Kikosi cha Houston

Vijana wa kitanzania waishio Houston, Texas,  jana wamefanikiwa kuingia katika fainali ya mataifa ya africa kwa soccer ya wanaume kwa kuifunga timu ngumu ya watoto wenye vipaji ya Ivory Coast  bao 3-2 katika finali kabambame ilofanyika Houston.

Timu ya Houston i liianza kipindi cha kwanza taratibu na kufanikiwa kupata bao la kwanza mfungaji akiwa Peter Bategeke kwa shuti kali la umbali mita 20, na kumshida kipa.

 Ivory coast walikuja juu na kufanikiwa kusawazisha na kuongeza bao la pili , lakini kipindi cha pili timu ya watanzania iliyokuwa ikiongozwa na James Shemdoe (Mourinho) ilifanya mabadiliko ya nguvu ya kuwaingiza  Kwame, Mohamedi, Sekulu, Andrew sanga, Hamisi Ndwata na Bitebo .

Alikuwa ni Kijana Hamisi Ndwata aliyeipatia houston bao la kusawazisha na la kuongeza kwa penalti safi za kufa mtu zilizotosha kuifanya houston kuifunga Ivori coast 3-2 na kutinga fainali.

Kwa maana hiyo Houston itavaana na majirani zao  zao Somalia katika fainali itakayochezwa Jumamosi ijayo. Nahodha wa Houston, Haruna,  na viongozi wa timu wanaomba watanzania wajitokeze kwa wingi kushuhudia ushindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Wabeba ma Box bwana.

    ReplyDelete
  2. wewe huoni kama kubeba box ni ujanja ,wewe hata kununua nguo ya ndani inakushinda, acha watu wahangaike

    ReplyDelete
  3. we anony wa kwanza mbona hatusemi kama wewe ni mchimba makaburi kinondoni acha jelous mind your bussines aight!!!!

    ReplyDelete
  4. Wabeba Box nao wana maisha,kama waugua Malaria,wakosa maji,wakosa umeme,lishe duni,wazembe na waisiojua nini maana ya muda na maisha.

    ReplyDelete
  5. hapo hakuna kijana hata mmoja wote ni wazee/madingi.Acheni kutudunganya.

    ReplyDelete
  6. HIVI HII WABEBA BOX WABEBA BOX NI NINI ?WATU WANATAFUTA MAISHA NA WANAISHI BILA KUMBUGUDHI MTU NA WANASAIDIA FAMILIA ZAO WE UNAESEMA HAYO MLO MMOJA UNAKUTOA JASHO,JARIBUNI KUFIKIRI NAMNA YA KUJIKWAMUA MAANA WE UNAESEMA BOX BOX HUNA LOLOTE MAANA HATA KUPATA NAULI YA KWENDA KUBEBA BOX HUWEZI,ACHILIA MBALI MCHONGO .TULIEMI NA WAPENI MOYO WENZENU ILI WAWE WANAKUMBUKA NYUMBANI.
    WADAU JP

    ReplyDelete
  7. DAWA YENU NI DC. TUNAWANGUJA MAY 22,HOWEVER, CONGRATS FOR THE FINAL.REPRESENT GOOD JOB.

    IT IS WHAT IT IS.

    ReplyDelete
  8. ROHO INAKUUMA EEE NYOOO!! NJOO NA WEWE KAMA UNAWEZA MAANA HATA VISSA SIJUI KAMA UTAPATA UATABAKIKI KUISHA KWENYE NYUMBA YA FAMILY NA WATOTO NA MKE HUMOHUMO

    ReplyDelete
  9. Baada ya mimi kurudi TZ baada ya kumaliza kile kilichonileta Texas nani hasa anacheza namba yangu?maana sikuacha mtu mbadala wa kuchukua nafasi yangu
    lkn naona kuna vipaji kibao hapo ambao enzi zangu walikuwa wanacheza tu kwa starehe na wala siom kw aushindani,je ndiyo sasa wamejirudi kuokoa jahazi letu la Houston?
    Kuanzia kushoto waliochuchumaa kama nawakumbuka ni beki anayetumia sana nguvu kukaba charles Ngalawa,kiungo Andrew Sanga,beki Kwame Mgongo-fimbo,anayefuatia simfahamu,mnyakyusa mwingine anayetumia sana nguvu kukaba nahodha Alune Mwassa,anyefuatia simfamau,na wa mwisho pia simfahamu
    Waliosimama kushoto,kocha Juma maswanya,anayefuatia simfahamu,kiungo mwenye kasi Sekulu"Atl boy",mshambuliaji mwenye nguvu peter "Bata"Batageki,wanaofuatia hao 4 siwafahamu,lkn namuona kijana namba 5 wetu wa kudumu Fahad"mwarab"na mwisho ni kocha Teacher
    Mnanikumbusha sana jamani,na mkienda DC mtulutee picha,sisi tupo hapa na saa hii tunaenda kula makongoro pale katikati ya jiji

    ReplyDelete
  10. Timu nzuri inacheza kitimu na inaelekea kuchukua Kombe.Alex Tibaigana Charles Ngalawa amechukua majukumu yako kwa hasira sana.Safari ya D.C Tutakupa habari .Difference bado zipo ila sio za kutisha sana zitakwisha baada ya Fainali.

    ReplyDelete
  11. Wapi wachezaji machachari niliocheza nao mechi za zamani za mataifa ya afrika, simba na yanga, dallas?,Menda-golikipa, Muddy chamsham-mkoba, Ignasi-namba nne, Dardakingi-namba mbili, Abu banzi-tatu, nakumbuka namba saba alikuwa Fred miwani, namba kumi na moja alikuwa Jenga, kipindi hicho mfungaji wa magoli yote alikuwa ni kimondo-Idi janguo. tuwakilisheni vijana.
    mbaba box mstaafu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...