JK akiongea wakati wa mkutano na waandishi baada ya kufungua mkutano huo. kulia ni bosi wa IMF Dominique Staruss-Kahn na shoto ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mstaafu Koffi Annan
sehemu ya wajumbe wa mkutano huo katika ukumbi wa twin towers
JK akiwa na naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr Asha-Rose Migiro, Waziri wa Fedha Mh. Mustafa Mkullo katika meza kuu ya mkutano huo wa siku mbili alioufungua leo katika ukumbi wa BOT Dar
Mkurugenzi mkuu wa IMF Dominique Strauss-Kahn akiwa na Katibu Mkuu wa Zamani wa Umoja wa Mataifa Mh. Koffi Annan kwenye mkutano huo

JK akifungua mkutano huo leo





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. INSHALLAH MKUTANO HUU UWE NA MALENGO YAKINIFU KWA NCHI ZA AFRICA NA ZILE ZINAZOENDELEA DUNIANI
    Mpili

    ReplyDelete
  2. natumaini kila kitakachojadiliwa kitafuatiliwa.

    Mimi ningeshiriki katika mkutano, ningeomba IMF, waache kutumia maneno "Third World countries". Hii noma hata tukijakuendelea bado tutaitwa Third world countries.

    Pili ningeomba wasimamishe misaada ya pesa bali watupe hata tuviwanda twamitumba (Secondhand factories). Maana msaada wa pesa hatusaidii. "Ukinipa samaki nitamla kesho nakuja kuomba mwingine. Ukinipa ndoano naijua mito iliko nitaenda kuvua samaki mwenyewe"
    ni hayo tu kwa leo
    P.E.D

    ReplyDelete
  3. Nimeingia leo huu ukumbi kwa kweli TZ kweli tambarare. Hata ma-delagate wenyewe walikuwa wanastaajabu Teknolojia iliyopo humo ukumbini.

    Tunachojiuliza, je PCCB wapo sahihi kusema yule jamaa amelitia taifa hasara?

    ReplyDelete
  4. Haya wale wake na vimada wa mashaka na shayo karibuni tena. manaake mkiona to imf mnawakumbuka mabwana zenu bila hata kufikiria the so-called financial crisis ni kitu gani au hao wanaopromote mentality ya finacial crisis wana agenda gani

    ReplyDelete
  5. BOONGE LA UKUMBI, HAPA NDIO MABILIONI YALILIWA. KWA KUMBUKUMBU NZURI YAFAA UITWE 'LIYUMBA UFISADI HALL'

    ReplyDelete
  6. Huu mkutano akaribishwe na Lyumba kwani ndiye aliyefanikisha ujenzi wa hizo Twin Towers za BOT, TEH!!! TEH!!!! TEH !!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  7. Mh Balozi,
    Hapo ni Bongo? siamini!!!!

    ReplyDelete
  8. LIUMBA NA KWEKA HELA WAMEKULA!!!!

    LAKINI KAZI WAMEFANYA, TENA NI QUALITY....

    WAPUMBAVU KIBAO WANAKULA HELA NA KAZI HAWAFANYI

    MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI

    ReplyDelete
  9. MIKUTANO YOTE ILIYONONA HUFANYIKA BONGO KUTOKANA NA SIFA YETU NZURI YA KUKUA KWA UCHUMI, LAKINI WABONGO TUNAENDELEA KUISHI KATIKA UFUKARA ULIOKITHIRI, MAJI JIJINI SHIDA, HUDUMA ZA AFYA NDIYO HIZO,ELIMU MPAKA VIBOKO, MLO TUNAVIZIA HITIMA AU AROBAINI VINGINEVYO UKISIKIA HODI UNAKAFICHA KAUGALI KASIONEKANE KALIVYO, LAKINI WENZETU WANAOTUTAWALA WANAENDELEA KUNONA NA IMF KUWAONA NDIYO KIPIMO CHA KUKUA KWA UCHUMI WETU.

    ReplyDelete
  10. Sipendi kuwa "Doubting Thomas!" au hata "Prophet of Doom!" katika mikutano kama hii.Lakini kwa kweli,"I think,I have had too much of these Puddings".Nilizisikiliza hotuba zote za Kikwete,Koffi,na Bosi wa IMF,I must admit that I was one of those "disappointed".Kitu kinacho nipa taabu ni kule kushindwa kwetu kutambua TATIZO LA KIUCHUMI LINALO ZIKABILI NCHI ZA KIAFRIKA NI LIPI na ndipo tufikirie nini kifanyike.Tunashindwa kutambua kwamba Mfumo wa Kiuchumi tuliourithi toka kwa Wakoloni (Post Colonial Economic Model),ni self-defeating,hauwezi kutunasua kutoka hapa tulipo na kuwepo kwa maendeleo endelevu!Hata kwa wale waliosoma na wana ujuzi wao wamebanwa na Mfumo na hawawezi "Kutumia kulingana na Mahitaji na Mipango Yao" bali "Watatumia kulingana na Kipato Chao"hata kama watakuwa na uwezo wa kutumia kupita kipato chao na kuweza kurejesha muda mfupi baada ya uzalishaji.Benki zetu zinasubiri zifuatwe,hazifuati wala kutafuta wateja!Riba za mabenki hazibadiliki kulingana na mwenendo wa biashara za kuweka na kukopa,bali zipo pale kama msahafu,mikopo iongezeke au isiongezeke kwa mabenki yetu hilo siyo muhimu sana.Kwao kilicho muhimu ni kujiepusha kukopesha wale wateja "wasio aminika!"hata kama mtu ana elimu yake na rekodi safi ya utendaji kazi na ujasiriamali!Wenzetu matajiri na walioendelea wanaishi kwa mtindo wa "Credit Cards",nunua kulingana na mahitaji yako lakini kwa kuzingatia uwezo wako wa kulipa!Sisi huku tunaishi kwa mtindo wa "Debit Cards",nunua kulingana na Kipato kile tu ulichonacho na sio zaidi,hata kama utakuwa na uwezo wa kulipa kwa mujibu wa mapato yako!In Tanzania,we do have a Cash-Buy economic system!Madhara yake katika Mzunguko wa Pesa katika uchumi ni mabaya sana!Madhara yake katika kuwafanya watu wajitume na kujitumikisha ni mabaya vilevile!Mtu mwenye mikopo benki atajituma zaidi kuzalisha ili alipe deni la benki kuliko yule ambaye hana mkopo wowote!Atajituma kwa kasi yake tu itakavyo mruhusu!Rasilimali ya kudumu kama Nyumba huwezi kumtarajia mtu aijenge au aipate kwa malipo Taslimu ya papo hapo!Hilo halikuwezekana kwa wenzetu nchi matajiri,na halitawezekana huku kwetu kwa watu mafukara kiasi hicho pamoja na elimu walionayo!Kadhalika,huwezi kumtarajia kila atakaye hitaji mkopo benki awe na Dhamana isiyohamishika "Mortgageable Asset".Katika mazingira ya kiuchumi ya aina hiyo ni vigumu kujenga Tabaka la Watu Wabunifu katika Jamii ambao kazi yao ni kugundua mambo mapya na kuyatoa kwa Jamii ili wayatafsiri katika vitendo!Taifa litazidi kuongezeka ki-idadi lakini halitakuwa na "Wabunifu".Na Taifa lisilo kuwa na Wabunifu wake,Taifa hilo litasinyaa na kutoweka katika Ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia!Tanzania tumekubali kuwa watu wa Kuomba tu Misaada kutoka Nje huku tukiruhusu Rasilimali zetu zikichukuliwa na Wajanja na kupelekwa nchi za nje.Tumekuwa mahodari wa kulalamika tu.Kwenye Mkutano wa G20 au G8 ujao,nimesikia kuna viongozi wa kiafrika watakao kwenda kuhudhuria mkutano huo,eti,kwa madhumuni ya kuwasilisha malalamiko tu ya nchi maskini toka afrika kuhusu ahadi nyingi zilizotolewa na nchi zilizo endelea lakini hadi sasa hazija tekelezwa,"misaada,misaada,misaada!".Hata kama IMF "itataka"kutusaidia,sisi wenyewe tukiwa hatujijui wapi kwenye matatizo,wapi tuanzie,hii misaada italeta faida gani hapa nchini?Au tunalimbikiza mzigo wa Madeni yatakayo kuja lipwa na Watukuu wetu? Mikutano kama hiyo na IMF japo ni muhimu haitaweza hata siku moja kutunasua kutoka hapa tulipo.We might as well forget about disengaging ourselves from the shackles of economic suppression and perpetual poverty!UMASKINI NA UFUKARA IS HERE TO STAY NDUGU ZANGU KWA UFINYU HUU WA MAWAZO!In case you did not know,"The Global Challenge is to make sure all Underdeveloped Countries remain dependable sources of industrial raw materials and are bonded permanently as reliable markets for the INDUSTRIALISED!"Kalagabaho.

    ReplyDelete
  11. Kwani IFM inamilikiwa na nani na dhumuni lake ni kuhakikisha nini? Wametumwa?
    Nani mwenye say kubwa IMF? Hiyo inaathiri vipi nyendo zake kwa nchi kama Tanzania. Kuna haja yoyote ya kufuata kila mapendekezo wanayotoa hawa jamaa au inawezekana kureject prposal zao?
    Nchi itakayofanikiwa ni ile isiyofuata mkumbo. Ahsanteni.

    ReplyDelete
  12. Kweli Tanzania hatutakaa tuendelee yaani Rais katutia aibu hivi (http://www.changes-challenges.org/concluding-plenary)halafu humu comment za watu eti ukumbi ulikuwa poa sana !!! sijui tunalaanaa ya namna gani!

    ReplyDelete
  13. so twin towerz ndo izi na izo kumbi?za liyumba?

    akya nani vile,sasa likumbi looote ili liko city center tena?foleni je wakija awa "wakubwa" si balaa
    ivi why msijenge mikoa mingine yenye vivutio vya utalii??IRINGA,MBEYA,KIGOMA-kule kwenye sokwe nk nk

    eti mnafunga barabara mnapanga viti ktk barabara ndo umekua ukumbi simply kiongozi gani anafungua PPF PLAZA-MWANZA 13/3/09

    mnakera sana,subiri tuingie uko tunageuza sheria TUTAWAFUNGA NYIEE??

    michu usibane,afu tupe NEWZ za mke wa rais wa zamani ithink malawi/zambia?kahukumiwa 3 yearz jail

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...