NDOA IFUNGWE AU ISIFUNGWE?
Hello kaka Michuzi habari yako?
Pole na majukumu. Mimi ninamatatizo kaka naomba unisaidie nipate msaada wa wanajamii nini cha kufanya.
Mimi ni mdada wa miaka 43, na kwa sasa naishi UK tangu mwaka 1998. Naomba nitoe historia fupi ya maisha yangu ili wanajamii wapate picha kamili.
Mimi nilikuwa nikiishi bongo na jamaa mmoja tulikuwa tunapendana sana tu, wote tulikuwa ni waajiriwa, tuliishi pamoja kwa miaka 5 na tulibahatika kupata mtoto mmoja wa kike, hatukuwahi kufunga ndoa tatizo lilikuwa dini - mwenzangu ni mwislam na mimi ni mkristo. Sisi tulikubaliana kufunga ndoa bomani wazazi wangu hawakuwa na tatizo kabisa kwa hilo, ila kwa upande wa mwenzangu wazazi wake ndio ilikuwa issue hawakutaka hata kusikia kitu kama hicho. Waligoma kabisa na kutishia kutohudhuria kama tukiendelea na uamuzi wetu huo wao walichotaka ni mimi kubadirisha dini ili niwe mwislam na mimi nikitu ambacho sikuwa tayari na hata wazazi wangu hawakuwa tayari kwa hilo.
Tatizo kubwa ilikuwa kila ifikapo mwezi wa Ramadhani wazazi wanakuja juu kwanini mimi sibadiri dini? kama siwezi kubadiri dini basi hapo hakuna mapenzi inamaana mimi simpendi kama kweli nampenda ningekubari kubadiri dini, kwa imani yao nikuwa mimi siwezi kumpikia futari ni dhambi mimi ni (khafir).
Mtihani wa kwanza siku moja wakaja nyumbani jioni ile tumerudi tu kutoka kazini wakasema wana mazungumzo basi wala sikusita kuwasikiliza he! wakaanza kwa kuniambia kuwa wao wamepata mtaalam(sangoma) wamemueleza matatizo yetu na yeye kawambia kuwa hilo mbona sio tatizo kubwa kazi yake ni ndogo sana ni kuwaroga tu hao. Kinachotakiwa ni mimi kwenda huko nikapewe dawa na maelekezo ili nikawawekee kwenye chakula na kuna nyingine niweke kwenye maji ya kunywa niwape Nikifanya hivyo tu basi tena wao wenyewe watanifuata na kuniambia wao wako radhi mimi kubadiri dini nilisikia mpaka mwili unanicheza kwa hofu na sikuamini kama niwao wananieleza kitu kama hicho.
Nilitikisa kichwa na kusema hapana siwezi. Kilichoniudhi zaidi ni mwenzangu nae akawa upande wao sio siri siku hiyo hata chakula sikula na hata usingizi sikupata.
Kweli nilichanganyikiwa halafu mimi tatizo langu ni msiri sana sikuwa na mtu wa kuongea nae hata kuomba ushauri,ila nikaanza kuwa na wasiwasi sio siri nikajua huko tuendako mambo sio shwari hatuta fika mbali. Nikapata wazo la kutafuta scholarship ili niweze kuondoka na kama ikiwezekana bora tutengane lakini tukiwa pamoja ni ngumu yeye alikuwa ananipenda na mimi nampenda labda nikiwa mbali itanisaidia.
Bahati nzuri nikafanikiwa nikapata chuo na yeye alichangia sana,nilipofika tu huku nikaingia chuoni na mbio za kutafuta makaratasi zikaanza napo bahati nzuri nikapata mtu akanisaidia nilipomaliza chuo na makaratsi nayo nikapata lakini huyo jamaa alikuwa ni kwa makaratasi tuu sikuwa na uhusiano nae mwingine.
Nikiwa chuoni nikampata jamaa mmoja tukaanza urafiki mwaka 2000 yeye kipindi hicho alikuwa single baada ya kuachana na mke na girlfriend wake. Baada ya kuwa marafiki kwa mwaka mmoja tukaamua kuishi pamoja ni mtu mzuri mwenye kujali sana familia yake yeye ana mtoto mmoja alizaa na mke wake wa ndoa na huyo mtoto ndio alisababisha yeye huyu jamaa kuachana na huyo girlfriend wake alikataa kuishi na mtoto wa huyu bwana na huyo mtoto kipindi hicho mama yake alikuwa na hari mbaya kiafya alikuwa kaathirika na madawa ya kulevya na ulevi wa kupindukia sasa huyu bwana alipoona yule mwanamke kakataa kabisa wakagombana sana na huyu bwana akaamua kuachana nae, ila bahati mbaya kipindi hicho yule mwanamke alikuwa mjamzito miezi 4 mwanaume akamuacha na mwanamke alipoona hivyo akaitoa ile mimba na walikuwa ni chui na paka anyway zaidi wanayajua wao.
Mimi na huyu bwana tumebahatika kupata watoto 2 mmoja wa kike na mmoja wa kiume nampenda sana na yeye ananipenda kusema ukweli ni mtu anaejua kupenda na kuiweka familia yake kwanza anawapenda sana watoto wake sana, jumla tunawatoto 4 hapa nyumbani 2 tuliozaa pamoja na mmoja aliyezaa na mkewe na mimi niliyezaa na mmbongo mwenzangu wote tunakaa nao kwa furaha na upendo.
Mimi nilimchukua mtoto wangu '03 na yeye tukamchukua wake mwaka huohuo wote walikuwa na miaka 6 baada tu ya kumchukua mtoto wangu niporudi tu huku nikamuandikia barua baba yake kuwa mimi na yeye ndio basi japo ilikuwa ngumu sana lakini sikuwa na jinsi.
Mtihani wa pili, huyu bwana tunakaribia miaka 8 tuko pamoja sio mtanzania lakini anaipenda sana Tanzania tumejenga nyumba pamoja huko nyumbani na kila kitu tumekuwa tunafanya pamoja na na kama ni mpango wa Mungu basi tunatarajia kufunga ndoa mwezi wa 7 huko nyumbani baada ya kumaliza ujenzi wa nyumba yetu kinachofuatia ni ndoa na maadalizi yote tayari tunasubiri tu watoto wapate summer holiday.
Sasa hapa ndio kuna tatizo mwenzangu simuelewi kwa sasa namuona ameanza mchezo mchafu mwanzo kabla ya xmas ya mwaka'07 kuna simu alipokea tukiwa mezani tunakula hiyo simu ni ya mdogo wake na yule girlfriend alieachana nae akamwambia eti yule mwanamke ana breast cancer he! alishtuka sana na alibadirika baadae akasema sasa anamwambia yeye ili iweje wakati hana mawasiliano nae?
basi tukawa tunamshangaa, haya tangu hapo kila mara ni simu mwisho mimi nikamuuliza mna biashara gani na hawa watu mbona sasa uko nao close namna hiyo? akaniambia kuwa huyu mdogo wa yule mwanamke wao ni wa Ghana anashida. Kwanza alimwambia eti aende nae huko kwao wakafunge ndoa ili apate makaratasi awalete watoto wake huku, huyu jamaa akakataa akamjibu kuwa yeye ana girlfriend wake na watoto na tunamipango ya kufunga ndoa siwezi kufanya kitu kama hicho,haya mimi nikakubari.
Basi ni msg. ni simu kila siku sasa hapo nikaanza kuwa na wasiwasi siku moja tena kama miezi 2 imepita tumekaa tunaongea akampigia simu eti anamuomba huyu jamaa yangu akamchukue nyumbani kwake ampeleke nyumbani kwa dada yake ambe ndio xgirfriend wa huyu yeye ana mtoto mdogo hawezi kusumbuka na train. Huyu akamkatalia akamwambia hawezi atakuwa kazini na akirudi anawapeleka watoto kutembea.
Sasa mwenzangu siku hizi hata simu yake huioni kutwa iko kiunoni na juzi kama wiki 2 zimepita alipigiwa simu shuleni mtoto aliumia aende kumchukua basi alikurupuka na simu hakuikumbuka akaisahau hapo na mimi ndio nikasema hebu nione kulikoni humu? Nimekuta msg. hizo sikuamini macho yangu alizozituma huyu kwenda kwa yule mwanake walieachana kwa kashfa na ugomvi mkubwa.
Kifupi nikawamba wamerudiana inavyoelekea kwa sababu kuna msg. huyu kamwambia j'pili niko off kama unakazi yeyote au unashida ya kitu chochote niambie nitafanya halafu kuna nyingine kamwambia angalia usifanye kazi sana kama unashida ya kitu chochote niambie ntakusaidia niwezavyo halafu akamuwekea kiss nyingi na hug.
Na yule nae anamwambia uko wapi saa hizi? utakuja? miss you a lot na hug na kiss nyingi ni mengi mengine hata siwezi kuyaweka hapa yananiumiza roho.
Sasa jamani niambieni juzi tu nimekuta condom moja kwenye wallet yake hapa kweli kuna usalama jamani? Mimi tangu hiyo juzi nimechanganyikiwa sana sielewi cha kufanya na wala sijamuuliza nilichokifanya ni msg. zote nimezii forward kwenye simu yangu na ile condom nimeichukua sasa kinachonifanya nisimuulize ni j'3 kuna conterner tunatarajia kulisafirisha la vitu vya nyumba yetu mpya naona kama nikimuuliza nitaharibu kila kitu na kwa jinsi nilivyo changanyikiwa kwa sasa hiyo j'3 naiona kama mwaka fikiria nguo za harusi ziko tayari kabatini ,pete,booking tayari yaani nikila kitu kiko tayari sasa nifanyeje jamani?
Sijamwambia hata ndugu yangu mmoja lakini nimechanganyikiwa. Jamani nawaomba mnipe ushauri sio kunishambulia na maneno kama unaona nimechemsha basi bora usichangie maana tayari nimechanganyikiwa msinizidishie naweza kufanya maamuzi yasiyo na maana nikajutia baadae.
Kibaya zaidi anawapenda sana watoto na wao wanampenda sana habagui, nikisema niondoke huu mji niende sehemu nyingine napo kazi nayoifanya ni nzuri nikihama huu mji sio rahisi kupata kazi kama hii na nimeajiriwa tangu 2005.
Pili ni watoto naona watanisumbua sana yaani sielewi cha kufanya naomba msaada please!!!
mdau Stella.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 99 mpaka sasa

  1. Cha kufanya huna ila wewe mchune to the maximum na wekeza bongo then ukiona mapenzi yamekufa mpige kibuti uangalie maisha yanavyoenda.

    ReplyDelete
  2. Stella,
    In short ulikuwa huoni kwa mapenzi yaliyokufunika.
    Huyu bwanapamoja na kuwa anakupenda inaonesha ni mkware tangu day one mlipokutana, na huenda anao mabibi zaidi ya huyo.
    Pili, inawezekana mapenzi anayokupa wewe pamoja na watoto yalizidishwa zaidi na wewe kutokumuingilia katika anga zake pasi na wewe kujua.
    Sasa basi, ukitaka kuona kama kama pundamilia ana rangi mbili basi anza kumkoromea.
    Mkalishe chini mweleze kuwa umeshafahamu yote yanayoendelea sasa kama ana lake jambo utaliona.
    Jitayarishe kwa lolote, yaani kupatana au kugombana.

    ReplyDelete
  3. Mdau stella pole sana i can imagine how seriousy the issue is.
    swali langu kwako ni kwamba je unaweza kuishi bila yeye?
    kama ndio kaana nae chini mwambie umejua kila kitu na akupe msimamo wake kama hakieleweki acha nae maisha yanawezekana bila yeye.
    kwa swali hilo kama jibu ni huweze kuishi bila yeye inawezekana ulijisahau mama ongeza mapenzi unajua mwanaume nae ni mtu anaweza kuwa alighafirika kidogo msamehe na muendelee na mapenzi ila cha muhimu ni kumbana maana akiendelea na mawasiliano nae ataweza kuendela nae ukichukulia walisha kuwa ni wapenzi.
    kwa upande mwingine inawezekana jamaa anataka kumfariji mama wa mtoto wake kwakuwa anajua anasiku chahe za kuishi na sikama anamapenzi ya kuzidi.
    La mwisho mshirikishe mungu kwa kipindi hiki maana sisi tunapanga lakini mungu nae huwa na mipango yake inawezekana yeye anajua zaidi
    dau

    ReplyDelete
  4. Ishii! Kweli manabii walisema, wenye macho hawataona na wenye masikio hawatasikia. Mtenda nae hutendwa, ulimtosa kaka yetu huku bongo sasa zamu yako. Ila kwa ushauri, tuliza mzuka hiyo mali isafiri kwanza, maana unaweza kulitibua. Ila na wewe ni soo! mchaga nini? lakini hizo r kwenye l zinakataa sio mchaga. Vipi mlishapimaa?! i mean urefu, uzito n.k si unajua tena hali si shwari

    Mdau Kiwoso ko Nkindi

    ReplyDelete
  5. pole sana dada stella kwa yaliyokukuta. hakika hilo laweza mtokea mwanamke yeyote. usitangulize hasira wala panic. tenga muda mkae muongee kuwa ana mpango gani na wewe. kuwa tayari kusikia lolote kutoka kwake. kua imara wala usiogope. maisha wakati mwingine ni tricky sana. all the best.

    ReplyDelete
  6. Kwanza Pole sana dada yangu.Wewe ni mwanamke mwenye heshima na unastahiri heshima.Kumbuka Bwana yako sio Mbogo hapo kuna tofauti ya mila au?always kutakuwa na matatizo.Pili huyu Bwana hana feelings na wewe kabisa,hawezi kukufanyia hivyo kama kweli anakupenda.Tamaa zimemjaa!!Wewe usihame nchi utawachanganya watoto,fanya kazi yako kwani ndio mume wako wa sasa,umeelewa?Ukihama inamaanisha unaogopa watu!watu sio wakuogopwa bali Muumba wetu.Muombe mwenyezi Mungu atakusaidia.Sikushauri kufunga ndoa nae kwani matatizo yatazidi na utashangaa mwenyewe.Kumbuka unapoamua kufunga ndoa ni kama kifungo umeingia na hautatoka mpaka siku ya kufa.Lea watoto wako huyo mume akitaka kuondoka mwache aende zake,ila kama unataka kukaa nae,tafuta siku nendeni Dinner mkae na umweleze jinsi anavyo ku kuaibisha.Mwambie yeye sio mtoto anaresponsibilities,watu tuna kua haturudii utoto.

    ReplyDelete
  7. pole sana dada

    ReplyDelete
  8. sioni kwanini unajali macontainer na material things more than urself. maisha yako huyajali? ni heri ulale chini na ukirudi bongo ushukie kwa guestroom lakini uwe na raha rohoni....akikuletea ukimwi hiyo nyumba utaikaa tena?

    unasema anawapenda watoto etc etc.....wewe je hujali kama anakupenda au lah? or that is not important to u? kama ni watoto wake atawaona hata kama hamuishi pamoja.

    first love urself ....hivi inaonyesha hujipendi. kwani lazima uhame mji? si utafute nyumba uhame and keep the same job. huyo hakupendi tena...hiyo simu yake kama walishaachana na nyie mmekua pamoja miaka nane waliipata wapi tena?.......

    hivyo anakula yupi....the ex girlfriend mwenye cancer au mdogo wake?

    mhhhhh pole and goodluck uamuzi wa mwisho ni wako

    ReplyDelete
  9. Pole sana dada but I guess that is life na inabidi ulikabili hili ukiwa umetulia akili. Usifanya papara. Mie naona kwana utliza kichwa then talk to him when calm and discuss the way forward. Hamna haja ya kuhama mji, if it doesnt work then life moves on. utahama mara ngapi? Here is an extract from a circualting email to give you comfort and courage "God doesn't give you the people you want, He gives you the people you NEED – To help you, to hurt you, to leave you, to love you and to make you into the person you were meant to be." All the best dear.

    ReplyDelete
  10. My Dia Stella,

    You have to tell him what you have discovered. Don't let the material things (container,wedding gown,rings, and wedding plans) to destroy your happiness.

    If you real love him monday is very far, and i know he can not stop the container bse the house wasnt for you but for his children.

    Remember, MFICHA MARADHI KILIO KITAMFICHUA.

    ReplyDelete
  11. andrew,
    dada pole sana kwa yote yanayokupata, lakini elewa kuwa what goes around comes around. japokuwa hutopenda kuelezwa wapi uliteleza unataka kujua wapi pa kurekebisha, elewa bado utakuwa hutibu ila unafunika kwa muda tu.kipindupindu (colera) huwa hatibiwi mgonjwa tu, bali hata mazingira anayoishi mgonjwa nayo hutibiwa pia. dada kumbuka kuwa hapo zamani ulimtosa mtu huko nyumbani ambaye hata hujatuelezea umemuumiza kiasi gani, kisa ni dini. mm nnavyoelewa mapenzi ni sacrifice, kama unavyosema ni kweli ww ulimpenda basi ungesacrifice, kwani kubadili dini kwa mtu unayempenda hiyo ni sacrifice tosha kumthibitishia upendo wako. lakini kwa sababu hukuwa na upendo wa kweli hukujali kumtosa. hilo pekee linaonyesa upendo wako ni wa kinafik, sasa leo umekutana na kiumbe anayejua kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, ukdhani umepata kumbe umepatikana. penzi la jamaa litakutesa maisha yako yote, huo ni mwanzo tu mamaa subiri picha kamili. umelizowa jitu la ghana sijui hilo, halina hata ubinaadam wala hajui mila zenu za kibongo, endelea tu kuparamia mijitu hujui hata asli yao hio ndio faida yake.
    rudi kapige magoti kwa baasha wako wa zamani ndio mambo yataenda mswano.

    ReplyDelete
  12. Kwanza dada pole sana, ila wanaume ndivyo walivyo wanakudanyanya siku ya kwanza vizuri na wanakuwa na maneno matamu, but ulitakiwa ujiulize mke wa kwanza wameacha, wa pili wameachana na kakupa visababu tu, wewe ukakubali tu sasa yamekurudi kuwa na wale wa kwanza nao hawakuwa na makosa huyo baba aliyokueleza wewe, sasa basi hiyo ndoa usifunge nae kwasababu tabia ishaanza kujionyesha, pia mkalishe chini umweleze kuwa umeyagundua yote hayo. umsikilize atasemaje?? wanaume wote ndivyo walivyo na hawabadiliki hata arudi yesu ngoooo

    Mimi ningekuwa mungu wanaume wote ningewapa adhabu kubwa sana

    Ni mkereketwa na wanaume

    dada zenjiiiiiii

    ReplyDelete
  13. STELLA kama wewe ni MKRISTO JUA sULUHUSHO LA MAMBO HAYO NI yesu Mmombe Mungu kwani hakuna lisilowezekana kwake.SuLUHISHO SI kalumanzira.Hakuna haja ya Kumchuna Mtu kwani adhabu /Garama zake ni kubwa mwisho wake angalie usiendekeze Mali ukasahau kuwa mapenzi na maongezi kwa mumeo ndio suluhisho kubwa.
    INAONESHA umepunguza mapenzi kwa mumeo kwani dawa ya mapenzi ni kupenda Kaenichini mjadiliusihofie kupoteza Konntena yashinde majaribu
    kwani inaonekana hujui kama kuna raha na karara ktk mapenzi kama unnavyo kerwa na mpenzi wako ndivyo naye anakerwa na ww huenda naye anafikiria jinsi ya kuto safririsha hilo kontena na vifaa vingine hivyo omba mungu uyashinde majaribu

    ReplyDelete
  14. NAFIKIRI FIKIRIA MAISHA YAKO NA FAMILIA YAKO MBELE KWANZAA LAKINI HAPO HUNA MME,JITAYARISHE KWA KUJENGA MAISHA YAKO YA BAADAE KAMA KUWEKEZA KWENU,KUWA NA MALI ILI LOLOTE LIKITOKEA UWE TAYARI UNA KITU,MAANA LOLOTE LAWEZA KUTOKEA

    ReplyDelete
  15. Stella Pole,
    Idea ya kukaa chini umweleza Hiyo j'3 ni nzuri,na usiwe mkali,muulize msimamo wake,HALAFU CHA MSINGI KUWA TAYARI KWA LOLOTE HALAFU MAKE SURE MAAMUZI UTAKAYOCHUKUA UWE UMESHAWEKA MAMBO YAKO SAWA BE IT UTAPRETEND KUWA NAE LAKINI UNA PLAN ZAKO.
    MAISHA YENEYEWE YAKO WAPI YA KUSONONEKA MY DEAR...!PILI USIACHE KUOMBA MUNGU AKUONGOZE ULIKO NI PAGUMU.

    ReplyDelete
  16. mimi ninavyoona endelea kumchunia tu ila mapenzi yale uliokuwa ukimpa punguza kidogo halafu jaribu kumrekebisha bila yy kujua kwanini unafanya hivyo mueleze maisha sio ngono?bila kusahau kuwekeza kwaajili ya watoto wako mama haio watoto ndio everything kwako japokuwa inauma sana you know what mydear ?all man wako hivyo hataukisema uachane nae utakutana na mungine ambae hata watoto hatawapenda as long huyo anaijali na kuipenda familia hayo mengine yanarekebishika tu dada usikate tamaa kuwa mjasiri mrekebishe watu huwa wanabadilika sikushauri uachane nae badilisha tu life style yako umbadilishe na taratibu za ndoa endelea nazo funga ndoa mama then you can fight for your love usikate tamaa ni shetani tu amempitia.
    take easy mydear kwenye maisha kuna milima na mabonde hiyo ndio milima komaa nayo usichoke.wishing you all the best.

    ReplyDelete
  17. Pole sana dada Stella,nakushauri usimwambie neno lolote kaa kimya..na wala suala la harusi usiliongelee tena hata kama nguo iko kabatini.....jikaze kiume dada yangu,mpe miezi kama miezi 3 hivi mchuneee mpaka last coin yake,malizia nyumba yako Bongo,nunua na mashamba huko Kibaha au Bagamoyo,ikiwezekana fungua na biashara bongo halafu beba watoto wako rudi nyumbani bongo uje ulee wanao na uondokane na stress....kama maisha ya unyumba dada yangu tayari umeshayaonja na unajua tamu yake na shubiri...achana nayo kwa sasa..Dada Stellah Mume mwema anatoka kwa Mungu...ni dhahiri kuwa hawa wanaume wote wawili hakuna aliye wa ubavu wako,usijitie kitanzi ukaishi kama mtumwa ndani ya nyumba yako eti kisa unataka kuvaa shela na kuimbiwa ana meremeta..utaletewa magonjwa ndani ya nyumba ufe mapema wakati watoto wako bado wanakuhitaji sana.Bongo kama umesoma vizuri utapata kazi nzuri tu tena inayolipa kuliko unayopata huko...nadhani wadau wataniunga mkono kwa hili.Pole sana huo hapo juu ni ushauri wangu kwako..Ila sasa kama mimi ndio ningekuwa wewe(If I were u)..with 42 yrs and 3 kids na maisha bora nisingeolewa tena..ningetia bidii katika kazi na kulea watoto wangu..mbona huku uswahilini kwetu wapo wadada wengi tu wanaishi vizuri tu na watoto wao..wanawazidi hata wale wanaoishi na wanaume ndani ofcourse 'regulator' anakuwepo japo si kwa wote!! its me makiromaro@yahoo.com

    ReplyDelete
  18. usiwe na haraka ngoja pelekeni kwanza hayo makontena bongo na kila kitu malizeni bongo mkishapeleka vitu vyote ndipo umkalishe chini!!!atakusikiliza tu!!!ila ukimwambia sasa hv lazima atakuwa jeuri wala usimwendee pupa sasa hv anaringa sababu anajua huna ujanja wowote wa kumuwekea jeuri!!!ila mkishamaliza kila kitu kukuacha ataona hasara pia nakusifu umecheza sana kumlengesha ainvest bongo maana mngejenga kwao angekutesa sana dada na kungekuwa hakuna jinsi ya kukusaidia so nakupa 5!!!!na uvute subira wala usihofu atatulia tu ukimweka chini!!!!

    ReplyDelete
  19. mh!! stori ya kizushi,,,
    sijui ila mapenzi hayang'ang'aniwi yan huwezi mganda mtu akikuchoka mwezangu.mwisho ufe na presha na wawafisadi wanao wapenzi,,
    SEMA NAE UMSIKIE MSIMAMO WAKE,yan akiamua kula kona thank god umepona,songa mbele na life lako kwanza u have gd job na bongo mwajenga sijajua hati ni both of you au yako?
    potelea mbali na mihela yenu yoote na mapenzi feki alonayo,
    duh pole sana kwa yule jamaa m-bongo mchawi yan yule hakukufaa kabisa alipoanza kuwa mchawi,ANYWAY KAMA ULIKUA HUJUI YAN KUNA DINI WANAAMINI MAJINI,UCHAWI,KUPUNGA MAPEPO nk yan kwao ni viumbe na kitu cha kawaida hahahahaaaa Mungu awaokoe na roho iyo!!so sad sana.
    KUNA MAFISADI NA WASANII WA MAPENZI WEE ASIKWAMBIE MTU,subiri jehanamu tu patakua hapatoshi

    ReplyDelete
  20. Dada stellah pole kwa misukosuko, najua inaumiza sana kuona mpenzi wako anakusaliti. Unaonekana imekuchanganya kwa kuwa mlipendana sana na uliamini hawezi kufanya jambo kama hilo, mimi kwa mtazamo wangu huyo bwana anakupenda bado na anajali pia pamoja na na hiyo condom uliyoikuta mfukoni kwake. cha kufanya wewe kumbuka kuwa umri umekwenda na kukaa kubadilisha badilisha wanaume utajapata wa ovyo kuliko, wewe angalia heshima yako kwanza anakujali na anakupenda na kukuheshimu, ikiwa katika hayo matatu hayapo waweza, ukafikiria kitu chengine, kama hayo matatu yapo we kaza buti tena mpe hahaba motomoto ili uweze kumrudisha habibi wako , mimi ulivyoelezea kuwa anapenda watoto wote hata wa kwako sawa nimepata picha huyo mume ni mzuri sana na anamoyo wa imani, wanaume wengi hilo huwasumbua kidogo na kuweka kaubaguzi, zaidi mmeshakaa nae na kuwa na malengo pamoja kiasi mmeshajenga na mnatarajia kufunga ndoa we kaza buti,Hata mama zetu walipitia mapito hayohayo, si jambo geni wala lisikupe pressure ukachanganyikiwa we poa moto fanya kama hujui kinachoendelea.

    ReplyDelete
  21. pole sana cha muhimu wewe kua mkweli kama muonyeshe yote anayoyafanya unayajua amue moja usipende kua mtumwa wa mapenzi wanaume ni wasumbufu mno jiandae kwa chochote kile anaweza akatulia au akachomoa itakua salma kwako.mpz hayana shule kila mtu angesoma na kufaulu usikate tamaa.utashinda usijionyeshe mnyonge kwa hilo.mamy.

    ReplyDelete
  22. hallo Stella...........
    Ebu chukulia mlikuwa mmeshafunga ndoa then ndio ukazifuma hizo sms. what culd u du?? ungedai talaka?? Tayari huyo ni mume wako (miaka 8 unaishi nae bila ndoa) na umezaa nae watoto 2, i think the best way ni kukaa nae na kumueleza. kwani ndoa ni nn?? kinachoonekana nyie ni kwenda kubariki tu, nyie mmekaa miaka 8 wakati kuna ndoa zinafungwa leo after 2 weeks zimevunjika!!
    -----------Yote kwa yote muathirika mkubwa hapa ni wewe.

    MJ, dar

    ReplyDelete
  23. Pole dada yangu ingawa na shaka na maelezo yako,unajua mapenzi yana hadithi nyingi, inawezekana kweli huyo jamaa si sahihi kwako au la kuna kitu umemfanyia ambacho kimembadili kabisa,la msingi kabla haujafanya maamuzi hakikisha hukuwahi kumfanyia kitu kibaya,pia la msingi kwamba inawezekana na wewe ulikuwa still unawasiliana a mtu mwingine bongo akakustukia so na yeye anajihami,ila kwa ushauri kwa umri uliofikia si lazima ume na munkari wa kuolewa angalia maisha yako na mtoto wako,kama kuolewa hata baadae utaolewa za kiutu uzima,ondoa hizo ndoto kama anakupenda kushakuwa na dosari......pole kwa yote.

    ReplyDelete
  24. Mambo mawili. Nashauri ukiandika andika kwa kifupi vinginevyo inakuwa vigumu mtu kusoma ujumbe wote. Halafu nimeona kuwa wazazi wake walikutaka "ubadiri" dini sijaelewa walikuwa na maana gani ila nafikiri kwa kuwa wewe si mwislamu wanaweza kuwa walikutaka ubadili dini.

    ReplyDelete
  25. pole sana mpenzi ila usijali wanaume ndivyo walivyo ndugu yangu, ila cha kufanya SAFIRISHA KWAMZA CONTENA LA MIZIGO SHOGA ANGU LOL! si bora umekuta msg kuna siku ungewakuta kitandani kwako, kwa hiyo akufukuzae hakuambii toka, ni vimbwanga tu mwenyewe mpaka uchoke kwa hiyo ww kula na kipofu,

    ReplyDelete
  26. Stella, pole sana! Ulimkosea sana kaka yetu wa Kibongo. Umekiri mwenyewe kuwa alikuwa akikupenda. Kama wazazi wake walikupa dawa kuwawekea wazazi wako--hilo halikuwa jambo la maana kutekeleza--ulifanya vizuri kukataa. Hata hivyo, ni ukweli ulio wazi kwamba yeye bwanako hakukukosea kitu chochote. Hakuwahi kukulazimisha kubadili dini, hakuwahi kukupiga ili ubadili dini na wala hakuwahi kukutukana kwa msimamo wako. Kama kweli wewe ulikuwa unampenda kama alivyokupenda yeye, usingechukua hatua ulizochukua za kumkibia, tena baada ya yeye mwenyewe kukusaidia akijua mwenzi wake umepata shule unakwenda kuongeza elimu ili mje kuishi maisha bora zaidi. Masikini, alifanya hivyo bila kujua ajenda yako moyoni! Baada ya hatua uliyoichukua wewe (ya kumtosa), hivi unafahamu ni kwa kiwango gani aliumia? Kwa mapenzi aliyokuwa nayo na namna alivyokusaidia kwenda Ulaya--unajua alivyoumia kwa kukukosa wewe? Mwenyezi Mungu siku hizi hakopeshi wala halazi damu--yanayokupata sasa ndio malipo yako yanayostahili--huna akili--AMUA UNALOWEZA!!

    ReplyDelete
  27. Stella,

    Reading from all these messages the following seems to be the message to you!
    Talk to this guy
    Materials are not important thean peace in your heart
    Dont leave your job
    He is already your husband after 8 yrs
    You discussion with this guy will determine your next course of action.
    Good luck

    ReplyDelete
  28. Pole sana dadaa!!
    Cha kufanya kwanza hakikisha konetena lako limekwea meli,then umpe ukweli.Nasema hivi kwa sababu kama kuumia roho tayari umeshaumia so sio ukose kila kitu,ukose mapenzi na mali tena ukose?no itakuwa ngumu kukosa vyote.
    tulia vumilia then mambo yakishakaa sawa unamwabia,majibu yake ndio utayafanyia kazi.Lakini sioni kama atajaacha manke watu wanojifanyaga wana mapenzi motomoto ni vimeo kweli,kwa kuwa huwa huwezi kuwashtukia kiurahisi.So akili kwa kichwa dadaa!!
    Elibariki

    ReplyDelete
  29. Da Stella
    Unatafuta kisingizio cha kumpiga kibuti jamaa baada ya kuona tayari ameshajenga na container tayari ziko njia moja?
    usitafute Sympathy huku una lako moyoni stella!
    Jamaa awe hakupendi halafu ainvest Tanzania badala ya kwao?
    Fikiri mara mbili shost!!!!!

    ReplyDelete
  30. wamama wengi wa kitanzania wanaumwa presha na visukari sababu ya matatizo ya ndoa waliyonayo na kuweka mambo mengi rohoni,dada wewe ni mkristo na unajua ndoa ya mkristo mume m1 mke m1 mpaka kufa kama uyo bwana anakuzingua we safirisha kontena likifika bongo ndo umuanzishie,mwambie ukweli bwana usije patwa na maradhi bure ukaacha watot wako wanateseka.

    ReplyDelete
  31. Dada yangu pole sana. kwanza coz upo njia panda,una watoto 3, unafanya kazi nzuri ,unaishi ulaya na pia kwa mujibu wa umri wako ni mtu mzima tayari. mapenzi yanakuja na kuondoka mwambie huyo jamaa kuwa unafahamu kila kitu anachokifanya so aamue kuwa na wewe ama arudiane na huyo mdada mwingine, najua atabisha kama kawaida yetu wanaume lakini muonyeshe kila ushahidi kuonesha kuwa unafamu anachofanya. Lakini Dada yangu usiwe na wivu kupindukia mpaka kusachi na kupekuwa vitu vya mumeo na hivyo ndiyo vinakufanya usiwe na amani moyoni sasa. anyway POLE sana......

    ReplyDelete
  32. POLE SANA DADA STELA HAYO NI MAMBO YA KAWAIDA ASIKUDANGANYE UKAMUACHA MUME WAKO.KUTOKANA NA MAELEZO YAKO HUYO KAKA ANAKUPENDA NA KUKUJALI PAMOJA NA UKWARE WAKE.WANAUME NDIVYO WALIVYO UNAWEZA USEME UACHANE NAE UKAPATA BALAA ZAIDI YAKE.WEWE MUELEZE KWA UTARATIBU KUWA UNAJUA KINACHO ENDELELEA LAKINI USIMKOROMEE WANAUME WANAPENDA WANAWAKE WAKUWAELEKEZA KWA UKARIMU KAMA WATOTO NASIO KWA UKALI.USIJALI HAYO NI MAISHA.ILA KAMA KWELI UNAMPENDA UNAITAJI KUISHI NAE ACHA KUMCHUNGUZA WEWE AMINI ANAKUPENDA NA WEWE NI ZAIDI BWANA KUWA NAMWANA MKE SIO SABABU CHA MAANA UPENDO.

    ReplyDelete
  33. Pole sana dada yangu nimeguswa na ishu yako, tatizo hapa hujaweka e-mail yako kuna mambo ya msingi nilitaka tuwasiliane kiutu uzima nawewe ili usijisikie upo matatizoni tena. kama vipi e-mail yangu hii hapa fredsimon65@yahoo.com.

    MLEZI WA WAMAMA

    ReplyDelete
  34. Stella, pole sana. Hakuna mtu asiye na mapungufu. Ni kitu cha kukaa na kuongea. Mambo kama hayo kwa wanaume wa kiafrica ni mengi sana. kuhama sio solution ya jambo lako. Kwa sababu una wasi wasi na container kuondoka wewe vumilia likiondokatu mwambie usiweke mambo rohoni utaumia sana. Ongea nae kwa upole. dont panic coz you might loose everything. Kama kweli unampenda atakusikiliza na he will realize what he is doing is wrong. Mimi ni mwanamke kama wewe na niko kwenye ndoa. I know how it hates. Ila sikushauri kuondoka. dont do something stupid. People will laugh at you. Muweke Mungu mbele usichanganyikiwe sana.

    ReplyDelete
  35. Dada yangu; kwa faida yako na kukusaidia kwa sababu umenigusa na mkasa wako; i'll be honest with you..mimi ni mwanaume; nikimwangalia huyo mwanaume wako kwa jinsi ulivomuelezea naona anafanana sana na mimi. Mimi napenda sana ku-do na wanawake tofauti, ila napenda sana watoto,..sana. Pia nina moyo ambao sipendi kuona mtu mwingine anaumia au namuumiza mtu kwa namna yeyote;especially girls. Nina msichana wangu ambaye ninampenda sana ; sijamuoa ila tumezaa naye mtoto mmoja; ila nna watoto wengine wawili na wanawake wa nje; na wote nawaonyesha mapenzi ya hali ya juu; na hata hao wasichana wote nawaonyesha mapenzi sana kwa njia mbalimbali; sijui kama unanipata nachosema hapa? USHAURI WANGU: USIMUACHE HUYO MWANAUME ; WALA USIMUAMBIE KWA SASA; ENDELEA NAYE NA MFUNGE NDOA; HUYO MWANAUME SIYO MBAYA; TAFUTA TU NJIA ZA KUMDHIBITI MKISHA OANA,ATABADILIKA KWA KIASI KIKUBWA INGAWA SISEMI KAMA ATAACHA KABISA. La sivyo dadangu; utatatanga na wanaume mpaka unazeeka na hauta pata ambaye hatakutenda; wanaume tuko hivyo wote; huwa its a matter of time tu kabla hajafanya madudu, lakini ukiwa na busara yanapita mnasonga. Kama huajanipata vizuri na unahitaji maelezo zaidi nicheki thru thopaz@yahoo.com

    ReplyDelete
  36. Stella,pole dada yangu mimi nakushauri kitu kimoja hapo lazima umwambie jamaa ajue kuwa wewe unafahamu ili uone responde yake atafanya nini,maana hujui labda yeye anajua wewe hujui kitu ndio maana anafanya hivyo.
    swala la contena wewe safirisha kule nyumbani bwana utawekeza kitu....Ndoa hupangwa na mungu wewe muombe mola tu.
    Mdau Manchester,
    Uk.

    ReplyDelete
  37. Mdada wa miaka 43, wewe ni mama mwenye miaka 43, 'stop denying' the truth and trying to minimize the problems you have.

    Baada ya kukuweka sawa, ukweli ni kuwa maisha ni mafupi na wewe siyo msichana wa miaka 23. Hivyo basi masuala ya kuzunguka kwa 'kuhifadhi txt msg' siyo mazuri kabiliana na 'mzee' mwenzio kichwa-kichwa.

    Nina maana mweleze kwa njia isiyo ya ugomvi jinsi ulivyo umizwa na kadhia nzima. Pia mueleze jinsi wewe na yeye mtavyoweza kuishi kwa raha, kwa kuweka 'manifesto' ya chama chenu ili muweze kuishi kwa raha mustarehe kwa miaka 20 ijayo. masuala hayo lazima m-yajadili kama kwa uwazi kabisa. Nini hupendi na yeye nini hapendi.

    Mwisho lazima mtambue uhusiano wenu mliuanza ukuwa na masuala mengi mazito kwa kila mmoja alikuwa na wake wa mwanzoni na mlizaa nao. Pia Mama umekubali kuwa uliumia roho ulipomwambia mzazi mwenzio wa mwanzo asiwe na habari nawe. Je bado unampigia pigia simu kama ndio acha, pia bwana mzee kama nae alikuwa na tabia kama hizo aache.

    Mwisho nyie ni watu wazima masuala kuwa oh wazazi wanasema hivi au vile, kwa kweli mna-behave kama vijana wadogo. Nyie endeleeni na masuala ya ndoa/partneship yenu kama watu wazima na mkionyesha hivyo wazazi,ndugu na jamaa zenu wataacha kuwaingilia.

    ReplyDelete
  38. Pole dada Stella.
    Mimi nasema ndoa ifungwe kwa sababu kuu moja, shemeji anakupenda na kosa alilolifanya ni la kawaida kabisa ambalo mwanaume yeyote anaweza kulifanya na kuna wanaume wanatabia mbaya mpaka unaweza kutamini awepo mtu pembeni akusaidie. kutokana na maelezo yako kitu alichokosea ni kurudiana na x girl friend wake na mambo mengine ya maisha yanaenda kama kawaida mwambie ulichogundua na pia mwambie kuwa haupo tayri kumpoteza akaeakijua hilo na umwambie bila hasira. ni hayo tu ndugu yangu, kila la kheri.

    ReplyDelete
  39. Stella, mimi nina kazi nyingi sana nasoma nina project natakiwa ku submit hivi karibuni la sivyo ningalikuandikia mambo mengi na tungewasiliana na nina imani ningekuweka sawa kwa neema ya Yesu ungejipa moyo na kutulia tu ukimtazama Yesu. KWA UFUPI FAHAMU KWAMBA HUYU MWANAUME NI MDHAIFU, KAMA MWANADAMU. ALIZOEANA NA HUYO MWANAMKE WAKE NA NDIO MAANA WAMERUDIANA TENA SIKU NYINGI WANYE. AMESHINDWA NA UZALENDO MAANA ALIKUWA ANAMPENDA NI MAKOSA YAKE NDIYO YAMEMFANYA AMUACHE LAKINI ALIKUWA ANAMPENDA NA WALISHAZOEANA. USIJALI, FUNGA NDOA TU NA MWAMBIE YOTE KWAMBA UNASIKITISHWA SANA NA HALI HIYO ILA UNAMWACHIA MUNGU, MAANA NAONA UTAKAPOMWACHA HAITAKUSAIDIA TAYARI UMEZAA WATOTO NAYE TENA 2?, UTAANZA TENA WAPI? WANAUME WENGI NI HAWAKAI NA MWANAMKE MMOJA HILO UFAHAMU. NA KWA UPANDE WA CONDOM, SHUKURU ANATUMIA KWA USALAMA WAKO NA YEYE. NAOMBA NIKUPE EMAIL YANGU: ak_abduel@yahoo.com, simu yangu 255 713 689665.
    OMBA SANA MKABIDHI MUNGU SHIDA YAKO NA MUNGU ATAMBADILISHA HUYU MWANAUME TABIA YAKE YA KURUDI NYUMA KWA WATU ALIOCHANA NAO.
    ANNA - DAR

    ReplyDelete
  40. WANAUME WAAMINIFU NI WACHACHE SANA, HAO WANAOKWAMBIA ACHANA NAE WAULIZE KAMA NI WANAWAKE WANAUME WAO WAAMINIFU! UTAACHA WANGAPI, NAJE HAO WATOTO UNAWAFUNDISHA NINI? NA UTAZAA NA WANGAPI. TULIA JTATU MUULIZE TARATIBU USIPANDISHE, NA ONYESHA MAPENZI, ZIDISHA UWEZAVYO. NDOA NYINGI ALMOST 80% MATATIZO NDO HAYOHAYO USIOGOPE. NA KAZANA KUSALI, YESU NI JIBU. ILA KUACHANA NAE SIKUSHAURI.

    ReplyDelete
  41. Dear stella

    unajuwa kila kitu muongozi ni mungu sasa basi chamsingi mimi sikushauri usafirishe hilo kontena unalosema hila unachotakiwa kufanya saa hizi nenda kacheki afya yako kwanza then your suppose to tell huyo bwanaako ukijikuta una matatizo kwenye damu yako na yeye anayo.una uamuzi wako uendelee kuwa naye au lah! mkijikuta hamna wote kamrishe chini mueleze maovu yake anaweza kukusikiliza sio kukaa na mawazo muda wote huo utakufa bure na ww una watoto wadogo bado wanakutegemea.
    mdau ngatunga abd temeke.

    ReplyDelete
  42. Dada Pole sana,
    Wanaume ndivyo walivyo,tofauti ni vile tu umejua kuwa ana mahusiano, wengine hatujui wala usishangae sana, ukiangalia wewe ni mwanamke wa ngapi kwake, utaona ni wa tatu(wale aliokutajia tu) huwezi kujua hata yule wa kwanza alijiingiza kwenye madawa na pombe kwa sababu ya frustrations za huyo bwana! Na huyo girlfriend alimkataa awali kwa sababu aliona akiingia ndani mambo hayatakuwa shwari akatafuta kisingizio cha kumchukia mtoto.
    Una kazi nzuri sana, una warithi tayari(watoto)unaowapenda, una miaka 43 (senior mother)na sio mdada kama ulivyosema,ungekuwa na miaka kama 30 ukafanyiwa hivyo ungeweza kuchanganyikiwa zaidi.naamini kwa umri ulionao, biologicaly hata sexul desire inaenda ikipungua, unaweza kuishi mwenyewe dada!!
    Ushauri wangu... mweleze, muonyeshe na evidence za sms, akikukoromea achana naye, akikubali akakiri kuacha ishi naye bila ndoa, na kwa kondom dada, asikuue wakati wanao bado wadogo ndugu yangu.Kama kujitahidi kuishi katika ndoa umejitahidi vya kutosha, ila Mungu hajapenda... kubali!!!!

    ReplyDelete
  43. Hallo Dada Stella,
    Mimi kama mwanaume nakupa pole sana kwa yaliyokupata na kisha nakushauri ifuatavyo;kwa mwanaume mwenye mke/mpenzi kuwa na mwanamke nje si jambo jipya wala geni kabisa ktk dunia hii,na maisha yakaenda vizuri sana bila tatizo,kama maisha yako yalivyo. Tatizo huwa linakuja pale mke anapogundua mahusiano ya nje ya mumewe ndipo mambo yanapoanza kuharibika na hii inatokana na jinsi mke anavyolichukulia jambo hilo na kulihandle,akalihandle vibaya mambo yanaharibika,na wala sikutanii. Hebu jiulize pengine alikuwa na uhusiano naye kwa zaidi ya miaka 2 kabla huja gundua, je kuna nini kilipungua ktk maisha yenu ya kila siku ktk muda huo wote?Kama hakukuwa na tatizo lolote na maisha yalikuwa tambarare sasa kwa vile umegundua una wasiwasi gani? Je wasawasi wako ni kugundua kuwa ana mpenzi au kuwa mapenzi yamepungua? Kama mapenzi unayapata kama kawaida pamoja na kuwa ana huyo wa pembeni,tatizo ni nini. Wakati mwingine huyo wa nje kuna kitu ana complement kwa mumeo kwa kile ambacho kwako hakipatikani.Wakati mwingine ni tamaa tu japo upendo haujapotea. Kwa uzoefu wangu suala la kumuuliza ni njia shihi lakini linahitaji uangalifu mkubwa sana na halihitaji haraka wala papara kabisa tena usiwe very direct uwe very technical,wanaume ni very defensive na hawakubali kushindwa kiurahisi,hivyo usitegemee atakiri mara moja na kuomba msamaha kiurahisi,atafanya kila njia kukataa kitu ambacho wewe utachukulia kama hakupendi,kumbe sivyo bali kwa fikra zake anaona kukubali ni kukuumiza. Sasa ukitaka kulazimisha unavyotaka wewe mambo yameharibika. Kwa mwanaume mwenye busara na upendo akishagundua kuwa mke wake amegundua anachofanya,lazima atabadilika,lakini jua hawezi kumuacha mara moja hivyo itabidi ujipe muda uone mwelekeo ukoje.Ogopa sana mwanaume anayekubali haraka haraka makosa yake na kisha kusema nisamehe mke/mpenzi wangu, nimekosa nimeacha sitarudia tena,usisikilize maneno angalia matendo yake.Pia kama walivyosema waliotangulia usiache kumuomba Mungu kila mara na pia kama kuna mambo uliyapunguza kwa mmeo yarejeshe mara moja na kama kuna uwezekano usipende kuwa mbali naye kila mara, hasa kwenye muda ambao anakuwa hana shughuli yoyote. Fanya uchunguzi au udadisi ujue ratiba ya shughuli za mumeo na hakikisha kama kuna uwezekano muda ule ambao hana kazi yoyote unaiziba ipasavyo,akisha kosa free time ujue umeshinda,hakuna mwanamke atakayevumilia wiki nzima au 2 bila kuonana na mtu wake naye mwanaume ataanza kuokuwa na imani na huyo mwanamke wa nje,na kwa uhakika mahusiano hayachelewi kwisha ktk mazingira hayo bila hata ya kutumia hoja za nguvu au nguvu za hoja.Fahamu kuwa mwanaume akiwa na muda mwingi wa free na pesa anazo ni tatizo kubwa sana tamaa na vishawishi havitakosekana, hivyo kazi ya mwanamke ni kujaza hilo gap kwa namna yoyote ile.

    ReplyDelete
  44. My dear Stella,
    Pole kwa hali unayopitia, ni ngumu ila jipe moyo utapita tu japo kwa kuumia sana. Hapo ulipo watafute viongozi wa kiroho washirikishe hili swala ndiposa utajua nini cha kufanya. Ila pia kumbuka kuungama kwa makosa yote uloyafanya kipindi cha nyuma hasa kwa kumuumiza mpenzio wa kwanza.Jitie nguvu usizungumze chochote wala usimfanyie fujo mpaka utakapoongea na viongozi wa kiroho.Si vibaya ukapima afya yako.

    ReplyDelete
  45. Chanzo cha matatizo yote haya ni wewe binafsi. Ulishafanya makosa tangu mwanzo. Msimamo wako wa kutobadili dini ya Ukristo ulikuwa sahihi, ila tatizo hukuwa Mkristo wa kweli, uzinzi haumpendezi Mungu.

    Sasa fanya hivi, rudi kwa Mungu mwombe msamaha, tafuta mawasiliano ya yule rafiki wako wa kwanza muombe msamaha.

    Mgeukie Yesu kwani anaitwa MSHAURI WA AJABU atakuelekeza hatua zakuchukua.

    TAHADHARI: Mali isiwe sababu ya kumpenda mtu, kwani mali huja na kuondoka ila UPENDO wa kweli haubase kwenye mali.

    "No one is too poor, too sinful or too insignificant to be JESUS friend"

    NITAMWOMBA YESU KWA AJILI YAKO AKUPE NJIA NJEMA NA YA BARAKA YA KUTOKA KATIKA HILO.

    ReplyDelete
  46. Dada Stella,

    Kwanza nikupe pole kwa mtihani mgumu ulionao kwa sasa, ikizingatiwa umeishi na huyo "mgombea mwenza" wako kwa takriban miaka 5 sasa.

    Ushauri wangu ni kama ifuatavyo:

    1) Kuhusu suala la dini, upande wa mumeo wamekosea. Mimi ni Muislam. Waambie wasome Al Quran, Suratil Maidah, Aya ya Sita, kama watashindwa kuelewa kilichoandikwa mule, basi wamtafute mwanazuoni aliyebobea katika Elimu ya Dini ya Uislam, ndiye atakayewafafunilia. Lipi leo likufanye wewe kuwa khafir? Mbona wapo watu makini kama Ustaadh Yussuf Makamba, ambaye, kama sikosei, mkewe ni Mkristo? Mimi, kwa kupitia aya hii, nimeoa mke Mkristo, tena Masjid, na Imam akafungisha ndoa, watu wakaswali, na sunna wakala! Kwa hilo wamekosea, walipaswa kuwafungisheni ndoa ya halali miaka 5 iliyopita, si kuwaacha kuishi katika zinna! Wamekosea, wakatubu! Wasijifanye wanaijua dini ilhali hawajasoma kilichoandikwa kwenye Mashaf!

    2) Kuhusu matendo ya mumeo, mkalishe chini, mwambie aamue moja, kati ya wewe au huyo aliyekuwa mpenzi wake. Aseme kweli, mwambie unajua kila kitu. Wewe huenda rizki yako haiko kwake, ndio maana mpaka sasa hakuna kitu kinaitwa ndoa kati yenu. Achague moja, si lazima uolewe na yeye. Anayejua rizki ya mtu ni Mwenyezi Mungu peke yake. Mbona Khadija (A.S.) aliolewa na Mtume Muhammad (S.A.W.) wakati akiwa na umri mkubwa tu? Kwani kwenye ndoa ni maelewano, na mapenzi, na si lazima kuwe na watoto.

    Ni mimi, MwanaHaki!

    ReplyDelete
  47. Dada yangu stella, pole sana kwa yaliyokukuta, ila ninakushauri tuliza kichwa chako kwanza, kaa kimya mpka mambo yenu yote yaende kama mlivyopanga, kwa vile wewe una watoto na pia bado hujazeeka utakuwa unahitaji ile kitu hivyo si vyema kwa mtu mzima kama wewe kurukaruka ni fedhehema, hata sisi wengi wetu tupo ktk ndoa ama mahusiano tu ya kinyumba bali asikudanganye mtu kama hawa wanaume wametulia ng'o hata sikumoja, wooooote wanafanana na hata kama kuna wanawake amabao nao hajatulia lakini si kama hawa wavaaa suruali(Wanaume) yaaaani nisikufiche ni soooooo, wanandoa wengi ni mayoe tu kila kukicha usiwaone/usisikie watu wanapendana ukafikiri ni shwaaari bila matatizo hilo hakuna dada. Unachotakiwa ni kujikaza ndoa yako ipite then komaa nae atabadilika tuuu wangu!!!!!

    Mkereketwa na Wanaume wanafiki wa mapenzi

    ReplyDelete
  48. Kwa kweli mimi mgumu, lakini duu hapa mshipa umenishuka!!! jamani dada yetu ana matatizo si ubishi. Kwa kweli dada pole kwa masaibu yaliyokupata, kwa hali uliyonayo nahisi ni imani yako ya kweli juu ya Muumba wako ndio itakayokusaidia, mimi kwa imani yangu naamini kwamba sio kwamba Muumba anauwezo tu wa kuondoa jabali lililoziba njia lakini pia ana uwezo wa kuzisafisha nyoyo kutokana huzuni, wasiwasi, vilio, majonzi na mengineyo, hivyo muelekee Mola muweza wa kila kitu kwa shida yako.

    ReplyDelete
  49. Pole sana Dada yangu.
    Inaumiza sana unapompa mtu moyo wako wote then yeye anauchezea.
    Dada Stella handle hili tatizo kana kwamba mlishafunga ndoa for the sake of watoto wako, tulia kaa nae ongea nae kwa utaratibu bila kuonyesha hasira yeyote bt akionekana pia ameshaamishia mapenzi kwa xgirl wake dada jaribu kuanza kufix maisha yako bila yake, inaweza kuwa ngumu sana na inaweza hitaji mda sana kustabilize bt usijali maisha si barabara iliyonyooka.
    Usijilaumu kwa yeyote uliyofanya nyuma bt yatumie kama tool kunyoosha maisha yako.
    Pole sana Dada kwa yote yaliyokupata ila usijali challenges zipo ile tulearn through it.

    ReplyDelete
  50. Mimi siwezi kukulaumu hata kidogo kwa kumuacha huyu mbongo na kwenda kuishi na huyo.
    Iliwahi kunitokea pia wala dini haikuwa sabb bt mimi kuonekana maskini ndilo lilikuwa tatizo bad enough mtoto akaungana na wazazi na kuoa mwanamke mwingine na kuniacha mi na mtoto so to u my dia hiyo ya kutaka uende kwa waganga na mume wako kusupport bila kujali penzi lenu ilitosheleza sana kuondoka sabb hakukuwa na future iliyoonekana kabisa.
    Ongea na huyo mwanaume rafiki na muamini Mungu mwombe atende sabb teyari huyo ni mume wako kwa hiyo miaka nane mliyoishi pamoja. usisolve hiyo tatizo kiasira tumia busara zaidi hapo. kuwa mbali na watoto ama mzazi wa watoto wako si rahisi. ila ukiona umeshindwa kabisaa kila njia na kuachana ndio suluhu sawa waweza kuachana lakibni hakikisha una uhakika na kuachana.

    ReplyDelete
  51. Mmmh Dada Mkuu Stella kwa mtu ambae ni msiri kama unavyodai kwa kweli unajua kusema maana nimesoma mpaka macho yananiuma. Hivi mimi naomba kukuuliza tu kaswali kadogo, Yaani wewe na na hiyo miaka yako yoote 43 huwezi kuchukua maamuzi ya nafsi yako mwenyewe na kufikiria maisha ya mbeleni na watoto wako mpaka uje kutuandikia kitabu humu bloguni ? Mimi naona wewe unatuyeyusha tuu ? Ama kweli age aint nothing but a number na kweli kusoma sio ujanja .Nimeamini mtu unaweza ukawa mtu mzima na madegree kibao lakini kichwani ziro kabisa ! Mimi naona ushauri wangu ni kwamba Hapa ukerewe kuna ma"shrink" hebu nenda NHS wakulipie uwe unaona shrink kwa wiki mara moja sijui tano labda atakusaidia gradually kukutia mawazo yanayokufaa kichwani...! Kwa Ufupi ni kwamba mama hayo ni mashauri ya kujichukulia wewe binafsi kwani wewe ndio unaeshuhudia hayo mambo na unaishi hayo maisha ! You have choices so use them wisely! Watu wengine bwana hivi mnatafuta ushauri kweli au ndio mnataka waosha vinywa tuwape live bin ukweli then kaka Michuzi awaonee huruma abanie comment zetu zisione mwanga wa jua ? CHAGUA BEGA DADA HUO NDIO UKUBWA AND THATS LIFE SO MAKE YOUR OWN CHOICEs and DEAL with IT! Cha msingi tuu kumbuka wewe una WATOTO na kwa hawa watoto your peace of minda nad your HAPINEss is what will make them to grow up and be strong and REsponsible people in the Society. You as their mother is the Root of their LIVEs so think of that and DECIDE ! .........Unaona sasa umenifanya na mimi niandike gazeti aaah watu wengine bwana ......

    ReplyDelete
  52. Pole sana Stella,
    SHAMBA HULIMWA, KUPANDWA MAZAO NA WATU HUFURAHIA SANA WAKATI WA KUVUNA NA MSIMU HUANZA MWANZO. KWAKO STELLA ULISHALIMA SHAMBA, UMEVUNA NA KUFURAHIA MATUNDA YA MAZAO YAKO. HUYO BWANA NI SAWA NA SHAMBA, FIKIRIA LINGEKUWA NI SHAMBA LAKO USINGELIMA? MIAKA 8 YA KUISHI NA KUZAA TAYARI HILO NI SHMBA LAKO HIVYO HUNA BUDI KULIMA, KUSAFISHA NA UVUNE. SIONI SABABU YA WEWE KUKATAA NDOA. FORGET ABOUT PAST KWAMBA ALIISHI NA MWANAMKE NA KUZAA MTOTO, ALIKUWA NA GIRL FRIEND WAKAACHANA NA KURUDIANA. SIKU ZOTE BARABARA HUWA HAIKOSI KONA NA KORONGO. SINA HAKIKA KAMA UNGEISHI MAISHA YOTE BILA KUKUTANA NA RABSHA ZA HAPA NA PALE. NAKUSHAURI UMUELEZE YOTE ULIYOYASHUHUDIA NA UMWAMBIE NI KWA SABABU UNAMPENDA NDIO ULITHUBUTU HATA KUSHIKA SIMU NA KUSOMA MSGS. MWAMBIE UNAMPENDA YEYE NA WATOTO ILI UPENDO HUO UENDELEE AJIREKEBISHE, MAMBO ANAYOFANYA NI YA KUPITA STILL ATARUDI KWAKO. KUHUSU NDOA FUNGA TU NDOA. HASIRA ULIYONAYO KUHUSU ITAISHA KAA CHINI NA FIKIRIA UTAKUWA KATIKA HALI HIYO MPAKA LINI. PIGA GOTI MUELEZE YESU SHIDA YAKO NA YEYE ATAFANYA MIUJIZA. JIBADILISHE NA WEWE MWENYEWE FANYA VITU AMBAVYO HUJAWAHI KUVIFANYA ILI NAE APATE MSHTUKO WA UNAYOYAFANYA ILI APAY ATTENTION KWAKO. MFANO KAMA ULIZOEA KUMTUMIA UJUMBE KWENYE SIMU ACHA, AU FUTA NAMBA YAKE YA SIMU ILI AKIKUPIGIA UMUULIZE NANI ANAEONGEA, LAZIMA NA YEYE ATAPATA TABU NA KUANZA KUKU ASSESS. NI HAYO TU STELLA, WISH YOU ALL THE BEST!

    ReplyDelete
  53. KAMWE SIWEZI KUKUSIKILIZA KUNGURU WEWE..!!
    WEWE HUYO KAKA MBONGO AMEKUWEZESHA UMEENDA HUKO KUFIKA HUKO UKAONA UMCHUKUE MTOTO NA KUSEPA KABISA YAANI HAPO PAMENIUMA SANA KWA KWELI SI VYEMA KAKA WA WATU AMEKKUWEZESHA KWENDA UKEREWE HALAFU UMESEPA YAANI NINAACHOOMBA UPATE UKIMWI TU URUDI BONGO MAANA NI FIRAUNI WEWE UMEPORA MUME WA MTU SASA MWENYE MUME KASHAMRUDISHA...NYAU WE
    KAKA BIJUU

    ReplyDelete
  54. Pole kwa challenge ngdogo ulio pata.Hapo hakuna cha kufanya zaidi ni kungoja contener lifike na kazi ikwishe then siku ya kupeana report ya ujenzi ndipi uchomekee hiyo inshu ya usaliti.Ila hata kama ukiachana na usimwache mtoto uliye mkuta nae mlee labda mtoto mwenyewe akatae.Hili ni jaribu lako inakubidi ulishinde jipe moyo ishi uikiamini wapo wenye matatizo makubwa ya ndoa kuliko yako.

    ReplyDelete
  55. UMEJIFUNZA, KUKIMBIA SEHEMU SIO KUYAKIMBIZA MATATIZO, KUYAKIMBIZA NI KUYATATUA. WEWE SI ULIKIMBIA TATIZO, NA UKABADILI NA URAIA, SASA INAKULA KWAKO. HALAFU HUYO UNAYEMHISI VIBAYA SI MGONJWA WA KANSA, ANAMPA SAPOTI DAKIKA ZA MWISHO, NI UBINADAMU, KAMA UMESEMA ANAJALI SANA, SI NDIO HIVYO.PUNGUZA WIVU NA ACHA UBINAFSI. FIKIRI WE NDO UNGEKUWA HUYO DADA, POLE ,INAKULA KWAKO.

    ReplyDelete
  56. Stela wewe ni Mkristo kwa maelezo yako, sasa mkumbuke Mungu wako wako wakati huu wa shida inayokupata achana na kufikiria habari ya mali unaona saa hizi unavyovyopata tabu ni kwa sababu umenyang'anywa mapendo. Lakini Mungu anakupenda daima! La kufanya piga magoti umwombe Mungu msamaha kwa makosa uliyofanya kusudi akusamehe na akusaidie katika hili halafu usifiche mweleze mwenzako uliyogundua mpaka sasa, kaeni muongee kurekebisha hali. Mungu atakurekebishia yote yaani utaona yote yameisha na kutulia kama unanawa. Huyo ni shetani anakuchanganya kwa sababu ukishiriki na shetani siku zote mwisho wake ni aibu. Usikate tamaa jikabidhi kwa Mungu sincerely na uwe mwaminifu kwake kabidhi tatizo lako kwake halafu kaa na mwenzako muongee taratibu bila jazba yatakwisha tu Stela hakuna lisilowezekana chini ya anga.

    Gabriel Mwalo

    ReplyDelete
  57. Dada Stella,
    Bwana Yesu Asifiwe,
    Naamini wewe ni mkristo. Kitu ni kimoja tu SIMAMA NA YESU atakupa jibu kama ndoa ifungwe au la? muulize mungu je huyo ndio ubavu wako? jibu utalipa, mungu anajibu maombi yoyote uombayo, kama utaomba atajibu kikubwa ni imani yako.
    kitu kingine: hakuna mahali palipoandikwa pasipo huyo baba wa watoto wako wewe huwezi kuishi. kikubwa da stela mrudie BWANA YESU naye mume wako mtarajiwa atakufuata tu na ataacha uzinzi.
    Jipe moyo dada.

    ReplyDelete
  58. pole sana dada, hii inatokea sana na wewe si wa kwanza na wala siyo wa mwisho, dada tulia na utengeneza maisha yako mwenyewe jitahidi kuishi kikamirifu , ukijijali wewe na watoto bila mwanaume, umeisha yaona mengi na hili lisiwe kizuizi cha maisha- litapita tu na utafungua ukurasa mwingine wa maisha kama ulivyo fanya na huyo bwana wa TZ, sasa kuhusu huyu bwana ni vigumu sana kuelewa anacho fanya na anachowaza, hata mimi sioni msimamo wake kamili , japo upo tu.Hivyo andaa siku moja na mkae sehemu nzuri na umuulize kiutaratibu kama kawaida yetu watanzania bila hasira na usionyeshe nia ya kumuacha bali mueleze kuwa unataka kutatua matatizo ya familia, na umuulize kwa nini unafanya hivyo? utapata jibu na mtayamaliza. ila tu: usiache kazi wala usihame mji , kwani ndoa huku ughaibuni siku hizi ni kitu kigumu hata kati ya watu wa nchi moja. na ndoa ujengwa kwa mazungumzo/maelewano. hivyo tafuta nafasi ya mazungumzo. asante na Mwenyezi awe nawe katika kpindi hiki chote akikujalia hekima, uvumilivu na amani. Ubarikiwe sana dada. Amen

    ReplyDelete
  59. STELLA HAKUNA MWANAMME ASIYEKULA NJE NAKUHAKIKISHIA. WEWE ENDELEA KUMPENDA LAKINI SHUKURU MUNGU ANATUMIA CONDOM. UKWELI NI KWAMBA YA NJE TAAM MNO

    SI UMEISHI BONGO UNAJUA?? GUEST ZOTE JUMAMOSI DAR ZIMEJAA. AKINA NANI WAMO HUMO????????????

    ReplyDelete
  60. Pole sana Stella,
    Maisha ndivyo yalivyo kuna milima na mabonde. Mtangulize Mungu katika kila jambo lako. Huyo bwana kumbuka hakuwa amegombana na huyo xgirlfriend, ugomvi wao ilikua ni juu ya mtoto wakashindana hapo labda yalikua ni maamuzi ya hasira kuachana ila mapenzi yao bado yalikukwepo. Mimi naona huyo bwana alikuja kwako kutokana na issue ya mtoto wake kushindikana kwa xgirlfriend na kwakuwa mmeshazaa na mko kwenye process za ndoa hivyo anashindwa kukuambia chochote maana kama angekuwa hana mpango na xgirlfriend, asingewasiliana nae na wala asingeficha simu na angekueleza ukweli. Hasira zako zitakapoisha ongea na huyo Baba watoto wako ujue msimamo wake kupenda watoto sio issue ikiwa wewe mwenyewe huna furaha nae. Akikuacha usijali sana piga goti kwa Mungu atakupa tu. Ukumbuke kuna mtu ulimpenda sana kabla ya huyo na iliwezekana kumuacha basi na huyo kama si mpango wa Mungu mtaachana tu kuwa tayari kwa lolote na pia kuhama mji sio solution utahama miji mingapi maana kila binadamu ana hila yake.

    ReplyDelete
  61. Ngojea kwanza container lisafirishwe. Halafu umpe vidonge vyake na aamue moja Ghana au TZ. Kama ulimaliza shule basi utakuwa ni mtu unayeweza kujitegemea ukijumlisha na child support. Yule mume wa Bongo hukumkosea lolote, dini, imani ya mtu ni kitu kikubwa na kama kulikuwa na kutokuelewana hilo liko nje ya uwezo wako. Na yeye kama alikupenda sana angebadilisha yake.
    Hivyo jibu la swali lako Ndoa isogezwe mbele mpaka next summer ili kukupa muda wa kuona kama amejirekebisha.
    Tofautisha kati ya "ri" na "li"

    ReplyDelete
  62. Hi Stella,
    Pole sana, lakin kwa umri wako na maelezo yako sioni sababu uyumbishwe na mwanamme mliyekutana kwenye kutafuta maisha. kama nimeelewa vizuri uliyoandika, huelekei kua mtu wa shida. what is ndoa at your age. shukuru mungu kakuonyesha hayo kabla hamjaoana, je ungeona wakati ushafunga pingu za maisha. Nakushauri achana naye maana hajui anachokitaka, endelea na maisha yako, nina hakika hushindwi kulea watoto wako. You are too old kuanza kulalamikia mambo ya hawa wajiitao wanaume wakati unaweza kuishi maisha yako mwenyewe yenye raha zote. Ni ungonjwa wa moyo my dear. Uliza walio ndani wakuambie.

    ReplyDelete
  63. Nigerian Ghananian mambo yao ndo hayo basi hapo dadangu pole sana wewe cha kufanya kaanae tu mchune mpaka unahahikisha kaisha na wewe unamwacha hio tabia haachi kamwe wapo hivo hao

    ReplyDelete
  64. Pole sana. pamoja na mashauri yote, suluhisho pekee ni wewe. wakati fulani pia lazima ufikie maamuzi magumu katika maisha kwa faida yako wewe. yataumiza kwa muda lakini in a long run you're gonna be happier. sit down with the man and talk it over, communication is very important. your peace of mind is important.

    Jambo hili lianze kwenu wawili kulizungumza na ikishindikana you can include the third party. nakubaliana na wazo kwamba tell the man what you discovered, otherwise if you continue keeping it to yourself, it will eat you untill you are finished. the best therapy is to talk it over and you are the one to start it coz you discovered the whole staff.

    the third party to be involved here, i would certainly recommend your pastor coz you are a christian, otherwise you are not a church goer and this will be a big problem not connected to the community of believers. your pastor can organise different sessions and start helping you solving different parts of your problems. our comments here cannot completely suffice in getting solution, what you need is different sessions with your pastor or any trustworthy proffessional counselor.

    Lastly I pray that God himself sees you thru. keep your fingers crossed, pray hard, it will be over someday.

    Blessings

    ReplyDelete
  65. STELLA DADA ANGU,

    UISLAM HAUNASHDA NA MTU ANAEBADILI DINI KWA AJILI YA MAPENZI, UILAM NI DINI ILIO KAMILI NA HAINA SHAKA NA TAJIRI, INA WAUMINI KIBAO DUNIANI NDIO MAANA HATA WATU MAARUFU WANABADILI DINI KUIFUATA BILA KUJALI KAMA WATAPOTEZA UMAARUFU WAO, SASA KWA WEWE BORA FUATA DINI YAKO NA MOLA ""WENU" ATAKUJAZI UMPATE MKIRISTO MWENZIO NA HUYO MKAKA MUISLAM ACHANA NAE NA YEYE ALLAH ATAMPATIA MWINGINE MWENYE IMANI KAMA YEYE

    WA ALLAHU AALAM

    MZEE WA BUNJU

    ReplyDelete
  66. container ni muhimu dada ...........wewe usimpe mambo ili kuepuka magojwa. Container likishatumwa then mwambie ukweli.Watu wasiseme ni material things kwa sababu hawawezi juu wewe umechangia kiasi gani katika familia or may be ulikuwa ni wajibu wake kutuma hilo container.Mwombe mungu akupe uvumilivu utayashinda.Then akikueleza ukweli kama mtaamua kuendelea mkapime HIV

    ALL THE BEST

    ReplyDelete
  67. Pole Sana kwa Yanayokukuta.
    In short,all men are almost the same...hamna haja ya kumwacha huyo mwanaume so long as he takes good care of the children...mchune kwa kadiri unavyo weza,zidisha mapenzi kwake na jaribu kuwa naye karibu kwa masaa mengi zaidi kadiri unavyoweza.

    ReplyDelete
  68. poverty,poverty,poverty,poverty,poor u...,
    since day one Ur biggest problem was poverty,in other world u r a gold digger.hate to say that,But that's what most Africans are.
    marry a guy for "makaratasi"!!what the fcuk is that?!u played other,now u r getting played.
    wheeeeew!

    ReplyDelete
  69. Dada stella, pole kwa yote. Napenda nikwambie kitu kimoja muhimu wanaume wote wanafanana na kwa taarifa tu ni wanaume wachache sana ambao hawacheat na kucheat kwa mwanaume sio kwamba hakupendi mkeo ni maumbile tu. Anaweza kuwa na mwanamke sio kwamba anampenda, ni kwasababu anataka tu afanye nae ngono. Am i married na kila siku namwambia mume wangu respect ni kitu muhimu sana na wananua kwambkuna mke na mpenzi ndio maana hakumuoa huyo baada ya kukataa kuishi na mtoto wake kumbuka kwamba sio kila mwanamke ni mke. wewe ni mke na anakupenda thats why anaficha simu yake usione anachat na nani kwani anajua impact yake. Ushauri tu sali sana na muombee mumeo kama mshauri mwingine alivyosema fight for ur luv.Mungu akubariki na nawaombea wanawake wenzangu wote mungu azisimamie ndio zetu.

    ReplyDelete
  70. Pole sana dada.
    Japo maoni ni mengi, naomba nongeze na yangu, i hope yatakupitia.
    Kama kweli wewe ni mristu, basi kumbuka kuwa si mali wala mwanaume ambaye anatakiwa akupe raha.
    Acha hayo ishi kama mkristu.
    Kama mali ni bora kwanza basi, vumilia mali iendelee kupatikana ukiuza roho yako.
    Kama mwanaume ni bora zaidi basi vumilia mengine uishi kama anavyotaka.
    Huwezi kupata vyote my dear.
    mimi huwa sielewagi watu wanaoishi maisha yasiyo ya kikristu wanapodai ni wakristu, na wanapokataa kubadili dini, wakati hata hawaijali, hivi inakuwaje? Kama ingekuwa mimi, nabadili dini mara moja!
    Nilishaona hawa watu wanaochanganya madada zetu kwa miaka halafu wanawarudia wapenzi wao wa zamani tena mmoja alikuwa mwenye ukimwi, wakashea chumba kimoja mzungu na dada zetu wawili mmoja hajapima mmoja anaumwa na wanajitahidi kutumia kondom kadiri wanavyoweza! mi hata shishangai, hichi kisa.
    Ila pole sana.
    Weka options zako mezani, ziangalie kwa makini na chagua moja. Ila kama ni mimi wewe nisingeacha kazi kwa muda huu, watoto watachanganyikiwa unless una akiba kubwa.

    ReplyDelete
  71. KWA MARA YA KWANZA "cha mtu mavi" NIMEKUWA BILA MAONI.SWALA LAKO ZITO SANA NA LIMECHANGANYA HABARI KUBWA SANA.YANI UKIUZA STORY YAKO HOLYWOOD WANATOA BONGE LA MOVIE NA INAWEZA KUWAHI SOKO LA VALENTINE.
    ushauri wangu mdogo ni kwamba huwezi ukakaa kimya kwani mapema utakavyo tatua hili swala ni vizuri zaidi kwako wewe na watoto wako.SASA INABIDI UTAFUTE UKWELI HUKO WAPI NAMUULIZE MASWALI YOTE KUHUSU KINACHONDELEA KWANI NI MZAZI MWENZAKO NA UNA HAKI YA KUJUA UKWELI.
    NA USHAURI WANGU BAADAE NI KWAMBA DINI ISIWE KIGEZO KWENYE SWALA LA MAPENZI NA INABIDI WOTE NYINYI WAWILI (YULE MBONGO) ,LITAKIWA KUWA NA MSIMAMO MMOJA NA MNGEWAACHA WAZAZI WAKASIRIKE KAMA WANATAKA KUKASIRIKA KWA MANUFAA YA MTOTO WENU NA KWA FURAHA YA MAPENZI YENU.
    MUNGU ATAKUSAIDIA KILA JAMBO LINA UFUMBUZI MBELE YA MOLA.
    mdau "cha mtu mavi"

    ReplyDelete
  72. Hi Da Stella!
    Pole sana na masahibu yakukumbayo. Nadhani kama ni kushauriwa, blog hii imekufanyia kazi nzuri. Ninachotaka kukwambia ni kwamba usijali watoa ushauri wanaoku-blame kwa kumuacha yule jamaa wa Tz. Kwa ufupi, it wasn't your fault. You did a good job kuvumilia kuishi bila ndoa, but hata ningekuwa mimi Usangoma nisinge ukubali. All I can tell you is to ask God to be on your side. He really is an awesome god, he knows why your life is in such a situation. Make sure you learn from your problems. Dont let all that make you any weaker. YOUR PROBLEMS SHOULD MAKE YOU STRONGER AND A BETTER PERSON THAN YOU WERE BEFORE. That's the purpose of all that trouble in your life.
    God is love,
    Mdau, USA.

    ReplyDelete
  73. Baada ya kupitia komenti za watu, nimegundua kuwa Stella angekuwa ni binti mwisilamu kanasa kwa jamaa mkristo ushauri ungekuwa tofauti.

    Nakumbuka kwenye blog hii dada mmoja mwisilamu aliwahi kuleta kesi hiyo alishambuliwa na kuulizwa dini ni nini bwana? Leo kaja mkristo dini haiguswi.

    Je inaonyesha kuwa mkristo kuolewa na mwisilamu ni haramu bali mwisilamu kuolewa na mkristo ni safi tuu?

    NIMEFUNGUKA MACHO.

    ReplyDelete
  74. aisee story yako ni ya mambo ya uswahilini kabisa. stori hizi huwa wanapiga watu amabo hata internet hawaijui.

    By the way, ulisahau, the most important element of love chemistry is dini. chagua wa dini yako au kama huna dini chagua asiye na dini, la sivyo huwezi kuepuka matatizo hayo.

    ReplyDelete
  75. DADA YANGU POLE SANA!ILA USISAHAU KUA KILA MFANYA DHAMBI HULIPWA HAPA KWANZA DUNIANI!
    ULICHOMFANYIA MPENZI WAKO WA MWANZO NDIO MALIPO YAKE YANAANZA TARATIBU HUO NI MWANZO TU!!MAANA HUKUTUELEZA NI JINSI GANI HUYO KAKA WA WATU YANI MPENZI WAKO WA MWANZO ALIVYOUMIA NA USALITI WAKO ULIOMFANYIA
    MAANA KWA MUJIBU WA MAELEZO YAKO YEYE NDIO ALIECHANGIA KUKUTAFUTIA CHUO THEN BAADA YA KUFIKA HUKO UKAJIFANYA UNAMCHUKUA MTOTO KWA LENGO ZURI PILI ALIPOFIKA HUKO UKAAMUA KUMSALITI BABA YAKE!!HUJATUELEZA NI JINSI GANI HUYO MWANAUME WAKO ALIVYOTESEKA,ILA KILA MTENDA HUTENDWA,USISAHAU HILO SASA NI ZAMU YAKO.
    CHAMSINGI MUOMBE MSAMAHA HUYO MP°ENZI WAKO WA MWANZO,AKIKUSAMEHE BASI UTAJIKUTA UNAPATA AMANI YA ROHO
    PIA INAONESHA WEWE ULIINGIA KTK PENZI LA HUYO JAMAA YAKO WAPILI KWA CARE ZAKE NA SIO REALLUV!!KAA FIKIRIA VIZURI UTAKUTA KILICHOKUFANYA UJIHISI UNAMPENDA NI CARE ZAKE NA SIO CHENGINE
    PIA WANAWAKE MNATAKIWA MLIJUE HILI UKIONA MWANAUME ANACARE SANA KUPITA KIASI AU ANAKUHONGA SANA UJUE ANAWALAKINI NA HAPA NDIPÖ WANAPOPATIKANA WAKINADADA WENGI KWA KUA MATERIALIST KUBABAIKIA MAPEDEJE(PRESIDENT DIRECTEUR GENERAL)WENYE MIJIPESA AU KUCARE KWA RAHA NA MIJIMALI WALIONAYO NAKUSAHAU KUA WAKINA KABWELA NDIO WANALUV YA UKWELI MAANA HANA KITAKACHOMFANYA AENDE NJE.
    POLE SANA ANGALIA ASIJEKUA NAE NI MUATHIRIKA MAANA NDIO STYLE ZAO KUHONGA NA KUCARE SANA!YANI WAPO KAMA MATAPELI SIKU ZOTE MATAPELI WANAKUA WAPOLE SANA NA MANENO MATAMU NA HAWAONI HASARA KUTOA VYAO.
    ILA KUMBUKA WAT GOES AROUND WAT COMES AROUND ULIMTENDA MWENZIO LEO UNATENDWA WEWE UNALALAMIKA,INAONESHA HUKUWAHI KUFIKILIA NI JINSI GANI MWENZIO MWENZA WA MWANZO ALIVYOUMIA NA NDIOMAANA MUNGU ANAKUONESHA PICHA KIDOGO TU YA ULICHOMFANYIA MWENZIO UKAMSALITI KWA MWAMVULI WA DINI
    ILA HUYO JAMAA SIO MWANAUME NA NDIO MAANA ALISHAACHANA NA MKE,GALI ALIYEFIKIA KUTAKA KUPATA NAE FAMILA BAADAE WEWE,CHUNGUZA UTAKUTA HAO WENZIO WALISHINDWA KUTOKANA NA SABABU MOJA AMA NYENGINE
    MICHUZI USIBINYE HUU NI USHAULI TOSHA UTAMSAIDIA BAADAE

    ReplyDelete
  76. hey,,,,dada how r u doin?well im disappointed n sorry to hear all this...unless u live dangerously life is worthy living n no life without risk...u need to risky ur life,,u need choose do or die,,u are in a danger zone n at stake,,your decisions today will determine ur entire future n destiny of u n ur children,,i wil advice this much,..take easy relax,seek the face of GOD,by praying,,let ur husband know all ur doubts,.at the earliest,listen dont bother to risk ur life n dont be too secrecy,,,n be READY for anything between u n ur husband,..U can live withour ur husband,,dada yangu siyo lazima mwanaume,,,u got beatiful children,,unless GOd wants u to live with this husband u can but otherwise,,,u better stay away....because where u are goin i can see is NOWHERE!life is too short to live negatively...u can be happy once more,,,,u can live alone,,n be used by God,,,JESUS IS our ultimate answer..RECEIVE Him today n He will be urs forever,,He will keep u safe n TRUE!!!reach me by colleenfra06@hotmail.com if u want more of my advice,..mdau india!!

    ReplyDelete
  77. jamani huyo mdau aliyosuggest movie kaongea la mbolea , Dadad Stella weka hii story in a "script" format na tafuta very dramatic ending , then uwapelekee macebrity wa Bongo man wanatafuta storyl;ines kama zako wafanyie movies !!

    ReplyDelete
  78. HUYO DADA ANASTAHILI KULIPWA ALIYOMFANYIA MPENZI WAKE HAPA HAPA DUNIANI MAANA INAONESHA NI HYPOCRIT!!AMEKAA NA MPENZI WAKE WA MWANZO KWA KUA ALIKUA HANA JINSI TU BUT ALIPOPATA MWANYA AKASAHAU MAZURI YOTE NA KUANZA KUTAFUTA VIJISABABU VYA HAPA NA PALE VYA KUTAKA KUTUONESHA KUA JAMAA YAKE WA MWANZO ALIKUA MSHIRIKINA KWA KUTAKA KUPÄTA SUPPORT AKIJUA FIKA DINI YA KIISLAMU HAKUNA KILICHOZUNGUMZIWA SANA KAMA KUKATAZWA KWA USHIRIKINA NA ZINAA
    DADA YANGU MUNGU ANAKULIPA HAPAHAPA DUNIANI KWANI ALISHA1SEMA MZINIFU ATAOLEWA AU KUOA MZINIFU MWENZIE,KITENDO CHAKO CHA WWE KUTOKUA MWAMINIFU,MWENZIO AMEKUSAIDIA UKAENDA CHUO UKAFIKA HUKO UKAANZA KUDANDIA WANAUME WENGINE NA UKAMCHUKUA NA MTOTO THEN UKAMBETRAY MWENZIO SO SASA HIZO NI ADAHABU ZA AWALI UNAZOANZA KUZIPATA.
    HAO WACHAGA WAMEWEKA MALI MBELE SANA NA NDIOMAANA UKIWAPA MADARAKA KIDOGO WANAKUA MAFISADI,CONTANER KITU GANI MBELE YA AFYA NA UTU WAKO.KUNA JAMII AMBAZO ZIMETOKA POLINI ZENYEWE UTU HAKUNA ILA UTUWAKO UKIWA NA MALI TU
    WALA MSIMSINGIZIE YESU!!ALLAH SUBUHANALLAH ALISHAKATAZA UZINZI!KINACHOTAKIWA TUBU KWA MOLA WAKO!MWOMBE MSAMAHA MWENZA WAKO WA MWANZO UPATE AMANI YA ROHO MAANA HAKUNA KITU KIZURI KAMA KUSAMEHEWA MAANA HUJUI AMETESEKA VIPI MWENZI WAKO WA MWANZO NA HUKUTUELEZA UNAJIFIKIRIA WWE MWENYEWE TU NA NDIO MAANA MUNGU ANAJARIBU KUKUPA FUNDISHO

    ReplyDelete
  79. MICHUZI UMEBINYIA MAONI YANGU SIO!!NIMEANDIKA MASUALA YA MANA SANA NA NIMEKOTI MANENO YAKATIKA BIBLIA NA QURAN TUKUFU!!NI YALE MAONI NILIYOANDIKA WANAUME WABAYA NI WALE WANAOONGA NA KUKEA SANA UJUE WANAKASORO PIA NIMEANDIKA WAT GOES AROUND WAT COMES AROUND TAFADHARI IRUSHE ITAMSAIDIA SANA HUYO DADA ATAJIFUNZA SIKU NYENGINE KUTOMFANYIA MTU UBAYA KWA JILI YA MALI!MDAU NA MKELEKETWA WA BLOG HII

    ReplyDelete
  80. pole sana kwa yaliyokukuta ila sio mwisho wamaisha.
    maisha ya siku hizi bwana lazima tuwe wakweli yanacontain mapenzi lakini na pesa pia.ndio happiness ni muhimu lakini raha shurti ujipe mwenyewe unaweza kuwa na mali nyingi lakini raha ndani ya nyumba hakuna.at ur age wala usihangaike na hii mijanaume.si una watoto wako tayari aka,we tulia tu saivi weka mambo yako sawa,akileta nyodo ondoka zako na watoto wako na wala usihame kama hutaki kuhama kwa sababu huyo mwanaume hakukuleta huku ulikuja mweneywe na wala asikutoe raha..labda uhame tu nyumba na watoto wako fanya kazi yako ukitaka kurudi bongo rudi,lakini kontena lile wala usiliachie kwa sababu yeye si kajifanya anakuonyesha ushenzi na wewe unamwonyesha vile vile.suala la mapenzi dada yangu utapata tu mwingine.hawa wanaume ndo walivyo huwezi kupata aliyekamilika lazima tu kutakuwa na kasoro fulani kwa hiyo basi kwa kuepukana na magonjwa na kila kitu wewe wala usjipe shida mwache kama kaamua kuwa na huyo mtu gal wake wa zamani.fanya kazi yako lea watoto wako.akitokea mwingine wa kukupenda pendana naye lakini wala usihangaike na huyo mtu...na uthibitisho hapo unao kabisa kwamba huyo jamaa anacheat we jikaze tu yataisha tu utazoea kukaa bila yeye.dont think that u cant stay without him u can sana kwa sababu hata yule wabongo si mlipendana sana yameishia wapi.siku hizi mapenzi hakuna ni machache sana,watu kwenye ndoa wana cheatiana sembuse nyie ..miaka 8 tu?watu wanakaa miaka 20 na bado mtu anatoka nje ya ndoa.so,wala usiwe na wasiwasi,tulia tuli safirisha mzigo wako yani weka mambo sawa kwanza,au kama na wewe mwenyew eunajiweza mambo yako huna haja hata na hilo kontena lake achana nalo kabisa ...kama unajiweza vzr na unafanya kazi nzuri inayolipa utapata tu hivyo vitu taratibu...lazima uwe na jeuri na wewe kidogo kumtingisha.lazima wanaume wajue kwamba kizazi hiki si kizazi cha kutegemeana sana,zaa watoto wako mwanaume hataki aende zake,kama una kazi nzuri maisha yanaenda.
    calm down.
    cha muhimu pia kingine ni Mungu dada,usimsahau kabisa huyu Mungu ukute ana makusudi yake tu anataka akuone utachukua uamuzi gani,kwahiyo omba omba sana tuu,na mambo yatakuwa mazuri tu wala usiwe na wasiwasi ila kwa sasa mwache kwanza,maana hata maandiko yanasema jisaidie kwanza wewe mwenywe na mungu naye ndio atakusaidia sio uombe tu bila kufanya effort yoyote.
    all the best.

    ReplyDelete
  81. Stella,

    Kwanza: Pole sana na matatizo.

    Pili: Sidhani kama ni busara sana kuomba ushauri kwa njia ya internet aur radio kutoka kwa jamii hasa kwa suala nyeti kama hili, kwani ushauri wenyewe unaongeza mamatatizo.

    Nashauri siku nyingine unapokuwa na tatizo kama hili, ni bora ukamshirikisha mtu mmoja au wawili faraghani kulingana na aina ya tatizo ulilo nalo. na hapo wawezapata ushauri wa kukufaa.

    Tatu: Inaniwiaga vigumu kukonkurudi baada ya kusikiliza upande mmoja tu. Hapa tunapata mabaya ya wenzi wako, lakini we totally know nothing abaout you. pengine wewe pia una matatizo???

    Anaway....

    Nakupa pole sana. Nakuomba upeleke matatizo yako mbele za Mungu. Mwombe sana naye atakuonyesha njia.

    Amina.

    ReplyDelete
  82. Dada umesahau usemi usemao "awali khul".Huyu jamaa ni player na usipokuwa mwanagalifu atakututia pabaya.Wewe peleka hilo Contena na fanya vitu vyako kiutalaam bila ya hasira wala kelele,ukishafika nyumbani mweleze kuw mchezo umekwisha kwani huyu jamaa hawezi kwacha huyo mwanamke anajua nachopata.. eheheheheh.Kama uliweza kumwacha wa kwanza huyu anakushinda nini?Kazi unasemani nzuri ,sasa lea watoto mwenyewe na usiweke kizingizio cha yeye kwani utakuwa mtumwa wa mapenzi na mwisheo utamalizwa.Hakuna haja y akuhama yeye ndiye atoke na mfuko wake wa malboro heheheheh.watoto watamuona siku utakayompangia.Kula raha maisha ni mafupi wacha kujitesa na chokoraa.

    ReplyDelete
  83. Bwana stella eehhe!!! wewe usijali wala nini wewe endelea zako na mipango yako ya harusi kama kawaida considering ur 43 walking down the aisle is not a joke Mungu amekuona, usiachane na mumeo kwani shetan uja kuvunja, kubomoa, kuharibu na kuua be strong cause is not a joke i know u're emotion wonded and feeling terribly right now but jikaze vizuri haviji kwa urahisi. kwanza huyo dada mwenyewe ana cancer karibia atakufa alafu wewe ukute umemwacha mumeo wa miaka 8 2gether stop joking go ahead and get merry, okay good lucky

    ReplyDelete
  84. AKINA DADA KAMA MNATAKA MAKARATASI BASO MUOLEWE NA WAZUNGU WAZEE SI WAINGEREZA WA KUJA KAMA NYINYI HASA HAWA WA NIGERIA NA GHANA SI WATU NI MATAPELI TU, KWANI WAO PIA NI WAKUJA NA SHIDA TUPU, MAKARATASI TAFUTENI VIJEBA VYA KIZUNGU, SI VIJANA PIA HAWAAMINIKI, UKIPATA KIJEBA MKE WAKE KAFA BASI HAPO UTAPATA KARATASI NA UTAISHI NAE NA KUMCHUNU PIA. WEW DADA ACHANA NAYE PAPER UNAZO NA SI YEYE ALIYEKUPA.

    ReplyDelete
  85. Hoja kama hizi kutolewa na binti wa miaka 15 - 25 sawa sio kwa bibi kama wewe
    wanasema ukiona nyani kazeeka ujue amekwepa mishale mingi , kwa umri wako hili liko ndani ya uwezo wako haistahili hata kuchukua maamuzi ya ajabu kama unavyodai mwenyewe,hakiuna cha ajabu alichofanya huyo bwana,hakumuacha huyo dada kwa kupenda kama ambavyo na wewe ulivyomuacha mzazi mwenzio cha msingi nendeni mkapime mkikuta mko fresh au nyote mmeathirika maisha yaendelee vinginevyo uamuzi unao mwenyewe bibi

    ReplyDelete
  86. Stella,

    Kwanza kabisa pole sana na yalio kukuta. Pili mie sikushauri umuache ila ningekushauri mkae nae na ukamwambia hilo dukuduku lako na pia mwambie hufurahii mambo yake anayofanya and then take it from there,

    Huwezijua anaweza akabadilika na akajirekebisha, saa nyingine binaadamu huwa tunapitiwa mie nachokuomba ni uhurumie wale watoto. Ila lazima mkae kuzungumza kwanza.

    NANA

    ReplyDelete
  87. Stella,
    Mimi nakupongeza kwa kummwaga huyo mwanaume wa mwanzo. Kama yeye na ndugu zake walianza mambo ya ushirikina ya kutaka kuroga wazazi wako nawe wangekuroga siku nyingine. Mshirikina anaua hata mwanae wa kuzaa ni bora ulipojiepusha. Kuhusu huyo mwanaume mwingine, kaa nae chini mjadili suala hilo bila jazba, busara na hekima vitumike, baada ya hapo utajua msimamo wake.

    ReplyDelete
  88. kweli nakupa pole toka moyoni inauma sana huyo mwanaume ni fisadi wa mapenzi... safirisha kontena fasta hao wanaodai ati material things sijui ushuz gani achana nao weka mambo sawa hakuna kitu inauma kama kuachwa na bwana unayempenda bila hata pipi wee inachoma sana machungu yanazidi mara mia nimepitia huko so naelewa vizuuri yani naungana na mtoa hoja wa kwanza hapo juu mwenzangu mwisho wa siku nyumbani ni nyumbani sasa hao watoto waje wakae kwenye mbavu za mbwa? kontena lishakuwa ndani ya maji ndo umuulize ukware wake!!! narudia tena kontena likishakuwa ndani ya maji ndo umuulize aseme anataka nini tujue mchele ni upi na pumba ni zipi pole dia

    ReplyDelete
  89. kheeeeeeeeee sijawai ona rubbish kama izi za baadhi ya annons,,,
    hii ni stori ya kutungwa tu jamen mbona mna jazba,mara dini oooh ukristo(okokeni sasa?)
    hahahaaaaaa michuzi hii ni kali comments 85 na usheee??
    duh wabeba box kwa kupenda umbea na udaku utawajua tu

    ReplyDelete
  90. Pole sana dada yangu! lakini wanaume wa west africa hamuwajui? muwe mnaangalia hata cinema zao.

    ReplyDelete
  91. Dada Stella

    Kwanza nakupa pole sana kwa yaliyokupata, na pili ningekuomba umshukuru Mungu kwamba hayo yote yanatokea hivi sasa kabla wewe na huyo jamaa hamja funga ndoa.Kumbuka wazungu wanasema"everything happens for a reason" inawezekana sana Mungu ameruhusu hali hii itokee kwa makusudi ili akuonyeshe ni mtu wa aina gani unayetarajia kufunga naye ndoa,na unajua ukishafunga ndoa ndo umeshajitia kitanzi kwani hata Biblia hairuhusu kuachana.Sasa badala ya kujisikitikia, tafakari hili jambo na chukua uamuzi wa busara, mshirikishe Mungu wako ukisali na kuomba kwa imani kubwa sana(ukiwa peke yako chumbani) au kupitia mtumishi wa Mungu ambaye amechaguliwa na Mungu kweli meaning Mlokole.Mwombe Mungu akufunulie Mume wako wa kweli ni nani? km ni huyu jamaa, utaona ishara na utaelewa, na kama si yeye,Mungu atakupa ishara vile vile.Cha kufanya, km kweli huyu jamaa ndiye MR RIGHT, basi mfunike kwa damu ya Yesu kwa kuvunja mapepo yote ya ngono,majaribu,tamaa etc..muite Mungu kwa kulia kwa uchungu na huyu jamaa asiangalie mtu mwingine yeyote except you!sambaratisha nguvu zote za giza zinazomfanya afanye yote hayo, kwani inawezekana sana huyo dada mwingine ameamua kutumia manguvu ya giza ndiyo maana unaona kibao kimegeuka ghafla;(wenzetu nchi zile za west na Central Africa ni maarufu sana kwa mambo hayo) kubali kataa lakini dunia ina mambo mengi ya ajabu lakini yote hayo usijali wewe shikilia Biblia na Damu ya YESU, na kesha ukisali na kuomba, ndugu yangu hakuna litakaloshindikana mbele za Mungu k.m kweli huyu Mume umepewa na yeye Mola kuwa wako wa milele. Lakini ukiona ishara kuwa si yeye, dada ningekushauri achane naye kabisa na uamini kuwa Mungu hapendelei huo uhusiano wenu ndo maana anakuonyesha hayo yote mapema ili ujitoe kwani bado una muda ndoa haijafungwa,mshikilie Mungu akupe Mume wa kweli, hangaika na wanao na kumbuka kumshirikisha Mungu katika kila jambo na si wanadamu pekee.

    ReplyDelete
  92. wabomgo kazi kweli...wengi wanasema mchune mchune, wengine usimwambie kwanza mpaka upeleke hilo container. tabia hii not good kwani mwanamke huwezi kutengeneza hela yako vizuri mpaka ,tu ategemee mwanamme~!!!!!!!! kwanza kama amesoma na ana kazi bibi anachoogopa kumove on....wala sidhani huyu anaogopa kuondoka kkwa ajolo ya watoto bali hana miguu kula kulala ni juu ya huyo mwanaume....kweli unaona condom unakaa kimya mpaka j3 mhhhhhhhhh.......

    what goes around comes around my dear......wachache wamekueleza ukweli you are very materialistic na ulimtosa baba wa watu now feel it

    ReplyDelete
  93. Dada Stella,
    Movie: Fireproof (2009) will be inspirational and guide you to do the right thing. If you get a chance visit these website: http://www.fireproofmymarriage.com/,http://www.thelovedarebook.com/love-dare-sample-chapter.pdf

    ReplyDelete
  94. HAYA NI MALIPO YA ZINAA,UNGEKUWA NA BUSARA UNGEOMBA USHAURI KABLA HUJAENDEKEZA TAMAA ZAKO.HUKU ULAYA TUNAWAONA WAKINA DADA WA KITANZANIA WANAENDEKEZA KUCHUNA HAWATAKI KUFANYAKAZI KAMA WENZAO WA MATAIFA MENGINE NA MAVUNO YAKE NDIYO HAYO.WAKO WENGI TU WANADANGANYWA NA FEDHA ZA WAUZA UNGA WA KI NAIJERIA UKIWAPA USHAURI WANAKUONA HUNA AKILI NA MPUMBAVU....MAMBO YAKIHARIBIKA WANAKUTAFUTA USHAURI...CHA KUFANYA NI KUACHA ULIMBUKENI NA KUJIPENDA NA KUJITHAMINI MIILI YENU,WATU WALA HAMUWAJUI BACKGROUND ZAO MUNAANZA KUWAVULIA CHUPI NA KUWAACHIA MWILI WACHEEZEE HADI TUMBO LIUMUKE...TAFUTA NOTI KWA NJIA HALALI NA MCHE MUNGU KWA KWELI UONE KAMA HUTAFANIKIWA NA KUPATA FAMILIA YENYE BARAKA.NA WENGINE MLIOBAKI HUKO MITAANI FANYENI HILI KAMA SOMO LENU LA KUJIFUNZA!

    ReplyDelete
  95. AnonymousJune 01, 2021

    Jina langu ni Edeni aliye Albania na ninafanya kazi katika benki kuu ya Albania katika jukumu la msimamizi kabla ya kuoa mke wangu, niliolewa na mfanyakazi wangu wa ng'ombe katika shirika langu na mimi ni aina ya mtu ambaye hana kujua kujua kuzungumza na rafiki wa kike sikuweza kuelezea mawazo yangu kwake kwa sababu mimi huwa namuogopa kila wakati na sijui kwanini na nadhani ni ukosefu wa kujiamini, ninajaribu mara kadhaa kuongea naye angalau kumwambia jinsi Ninahisi juu yake lakini sikuweza.
    Hizi ndio sifa ambazo nimepata kwake ambazo zinanifanya nimpende hapa ni kama ifuatavyo, yeye ni mrembo sana, anayejali, Tabia ni mzuri sana, Mwenye tamaa, haogopi, hana ubinafsi, anavutia na ana akili.
    Nilimwalika kwenye chakula cha jioni kadhaa lakini niliogopa kupeleka ujumbe, msichana huyo anaitwa Ajola, lazima nifahamishe rafiki yangu juu ya kile nilikuwa nikipitia na kwamba rafiki yangu wa karibu alinipata barua pepe kutoka kwa Daktari inayomsaidia kumaliza vita kati ya rafiki yangu wa karibu na mkewe kama miaka miwili iliyopita.
    Siamini kamwe uchawi wowote kwa sababu mimi ni mtu wa dini lakini niliweka tu njia ya kuwasiliana na daktari huyu na namuelezea juu ya msichana huyo kwamba nampenda na ninataka awe mke wangu na daktari aliniuliza nifuate hatua kadhaa ambazo nilifanya na baada ya wiki moja tu Ajola aliniita kwa nafsi yake na kuniambia kuwa ananipenda na ndio sababu ya harusi yetu na tulimwalika daktari siku ya harusi yetu na tunaadhimisha siku yetu ya harusi leo na Nina furaha sana
    Ikiwa unakabiliwa na shida yoyote maishani tafadhali usisite kuwasiliana na Daktari huyu kwenye barua pepe ifuatayo spellpecialistcaster937@gmail.com

    ReplyDelete
  96. AnonymousJune 01, 2021

    Naitwa Jame mimi ni kutoka Mexico, niliolewa miaka 5 iliyopita na watoto wawili na tunapendana kama familia, mke wangu alikuwa akiishi katika nchi yetu kabla na baada ya mimi kumleta Mexico na watoto, ili, anaweza kuondoka pamoja kama familia bila kutengana na baada ya miezi 5 nilipata kazi naye anafanya kazi na mimi lakini kampuni tofauti, hata hajui kuwa tayari ameshirikiana na meneja wake mahali pa kazi kwa sababu meneja huyo anamjaribu pesa na vitu vya vifaa, niliona tabia nyingi mbaya nyumbani kwa kuweka mbali simu yake kwa kuweka nenosiri kwenye simu yake ambayo haijawahi kutokea hapo awali na kama mume nilimuuliza alisema akibainisha, siku moja alikuja nyumbani na talaka barua na anafunga nyuma yake na kuondoka na meneja wa ofisi yake.
    Nilijaribu kila jaribio linalowezekana la kumsihi na kumaliza suala hilo lakini alisisitiza na nampenda sana na aliacha watoto wawili sijui nifanye nini tena, ninasikiliza ushauri wa Radion wa spell caster juu ya radion na kwenye Tv na mimi tuliwasiliana na Daktari na oi akamweleza na akaniuliza nifuate hatua kadhaa na baada ya masaa 48 mke wangu alirudi na kuanza kuniomba msamaha na yeye wakati huo hakuwa na tabia ya ajabu tena na yeye hata ananipenda zaidi.
    sasa anapenda na anajali bila masharti - hii inaweza kuwa mguso mzuri sana, lakini muhimu hata hivyo. Mke mzuri anampenda mumewe bila masharti. Yeye hawekei vizuizi au vigezo kwa tabia ya jumla, hamhukumu mtu huyo, na hamtupi wakati wa ugomvi, licha ya shida zake mwenyewe. Hata ikiwa amekosewa, anajaribu kutatua suala hilo kuliko kumlaumu mtu huyo. Hizi ni sifa muhimu ambazo hufanya mke mzuri na kujenga uhusiano wa imani na uaminifu. Kujali pia kunatafuta kutathmini ikiwa anaishi vizuri na marafiki wako, familia, na jamaa wa karibu. Mwisho wa siku, alirudi kwenye maisha yangu.
    ikiwa unakabiliwa na shida hiyo hiyo na unahitaji suluhisho tafadhali wasiliana na Dr.Pellar kwa suluhisho la shida yako, hii ni barua pepe yake drpellar@gmail.com

    ReplyDelete
  97. AnonymousJune 01, 2021

    Jina langu ni Edeni aliye Albania na ninafanya kazi katika benki kuu ya Albania katika jukumu la msimamizi kabla ya kuoa mke wangu, niliolewa na mfanyakazi wangu wa ng'ombe katika shirika langu na mimi ni aina ya mtu ambaye hana kujua kujua kuzungumza na rafiki wa kike sikuweza kuelezea mawazo yangu kwake kwa sababu mimi huwa namuogopa kila wakati na sijui kwanini na nadhani ni ukosefu wa kujiamini, ninajaribu mara kadhaa kuongea naye angalau kumwambia jinsi Ninahisi juu yake lakini sikuweza.
    Hizi ndio sifa ambazo nimepata kwake ambazo zinanifanya nimpende hapa ni kama ifuatavyo, yeye ni mrembo sana, anayejali, Tabia ni mzuri sana, Mwenye tamaa, haogopi, hana ubinafsi, anavutia na ana akili.
    Nilimwalika kwenye chakula cha jioni kadhaa lakini niliogopa kupeleka ujumbe, msichana huyo anaitwa Ajola, lazima nifahamishe rafiki yangu juu ya kile nilikuwa nikipitia na kwamba rafiki yangu wa karibu alinipata barua pepe kutoka kwa Daktari inayomsaidia kumaliza vita kati ya rafiki yangu wa karibu na mkewe kama miaka miwili iliyopita.
    Siamini kamwe uchawi wowote kwa sababu mimi ni mtu wa dini lakini niliweka tu njia ya kuwasiliana na daktari huyu na namuelezea juu ya msichana huyo kwamba nampenda na ninataka awe mke wangu na daktari aliniuliza nifuate hatua kadhaa ambazo nilifanya na baada ya wiki moja tu Ajola aliniita kwa nafsi yake na kuniambia kuwa ananipenda na ndio sababu ya harusi yetu na tulimwalika daktari siku ya harusi yetu na tunaadhimisha siku yetu ya harusi leo na Nina furaha sana
    Ikiwa unakabiliwa na shida yoyote maishani tafadhali usisite kuwasiliana na Daktari huyu kwenye barua pepe ifuatayo spellpecialistcaster937@gmail.com

    ReplyDelete
  98. AnonymousJune 01, 2021

    Naitwa Jame mimi ni kutoka Mexico, niliolewa miaka 5 iliyopita na watoto wawili na tunapendana kama familia, mke wangu alikuwa akiishi katika nchi yetu kabla na baada ya mimi kumleta Mexico na watoto, ili, anaweza kuondoka pamoja kama familia bila kutengana na baada ya miezi 5 nilipata kazi naye anafanya kazi na mimi lakini kampuni tofauti, hata hajui kuwa tayari ameshirikiana na meneja wake mahali pa kazi kwa sababu meneja huyo anamjaribu pesa na vitu vya vifaa, niliona tabia nyingi mbaya nyumbani kwa kuweka mbali simu yake kwa kuweka nenosiri kwenye simu yake ambayo haijawahi kutokea hapo awali na kama mume nilimuuliza alisema akibainisha, siku moja alikuja nyumbani na talaka barua na anafunga nyuma yake na kuondoka na meneja wa ofisi yake.
    Nilijaribu kila jaribio linalowezekana la kumsihi na kumaliza suala hilo lakini alisisitiza na nampenda sana na aliacha watoto wawili sijui nifanye nini tena, ninasikiliza ushauri wa Radion wa spell caster juu ya radion na kwenye Tv na mimi tuliwasiliana na Daktari na oi akamweleza na akaniuliza nifuate hatua kadhaa na baada ya masaa 48 mke wangu alirudi na kuanza kuniomba msamaha na yeye wakati huo hakuwa na tabia ya ajabu tena na yeye hata ananipenda zaidi.
    sasa anapenda na anajali bila masharti - hii inaweza kuwa mguso mzuri sana, lakini muhimu hata hivyo. Mke mzuri anampenda mumewe bila masharti. Yeye hawekei vizuizi au vigezo kwa tabia ya jumla, hamhukumu mtu huyo, na hamtupi wakati wa ugomvi, licha ya shida zake mwenyewe. Hata ikiwa amekosewa, anajaribu kutatua suala hilo kuliko kumlaumu mtu huyo. Hizi ni sifa muhimu ambazo hufanya mke mzuri na kujenga uhusiano wa imani na uaminifu. Kujali pia kunatafuta kutathmini ikiwa anaishi vizuri na marafiki wako, familia, na jamaa wa karibu. Mwisho wa siku, alirudi kwenye maisha yangu.
    ikiwa unakabiliwa na shida hiyo hiyo na unahitaji suluhisho tafadhali wasiliana na Dr.Pellar kwa suluhisho la shida yako, hii ni barua pepe yake drpellar@gmail.com

    ReplyDelete
  99. AnonymousJune 01, 2021

    Naitwa Jame mimi ni kutoka Mexico, niliolewa miaka 5 iliyopita na watoto wawili na tunapendana kama familia, mke wangu alikuwa akiishi katika nchi yetu kabla na baada ya mimi kumleta Mexico na watoto, ili, anaweza kuondoka pamoja kama familia bila kutengana na baada ya miezi 5 nilipata kazi naye anafanya kazi na mimi lakini kampuni tofauti, hata hajui kuwa tayari ameshirikiana na meneja wake mahali pa kazi kwa sababu meneja huyo anamjaribu pesa na vitu vya vifaa, niliona tabia nyingi mbaya nyumbani kwa kuweka mbali simu yake kwa kuweka nenosiri kwenye simu yake ambayo haijawahi kutokea hapo awali na kama mume nilimuuliza alisema akibainisha, siku moja alikuja nyumbani na talaka barua na anafunga nyuma yake na kuondoka na meneja wa ofisi yake.
    Nilijaribu kila jaribio linalowezekana la kumsihi na kumaliza suala hilo lakini alisisitiza na nampenda sana na aliacha watoto wawili sijui nifanye nini tena, ninasikiliza ushauri wa Radion wa spell caster juu ya radion na kwenye Tv na mimi tuliwasiliana na Daktari na oi akamweleza na akaniuliza nifuate hatua kadhaa na baada ya masaa 48 mke wangu alirudi na kuanza kuniomba msamaha na yeye wakati huo hakuwa na tabia ya ajabu tena na yeye hata ananipenda zaidi.
    sasa anapenda na anajali bila masharti - hii inaweza kuwa mguso mzuri sana, lakini muhimu hata hivyo. Mke mzuri anampenda mumewe bila masharti. Yeye hawekei vizuizi au vigezo kwa tabia ya jumla, hamhukumu mtu huyo, na hamtupi wakati wa ugomvi, licha ya shida zake mwenyewe. Hata ikiwa amekosewa, anajaribu kutatua suala hilo kuliko kumlaumu mtu huyo. Hizi ni sifa muhimu ambazo hufanya mke mzuri na kujenga uhusiano wa imani na uaminifu. Kujali pia kunatafuta kutathmini ikiwa anaishi vizuri na marafiki wako, familia, na jamaa wa karibu. Mwisho wa siku, alirudi kwenye maisha yangu.
    ikiwa unakabiliwa na shida hiyo hiyo na unahitaji suluhisho tafadhali wasiliana na Dr.Pellar kwa suluhisho la shida yako, hii ni barua pepe yake drpellar@gmail.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...