Mimi ni mpenzi sana wa blog yako namoja kinachonivutia mashairi kwaiyo leo nimependa nikutumie hili shairi baada ya kukosa burudani kwa masiku kidogo.
naomba usitoe email yangu
Mdau
--------------------------------------------------------------------------
PWEZA
Pweza nimemkinai,kumla namkataa
Tena amenacha hoi, simtaki nawambia
Msije nita bedui ,unyongeni nitakuwa
Ukweli amenitesa , pweza simtaki tena.
Nilimpenda rohoni, kijijini kuhamia
Karibu na baharini, wavuvi kuwangojea
Kila wakitoka pwani, pweza niliwawania
Ukweli amenitesa , pweza simtaki tena.
Nikamfata sokoni, mnadani kununua
Bei sikujali kwani, pweza nilihitajia
Hujihisi burudani, kila ninapojilia.
Ukweli ametesa pweza simtaki tena.
Hukimbilia nyumbani, kupika nakazania
Namkosha pweza ndani, naviungo humtia
Humshemsha chunguni, nasupu nikajinywea
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Pindi ninapotamani kukaanga huamua
Mafuta sijali kwani kama yatanirukia
Hutaka awe laini, nasaladi hujilia
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Sasa tena sitamani, pweza nimemkataa
Kwenye yake madhumuni, mabaka amenitoa
Madawa hospitalini, wameshinda kunipea
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Waganga nadarubini, sababu wakanipea
Kuwa pweza sitamani, niko na aleji pia
Hataki tena mwilini, kakinai nawambia
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
PWEZA
Pweza nimemkinai,kumla namkataa
Tena amenacha hoi, simtaki nawambia
Msije nita bedui ,unyongeni nitakuwa
Ukweli amenitesa , pweza simtaki tena.
Nilimpenda rohoni, kijijini kuhamia
Karibu na baharini, wavuvi kuwangojea
Kila wakitoka pwani, pweza niliwawania
Ukweli amenitesa , pweza simtaki tena.
Nikamfata sokoni, mnadani kununua
Bei sikujali kwani, pweza nilihitajia
Hujihisi burudani, kila ninapojilia.
Ukweli ametesa pweza simtaki tena.
Hukimbilia nyumbani, kupika nakazania
Namkosha pweza ndani, naviungo humtia
Humshemsha chunguni, nasupu nikajinywea
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Pindi ninapotamani kukaanga huamua
Mafuta sijali kwani kama yatanirukia
Hutaka awe laini, nasaladi hujilia
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Sasa tena sitamani, pweza nimemkataa
Kwenye yake madhumuni, mabaka amenitoa
Madawa hospitalini, wameshinda kunipea
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
Waganga nadarubini, sababu wakanipea
Kuwa pweza sitamani, niko na aleji pia
Hataki tena mwilini, kakinai nawambia
Ukweli amenitesa pweza simtaki tena.
pole sana mdau shairi lako ni muafaka...kwani yaliyokukuta si madogo..hata mie kipindi fulani pweza alinipa aleji lakini docta nikapata wa kunitibia sasa nakula kwa kujipimia.
ReplyDeleteSupu ya pweza ndio yenyewe, nanihii inakuwa hailali.
ReplyDeleteJamani hili ni shairi na shairi linakuwa na maana iliyojificha ambayo mtungaji anataka wasomaji waumize akili zao kulichambua.
ReplyDeleteSasa hapa mtungaji anazungmzia PWEZA lakini ni pweza gani?
HONGERA MALENGA...UTENZI UMETULIA MNO. UJUMBE, VINA, VYOTE MUURUA...LAKINI NI ALEJI TU NDIYO HOJA AU?........KWANI MAMBO YA PWEZA S'MCHEZO BWANA! HAHAA
ReplyDeleteMDAU
JP
Big up malenga wetu,japo naona wasomaji wameshindwa kung'amua ujumbe uliopo, nionavyo mimi ujumbe unahusu onyo juu ya hili GONJWA HATARI-VVU,kama nimekosea nisahihishwe tafadhali.
ReplyDeletemtoa maoni juu kweli,huyu jamaa anamaanisha Tahadhali ya ugonjwa wa UKIMWI,maana pale pia kasema alikuwa anajikaangia hata mafuta kumrukia hakujali,naona alikuwa ana maana hata CONDOM alikuwa havai anataka ale nyama yenyewe
ReplyDeleteUmejitahidi Mahenga wetu Hongera
PWEZA
ReplyDeleteMoyo kukinai,kuacha mbovu tabia
taaban bin hoi, humtaki watwambia
Hutaitwa bedui,pweza kumkimbia
Pweza hatufai, wala kumkurubia
Ulmipenda rohoni, na magesti kuhamia
Pakavu na baharini, kote kuvinjairia
Watokapo ndani,nawe uliwaipamia
Pweza sote hatufai, wala kumkurubia
Uliwafuta sokoni, kwa fedha kununua
Bei poa jamani, mradi moyo kufurahia
Hujihisi burudani, kila ukiparamia.
Pweza sote hatufai, wala kumkurubia
Kwa pupa nyumbani, kazi kufakamia
kwa mziki na asumini, uturi kunukia
Vifupi vigauni, na vidani kupambia
Pweza sote hatufai, wala kumkurubia
Kila ulipotamani, kuwa beep huamua
Huwaita chumbani,Esta na Malia
Hutaka wawe laini,urojo hujilia
Huna kinga jamani, peku huingia
kwa sasa hutamani, pweza wamkataa
Miwasho mapajani, mabaka amekutoa
Tiba hospitalini,bado haijatokea
Pweza hatufai, wala kumkurubia
Waganga na darubini,waijua sababu
Mwili hauna amani,dhiki na tabu
Kinga za mwilini, kufifia taratibu
Pweza hatufai, wala kumkurubia
Hongera kuamua, kwa msimamo thabiti
Sote tungejua, majuto ni laiti
Giza penye jua, ndio usmart
Pweza hatufai, wala kumkurubia