hapa sio gereza la keko ama segerea, ni shule ya msingi ya uhuru ya wasichana. karibu shule zote za dar zimejengewa uzio wa namna hii. wadau hii imekaaje?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Umenifurahisha Mithupu na picha hii karibu na kwetu.Nimeipenda hii miaka yote hapo palikaa vurugu tu,sasa afadhali inaeleweka wapi eneo la shule na wapi eneo la wapita njia.

    ReplyDelete
  2. I think that's good idea, because students don't get distractions from out side

    ReplyDelete
  3. Uzio katika maeneo mbalimbali hutegemea mazingira yanayolizunguka eneo hilo. Mahali kama hapo Shule ya Uhuru panastahili uzio wa nguvu kama unaoonekana hapo

    ReplyDelete
  4. kulikua na uzio wa kumwaga Kinondoni Muslimu na bado mitoto ikachanganyikiwa. ukuta hatasaidia wale wasio taka kujisaidia wenyewe.

    ReplyDelete
  5. Habari njema ni kwamba Waziri Profesa Maghembe alitoa waraka mwaka jana akipiga marufuku kuweka mafremu ya maduka kwenye kuta za shule. Japokuwa la kushangaza ni kuwa pale sekondari ya jangwani upande wa Morogoro Road, Utawala na hususan bodi ya shule ilimpa mwarabu/mwekezaji eneo lile eti ajenge ukuta halafu aweke show room ya magari. Utawala unajitetea kuwa ilipewa kibali na Tanzania Building Agency kwa kuwa ndiye mmiliki wa jengo hilo ambalo ni la serikali. Lakini kisheria mwenye mamlaka ya kutoa kibali cha ujenzi ni Manispaa ya Ilala na siyo TBA. Kama siyo timely interevention ya Mkuu wa Mkoa Abbas Kandoro pale biashara ingekuwa kama kawa. Hiyo ndiyo habari yenyewe!!!

    ReplyDelete
  6. Dar bila uzio unaweza kukuta watu wanajimegea eneo lako mpaka uani na ukienda mahakamani unakuta mtu ana hati miliki ya eneo ambayo ina mika si pungufu ya 20 wakati yako ina miaka 10, waulize Yanga uwanja wao ulivyomegwa kifisadi na hata kudai wanashikwa na kigugumizi sijui waliuziana kishkaji? Hako kafensi ni muhimu sana hata ukizingatia humo ndani kuna tubinti Ambato tunapofika darasa la sita na la saba vinaanza mambo yetu yaleeee. SO WEKA GETI TU…

    ReplyDelete
  7. Good, mitaa hiyo huwezi kuweka fence yenye "louvres" kwa kuwa kunamsongamano kibao na hao vibaka watapata njia rahisi ya kushukia upande wa pili! inapendeza, na inapunguza utoro wa watoto shuleni.

    ReplyDelete
  8. Huo ulikuwa ni mtaji babake. Watu walitoa suggestion kwa lengo la kupata kitu kidogo. Hapa namaanisha kwamba maafisa na madiwani husika walipata kitu cha juu! Hakuna mtu anatoa wazo la maendeleo hapo bongo kama hakuna kitu cha juu babake. Hivi tujiulize, wakati wazazi na wagonjwa wengine wanalala hospitalini chini bila hata ya chandarua, ni wazo zuri kwa halmashauri ya jiji kuanza kujenga hizo kuta? Kwani hakuna maafisa wanaoangalia maeneo yasivamiwe? Nawakilisha!

    ReplyDelete
  9. Wazee wa kukojoa ukutani chaka jipya hiloooooo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...