Ndugu Wazalendo,
 
Kwa Masikitiko makubwa TPN inatangaza kifo cha mwanachama mwenzetu Mz. ERIC MUNISI ambaye amefariki usiku wa Jumatano Kuamkia Alhamisi akiwa usingizini. 
 
Mz. ERIC MUNISI alikuwa ni Mwanachama hai wa TPN; Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TPN; Pia alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Fortune Real Estate moja ya makampuni yaliyoanzishwa chini ya kimvuli TPN. Pia alikuwa moja kati ya Wanahisa wa Kampuni nyingine ya Ukulima na Ufugaji ya FUGALIMA ambayo pia ilianzishwa chini ya kivuli cha TPN. Mbali ya kujishughulisha na TPN pia alikuwa ni mjasiliamali ambaye alikuwa akiendesha kampuni zake.
 
Kesho saa sita kamili (Saa 6.00 Kamili Mchana) kutakuwa na utaratibu wa kuuaga mwili wa Marehemu mpendwa wetu ERIC MUNISI nyumbani kwa kijana wake maeneo ya Msasani Karibu na kwa Warioba. Kwa mawasiliano ya location tunaweza kuwasiliana na:
 
Mz. Fadhili No. 0763 820 045 
Mz. Ndanshao : 0754 266 054 
na 
Mz. Consolata Tel. 0713 334 078
 
Tumepanga kama TPN tufike msibani saa tano asubuhi. TPN itatoa barua ya rambirambi kwa niaba ya wanachama wote na TZS 200,000. Tunawaomba wanachama wote wenye nia ya kutoa rambirambi binafsi wawasiliane na Mhazini Consolata 0713 334 078 ili zikusanywe kwa pamoja na kuikabidhi familia.
 
Baada ya kuuaga,  mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro kwa Mazishi siku ya Jumanne.
 
Tuungane na familia ya wafiwa kumwomba Mungu awafariji na kuwapa nguvu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
 
Wasalaam
 
Sanctus Mtsimbe
President TPN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. TPN ni Tanganyika Packers?

    ReplyDelete
  2. Mstimbe TPN ndo nini, Maana ndo mara yangu ya kwanza kusikia TPN.
    Kwa nini usieleze kwa kirefu kwani hayamkini inawezekana kuna watu ambao ni mara yao ya kwanza kusikia hilo kama nilivyo.

    ReplyDelete
  3. kweli anony wa pili, mmojawapo wa hao unaowasema ni mimi. Hii ni sawa na kusema "kitu hicho" wakati hata hujataja kitu chenyewe.

    ReplyDelete
  4. David VillaApril 28, 2009

    Nyie TPN,kuna siku mlijitangaza humu,nikaingia kwenye website yenu nikaomba unachama,yapata miezi kama mitatu au minne hivi imepita hakuna jibu.mnanipa wasiwasi.Anayebisha tuwasiliane nimpe maelezo.atyini@yahoo.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...