nawasili hapa uhabeshi kwa kajivekesheni ka siku kadhaa. hapa globu ni marufuku na inabidi uchimbe hasa ili uweze kupiga libeneke kama hivi. lakini wadau wengi, kama sio wote wa hapa, hawaipati globu ya jamii na wanalaalmika ile mbaya
jiji la addis ababa kwa mbali kule. pamoja na matatizo ya mara kwa mara has vita vya wenyewe kwa wenyewe, hawa jamaa wako fiti kinoma kwenye miundombinu na mambo memngine muhimu. ila basi tu. masnepu ya taun baadaye kidogo...


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 28 mpaka sasa

  1. EEbana eeh snepu safi but tuletee matokeo ya mech ya mambaz na staazi
    mdau
    sauzi

    ReplyDelete
  2. Pole na Safari Ethiopia. Kuna habari kutokea Ethiopia zinazo sema, Mtanzania amechaguliwa kuwa Mwakilishi mkazi wa shirika la chakula duniani (WFP) Kwenye umoja wa Afrika na Kamisheni ya Uchumi ya Africa (ECA) ni kweli? Na nina? Kama ni kweli, ni sifa kubwa saana kwa taifa letu.

    ReplyDelete
  3. michuzi sio siri mie bado nusu na ushamba wangu niseme umefanya utundu wa picha zako nyuma umeweka picha kwamba hapo si adis ababa ni visiwa vya maritius huko, michuzi baba umependeza hizi serikali zetu zinajuwa kweli kujenga ma hotel ya watalii na kula pesa kule vijijini wanapasahau mpaka majeshi ya gorilla yanajitengeneza hawana habari. from Mkwasa

    ReplyDelete
  4. Ni kweli Addis ulinzi mkali kila sehemu mpaka ndani ya hotel kama hiyo Sheraton ni kawaida kuona askari kanzu wakisalimisha bastola zao reception.

    Karibu na makao ya AU usilogwe kupiga picha marfuku maana kuna majengo ya wizara nyeti haraka haraka utabebwa juujuu staili ya tanganyika-jeki. Si umeona mwenyewe askari brigadi nzima na mitutu eapoti Addis utadhani vita itaanza saa hiyo hiyo hapo eapoti.

    Ila Balozi nakushauri ukatembelee soko 'kubwa kabisa afrika' hapo Addis na pia usisahau kutembelea makao ya Haile Sellassie utuletee taswira ya maeneo hayo.

    ReplyDelete
  5. mdau naona unawakilisha kampuni yetu ya mawasiliano huko uhabeshi (nembo kwenye bag ya Laptop)

    ReplyDelete
  6. Mkuu wa wilaya na balozi ...!!

    Nakukubali kwa vakesheni kaka, keep on exploring ze weldi.

    ReplyDelete
  7. Hivi picha huwa unajipiga mwenyewe au kuna mtu maalum ambaye huwa anakupiga masnepu mara zote unapokuwa katika safari zako??? Naomba jibu Bro Michuzi - Usibanie Pls

    ReplyDelete
  8. mzee mzima,
    hongera sana. kati ya mahoteli ninayoyazimia Africa ni Sheraton Addis. Napafahamu sana mtu wangu. Du, uko juu sana mtu wangu. Hapo nimeshawahi kutesa na mimi miaka hiyo nikila nondoz pale Addis Ababa University. Du, wewe muhabeshi ukimwona mwambie Chegere yelem, maana yake hakuna matatizo. Umwambia nkwante na matachu, betam amasaginalo.
    Umenikumbusha mbali sana mzee.
    Alafu mademu wako bombaaa! Utembelee London cafe kule Bole ppia

    ReplyDelete
  9. Mithupu yule kule nyuma my waifu wako nini? Sasa angekuwa karibu mngekamilisha snepu. Mithupu mbona watuzingua hivi unamficha maiwaifu wako unawaogopa majitu wengine humu wasije iba nini?! LOL Kwa mavekesheni hongera...sasa kale kajifulanaz kamebahatika nako kupata kajivekesheni safari hii..

    ReplyDelete
  10. Acha michu! Nimewahi shuka hapo. hawana lolote. Wewe unaangalia Addis tu. nenda kule ndani interior. Utashangaa kama hawa watu wako Duniani au vipi!. Ni sawa sawa na kwenda Chake chake au Mkoani uadhani wale watu ni maskini sana. Kumbe wamejazana Karioakoo na maghorofa marefu kabisa.

    Usiangalie kitabu kwa uzuri wake wa nje.

    ReplyDelete
  11. Suti nzuri sana bro.

    Mdau US

    ReplyDelete
  12. Aisee, wa-demu wa hapo si mchezo. Kama huna maywife wako sijui kama utarudi hivi hivi...!

    ReplyDelete
  13. Nadhani hapo upo Sharaton Hotel maana naona hiyo swimming pool inafanana na ya Sheraton..Hiyo Hotel si mchezo imetulia...Mdau wa Kigali.

    ReplyDelete
  14. michu kula bata dogo ndani ya addis kiwanja poowaaa kama per diem mkwanjaaa...libeneke la mtandaoo diliuvumba.....

    ReplyDelete
  15. Usisahau kutembelea "Merikato" kwa machingas!

    Halafu utueleze utakayoona.

    ReplyDelete
  16. huyo demu ni shemeji tu wa mheshimiwa balazi na DC wa Tegeta,mwenye demu jakaya alitangulia Libya kwanza.

    ReplyDelete
  17. wasalimie huko! ila kaka michu mi sikuelewi wewe ni balozi wa nanihii, then blog yako inafadhiliwa na nanii na hapo naona mkoba wako wa laputopu una chata ya vod...!! sasa huoni kama huo ni uchonganishi??

    ReplyDelete
  18. Mithupu umenikumbusha hapo ADDIS si mchezo, baridi ile mbaya!!. Kuoga maji ya moto tu. Soko kubwa lile lina vitu vizuri sana, nilimnunulia my wife gauni handmade na mimi nakanunua mashati handmade ya hariri bomba sanaana.Cheki Aiport ukitoka nje du, daladala hadi mlangoni!!!!! gari wanazo za zamaniiiii!!! vi-fiat vi-saloon utachoka mwenyewe. Fly Over moja, heri wao kuliko sisi bongo. Mnara wao bomba sana. Orthodox church nk si mchezo.
    Kwa ndege tu wako juu.Mademu hela yako tu, wazuuri hao ndio ma-queen wa africa. Bila shaka umedandia lift ya JK kwenye ndege yake, uongo???

    ReplyDelete
  19. Zain watakufuta kazi, unabeba laptop bag ya timu pinzani?

    ReplyDelete
  20. Nafikiri sasa wewe unashindana na Vasco Dagama.

    ReplyDelete
  21. mwakilishi wa WFP AU na EAC ni jamaa mmoja wa kichagga Abnezer Ngowi.

    ReplyDelete
  22. sawa sawa michuzi ic

    ReplyDelete
  23. KAKA UMETOK POA NA SUTI ILA HILO ULILILOVAA NDANI SIJUI LI T-SHIRT JEKUNDU UMEMECHISHA NA NINI AU CHUPI KAMA SI SOKS....TUMTUMIE ZEZE PICHA AKUWEKE KWENYE FASHION POLICE PLZ......LOL

    ReplyDelete
  24. wewe misupu mwenzetu mbona kila siku huko vekesheni? mara uabeshi mara newala mara ujerumani mara ukerewe yaani mwenzetu wewe una bahati sana. Unakwendaga na mai wafu wako lakini maana hao watoto wa kiabeshi sio mchezo. enewei kula raha kufa kwaja.

    ReplyDelete
  25. Photo-Journalist na SUTI wapi na wapi mzee, wewe zako ni Jeans na Tshirt na SAFARI BOOT, sana sana na kikoti chako cha wapiga picha cheny vifuko kibao mbele na nyuma, hiyo ndo fashion ya
    maphoto-journalists. Hapo hupendezi kabisa kuwa mwandishi mpiga picha. Suti waachie mafisadi , wewe si fisadi wa EPA.

    ReplyDelete
  26. Bro wewe ni shushu nini? mbona kila anapotia timu mkuu wa kaya na wewe upoo?
    Acha kutuzuga hizo sio vekesheni uko mzigoni kiaina , haya bwana ila hapo Addis usikose kwenda kujirusha Star Night club uone utakavyogombaniwa kama mpira wakona na University Students

    ReplyDelete
  27. Bwana michuzi naomba usiniweke kapuni. Kwanini huwa husemi ukweli kuwa unakuwa unafuatana na misafara ya serikali na badala yake unajifanya kuwa uko vekesheni? Unajua nimekuwa nikifuatilia sana story zako nimegundua na wewe ni mmoja wao.Wewe unatuzugu huta hapa lakini mwenyewe unajua unachokifanya endelea na mwendo huo huo wakuvaa kofia mbili lakini. Umekuwa fundi sana wakuweza kujitenganisha na wenzako muda muda umekwisha. Umepata washabiki wengi sana kwasababu ya kuweka kila kitu mtu anachoandika lakini wanafahamu wanajua kuwa wewe sio mwenzetu unawakilisha wenzako. Hongera sana mzee wa vekesheni. sisi yetu macho tu na masikio.

    ReplyDelete
  28. Wananchi kwa chuki, sijapata kuona. Kila mtu hapa anafahamu kuwa Balozi Michuzi ni mfanyakazi wa Daily News na amesema mara nyingi hasa wageni wanapomtembelea ofisini kwake. Pia wanafahamu kuwa yeye ni mpiga picha wa serikali kwa kuwa anafanya kazi katika gazeti la serikali na ameanza kupiga picha kabla ya wadau wengi hapa kuzaliwa. Pia ni mfanyabiashara na ametuonyesha maduka yake ya picha na kuwashukuru wadau wanaoumpetmbelea au kumpa kazi za kupiga picha katika shughuli zao.

    Sasa, sijui hii chuki imetoka wapi. Pia nadhani wadau wengine wana roho ya kutu au korosho, hawapendi maendeleo ya wenzao. Matatizo ya serikali ya wizi wa fedha za wananchi hazihusiki kabisa na blog hii wala na Balozi. Kama kuna kosa dogo nililoliona la Balozi Michuzi ni tabia ya awali ya kubana maoni hata yale yasiochafua hali ya hewa pamoja na maoni mengi ya kwangu binafsi, hasa yanayohusu CCM. Lakini nimeona tofauti sana katika miezi michache iliopita na maoni mengi sasa yanachapishwa hata yanayomtukana yeye binafsi kama ya hapo juu. Nadhani pia, kama sikosei Balozi Michuzi amebanwa sana na kazi, inabidi ampe mtu kibarua cha kumsaidia kuiendesha hii blogu ya jamii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...