JK akiwa katika mazungumzo na kiongozi wa Mabohora duniani Dr.Syedna Mohamed Burhanuddin wakati alipokwenda kumsabahi kiongozi huyo katika msikiti wa mabohora uliopo Upanga jijini Dar
JK akiwa na kiongozi wa Mabohora duniani Dr.Syedna Mohammed Burhanuddin baada ya kiongozi huyo wa Mabohora kumvika mgolole maalum wakati JK alipokwenda kumtembelea katika msikiti wa Mabohora ulioko Upanga jijini Dar


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. MBONA ANAINAMA CHINI!!! SURA IYO VIPI AU NDO "UTAKATIFU WENYEWE IMAN YA KIBOHORA"??
    ivi awa wanaamini katika nini??

    ReplyDelete
  2. Samahani kuuliza c ujinga.Mabohora(neno siyo geni) ndiyo watu au dini gani?,wanaabudu vipi? na historia yao kwa ufupi.Anayewaelewa naomba anisaidie kunielimisha.

    ReplyDelete
  3. Kiongozi huyo wa Mabohora amekula chumvi nyingi, yaani ana umri zaidi ya miaka 90, ndo maana kusimama wima amenyooka inamwia tabu.

    ReplyDelete
  4. muulize polisi wa kibongo watu wasioa angalia watu machoni ni nani? utapata jibu zuri sana

    ReplyDelete
  5. jamani mimi najua mabohora kwa kimombo ni passion (yaani matunda. sasa hii bohora ni imani gani tena?

    ReplyDelete
  6. Mabohora wanafuata dini ya kiisalamu (Madhehebu ya SHIA), wanaabudu kama waislamu wengine.

    Wengi wa mabohora wanatoka jimbo la Gujarat huko India, na wameenea kote ulimwenguni. Wengine wanatoka sehemu ya Yemen. Hapa Tanzania wako karibu 7,000. Wengi wao wamezaliwa hapahapa Tanzania, mababu zao walitoka India na wameishi Tanzania karibu ya miaka 150. Wengi wamezaliwa Dar es Salaam, Zanzibar au Tanga, Lakini hivi sasa wengi wao wako bongo.

    Mabohora wengi ni wafanya biashara wa vifaa vya ujenzi na vitambaa.

    Kiongozi wa Mabohora Dr. Syedna Burhanuddin ana umri wa miaka 98, na anatembelea wafuasi wake kila nchi waishio.

    Katika historia yao, waislamu wa Mabohora wamekuwa wakiheshimiwa kwa tabia yao ya amani na kujitegemea. Hii imewezekana kwa kiasi kikubwa kwa sababu ya mifumo ya jumuiya ya kijamii, kiutamaduni, uchumi na elimu ambayo inawahimiza Mobohora kusaidiana hususan kusaidia maskini.

    Si tu kwamba wanafanya shughuli hizi kuwanufaisha wanajumuiya pekee, bali pia wanahakikisha kuwa wanakuwa wachangiaji muhimu katika maendeleo na mafanikio ya taifa.

    Njia mbalimbali zimekuwa zikitumika ili kufikia lengo hili.

    Kupanga familia: Familia zinazoweza kufanya hivyo zinaweza
    Kuchukua zile familia ambazo ni maskini kuzileta na kutoa misaada muhimu.

    Kufundisha biashara:- Wanachama wanahimizwa kutoa mafunzo ya kitaalamu na Kiweledi pamoja muda wa kujifunza kwa wote unaowakukua ili baadae waje waweze kujitegemea kiuchumi.

    Misaada ya Kifedha:- Mikopo isiyo na riba na namna nyingine za misaada ya Kifedha imekuwa ikitolewa kwa wale wanaohitaji.

    Nafikiri nimeelimisha ya kutosha... kujua mengi zaidi uliza maswali kwenye blog hii ili nijaribu kuzijibu kinaganaga.

    - Bohora...

    ReplyDelete
  7. Bohora hao ni dini ya kihindi haswa gujerat na huyo kiongozi wao anaishi kule mumbai,tena wamegawanyika katika vikundi viwili yaani wale wanaomuabudu huyo mzee pichani na wanajulikana kwa jina la wenye vyeti na wale wanaompinga huyo mzee yaani wasio na vyeti (hivyo vyeti ni vitambulisho vitakavyowachukua hao mabohora eidha peponi au jahanamu...ni kundi lenye wafuasi takriban 20,000 kote duniani!

    ReplyDelete
  8. Yakhe JK,huyo mzee mchawi kweli kweli...kaja kukuibia bila wewe kujua...na wewe kuchekacheka tu!!!

    ReplyDelete
  9. hii dini ya bohara naona ni kiboko. Yaani Raisi ndio amemfata huyu imamu kwenye msikiti badala ya imamu kumtembelea Raisi?

    ReplyDelete
  10. Ndugu Michuzi,

    Nafahamu kuwa una haki ya kuchapisha maoni unayotaka. Sijatukana na nilieleza kwa nini kuna mabohora wa aina mbili Kenya na kuna wale wanaolalamika kuwa hawana uhuru na kulazimishwa kulipa ada kila mwaka mwa kiongozi wao na kulazimishwa kuenda misikitini kila siku. Pia wanalazimishwa kuacha ndevu wanaume an kuvaa baibui za rangi rangi kwa wanawake wao.

    Kama unapinga maoni kama haya, pasi utuambie kabisa ili tusipoteze muda wetu kuandika maoni pengine wewe binafsi huyapendi kwa sababu zako mwenyewe. Muulize bohora yoyote atakuambia kuwa nayosema ni kweli. Tunachoka na tabia hii ya censorship bila ya mtu kutukana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...