bahati iddi nzimano mwenye umri wa miaka 30 sasa ni mmoja wa walemavu wachache ambao ni mfano wa kuigwa. akiwa amezaliwa akiwa hana mikono, mwanamke huyu wa shoka hakuuruhusu ulemavu wake umgeuze omba omba. alisoma hadi kidato cha nne, akaendelea na maisha kama mtu wa kawaida na sasa ni mjasiriamali. baada ya kupata msaada wa mtaji wa shilingi milioni 5 toka kwa JK, amedhamiria kuendesha maisha yake kama mtu asiye na ulemavu. Muangalie na msikilize bahati kwa kubofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Nimefurahi sana na Bado ninaimani kubwa sana kwa rais wetu JK,kwa kuonyesha upendo kwa watanzania, kwa pale anapotaka kusaidia zaidi lakini uwezo unakuwa mdogo!!! Ila usikate tamaa katika hii kazi ya kuthamini binadamu kwani naamini kabisa Mungu yupo pamoja nawe na atakuwa na wewe mpaka dakika za mwisho katika kuliongoza taifa letu la Tanzania kwa kutuonyesha upendo na kuwa mkali pale ambapo mambo ayaendi vizuri.

    Mungu akubariki wewe na familia yako na Heri ya mwaka mpya.

    Mdau kutoka canada!!!!!!

    ReplyDelete
  2. Huyu ni yule Bahati wa Tabora. Kama ndiye hongera sana. Bahati kweli ni mfano wa kuigwa. Nasikia anaandika kwa kutumia vidole vya mguu na leg writting yake ni kiboko.
    JK anasaidia watu wengi kulingana na uwezo wake kama Rais, lakini pia kama Binadamu mwenye mapenzi mema. Ukimtazama hata kwa macho unaona kabisa dhamira yake ya dhati kutoka moyoni. Tatizo ni haya mambo mengine.

    ReplyDelete
  3. Pole sana Bahati. Mwenyezi Mungu alikuwa na makusudi yake kukuleta duniani ukiwa kama ulivyo. Zidi kumwomba na atakusaidia zaidi maana huwezi kujua makusudio yake. Pia Bravo JK kwa big assistance kwa mama huyu. Kweli rais wetu mpendwa anajali watu wake.
    Mdau

    ReplyDelete
  4. Huyu dada ni mpiganani, nakumbuka miaka ya tisini alikuwa anasoma shule ya sekondari Mihayo pale Tabora wakati mimi nikiwa Kazima, tukafanya mtihani wa form II akafaulu na mpaka kumaliza Form IV. Sifa mojawapo pekee ambayo pale Tabora watu walikuwa wanasema mungu hamnyimi mtu vyote ni Umbile lake. Kwa kweli dada huyu ana umbile la kike hasa yaani "figure namba nane", ila pamoja na hilo hakubweteka kama dada wengi wanavyofanya kusubiri mabuzi yeye ni mchakarikaji na kama sikosei alikuwa analelewa kwa Masista pale Jmbo kuu Tabora. Hongera sana dada yangu natumai umeshapata na shemeji wa halali lakini bado hutaki kubweteka.

    ReplyDelete
  5. Hongera Da Bahati kuonyesha kuwa kila mtu anaweza kujitegemea. Hongera Rais wetu kwa upendo wako si kwa Bahati tu bali kwa watu wote. Wenye kusikia hotuba zako wataamini kuwa wewe ni mtu wa haki. Huvumilii maovu lakini katika kuwashughulikia umetamka bayana kuwa ni lazima kuwa makini asionewe mtu bure. Hiyo ni tabia ya kiwalii. Mwenyezi Mungu atakusimamisha ukamilishe uliyokusudia na malipo yake hapa duniani ni wanao watakao kuwa wema na kesho uatapata pepo yako mpendwa wetu.

    ReplyDelete
  6. Heri amkumbukae Mnyonge maana ataokolewa mara yapili, endelea JK
    Kazi yako inavutia!!!!!!!!!!!

    Mdau kutoka canada!!!

    ReplyDelete
  7. dada bahati ni mfano wa kuigwa si kwa walemavu tu pia kwa wale waliozaliwa bila dosari, honera sana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...