KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!
MKUTANO WA CCM SHINA LA READING
WANACHAMA WOTE –CCM READING
WAKEREKETWA WOTE-CCM READING
WAPENZI NA WANAMAPINDUZI WOTE WA READING
TAREHE: 19/10/08 SAA 8 MCHANA HADI SAA 12 JIONI
MAHALI: UKUMBI 79 LONDON ROAD,
READING RG 1 5BY.
KADI ZIPO KWA WANACHAMA WAPYA. KUMBUKA KUJA NA PICHA. BEI YA KADI NI POUND TATU NA POUND KUMI NA MBILI ADA YA MWAKA MZIMA.
TUMEWAALIKA WAGENI KUTOKA:
MWAKILISHI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA UHAMIAJI [IMO]
KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA NCHINI UINGEREZA [UK]
MWAKILISHI WA MUDA WA JUMUIYA YA WATANZANIA- READING.
AJENDA KUU: UCHAGUZI WA WAJUMBE 15 WA HALMASHAURI KUU YA TAWI LA CCM UINGEREZA.
KWA MAELEZO ZAIDI TAFADHALI WASILIANA NA:
MAIRA BENJAMINE MIGIRE- 07799212095
KATIBU WA CCM SHINA LA READING
WOTE MNAKARIBISHWA – KUTAKUWA NA CHAKULA (free of charge) NA MUZIKI BAADA YA SHUGHULI ZOTE.
KIINGILIO BURE!!!!!!!!
Akhasante.
endeleeni huko huko
ReplyDeleteYaani wanawatega wadau kwa kutumia pilau, duh si mchezo.... wakiongeza na tshirt na kofia lazima wawapate wachache wasiosoma alama za mda
ReplyDeletewanamapinduzi? mapinduzi gani? CCM ilipinduwa nini na lini? hichi chama ni cha zanzibar? zanzibar ndiko kulikofanyika mapinduzi, tanganyika kumepatikana uhuru. hata sherehe za nchi (ooppss vile zanzibar ni nchi?) zanzibar hushereheka mapinduzi wakati tanganyika husherehekea uhuru.
ReplyDeleteMmeanza; nasema mmeanza,tunatafutana ubaya hapa. Well!! napenda kuchukua nafasi hii kuwakumbusha wadau wote mtakaoenda kwenye huo mkutano kubeba papers zenu na ziwe halali, kwani atakayeshukiwa na wajomba mimi tena hapo sina lawama. Kunradhi kwa wale mnaoona upuuzi huu wa kubaguana kiitikadi ili hali sote ni ndugu na tupo ughaibuni kusaka maisha kama nitawabughudhi kwa hili. Narudia!!! sina utani kwa hili lazima wajomba watie timu, sijui iweje, lakini lazima watatia timu.
ReplyDeleteWakatabahu.
NA MIMI NATAKA KUGOMBEA UONGOZI CCM LAKINI NAULIZA TU KUWA NAFASI HIZI ZA UONGOZI ZINAINGIA KATIKA ILE MISHAHARA MIPYA YA CCM YA KIMA CHA MILIONI MBILI ? TUENDELEZENI MAPINDIZI
ReplyDeleteMkereketwa
CCM walijaribu kuileta Marekani lakini kutokana na kupingwa na wengi naona imeshindikana. CCM iishie huko huko kwa wanyalu Uingereza.
ReplyDeletei have got one "pathetic"
ReplyDeleteYou guys don't have life? Kila jumamosi ni mikutano ya CCM. You need a new hobby my friends
ReplyDeletemsituchanganye nyie mnaojiita watu wa ccm reading chama kipo kwa ajili ya matumbo yenu yaan mpaka karne hii mnawashabikia hao mafisad(magaidi)tuondokeen na uchawi wenu
ReplyDeletekaka/dada wa hapo comment ya juu hata hapa u.k imepingwa hii iko kwa watu wa bara tu,watu wa visiwan wajanja na hao walioko ni hao hao tu hakuna wapya nan atakwenda kwenye huo upuuz wao na lazima niwashtue wajomba maana wengi wao wameoza ndio wanajitia ccm
ReplyDelete