JUMUIYA YA WATANZANIA MANCHESTER
SHEREHE YA SIKU YA UHURU WA MTANZANIA
Wanajumuiya mnakaribishwa kwenye sherehe ya uhuru wa mtanzania itakayofanyika tarehe 13 December’ 2008 kuanza saa 12 jioni hadi saa 6 usiku, kwenye ukumbi wa Marlborough street ambao upo Oldham, post code OL4 1EG Kufika kwenu ndio kufanikisha sherehe hii, Kadi ya mwaliko itatolewa mlangoni.
Asanteni na karibuni sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Masahihisho sio uhuru wa mtanzania, ni uhuru wa mtanganyika au mtanzania bara, wazanzibari au watanzania visiwani hatusherehekei uhuru, tunasheherekea siku ya mapinduzi na si disemba ni januari kumi na mbili.

    Pia mbona mnatushangaza kadi za mualiko kutolewa mlangoni! mtu hualikwa kwa kadi na aghlabu hufika na kadi alipoalikwa, sasa nyinyi mnataka mtu afike ndio mumualike? mbona mnafanya mambo kinyume nyume?

    ReplyDelete
  2. Kusheherea uhuru wa nani yakhe???minyororo ya utumwa mpaka leo yapo shingoni na yakikazwa ndio hivyo...'THE END'

    ReplyDelete
  3. Tunasherekea nini!ukimwi,maradhi,vita,ufisadi,rushwa,umasikini,uongozi duni,madeni...niendelee jamani?
    Licha ya hiyo nimebaki kwetu na sitatoroka kubeba maboksi!

    ReplyDelete
  4. siku ya uhuru 13dec 08?????
    tarehe gani iyo na uhuru wa nchi gani???
    IVI TANGANYIKA NI NCHI???TANZANIA NI NINI ASA JAMANI
    jaman tufafanue tuelewe,,mana Pinda alisema na wengine ati tanganyika ilishakufa bt nastaajabu zenji yaexist kama nchi tena wana bendera na wimbo!!
    basi tuwe na tanganyika na zenji=tanzania siku ya muungano
    au tusifanye mapinduzi na uhuru wa tanganyika ziwe sikukuu,,,kwaza zaleta utengano
    HAIJATULIA HII

    ReplyDelete
  5. wakazi wa Machester namtafuta Victor Mashamba please muhimu anitumie ujumbe mfupi:+255 783 418864.Mdau lady S

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...