander Training Wings na alishastaafu miaka 5 iliyopita na sasa mkuu wa mkoa.DUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU Bongo hakuna watu wenye nguvu za kufanya kazi mpaka tuchukue wastaafu.
    Okay labda anabusara na kiongozi Mzuri nani anajua?

    Kenge

    ReplyDelete
  3. Kuna teknolojia za kuzalisha umeme kwa kutumia maji moto. Tunatengeneza hela ya kutosha kwa njia za utalii hapo? Tumeshafanya utafiti kuona kama tunaweza kufua umeme maeneo ya hapo?
    Wakatabahu,
    Mdau

    ReplyDelete
  4. Namkumbuka Mh. Kalembo wakati huo alikuwa ni Brigedia wa kambi kule Biharamuro ni kiongozi safi sana anajua kunyosha watu maana wanajeshi walikuwa wanamuogopa kama simba. But ni mtu social sana nakumbuka alikuwa kila jioni anawakusanya wanajeshi bila kujali kama ni kopro au meja nakwenda kucheza nao mpira wa mikono alikuwa fiti sana kimazoezi. Pia sisi watoto wa kambini tulikuwa tunampenda sana maana hata akikuta wapi anasimamisha Land Drover yake ya kijeshi na kuwapa lifti kitu ambacho ni aghalabu sana jeshini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...