
Wakuu wa Wilaya wapya, sita wanawake kati ya 15 walioteuliwa na Rais hivi karibuni wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza semina elekezi mjini Morogoro, majina na Wilaya zao kwenye mabano , kutoka kulia ni Fatma Mwassa ( Mvomero), Queen Mlozi ( Ukerewe), Fatma Ally ( Nanyumbu), Mery Silla (Arumeru), Dk Rehema Nchimbi ( Newala) na Angelina Mabula ( Mulemba)., mafunzo hayo ya awali yalifanyika kuanzia Mei 5,hadi 8, mwaka huu.
Picha na mdau wa mji kasoro bahati John Nditi.
Huyu Dr Nchimbi ana uhusiano na Dr Nchimbi yule mwingine? Wamesoma chuo kikuu kimoja udokta?
ReplyDeleteDuu! Fatuma ameenda hewani utafikiri Hasheem Thabeet!
kina mama oyee
ReplyDeleteHaya ndiyo mambo! One day "we can" mwana mama ataongoza hii nchi na mambo yote yatanyooka! Hongereni na wote wanaonekana ni kina mama wa haja! Kikwete tunakupongeza. Tafadhali ongeza kina mama kwenye serikali yako pia.
ReplyDeleteHuyu Dr Nchimbi (Rehema) ana PhD (History) na alisoma chuo kikuu cha Cape Town, Afrika Kusini.
ReplyDeleteWe annon wa kwanza kutoka kulia sio kushoto..aliepanda ni Bi-Angelina Mabula kama ni macho yangu na picha inayonieleza!!
ReplyDeleteMdau hao juu Dr Rehema nchimbi hana undugu na Nchimbi waziri. Ni Majina tu ya Ukoo yanafanana na wote ni Wangoni.
ReplyDeleteKweli kabisa anony wa 6:42. Huyo anony wa kwanza lazima ana makengeza. Aliye kwenda hewani ni angelina mabula (chata ya kisukuma maana ndio wanawake wanao kuwa warefu). Huyo fatima ni yule tunyetunye wa mwanzo kulia. Anony wa kwanza soma kwanza maelezo siyo kukariri kuwa kila picha ikiwekwa lazima itaandikwa kuanzia kushoto kwenda kulia.
ReplyDeleteHivi zinatumika criteria gani katika kuwachagua wakuu wa wilaya na mikoa? Elimu za wachaguliwa nazo zinazingatiwa? Kama hazizingatiwi, je hatufikiri kua hii inaweza kuwa ni sababu mojawapo why Tanzania mpaka leo miaka 40 na ushee baada ya uhuru hatuna maendeleo ya kujivunia? Kama ni hivyo, je hatufikiri kwamba itakua ni vyema kubadili style ya kuwachagua hawa watu?
ReplyDeleteHuwezi mchagua mtangazaji redio ati kwa kua anatangaza vizuri mpira wa simba na yanga na kumweka kuwa mkuu wa Wilaya, then ukategemea kwamba atafanya wonders kama mtendaji-muhusika (CEO) wa wilaya ama mkoa wakati hajui hata kutengeneza strategic plan ya kaidara kadogo katika ofisi isiyofahamika. Hata kama ukimweka morogoro kwa wiki mbili kumfundisha leadership and administrative skills, ingawa mda huu mara nyingi hutumiwa kuponda maraha zaidi ya kujifunza, vilevile huu ni upotevu wa resources za nchi kwani kuna watu wengi tu ambao wako qualified from the beginning na kama wangepewa mikoa ama wilaya wangeweza boresha mambo from day one wanapoingia ofisini.
Mwangalieni Obama... Kateua vijana wa miaka 20 na 30 katika administration yake sio kwamba kawapendelea, ila kwa kua anauhakika kwamba they can do the quality job to meet the specifications he wants. Not just because hao jamaa ni ndugu wa shemeji, ama shangazi wa jirani , ama ni nyumba ndogo ya zamani, ama ni nyumba ndogo tegemezi (ya future)
Lets stop huu utani watanzania. Lets get serious. Kama twataka maendeleo inapaswa kuachana na stereotypes zisizo na tija.
Kikwete, kazi kwako baba...
Wadau naombeni mnisaidie,sijui ni macho yangu au ni kweli, huyu dada Angelina Mabula nimemfananisha na Angelina Lubala!
ReplyDeleteHujakosea ndiye Angeline Lubala unaemfahamu, jina la Mabula nila mume kwakuwa wenzetu huwa wanaazima majina wakiisha olewa
ReplyDelete