
Ndugu zangu waandishi wa habari,
Naomba nianze kwa kuwashukuru nyote kwa kupokea mwaliko wangu wa kuwaita katika mkutano huu na pia kwa kuja kwenu hapa kunisikiliza. Nataka niwahakikishie kuwa nathamini sana heshima hiyo mliyonipa.
Nimeitisha mkutano huu kufuatia tuhuma nzito, ingawa ni lazima niseme pia ni za kipuuzi, zilizotolewa na Mwenyekiti wa IPP, Reginald Abraham Mengi, dhidi yangu na wafanyabiashara wengine wanne akituhusisha na kile alichokiita “mafisadi papa“, alizozitoa wakati akilihutubia Taifa kupitia kituo chake binafsi cha televisheni cha ITV tarehe 23 Aprili, 2009.
Mara baada ya kutoa matamshi yake, nilihojiwa na baadhi ya vyombo vya habari vilivyonitaka nitoe maoni yangu. Niliwaambia kuwa sitaki kujibizana na mzee mwenye umri mkubwa unaozidi hata wa baba yangu. Hata hivyo, baada ya kupata nafasi ya kuangalia mkanda mzima wa maelezo yake, na kuona athari mbaya ya uzushi, chuki na sumu iliyomo, nimeona kuna haja ya Watanzania kuufahamu ukweli hasa ulivyo.
Naelewa kwamba tayari Serikali na vyombo vyake vimeshatoa kauli za kumuonya Mengi kuhusu kauli alizozitoa. Waziri wa Nchi anayeshughulikia Utawala Bora, Mheshimiwa Sofia Simba, amemtahadharisha Mengi kwamba kitendo chake cha kutumia vibaya vyombo vyake vya habari kuwachafua washindani wake wa kibiashara hakikubaliki.
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa George Mkuchika, amesema Wizara yake inafanya uchunguzi wa matamshi ya Mengi kwa kuupitia mkanda wenye maelezo yake na ikibainika amevunja sheria atachukuliwa hatua.
Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda, amemuonya dhidi ya kuwahukumu watu ambao kesi zao bado zinaendelea Mahakamani. Na Jeshi la Polisi nalo limeeleza kumshangaa kwake Mengi kutokana na siyo tu kutowasilisha ushahidi wa shutuma zake kwa vyombo vinavyohusika lakini pia kumueleza Mengi kuwa hana jipya alilosema zaidi ya kurejea mambo yaliyokwisha fanyiwa au yanayoendelea kufanyiwa kazi na vyombo vinavyohusika. Pamoja na kuheshimu na kuthamini maelezo hayo ambayo yamemuumbua Mengi lakini bado nahisi binafsi nina wajibu wa kutoa maelezo ya kina kuhusu kiherehere hiki cha Mengi.
Kwanza, nataka niweke wazi kwamba tuhuma zote zilizotolewa na Mengi dhidi yangu ni za uongo na ni upuuzi mtupu. Tuhuma hizo ni mwendelezo wa wimbo ule ule ambao amekuwa akiuimba kwa muda mrefu sasa na tayari nilikwishazitolea kauli huko nyuma. Nilipofanya mkutano na waandishi wa habari kama huu mwaka jana, nilisema wazi kwamba sihusiki na tuhuma zote zinazoelekezwa kwangu na nikatoa changamoto kwamba iwapo wale wanaotoa na kusambaza uzushi huo wana ushahidi wa wale wanayoyasema, basi kwa sababu nchi yetu inafuata utawala wa sheria, walipaswa wapeleke ushahidi wao katika vyombo vinavyohusika ili sheria ichukue mkondo wake. Hakuna aliyefanya hivyo.
Hata baada ya Mengi kurudia tuhuma hizo wiki iliopita, nilimpa taarifa kupitia vyombo vya habari niliyoitoa tarehe 29 Aprili, 2009, nikimtaka ndani ya siku mbili (2) awe amewasilisha kwenye vyombo vya sheria vinavyohusika ushahidi wa tuhuma zake dhidi yangu kwamba mimi ni fisadi na kwamba mimi ni muuaji ninayepanga mauaji dhidi yake na watu wengine aliowaita “watu waliojitolea kupambana na ufisadi”. Kama akishindwa kufanya hivyo, basi aniombe radhi hadharani. Na nilimwambia wazi kuwa asipofanya mojawapo kati ya hayo, nitakuwa na haki ya kumuanika ili Watanzania waelewe tabia na hulka ya mtu huyu. Hakufanya chochote kati ya hayo. Na hawezi kufanya hivyo kwa sababu anaelewa kuwa alichokisema ni uzushi alioutunga mwenyewe. Ni kutokana na kushindwa kwake kuwasilisha ushahidi huo ndiyo maana nimeona sasa nifanye mkutano huu ili kuweka kumbukumbu sahihi.
Nimetafakari kwa kina athari zinazoweza kulifika Taifa letu ikiwa mwenendo wa watu kama Mengi kujipa haki ya kuchafua wale anaowaona ni washindani au wapinzani wake utaachiwa uendelee, na hasa kutokana na sumu mbaya iliyomo katika maelezo anayoyatoa na malengo aliyoyakusudia kwa kutoa maelezo hayo. Nimeona sitakuwa natenda haki kwangu, kwa familia yangu, kwa wapiga kura wangu wa Igunga, kwa Chama changu cha CCM, na kwa Watanzania wenzangu kwa ujumla iwapo nitakaa kimya.
Kuendelea kwangu kukaa kimya kunaweza kukapelekea Watanzania wakaziamini propaganda chafu za Mengi zenye dhamira potofu na ovu kwa nchi yetu. Kwa hivyo, kama mzazi na kama mwanafamilia kwa upande mmoja, na pia kama Mbunge, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambazo zote ni nafasi za kuchaguliwa nilizopewa kutokana na kuaminiwa na wale walionichagua kwa kura nyingi, nina wajibu wa kukemea uchafu na uovu unaotaka kupandikizwa na Mengi ambaye watu wanajiuliza amepata wapi uhalali wa kujifanya msemaji wa Watanzania wakati hawajawahi kumchagua katika nafasi yoyote na hivyo hana ridhaa yao.
Taifa letu limepita katika vipindi vingi vya majaribio makubwa lakini limebaki kuwa taifa imara na la kupigiwa mfano katika Bara la Afrika. Tanzania ni nchi ambayo bado wananchi wake wanapambana kuyaondoa matatizo makubwa ya umasikini, ujinga na maradhi lakini inasifika duniani kote kwa umoja na mshikamano wa watu wake, na amani na utulivu walioujenga. Haya yamefikiwa kutokana na misingi madhubuti iliyojengwa na waasisi wa Taifa hili.
Leo hii anapokuja mtu kama Mengi ambaye kutokana na tamaa, uroho, wivu, chuki, fitina, ubaguzi na ubinafsi uliovuka mipaka alio nao na kujipa jukumu la kuivunja misingi hii, sidhani itakuwa ni haki kuendelea kukaa kimya na kumwacha afanikishe malengo yake hayo. Hatuwezi kukaa kimya maana kufanya hivyo kutakuja kuligharimu vibaya sana Taifa letu.
Historia ya Mengi inamuonyesha kwamba ni mtu anayependa kuanzisha ugomvi katika mambo yanayohusu maslahi yake binafsi lakini unapopamba moto na kuona anazidiwa, hutafuta hifadhi kwa kulia lia na kutaka aonewe huruma na kutaka kuliingiza Taifa zima. Katika kufanikisha hayo, amekuwa akitumia vyombo vyake vya habari kuwapotosha wananchi ili waone anaonewa au eti anapigania maslahi yao.
Ameanzisha ugomvi na watu wa kada mbali mbali kuanzia Maaskofu hadi kikundi cha wachekeshaji cha Ze Comedy. Huyo ndiye Reginald Abraham Mengi.
Alianzisha ugomvi na wamiliki wa vituo vya televisheni vya DTV na CTN mwaka 1994 kwa hofu tu ya kwamba watakuwa washindani wa kituo chake cha ITV na akafika hatua ya kuwazushia kwamba wanataka kumuua, akaufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Alianzisha ugomvi na aliyekuwa Waziri wa Utawala Bora, Mheshimiwa Wilson Masilingi, baada ya kushindwa zabuni ya ubinafsishaji wa Hoteli ya Kilimanjaro, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima. Katika kudhihirisha jinsi alivyo mtu wa chuki na visasi, kutokana na kuikosa tu hoteli hiyo, amekuwa hakanyagi na hata hashiriki shughuli yoyote inayofanyika katika hoteli hiyo.
Akaanzisha ugomvi na aliyekuwa Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda, Mheshimiwa Shamim Khan, kwa kutakiwa afute maelezo katika maji ya kunywa yanayozalishwa na kampuni yake kwamba yalikuwa ya chemchem wakati hayakuwa hivyo, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na aliyekuwa Waziri wa Mazingira, Mheshimiwa Edward Lowassa, aliyemkanya Mengi asitumie nafasi yake kama Mwenyekiti wa Baraza la Mazingira kuwakomoa washindani wake wa biashara kwa kuwazushia tuhuma za kuchafua mazingira na kuvifungia viwanda vyao, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Basil Mramba, baada ya kumnasa akikwepa kodi katika uendeshaji wa biashara yake ya bahati nasibu ya BINGO, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na kampuni ya Habari Corporation iliyokuwa inaongozwa na Jenerali Ulimwengu baada ya kufichua habari za jinsi alivyoifilisi benki ya NBC, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na mfanyabishara Yusuf Manji ambaye kwanza walikuwa wakigombea uendeshaji wa mchezo wa bahati nasibu, na baadaye akajenga chuki naye binafsi kwa sababu tu alifanikiwa kuusuluhisha mgogoro wa Yanga ambao Mengi ulimshinda, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na Mheshimiwa Adam Malima ambaye alihoji Bungeni jinsi Mengi anavyotumia vibaya vyombo vyake vya habari kwa kutangaza habari za kujitukuza binafsi zaidi ya hata vinavyotangaza habari zinazowahusu viongozi wa kitaifa, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na mfanyabiashara Tanil Somaiya baada ya kumuona kijana huyo aliyekuwa wakala wa kuuza bidhaa za viwanda vyake Mengi (kabla ya kuviua mwenyewe), ameweza kujiimarisha na kupata mafanikio makubwa ya kibiashara hata kumshinda yeye Mengi, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Akaanzisha ugomvi na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Lawrence Masha, kwa kuja na madai ya kutaka kuhujumiwa, akataka kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima. Na orodha hii inaendelea na inaendelea.
Sasa ameanzisha ugomvi na mimi, baada ya kuona kwamba mimi nimekuwa mshindani wake mkubwa katika umiliki wa vyombo vya habari hapa nchini, anataka pia kuufanya ni ugomvi wa nchi nzima.
Huyu ndiye Reginald Abraham Mengi.
Tena kwa jinsi alivyo mtu wa visasi na chuki, akishajiingiza katika ugomvi na watu, huhakikisha kuwa habari za watu hao hazitangazwi wala kuandikwa katika vyombo vyake vya habari. Kama ni kutangazwa au kuandikwa basi huwa ni kwa kuwashambulia binafsi na kuwachafulia majina tu.
Hivi ni kwa nini tuendelee kumvumilia mtu kama huyu? Kwa nini anapokuwa na matatizo yake binafsi na wale anaowaona wabaya wake kibiashara au pengine hata kisiasa aiingize nchi nzima na wananchi wote?
Nimeamua kuitisha mkutano huu ili kuwaeleza, na kupitia kwenu kuwaelewesha Watanzania, wamjue Reginald Abraham Mengi katika sura yake halisi na dhamira zake chafu na ovu, na kumtambua kwamba mtu huyu ni nyangumi wa ufisadi katika nchi hii. Nimeamua kuwaondolea Watanzania ngozi yake ya kondoo aliyojivika ili waweze kuiona sura yake halisi ya mbwa mwitu anayojaribu kuificha. Nafanya hivi ili kulinusuru Taifa lisije likatumbukia kule Mengi anakotaka kulipeleka.
Wanasaikolojia wanasema mtu anapotuhumu wengine kuwa na tabia fulani, mara nyingi huwa yeye ndiye mwenye tabia hizo. Hiyo ndiyo hali halisi inayoonekana kwa Mengi kutokana na yale aliyoyasema katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Ukweli wa mambo unathibitisha kwamba ni yeye ndiye mwenye kuhusika na yote hayo aliyotutuhumu sisi kuwa nayo. Hapa nitatoa mifano michache tu ya ufisadi mkubwa sana wa mtu huyu.
Reginald Abraham Mengi, nyangumi wa ufisadi, alianza kuifisidi nchi kwa kushiriki katika vitendo vya ufisadi vilivyochangia kuifilisi iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), ambayo ni mali ya Watanzania na hatimaye kupelekea kubinafsishwa kwake kwa bei poa. Akitumia kampuni yake ya Anche Mwedu Limited (AML), alichukua mkopo mwanzoni mwa miaka ya 80 wa mabilioni ya shilingi ambayo amegoma kuyalipa hadi leo na kulazimisha suala hilo kufikishwa Mahakamani.
Mkopo wa kwanza ulikuwa kupitia Akaunti Nam. 6543000020 (uliotolewa kupitia Overdraft Agreements) ambao ulifikia jumla ya shilingi 3,255,429,100.75 ambao hadi Januari 1996 ulifikisha riba ya shilingi 1,737,862,471.75.
Mkopo wa pili chini ya kampuni hiyo hiyo (kupitia Loan Agreements) ulikuwa ni kupitia Akaunti Nam. 10430000008 ambao ulihusu jumla ya shilingi 386,746,631.06 hadi kufikia Januari 1996.
Mkopo wa tatu ulihusu Akaunti Nam. 654300584 (kupitia utaratibu wa Government Guarantee) ulikuwa wa jumla ya shilingi 1,803,137,210 hadi kufikia Januari 1996.
Na wa mwisho kupitia utaratibu wa heading interest on jotter/suspense account ulikuwa wa jumla ya shilingi 417,689,254.10 hadi kufikia Januari 1996.
Jumla ya fedha zote za NBC ambazo akidaiwa Mengi kupitia kampuni yake ya Anche Mwedu Limited (AML) hadi kufikia Januari 1996 zilikuwa ni 5,863,002,196.45. Fedha hizi hadi kufikia sasa 2009 pamoja na hesabu ya riba zinafikia takriban bilioni 28.
Hivi ndivyo Mengi alivyochangia kuifilisi NBC, benki ya wananchi masikini wa Tanzania. Fedha hizi zilizochukuliwa na Mengi, shilingi bilioni 28, zinaweza kujenga shule za sekondari 100 ambazo zingeweza kuwanufaisha watoto wa kimasikini wa Tanzania.
Ukiacha ya NBC, Mengi huyu anayetaka aonekane ni msafi kiasi cha kujipa uthubutu wa kuwatukana watu wengine kuwa ni mafisadi, alichukua fedha nyingi kupitia msaada wa nchi wafadhili wa “Commodity Import Support” ambazo hakuzilipa hadi leo.
Hizi ni fedha zilizotolewa kwa njia ya mkopo ili kuwasaidia wafanyabishara kuweza kuagiza bidhaa na zinaporejeshwa ziwasaidie wananchi kwa kuendeleza miradi ya maendeleo hapa nchini kama vile ujenzi wa shule na zahanati. Wafanyabishara wengi tulikopa lakini tumelipa na tunaendelea kulipa. Mengi anayedai ana uchungu na Watanzania anawaongezea umasikini kwa kuchota fedha hizo na baadaye kuruka na kukataa kuzilipa hadi leo. Kati ya fedha hizo ambazo Mengi alichukua ni kama ifuatavyo:
- Norway CIS 1988/89 IPP – Anche Mwedu- NOK (M) 6.00
- Norway CIS 1989/90 - IPP – Anche Mwedu - NOK (M) 4.00
- EEC CIS 1988/89 - Bonite Bottlers - EEU (M) 0.5199
- Japan CIS 1991/92 - Bonite Bottlers -JY (M) 160.000
-Japan CIS 1991/92 - Medicare - JY (M) 115.000
-Canada CIS 1988/89 - Anche Mwedu - C$ (M) 0.5
- Italy CIS 1988/89 - Anche Mwedu - LIRA (M) 1,774.50
- Japan CIS NPG–9-1997 - Anche Mwedu- JY (M) 20,000,000
- Japan CIS NPG–5-1994 - Bonite Bottlers - JY (M) 160,000,000
Fedha hizi zilizo katika sarafu tofauti za kigeni zikibadilishwa kwa shilingi za Tanzania pamoja na riba kwa miaka yote tokea zilipochukuliwa zinafikia mabilioni ya shilingi. Na hizi ni sehemu tu ya fedha zote alizochukua ambazo kumbukumbu zake tumeweza kuzipata baada ya kumbukumbu nyengine kupotea katika mazingira ya utatanishi. Badala ya kurejesha fedha hizi alizozikwapua robo karne iliyopita, Mengi alizitumia kujitajirisha.
Kuonyesha jinsi alivyobobea katika ufisadi, Mengi alikula njama na kushirikiana na afisa mmoja wa Hazina kutengeneza barua ya eti kuthibitisha kwamba alishalipa fedha hizo huku akijua kuwa hakulipa chochote. Pakifanyika ukaguzi huru hata leo hii itathibitika kwamba hakulipa fedha hizo na iwapo anakanusha haya, namtaka akubali kufanyika ukaguzi huo huru. Mtu yeyote wa kawaida angeshangaa Mengi amepata wapi utajiri alio nao katika kipindi kifupi namna hii lakini vielelezo hivi vinatoa majibu ya uhakika.
Tukiacha ufisadi huo, Mengi kwa kutumia nafasi yake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji yenye wajumbe watatu (3) tu ya kampuni ya NICO ambayo ni kampuni iliyoanzishwa kusaidia Watanzania kuwekeza katika biashara na viwanda, amefanya ufisadi mkubwa kwa kukiuka maadili ya kibishara pale alipoitumbukiza kampuni hiyo katika kununua hisa kwenye kiwanda cha Interchem Pharma Ltd kinachomilikiwa na familia ya Mengi, wakati akijua kwamba kiwanda hicho kilikuwa njiani kufilisika.
Huku akijua hali mbaya ya kiwanda hicho alitumia nafasi yake kuziteketeza Shilingi bilioni 2.558 fedha za Watanzania masikini wasiopungua 22,000 wenye hisa katika NICO kwa kuifanya inunue asilimia 51 ya hisa (majority shareholding). Kiwanda hicho sasa kimewekwa kwenye orodha ya kufilisiwa baada ya kushindwa kujiendesha chini ya mwaka mmoja tokea Mengi kuizamisha NICO.
Mfanyabishara wa kawaida tu anayeheshimu maadili hawezi kufanya utapeli kama huu kwa kampuni ya wananchi masikini aliyopewa dhamana ya kusimamia uwekezaji wake.
Akiwa mhasibu na mfanyabiashara alijua kuwa kiwanda hicho kinakufa lakini alitumia hila na ujanja wa kusuka mipango yote ya kuiingiza NICO katika hasara ili kunusuru kampuni ya familia yake. Ukweli huu unabainishwa katika kitabu cha Prospectus cha NICO cha Oktoba 2007. Kama amebaki na chembe ya aibu, Mengi anapaswa arejeshe fedha hizi za wanahisa wa NICO.
Ufisadi mwengine wa dhahiri uliofanywa na Mengi ni pale alipoingia ubia na Serikali katika umiliki na uendeshaji wa kiwanda cha TANPACK Industries Ltd. Bila ya kumjulisha mbia mwenzake yaani Serikali, Mengi kisiri siri alitumia dhamana ya TANPACK kwenda kukopa shilingi milioni 600 kutoka benki ya NBC na kuzitumia kwa njia anazozijua yeye. Benki hiyo ilipochachamaa kutaka ilipwe fedha zake, Mengi alitaka TANPACK ilipe lakini Serikali, ikiwa mbia, ilikataa kulitambua deni hilo ambalo haikulijua. Matokeo ya ufisadi huo wa Mengi, TANPACK ikafilisiwa na kufa.
Huyo ndiyo Reginald Abraham Mengi, nyangumi wa ufisadi, katika sura yake halisi. Anawahujumu maskini huku akijidai kwamba anawaonea huruma. Mtu muadilifu hawezi kusema anawatakia wananchi masikini mema huku anafanya maovu kama haya yanayovuruga misingi ya kusaidia masikini hao hao.
Lakini mbali na hayo, ngoja niwachekeshe kwa kuwaeleza jinsi mtu huyu alivyokubuhu katika kujenga chuki na fitina kwa kujifanya mtetezi wa wale anaowaita “wazawa“, huku akiwa na lengo la kujinufaisha binafsi kwa kutumia mgongo wa chuki na fitina hizo anazopandikiza.
Mwaka 1994, alitoa kauli zake zenye sumu ya ubaguzi pale alipodai kwamba sehemu kubwa ya maeneo ya katikati ya Jiji la Dar es Salaam inakaliwa na Watanzania wenye asili ya Kiasia na kwamba “wazawa“ hawapo katika maeneo hayo. Aliyekuwa Rais wakati huo, Mzee Ali Hassan Mwinyi, akamuagiza Waziri aliyekuwa akishughulikia masuala ya ardhi, Mheshimiwa Edward Lowassa, kumpatia Mengi eneo kubwa la ardhi katikati ya jiji karibu na ilipo International House. Lakini mara tu alipopewa eneo hilo akaliuza kwa Fida Hussein, mfanyabishara Mtanzania mwenye asili ya Kiasia. Huyo ndiye Reginald Abraham Mengi, nyangumi wa ufisadi.
Biashara pia ina maadili yake na mwenendo wa mfanyabiashara na biashara zake unaweza kuonyesha ni kwa kiasi gani anafuata au hana maadili. Mambo kadhaa ninayoyafafanua hapa chini yanatoa mwongozo wa kumjua vyema Mengi:
Inafahamika kwamba utajiri wote wa Mengi ameupata katika kipindi cha kama miaka minane, kuanzia 1984 hadi 1992. Watanzania wanapaswa wajiulize amewezaje kuwa tajiri ghafla katika kipindi hicho kifupi? Lakini hata baada ya kuupata utajiri huo, sasa biashara zake zinasuasua na zimeanguka. Amewezaje kuvurugikiwa kiasi hicho? Kwa mtu yeyote anayeelewa misingi ya biashara atafahamu kwamba Mengi hana uwezo wa kuendesha biashara.
Utajiri wake ulitokana na kukwapua fedha kupitia mipango ya ujanja ujanja na kutolipa madeni. Haya yalifanyika huku kumbukumbu zake zikipotea katika mazingira ya ajabu ya majengo kuungua na nyaraka kupotea. Alijifaidisha kwa fedha hizo na sasa zimemalizika. Amebaki kulia wivu na kuonyesha chuki kwa njia ya kutaka kuwakomoa wale anaowaona wamefanikiwa katika uendeshaji wa biashara. Asichokielewa ni kwamba baadhi yetu hatukuamka tu na utajiri bali tumetokana na familia zenye rekodi ya kujishughulisha na bishara tokea mwaka 1852 huko Tabora.
Dalili nyengine ya ufisadi wa Mengi ni rekodi yake ya kuua kampuni zake. Ni vyema ikaeleweka kuwa mfanyabiashara makini na anayezimudu biashara zake hawezi kuua kampuni.
Mfanyabiashara huua kampuni kwa ama lengo la kukwepa kodi, au kukwepa kulipa madeni, au ameshindwa kibiashara na hivyo hawezi kuiendesha tena kampuni yake. Katika kipindi chake kifupi cha kujishughulisha na biashara, Mengi ameshaua kampuni nyingi.
Baadhi tu ya kampuni alizoziua ni pamoja na Tanzania Kalamu Industries Ltd., Anche Mwedu Ltd., TANPACK Tissue Industries Ltd., Chemical Industries Ltd., Bodycare Ltd., na Medicare Ltd. Hebu tujiulize ni kwa nini Mengi anaua kampuni zake halafu anatafuta mchawi kwa wale waliofanikiwa? Bila shaka ameziua kampuni hizo kwa lengo la kukwepa kulipa kodi na kulipa madeni, mambo ambayo ni ufisadi mkubwa. Binafsi sina mchezo wa namna hiyo.
Mfanyabiashara mzalendo pia hupimwa kwa utashi wake wa kulipa kodi na kutoa ajira za uhakika kwa wananchi wenzake. Kama unawatakia heri na ni mtetezi wa wananchi masikini kama Mengi anavyotaka aonekanwe basi utatoa ajira za kudumu na za uhakika, na utalipa kodi ambayo malengo yake ni kuiwezesha Serikali kuhudumia masikini hao kwa kuwapatia matibabu na madawa katika hospitali, watoto wao kupata elimu bora na yenye manufaa, kujengewa miundombinu na hata kupatiwa chakula ikibidi pale nchi inapokumbwa na ukame au njaa.
Kama unawadhulumu wananchi masikini kwa kutowapa ajira za kudumu na badala yake kuwaajiri kama vibarua wa siku na kama hulipi kodi unawezaje kusema unawasaidia wananchi wanyonge? Mengi anafahamika kwa kutimua wafanyakazi kila mara na kutowalipa haki zao na pia kukwepa kodi huku akidai kwamba kampuni zake siku zote zinapata hasara.
Huu ni udanganyifu kwa sababu kama kampuni hizo zinapata hasara haya mamilioni ya fedha anazodai kuzitoa kama michango anazipata wapi? Katika kuendeleza udanganyifu wake na kujaribu kuchezea akili za Watanzania, Mengi amekuwa anakwepa kodi ambazo zingeweza kutumiwa kusaidia kuwaondoshea matatizo wananchi walio wengi na badala yake amekuja na mtindo wa kualika walemavu wachache na kuwapa chakula na kisha kuvitumia vyombo vyake vya habari kwa staili ya Kim Jong Il, Kiongozi wa Korea Kaskazini, ya kusifiwa na kutukuzwa kwa kuandikiwa habari, kutolewa picha na kuchapishiwa makala maalum kila siku za kumpamba.
Amekuwa akiwakaanga wananchi masikini wa Tanzania kwa mafuta yao wenyewe. Binafsi ninajivunia rekodi yangu kwamba kampuni zinazomilikiwa na familia yangu zimetoa ajira za uhakika kwa wafanyakazi takriban 6,000 na pia zinalipa kodi inayostahiki Serikalini. Ninaona fahari kusema kwamba kampuni zetu zinatambulika hata na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba zinaongoza katika ulipaji wa kodi hapa nchini. Hiki ndiyo kipimo cha uzalendo kwa nchi na siyo ule wa kutafuta kuonewa huruma kwa kuwazushia maovu watu kupitia vyombo vya habari ulivyovianzisha kukutukuza wewe na kuwachafua wengine.
Mbali ya hayo, Reginald Mengi huyu huyu ambaye amenituhumu mimi na wengine kuwa tuna akaunti za fedha nje ya nchi ambako ndiko tunakoweka fedha zetu na akadai huo si uzalendo, yeye mwenyewe ana akaunti ya fedha za kigeni nje ya nchi. Nampa changamoto akanushe kwamba hana akaunti ya fedha za kigeni nje ya nchi.
Mengi huyu huyu pia anatutuhumu sisi kutumia fedha zetu kuanzisha magazeti ya kumchafua yeye na eti “wale wanaomsaidia Rais Jakaya Kikwete kupambana na ufisadi“. Anayasema haya wakati yeye anaongoza kwa kuanzisha magazeti, tena mengine yakionekana wazi wazi kwamba yameanzishwa kupambana na watu fulani fulani ambao ni mahasimu wake kibiashara au kisiasa. Tayari ameanzisha magazeti ya The Guardian, This Day, Nipashe, Kulikoni, Sema Usikike, Taifa Letu, Alasiri, Lete Raha, Kasheshe, Acha Umbeya na mengine mengi anayoyafadhili kwa mlango wa nyuma. Hivi yeye amepata wapi fedha za kuanzisha magazeti haya yote?
Kwa muda mrefu nilikuwa nikihisi kuwa Mengi ndiye aliye nyuma ya kampeni zote chafu za kutuchafua baadhi yetu. Siku zote amekuwa akikanusha hilo kwangu lakini sasa amejianika na kujidhihirisha wazi kuwa ndiye kinara wa mbinu hizo chafu.
Wakati fulani mwaka jana, akiwa hewani umbali wa futi 35,000 kutoka usawa wa bahari, aliwaambia watu aliokuwa nao kwamba Jumatano inayofuata “tutammaliza Rostam katika MWANAHALISI”. Nilipopata habari hizo nilimpigia simu na yeye alikanusha vikali kuwa hakutamka maneno hayo. Nilimuamini lakini ilipofika Jumatano, kweli MWANAHALISI lilikuja na habari ya kunichafua kama alivyokuwa ameahidi Mengi.
Katika kipindi cha takriban mwaka mmoja uliopita, nilipata taarifa kwamba ni Mengi ndiye aliyekuwa akiendesha na kusimamia kampeni ya kunisakama kwa kupika na kusambaza habari zote chafu zilizolenga kunichafua. Nilipoonana naye kumueleza juu ya taarifa hizo, siyo tu aliruka sana bali pia aliapa kwa jina la mama, mke na mtoto wake kwamba hahusiki kabisa na kampeni hizo na kwamba hata yeye anakerwa nazo. Kujitokeza kwake wiki iliopita na tuhuma chafu dhidi yangu zisizo na ushahidi wowote sasa kumeweka kila kitu hadharani kwamba yeye ndiye kinara wa uchafuzi huu wenye lengo la kuleta chuki na mifarakano katika nchi.
Najua atakanusha haya kwa sababu yeye ni mwepesi wa kulalamika kuwa anaonewa huku akidhani amepewa haki na Mungu ya kuonea wengine.
Kwa upande mwengine, tabia na mwenendo wake havishangazi sana. Anaonekana kuchanganyikiwa. Hatua ya mzee wa zaidi ya miaka 70 anapofikia kuwaita wengine wauaji pasipo kutoa ushahidi wowote na pia kurejea madai ya kutaka kuuliwa au kudhuriwa mara kwa mara ni dalili ya kuchanganyikiwa. He is a paranoid old man!
Ni vyema Watanzania wakafahamu kwamba kila anapokabiliwa na matatizo au anapotenda maovu, kimbilio lake la haraka la kujifichia limekuwa ni kusaka huruma kwa wananchi kwa kutaka aonekane ni sehemu yao na kwamba anaonewa kwa kuwatetea wao. Ukweli ni kwamba amekuwa akifanya hivyo ili kutafuta hifadhi na kinga akijua ana madhambi mengi.
Kwa ufupi, Reginald Abraham Mengi ndiye kinara wa fitina zilizoivuruga nchi na hata kujaribu kuvuruga mipango ya Serikali ya kuwatumikia wananchi na kutekeleza ahadi zake. Halafu mtu huyu anapata ujasiri wa kudai eti anamuunga mkono Rais Jakaya Kikwete. Ameingiza vurugu kila mahala alipotia pua yake. Nchi imekuwa haiendi. Kila kukicha, shughuli imekuwa ni porojo zake na malumbano tu yanayotumia muda mwingi ambao ungeweza kutumika kuendeleza nchi na wananchi wake.
Niseme kwamba tofauti na yeye ambaye ameishia kutoa porojo zake bila ya kutoa ushahidi wowote na kufikisha hoja na ushahidi wake kwa vyombo vya sheria vinavyohusika, mimi nawagawia hapa baadhi tu ya ushahidi wa ufisadi wa Mengi ambao pia nakusudia kuuwasilisha pamoja na maelezo haya kwa vyombo hivyo ili wamchunguze Mengi na kuchukua hatua zipasazo. Kwa upande mwengine, nimewaagiza wanasheria wangu kuzifanyia kazi tuhuma za uzushi alizozitoa na kuchukua hatua za kisheria zinazofaa dhidi yake.
Nimalizie kwa kusema Reginald Abaraham Mengi hana mamlaka wala nguvu ya kimaadili (moral authority) ya kuwanyooshea vidole wengine kwa kuwaita mafisadi wala ya kujifanya ni shujaa wa kupambana na ufisadi. Sote tunakubali kwamba kuendesha vita dhidi ya ufisadi ni lazima lakini wale wanaopambana ni lazima vile vile wawe watu safi. Ukweli wa maelezo haya unaonyesha wazi kuwa Mengi hana sifa hiyo bali ni nyangumi wa ufisadi anayejaribu kuficha ufisadi wake kwa kuchafua watu wengine. Watanzania si wajinga kama anavyodhani yeye. Wanaelewa mchele ni upi na pumba ni zipi.
Nawashukuru kwa kunisikiliza.
Ahsanteni sana.
Safi sana Mhe RA. Sasa baada ya kutumegea uchanganuzi wa ufisadi wa RM, tunaomba utumegee uchanganuzi wa ufisadi wako mwenyewe ili tuweze kulinganisha na kulinganua nani fisadi papa na nani fisadi dagaa!!!
ReplyDeleteHii kali, duuhhh
ReplyDeletewote mafisadi tu,Mengi ni fisadi,Rostam Aziz ni fisadi na vikundi vyenu vyote.Watanzania tushaliwa tu,hata Michuzi ni Fisadi,najua hutatoa comment yangu ,lakini wewe ni fisadi wa kutotoa comments za wanaume.
ReplyDeleteONYO;IPO SIKU MOJA KIWEMBE KITAWARUDIA.
MBIO ZETU TOKA UHURU MPAKA HAPA TULIPO...sheria ifate mkondo wake kujua kati ya hawa wawili nani ni papa/nyangumi..nakaribia kupasuka kichwa na nachelea kusema Tanzania bila Mwalimu ni sooo.
ReplyDeletewanasema mafahari wawili wanapozichapa zinazoumia ni nyasi...
ReplyDeletehapa kunawezekana wamedhulumiana kama si kuibiana mabibi....
sisi yetu macho na masikio, ila wasije wakachapana risasi tu.....
ni bora kuwa maskini na mwenye amani ya mawazo, kuliko tajiri mwenye msongo wa mawazo.....
kila la kheri, huo ndio uhuru wa kujieleza.....
Michuzi usitujazie nafasi watu wote ao awana shida ya kununua unga nusu na robo,Wanatuyayusha tuu.
ReplyDeleteRostam mbona leo ndio unajitokeza? Sikuzote umesemwa na watu wengi Kuhusu Richmond,Dowans na Kadhalika huku jitetea....hapa naona umepata pa kukanyagilia jibu kwa nini watu wa Dowans wanatumia emails za Caspian na vitu msingi kama weka aliyowasema mengi Hadharani kanusha sio kutuletea mengine...tafuteni pakupigania mtatuumiza wananchi bure!
ReplyDeleteNi heri ungeendela kuchuna kama ulivyokuwa umefanya mwanza hapo umeharibu Ndugu.
Mdao aliyeshindwa kukaa kimya!
huyu Rostam Aziz asitake kujifanya ana uchungu na nchi tena ukome kabisa kujidai eti watanzania wenzangu hakuna mwenzako hapa utajiri wote ulio nao ?
ReplyDeletekwanza ungekuwa huna kosa usingemmaind mengi mwarabu koko wa igunga!
michuzi ukinibania hii nakuhesabia kama fisadi na ukija sweden nakuzomea LOL kumradhi bro huyu jamaa rostam ananikera sana
Jamaa kasema kweli huyo Mengi ni mbaguzi mkubwa anayetumia vyombo vyake vya habari kwa manufaa ya ufisadi wake. Tusubiri majibu yake kama ana jipya lolote.
ReplyDeleteYeees michuuuz anashusha vituuuuz!
ReplyDeletethanks for the latest
Sasa hatuko mbali sana na yaliotokea kenya, Hao wezi walioamua kuumbuana, yangu macho! Huyo rostam anamsaidia mwenzie kueleza jinsi biashara zake zilivyoanza na hata anaeleza wazi kwamba ni mikopo ya benki hii imekaa vizuri lakini yeye anabiashara ambazo hazina mwanzo zinakulupuka na kuwa na mitaji ya mabilioni ambazo hatujui kazitoa wapi mimi nafikiri huyo meneja wa kampeni za uraisi anajua kinachomfata na atakiona sasa maana tumemshutukia.
ReplyDeleteMweeeeee Watanzania tumekwisha! Hivi hii mikopo haina mikataba? YA ALL ECONOMIST NEED TO SHRED YOUR CERTIFICATES AND GO BACK TO SCHOOL! I'm really pisssed with this nosense in Tanzania. We need to implement some credit history system. Yaani mtu anachukua mkopo wa kwanza, wa pili wa tatu na wanne. Na eti hata mmoja hajalipa! This is amazing. Kwani Bank hazina uwezo wa kuangalia history ya mkopo ya mtu kabla ya kumpa mkopo? Ama kweli hii serikali ya Tanzani na wanausalama wamelala. How could one person hujumu nchi like this na viongozi wanajua huyu Mengi anafanya nini and amazingly they do not do anything? Na zaidi eti anaingia ubia na serikali hii, men I feel like like crying, kama haya yaliondikwa ni kweli, basi watanzania sisi ni wapuuzi wa hali ya juu!
ReplyDeleterostam aziz anamtuhumu mengi kwa kukopa, lakini kukopa sio dhambi na kuna bankrupcy laws kama mtu akishindwa kulipa
ReplyDeleteyeye rostam hajakopa bali ni mwizi
michuzi usibane hiii
kweli sisi wajinga kweli mengi na rostam ndio wanaowakilisha serikali kwa kutaja mafisadi serikali mkoo wapi jamani mnawafanya wananchi wajinga namna hii aibu tupu .hivi hatuna kazi zaidi kuzungumza maendeleo na kukaa kusikiliza mambo ya mengi na rostam kweli serikali inavuta mdaa tuu .mtu kama mengi yeye mfanyabiasha inakuhusu nini mambo ya mafisadi wakati wewe mfanyabiasha huko ni kwishiwa kiuchumi na rostam kama kweli msafi asingemzungumzia mengi angenyamaza ,sasa sisi hatuna kazi haa mengi haa rosatm kweli tuna akili.serikali iko wapi iseme ipo kwa mengi au rostam au kwa wananchi nini huu ujinga wakutangaza habazi huyu yupo hivi badili ya kutafuta maaendelo ,hata kama rostam kaiba kweli wewe mengi unafikiri kutakuwa maendeleo kwa wananchi .
ReplyDeleteHuyu Rostam ni hatari sana tena sana. Hana aibu hata chembe katika moyo wake na sura yake. Huyu ni fisadi aliyebobea na nadhani suluhisho ni lazima adhibitiwe la sivyo tutalia sana na hii kero ya ufisadi bila ya kupata suluhisho. Serikali mpo wapi nyie vibaraka wa hawa mafisadi papa. Kumbukeni wananchi wanateseka mbona mnaelea huyu muuaji? Ni madhara mangapi ameyasababisha katika muda wote huu alioachwa akiendelea kufanya mambo yake. Asitufanye sie wote mabwege hapa, hatari yaja tuwe waangalifu jamani.
ReplyDeleteMkiona Michuzi amebadilisha gari mjue ni pesa aliyokatiwa na Rostam kwa kuweka hii article hapa, Rostam anajua hii blog ya jamii inatembelewa na watu wengi!!
ReplyDeleteWajinga ni sisi tulio liwa.Sio Uongo kwamba nchi hii imefilisiwa na Waasia. Hawa jamaa wanakuja Tanzania wakiwa hohehahe lakini muda tu, eti ni matajiri wa kutupwa. Wamefanikiwa wapi hilo? WIZI
ReplyDeleteNi waasia ndio walio ifilisi NBC Rostam hajui hilo.
Sisi watanzania tusiwe wajinga na huyo Rostam asitufanye wajinga. MEngi hata kama alikopa mihela yote hiyo alifuata utaratibu. Deni kama ameshindwa kulilipa wanaopaswakumdai kwa utaratibu ufaao ni wakopeshaji. Hatuwezi kumlaumu mkopaji. Sasa Rostam atueleze hiyo mihela yake aliipata wapi?
Sasa Rostam anajinona msafi basi ajibu tuhuma za Richmond. Data tunazo na akicheza tutazianika zote. Vipi Kagoda? Data tunazo, na ajibu kama ni mwanaume. Doweans JE?
Nirudie Mengi alikopa na data zipo wazi. Je Richmond data zake zi wapi? Kagoda zi wapi?
Tumuulize Rostam, Mengi ameshtakiwa wapi? Lakini wao waliotajwa na MEngi wana kesi za kujibu. Ninakubali kwamba mfungwa ni innocent hadi ahuklumiwe, lakini pia tujue Lisemwalo lipo na kama halipo laja.
Si ajabu hao walioshtakiwa wataachiliwa na kuitwa wasafi kwani wana uwezo wa kubadili sheria ka mihela yao huku kibaka anaye iba mboga sokoni kwa ajili ya kupata mlo wa siku anapigwa kufa. Hilo li wazi na tumelizoea na hivyo kamwe hatungojei eti hadi sheria ichukue mkondo wake kwani sheria nazo kuna dalili za kupindishwa. LLakini ukweli unabakia kwamba HAO WAASIA ni Wezi wakuu.
Ninamsifu sana Mchungaji yule aliye waita MAGABACHOLI. Zamani tulimwona mpuuzi leo ukweli unaonekana wazi.
NIna msifia sana Id Amin. Aliwatimua sio kwamba alikuwa mjinga bali alijua cha kufanya. Hawa jamaa ni wezi wakubwa sana, na ukweli unaonekana sio hapa Tanzania tu bali hata na kule Kenya mlisha sikia. KWanini ni wao tu? KWa sababu ni WEZI wakubwa. Walahi hii nchi itafikia mahala tutaondoka na roho za hawa wezi wakubwa wasio jali mtu mweusi.
Mengi anawajali sana wafanyakazi wake. Hebu ulizia ma hausgeli wa wahindi na vjana wanao piga box kwao wanatendwa vipi. Jamani msiseme. Wanakula mateso.
Hawa jamaa wameinunua nchi sio kidogo. Akina Sofia Simba ni nani hajui kwamba kipindi cha kampeni alikwenda kuwalilia wkampa fungu la kufanyia kampeni? Au anahitaji tutoe siri nini. Hawa mawaziri wanao watetea nyie muwaone hivi hivi tu. Wakifika majumbani kwa hawa Waasia wanajikunja utadhani ni mbwa kaona Chatu, shikamoo nyingi na kuomba kama mtoto mdogo. Na hawa jamaa wanafahamu hilo hivyo wanawafungia kitita cha kampeni na hao akina Sofia SImba wanakurupuka wasijue watalipa fadhila siku. Ndio sasa tunamwona waziri anajaribu kusimama na kudai eti jamaa ni wasafi na Mengi ndio mbaya. Mjinga wa mwisho huyo anauza ndugu yake kwa vijisent vya kupigiwa kura. Wakome na kweli tusiwachagueni watu wa namna hii kamwe. Nywiiiii!
Asante Mh Rostam kwa kujibu mapigo na kutufafanulia kwa uwazi. Na tunashukuru kwa kutupa mwanga umma wa watanzania haya mambo yanavyokwenda. Mambo uliondika hapa ni mazito ambayo itachukua muda kidogo kwa wananchi wengi kuyaelewa, na tunategemea kwamba vyombo vya sheria pia vinafuatilia. Nadhani pia kuna kesi kati yenu inayoendelea ambapo
ReplyDeletemafisadi papa watajulikana.
Kikubwa amabcho Mengi amekianzisha na tunachokitaka ni kampeni ya kupambana na ufisadi. Inawezekana jina lako liko kimakosa ni kiasi cha kujisafisha na kushirikiana kuendeleza mapambano. Inawezekana Mengi naye anahitaji his own reality check naye ni kumsafisha. Lakini lengo ni vita dhidi ya ufisadi and you can be a suspect and all you have to do is to prove innocent.
Reginald Mengi hata kama ni Fisadi mali zake zinaliwa na wanyonge pia,Rostam anazipelekwa kwao Uarabuni!!! Big up Reginald Mengi kwanza anfanya Investment hapahapa bongo watu wanafaidika in one way or another! Vya Rostam anakula na Mafisadi wenzie tu hatuoni lolote la kutusaidia watanzania!!Reginald Mengi kawafanyia wanyonge mambo mengi mazuri ambayo hakuna hata fisadi mmoja anayewaza kufanya hivyo hata kama ni 0.001%,angalieni walemavu hizo baiskeli wanazoendesha nyingi zimekuwa donated by Mengi,anapeleka watoto India matibabu ya Moyo just to mention few achilia mbali wanafunzi wa vyuo vikuu wengi anawasomesha! Rostam kashafanya nini kwenye jamii!! Rostam tatizo sio Reginald Mengi,tatizo unakula peke yako....vitoe na masikini tuvione tujengee hata hospital basi kama alivyotujengea Mengi hospital ya Magonjwa ya Moyo! Rostam jitolee hata kusomesha watoto yatima wewe unataka wako tu ndio wakasome Ulaya!! Rostam Tugawie na sisi basi hizo mali zako,Nenda zako Rostam najua hata nikija kukuomba msaada hutanpa hata shilingi kumi na kama utataka kunipa ni lazima uitishe waandishi wa habari na uonekane kwenye Runinga,uliza wale wagonjwa wanaopewa msaada na Mengi pale Ocean Road Hospital kama Mengi ameshawaweka kwenye Runinga yake au waulize wanafunzi wa vyuo vikuu wanaosomeshwa na Mengi wakuambie! Mengi uko juu,nami nakuombea mema siku zote...Nakubali kuwa hakuna aliye mwema chini ya jua lakini ikumbukwe kuwa Wema husitiri wingi wa dhambi!!!!..by makiromaro@yahoo.com
ReplyDeleteMengi ni mnafiki hana lolote. sasa kuwaita walemavu na kula nao mlo mmoja wakati unaiba mabilioni ya fedha za maskini ni kitu gani kama sio unafiki. unajifanya mtu mwema na kasauti kako ka kijizijizi ili tukwonee huruma! tumekufahamu baba huna lolote mwizi mkubwa weee.
ReplyDeleteHapo Rostam atakimbilia ohhh watanzania wabaguzi wa rangi...nyie subirini mtasikia!!!! Rostam kubali wewe ni Fisadi ukweli unauma!!
ReplyDeleteEndeleeni Kugombana sie tufaidi na Undani wenu.
ReplyDeleteKaka michuzi hao wanaume wote ni mafisadi. Wanatupigia kelele kwani wengine hatujui hata tutakula nini kesho! Vyombo husika viwachukulie hatua inayopaswa, uzuri wamejitaja wenyewe!
ReplyDeleteWOTE MAFISADI HAMNA ATAKAEPONA! MENGI HUNA MPYA UKIONA WENZAKO WANANYOLEWA ZAKO TIA MAJI,ROSTAM FISADI,NA MENGI FISADI WOTE MAFISADI WACHAFU SI WIZI TU ATA MAFISADI WA WANAWAKE KILA CFA MNAZO NYINYI, AIBU SANA MWANAUME MZIMA UMEVAA SUTI UNAKAA KWENYE SCREEN UNAMKASHIFU MWIZI MWENZIO HATUNA INTEREST NA UGOMVI WENU TUNATAKA MKONO WASHERIA UWAADABISHE KM MLICHUKULIANA MABIBI AU WIVU ITS NONE OF OUR BUSINESS. MENGI KIUMRI NI MKUBWA KWAREKODI YAKO ULIYOIWEKA TANZANIA UMEINYEA MWENYEWE HESHIMA IMEPUNGUA KWANZA KUCHEZA NAWATOTO WADOGO ETI UMEOA BINTI SAWA NA MWANAO WA MWISHO, FINALI UZEENI MRUDIE MKEO MKAZEEKE PAMOJA, HIZO NILAANA ZAMKEWE, ACHA UFISADI UTAFIA GESTI,TENA URUDI MACHAME UKALIME USITUTIE AIBU WACHAGA KM UMEFILISIKA NENDA KALIME MACHAME KM SWAI KIPARA HUKO NI KUCHANGANYIKIWA NAFKIRI FAMILIA YA MENGI WAKAMPIME AKILI ANA MATATIZO YA AKILI UTAKUFA KIFO KIBAYA, HAONI HAYA KUGOMBANA KILA CKU YEYE TU TENA NAWATOTO WADOGO WIVU TU WAMEPATA HELA ANATAKA TAJIRI AWE YEYE TU, WAPO WATU WENYE HELA ZAO WAKO KIMYA HAWAITAJI KUJINADI KINA MKONO. NA ROSTAM KM NI BIFU HATUITAJI KUJUA MNA UGOMVI GANI KWENYE MASKIO YETU SISI TUNAWAZA TUTAKULA NINI? HELA ZETU MMESHAIBA ZAKUTOSHA MZIRUDISHE. KAZI KUJIKOMBA KWA MASKINI HALI MKIJUA MNATUMIA MGONGO WETU KUJINUAISHA SHAME ON YOU! TENA TUSIWASIKIE TENA MKOME HUKO HUKO. MENGI NAONA UNAKARIBIA KUFA NENDA KWA SHEIKH YAHYA AKAKUTABIRIE HATIMA YA MAISHA YAKO IKIWEZEKANA AKUONGEZEE CKU NAONA ZIMEISHA. MKEREKETWA.
ReplyDeleteWOTE MAFISADI HAMNA ATAKAEPONA! MENGI HUNA MPYA UKIONA WENZAKO WANANYOLEWA ZAKO TIA MAJI,ROSTAM FISADI,NA MENGI FISADI WOTE MAFISADI WACHAFU SI WIZI TU ATA MAFISADI WA WANAWAKE KILA CFA MNAZO NYINYI, AIBU SANA MWANAUME MZIMA UMEVAA SUTI UNAKAA KWENYE SCREEN UNAMKASHIFU MWIZI MWENZIO HATUNA INTEREST NA UGOMVI WENU TUNATAKA MKONO WASHERIA UWAADABISHE KM MLICHUKULIANA MABIBI AU WIVU ITS NONE OF OUR BUSINESS. MENGI KIUMRI NI MKUBWA KWAREKODI YAKO ULIYOIWEKA TANZANIA UMEINYEA MWENYEWE HESHIMA IMEPUNGUA KWANZA KUCHEZA NAWATOTO WADOGO ETI UMEOA BINTI SAWA NA MWANAO WA MWISHO, FINALI UZEENI MRUDIE MKEO MKAZEEKE PAMOJA, HIZO NILAANA ZAMKEWE, ACHA UFISADI UTAFIA GESTI,TENA URUDI MACHAME UKALIME USITUTIE AIBU WACHAGA KM UMEFILISIKA NENDA KALIME MACHAME KM SWAI KIPARA HUKO NI KUCHANGANYIKIWA NAFKIRI FAMILIA YA MENGI WAKAMPIME AKILI ANA MATATIZO YA AKILI UTAKUFA KIFO KIBAYA, HAONI HAYA KUGOMBANA KILA CKU YEYE TU TENA NAWATOTO WADOGO WIVU TU WAMEPATA HELA ANATAKA TAJIRI AWE YEYE TU, WAPO WATU WENYE HELA ZAO WAKO KIMYA HAWAITAJI KUJINADI KINA MKONO. NA ROSTAM KM NI BIFU HATUITAJI KUJUA MNA UGOMVI GANI KWENYE MASKIO YETU SISI TUNAWAZA TUTAKULA NINI? HELA ZETU MMESHAIBA ZAKUTOSHA MZIRUDISHE. KAZI KUJIKOMBA KWA MASKINI HALI MKIJUA MNATUMIA MGONGO WETU KUJINUAISHA SHAME ON YOU! TENA TUSIWASIKIE TENA MKOME HUKO HUKO. MENGI NAONA UNAKARIBIA KUFA NENDA KWA SHEIKH YAHYA AKAKUTABIRIE HATIMA YA MAISHA YAKO IKIWEZEKANA AKUONGEZEE CKU NAONA ZIMEISHA. MKEREKETWA.
ReplyDeleteRostam bado wewe ni fisadi tuuuu, hata ukijifaraghua.Nenda mahakamani kama kweli siyo fisadi papa na hizo data zako. siyo kutuzingua watanzania.Tunakufahamu vilivyo wewe ni fisadi.
ReplyDeleteduh unajifanya unauchungu na wa tz wakati ww mrani sio la raia wa tz.rostamu.mwizi wa mali za umma na kibaka unastaili kuchomwa moto ka kibaka wengine.misupu usinibanie mimi maana ntakuimbia wimbo wa taifa buree
ReplyDeleteNi matumaini yangu makubwa, kuwa tunavumilia huu ujinga wa wafanyabiashara hawa, tukitegemea kuwa vyombo vya sheria, vinawasikiliza, vikitegemea watatoa moja au zaidi ya moja, clues za kesi za kifisadi, au wizi, ambao umeshindikana kushtakiwa mtu hadi sasa.
ReplyDeleteNadhani PCCB wanapata some inputs kujaziamashimo yao katika kesi pending, au dondoo walizoshapewa na wasamaria wema hapo kabla, tunataka wawaite hao wawahoji, kama kuna kesi basi watulipe fidia japo kwa kukaa rumande siku moja.
Tanzania hoyeee!
Michu,
ReplyDeleteHuyu bwana Rostam maneno mengi ila point ni zero,wengi amewataja hapo wagomvi wa mengi inaonekana kabisa anawatetea majina yale yale ambayo tz wanalia nayo,
second,hizo habari zote za mengi it looks personal ya kwamba issues btn mengi himself na huko alikokopa hizo hela wether amerudhisha au hajarudisha its between him na hizo campuni as long as hakuumiza mtanzania na hata hiyo crdb its btn him and that bank nothing to do with goverment,yeye mengi na hiyo bank ndiyo wakabane.huyu muhindi anajitetea pumba,he sounds so desparate and guilty.
mengi ni fisadi na hafai kwa jamii,ingekuwa china ni kunyongwa hadharani,huyu ni muhujumu uchumi.nashangaa chadema kumtetea,au ndo damu nzito kuliko maji
ReplyDeleterostam kiboko,kamchambua mengi inavyotakiwa,ilobaki awape takururu document ili mengi adandie karandinga fasta kwenga segerea.juku uraiani hatufai tena.
ReplyDeletehey huyu Rostam asijaribu kujifanya kinara kupambana na Mtanzania mzalendo,mimi binafsi huyu Rostam na shutuma zake bado hajaniconnvice lolote,swala la mafanikio ya mengi katika kipindi cha miaka 8 kama alivyosema kinahusiana vipi? kama ni hivyo sasa haina maana ya watu fanya biashara na kupata mafanikio,Rostam rudi kwenu na Naomba Rostam achunguzwe kuhusu uraia wake kabla mambo ya uraia wa nchi mbili haujapitishwa Tanzania sababu mpaka hapo tayari analidanganya Taif kua yeye ni Mtanzania,nipo kwenye nchi ya ubaguzi sana so sioni kama hili ni kumbagua Rostam kwa sababu tu ni mweupe,hapana nataka tu kuona ni jinsi gani anakiuka sheria za nchi yetu
ReplyDeletemichuzi mie hapa nachanganyikiwa labda sababu sipo tanzania hv kwani mengi aliita vyombo vyote au alitumia chombo chake tu maana nilisoma habari zake kwenye magazeti yote kupitia mtandao sasa hapa wanavyosema mengi alitumia vyombo vyake nashindwa kuelewa kabisa!pia ingekuwa mie ndio serikali hapa ningewachunguza hawa jamaa wote wawili na hata hao kina manji maana hapa nilichojifunza kwamba kuna michezo michafu hawa wote wanaicheza sasa kuna sababu za msingi kwao ambazo sie hatuzijui ndizo zinazopelekea kuoleana siri zao za jinsi wanavyo dhulumu mali za wananchi wa tanzania kama mafisadi!!!tunaomba serikali ikamate wote hawa na kuwafanyia uchunguzi kama kweli shutuma wanazotupiana zina ukweli!pia nawaomba sana viongozi wa tanzania waache kushabikia mafisadi bali wakae katika upande wetu sisi wananchi nasima hivyo kwasababu nimeshaona dalili mapema baadhi ya mawaziri wameshajiingiza upande mmoja kwenye hii ishu ya rostam na mengi!mungu ibariki tanzania mungu ibariki africa inauma sana tunapoona mali za watanzania zinabinafsishwa kila kukicha kumbe kweli kuna ufisadi ndani yake hz ishu za NBC sie tulikuwa hatuzijui kabisa na tunakoenda tunaweza kuja kujua mengi sana ngoja na mie niwe naziandika kwenye notebook yangu hz tuhuma kama kumbukumbu ili na nchi ikija uzwa niwe najua ni nani na nani wamehusika!!!
ReplyDeleteKumekucha mengi namjua ni fisadi siku nyingi lakini sasa anaumbuka safi sana!!!! hakuna msafi bongo bora lifumuke vita kama sierra leone tu hamna lolote
ReplyDeleteSPIKA wa Bunge la Tanzania Samuel Sita, amewataka wafanyabiashara na wanasiasa wanaotuhumiana kupitia vyombo vya habari kuachana na tabia hiyo na kuziacha sheria za nchi zichukue mkondo wake.
ReplyDeleteAkijibu swali kutoka kwa mmoja wa wanahabari aliyetaka kujua maoni yake kuhusiana na wafanyabiashara wanao hukumiana kwa kuitana mafisadi, Sita alisema kitendo hicho siyo kizuri kwa sababu kuna sheria.
"Nasita kidogo kuwasema wafanyabiashara kwa sababu labda wana maslahi yao binafsi, lakini suala la kuhukumiana siyo zuri, tuache sheria zifuate mkondo wake, kama mtu tayari kafikishwa mahakamani tuache mahakama ifanye kazi na pale itokapo hukumu ndio tumuite fisadi au majina yote yale mabaya," alisema Sita.
Sita ambaye alikuwa mgeni rasmi katika siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, aliyasema hayo jana nje ya ukumbi wa Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Mapema wakati akitoa hotuba yake Sita aliwataka wanahabari kutokubali kutumiwa na wanasiasa na matajiri ili kutoa habari zisizo na tija kwa nchi pamoja na kuingiza chuki na ubinafsi.
Patamu hapo lete uhondo sisi yetu macho tu, kumbe kuna mengi yamejificha masikini Tanzania.
ReplyDeleteMENGI NI FISADI NAMBA1 TANZANIA HAKUNA ASIEJUA HILO!!KAJITAJIRISHA SANA KWA KUPITIA UONGOZI MBOVU.
ReplyDeleteANATUMIA KIVULI CHA UZALENDO KUJINUFAISHA YEYE BINAFSI
MENGI NA MAFISADI WENZIE WA KIHINDI NA HATARI KWA TAIFA LETU.
ReplyDeleteASITUDHARIRISHE KWA KUTUMIA UMASKINI WETU KUJINUFAISHA BINAFSI.
MENGI ANATUTUKANA WAZALENDO ANAFIKIRI SISI NI MAMBUMBU KIASI HICHO?
YESI LILIPUANENI NCHI IFAIDIKE TUJUE MADHAMBI YENU!!SAFI SANA MAANA WANANCHI HOHE HAE TUTAPATA WAPI DATA HIZO.
ReplyDeleteHII NDIO STAIRI MAFISADI MAMBO YAO YANAVYOTAPAKAA MTAINI HUA TUNAPATA DATA KWA STAILI HII
Anasema "Watanzania si wajinga kama anavyodhani yeye. Wanaelewa mchele ni upi na pumba ni zipi"?!
ReplyDeleteWatanzania Tungekuwa si- wajinga "kama anavyosema Rostam", Nyie mafisadi wala msingekuwa viongozi wetu Kamwe!!
Mheshimiwa rostam.hupo katika madaraka muda mrefu.je haya ulikuwa unayajua muda mrefu? na kama ulikuwa unayajua hayo ulichangia nini kuokoa mali ya watanzania ambao wamekuchagua?je kuna watu wangine ambao unaweza kutupa majina yao na figure zao ambazo wameliebia taifa hili.
ReplyDeleteRostam amechelewa kutoa tuhuma na data hizo kwa wananchi. Huu ni muda wake wa kukanusha na kuwaeleza wananchi ni kwa vipi yeye si FISADI PAPA, si muda wa yeye kutuonesha nani fisadi zaidi yake (FISADI NYANGUMI). Amechelewa kusema kwamba mengi ni fisadi na anaonesha hana uchungu hata chembe na TAIFA hili, yeye akiwa kama mwanasiasa, mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM na mbunge wa wananchi, alikuwa na nafasi ya pekee ya kuanika uovu huo wa Mengi ndani ya chombo husika (Bunge) tena kwa muda muafaka. Haileti maana tena wakati anapoona ameumbulia na yeye ndo aanze kutapa tapa, huku nikuonesha kwamba alikuwa analinda maovu ya mwenziwe ili na yeye yake yalindwe! Huyu Rostam ndo ametudhihirishia wananchi kwamba kuna mengi maovu yanafanyika hapa nchini na hao wafanya biashara na wanasiasa lakini yapo chini ya carpet mpaka watofautiane kimaslahi ndo siri huvuja! Hali inatisha, ukiangalia kiundani utagunduwa kwamba kumbe nchi hii ni mali ya wafanyabiashara wachache, viongozi wetu wapo kama NEMBO tu, na sisi wananchi ni sehemu ya bidhaa za hao so called matajiri wa Tanzania!
ReplyDeleteKwa maelezo ya Rostam ni wazi kwamba anawaambia wananchi kwamba yeye nifisadi (papa) lakini mengi kamzidi kidogo nifisadi mkubwa (nyangumi). Wananchi we will make no distinction kati ya papa na nyangumi, wote ni mafisadi shimo lenu moja...!
Mungu mkubwa. Nimekubali jasho la masikini haliliwi.Anachosema Mr RA ni kuwa yeye ni fisadi lakini RM amemzidi. Sawa tumeliona hilo lakini je tatizo ni kuwa amekasirika kutajwa na fisadi mwenzake au ni kuwa ameonewa kwa sababu yeye ni mdogo kiufisadi kwa aliyemtaja? Watanzania inabidi tujiulize mara mbili mbili. Juzi RM alibanwa na Waziri wa Utawala bora pamoja na waziri wa habari kuwa amekiuka utaratibu wa nchi. Je mbona hawajajitokeza kumkaripia RA??? Watanzania hapa kuna jambo, na tusipokuwa makini tutamezwa na hawa mafisadi. Ni kweli unapotaka kupambana na ufisadi ni lazima uwe msafi lakini je wasafi wana sauti katika nchi hiyo iliyobatizwa kuwa nchi ya kimaskini na ufisadi? Hamna cha ubaguzi hapo, RA ni fisadi na aache kulalamika kutajwa... Ninachoomba ni vyombo husika kufanya kazi yake.. Lakini je vitaweza fanya hivyo wakati vishaanza kumtetea RA.
ReplyDeleteMungu iokea Tanzania, Mungu iokoe Afrika
Mchizi unatuyeyusha bwanaa, Hii ndio mihabari ya Bongo Aimsaidii kitu mla VUMBI.
ReplyDeleteenuf is enuf, wanatupotezea mda wa kukaa tukiwajadili wao.Siku hizi sina hata mzuka wa kusoma magazeti ya IPP na haya yanayomilikiwa na Habari corporation kwa ajili ya ushenz kama huu.
ReplyDeleteNi wakati wa JK akiwa kama mtu wao wa karibu awaweke pamoja waelewane.Ni wazi kuwa kati yao hakuna msafi, Rostam fisadi na Mengi ni mkwepa kodi so ifikie wakati wajitambue kuwa wamewakosea watanzania badala ya kutafuta public attention.
Mungu Ibariki Tanzania
Mengi kuwa fisadi hakumaanishi shutuma juu ya RA na marafiki zako zinasahauliwa.
ReplyDeleteUkweli ni kwamba ukifanya test ya the better of two evils mzee Mengi anapita. Michango yake kwa jamii tunaiona. Na anatuwakilisha wazawa katika vita hii ya mapapa na manyangumi ya ufisadi.
Sheria inapasa ifuate mkondo hapa RA.
JK wakati wa ku earn mshahara wako ndu huu, si ukupanda ndege kila siku kama condakta wa dala dala
John
Michuzi kwa nini unafagilia haya MALUMBANO ya CCM sana.Najua ww ni CCM damu lakini vitu vingine uwe unafumbia macho.Achana na upuuzi huu,hawa kina MENGI na RODHAM wanapigania biashara sio taifa wala watanzania.Achana nao.
ReplyDeleteSafi Sana Rostam! Mimi amenikosha kwa kusema utajiri wake haujakwenda kwa 8 years,they had business since 1865! Mengi bwana we mwizi tu! Mtu Mzima sasa Game naona imerudi reverse utakoma babu! Unacheza Na Watoto wa Mjini! Watu Wana Data Zote Wame Flow ipasavyo! Sio wewe unasema Ana marafiki! Sasa we ukiwa na rafiki Msen*** kwa maana hiyo na wewe uwe Msen***???wazee wengine bwana!
ReplyDeletemengi ni mtu mbaya sana anachukua mabilioni ya shilingi kwa ajili ya walemavu kupitia NGOS zake alizoanzisha halafu badala ya kuwasaidia walemavu anawapa chakula cha usiku mmoja halafu anakutana nao baada ya mwaka,then anatuma video kwa wazungu wake kwamba anawasaidia maskini wakishirikiana na mama RWAKATALE..nani asiyejua kwamba mengi ananyanyasa wafanyakazi wake kuanzia vibarua mpk kwa mabosi ndani wote wanakufa na maumivu yao heko Rostam umetupa ushaidi yeye ameshindwa kuutoa wengi wameathirika naye kwa tabia yake chafu na watoto zake..ipo mifano mingi tu ya walioathirika kwa ajili ya ufisadi wake wa kudhurumu wengine jasho lao..
ReplyDeleteKaka hapa umenigusa sana kuweka hii habari, kweli mengi ni mtu mbaya sana mie ni mmoja wa waloathirika na ubaya wake jamaa ni mnafiki tena snitch,wale waliofukuzwa na mengi mwezi october mwaka jana ndio watajua, na hii inaweza kuja kumcost, aache usanii kabisa watanzania sasa sio wajinga kiasi hicho,la muhimu aelewe na kukubali matokeo kila lenye mwanzo lina mwisho.
ReplyDeletekuwa na utajiri sio dhambi lakini sio kama huu wa mengi ni wa kudhulumu haufai mwizi tuu huyu jamaa...kwani huyu si ndio kawabania CLOUDS FM wasianzishe TV yao ili isilete ushindani na EATV huyu mtu ni "COWARD" ndo mana anakimbilia kwa wananchi ili wamsaidie kupambana hana lolote hayo yote watz wanayajua lakn ROSTAM katoa ushaidi unaoeleweka. mengi mwizi tu na ni mmoja kati ya waliokuwa wanasapoti UJAMBAZI kwa kuwasaidia wachaga wenzake wenye mtandao huo.mengi kwishinei braza
ReplyDeleteninachoshindwa kuelewa ni where is the government? mbona hawaingilii hili suala?how can mtumishi wa wananchi(rostam aziz) aruhusiwe kutumia public resources(hizo evidence) kupigana vita binafsi?na huyo mengi pia anaruhusiwa vipi kuwa na public resources kupigana na rostam aziz?jamani wadau hii imekaaje?mbona huko tanzania kuna movie namna hii maana sitaki kuamini its real because if it is then hakuna nchi tena kumebaki jina tu.
ReplyDeletehuu upumbavu wote unaendele ni kashfa kubwa kwa sisi wananchi . Kama mafisadi wanaweza kuumbuana nje nje bila kuogopa sheria zitakazo chukuliwa juu yao . Tulipiga kura kuchangua viongozi ..Serikali yetu iko wapi ??????
ReplyDeleteIshakuwa so Mengi naumbuka lakini sifa yamatajiri wengi bongo ni ufisadi haya ya Mengi watu walikuwa wanayaona lakini walikuwa wanaogopa kuyasema.Lakini sasa hii ni fisadi vs fisadi war,sasa tuone nani atachukua point kwenye mpambano huu.
ReplyDeleteHuyu Rostam anamwita RM fisadi na kataja pesa alizokopa na kuingia nazo mitini,hivyo basi kama yeye siyo fisadi papa atueleze kiasi cha pesa alichokopa kama alivyoeleza na namna alivyozirudisha na riba zake.
ReplyDeleteYap, kweli mambo makubwa Mengi amezoea kulalamika sana na anaonekana anataka kuanzisha matabaka ya watu waTZ wawachukie wahindi na yeye aendelee na uzalendo wa Ki-Chaga.
ReplyDeleteRostam ni mwizi, lakini wizi wake "ni wa kupewa sio wa kuutafuta kwenda kuiba", yeye anatumiwa na wakubwa kupitia account zake.
Lakini Mengi ni mwizi wa kuutafuta. Yaani anakwenda kuwarubuni watu ili yeye aibe na baadaye kuwadhulumu hao hao alioiba nao.
Kwanza mengi sikumpenda pale aliposema watu watano tu ndio mafisadi papa. Ukiingalia kwa mtizamo mkubwa huyu mengi ni "racist- mkubwa", huwezi wasema watu wote hao ambao ni waTZ wenye asili ya kihindi au kiarabu kwamba wao tu ndio wezi papa uongo mkubwa , huo ni kutafuta uchonganishi na kuamua kutafuta watu waanze kutupiana mawe na kuharibu mali za wahindi au waarabu ambao hawana hata tatizo na mtu TZ.
Rostam nimekukubali wewe mwarabu mjanja , umezaliwa pwani, wazazi wako walikuwa katika biashara toka enzi za mababu zako. Mtu kama Mengi mchaga tu katokea huko milimani anakuja na makelele mengi wakati hata wazazi wake hawakusaidia chochote wakati wa uhuru wa nchi hii.
Somaiya ni WATZ wahindi ambao heshima zao zinastahili kubebwa, sio tu na kila MTZ bali kila mwanaharakati, hawa wamepigania sana nchi enzi zile za TANU , TZ kupata uhuru na matunda ya kazi zao eti leo zinaitwa ufisadi papa.
Rostam amesema wazi kwa kuonyesha jinsi Mengi anavyoweza gombanisha watu kwa faida zake mwenyewe. Na ni kweli Mengi anakwenda kufilisika sasa hivyo anagombana na kila mtu.Ndio maana watu huwa hawapendi wa-chaga kabisa , maana ni wanafiki sana, wanataka kila kitu wawe wao tu. Ni bora mhindi, mwarabu, mhaya, msukuma,kuliko M-chaga.Mchaga bwana ni mnafiki sana,ndio maana enzi za nyerere waliishia kuwa huko chini tu, maana wanataka kugombanisha watu kama wakikuyu au waganda kwa manufaa yao tu.
Mengi mwongo tu, huwa namuona muongo tu siku zote nz anatumia ngozi yake nyeusi kuwamaliza watu amabo yeye kawakuta ni matajiri.
Ndio maana mungu akamuachia maradhi na kuuweka katika nyumba yake, ili ajifunze, na bado haelewi.
Mengi mnafiki mtupu, muongo , mwizi mkubwa huyo.Na kweli yeye ndio Nyangumi fisadi.
wewe anonymous uliyepost comment tarehe 04 may saa 3.55pm uliyesema mwarabo koko mshamba sana. Kila mtu mweupe unamuona mwarabu kwa taarifa yako huyo Rostam si mwarabu ni mbulushi ana asili ya Kiiran. Chunguza kwanza usitoe comment hovyo hovyo.Halafu mambo ya ukabila yamepitwa na wakati wewe mwenyewe uko nchi za watu Sweden ungekua unaona rangi yako ya maana ungebaki bongo!Tanzania watu wote sawa usitake kuleta mambo yaliyopitwa na wakati!kula kona huko!
ReplyDeleteJamani kama haya aliyoyasema Rostam ni kweli basi sijuwi yeye alivyoitapeli nchi yetu ni kiasi gani mpaka Mzee Mengi akaongea na kumtaja Rostam na wanzanke kuwa ni mafisadi papa! Wewe Rostam kwa nini miaka yote ulikuwa hujamtaja fisadi Mengi mpaka alipokusema wewe fisadi ndo ukaita waandishi na kuanza kujiteteya,mie naona ni vizuri ujiuzulu ubunge na Wanyamwezi wachaguwe munyamwezi mwenzao. Tumechoka na nyie mafisadi wakubwa!!
ReplyDeleteUpele umepata mkunaji!!! Ni kweli wote mafisadi lakini tabia ya mengi kuwaibia masikini halafu kujifanya yupo upande wao ndiyo ufisadi mbaya zaidi. Mchanganuo wa Rostam unaeleweka na umeanika ni jinsi gani Mengi inavyolihujumu taifa na pia kuvunja utulivu uliopo
ReplyDeleteKusema ukweli, RA hapo umenifungua macho maana huyu RM nilikuwa namuona hero wa nchi lakini sasa nimeanza kupata mawazo tofauti kabisa. Tanzania Tambarare sana tu!
ReplyDeleteWatanzania wenzangu tusiwe wajinga uyu Mhindi na wenzake ndio wanaoua nchi yetu. Ninashangaa watanzania mnaposema wote mafisadi, ukweli nikwamba hawa jamaa wamewatawala mpaka viongozi wetu walivyokuwa wapumbavu. Si kwamba namtetea Mengi, lakini wahindi ni wapumbavu sana na wanachokifanya ni kuungana na kuwaonga baadhi ya viongozi wetu hili wawalinde. Kwa upande wa mengi naye anamakosa mengi lakini hawa wahindi ni wauwaji wakubwa.
ReplyDeleteJamani..kama nimemuelewa vyema mheshimiwa RA ni kwamba kuna mafisadi wanafahamika sana lakini hawafichuliwi na wakubwa mpaka hapo watakapokuwa kwenye bad books zao.
ReplyDeleteMaana kweli kama RA na vyeo vyake vyote hivyo alikuwa anayafahamu maovu ya Mzee Mengi, alikuwa anangoja nini kuyafichua? Ni wangapi wengine anaojua maovu yao lakini anakaa kimya mpaka wamseme yeye? Wananchi wa Igunga...kazi kwenu....Mchele ni upi na pumba ni zipi?
Rostam Azizi ni fisadi toka ujana wake ulizeni Waburushi wa Nzega, alipokuwa UK aliwahi kufanya mambo fulani ya kuiba taji la Miss World. Mimi simshangai ulizeni hii skendo mtasikia
ReplyDeleteakome akomae huyu mtu anajifanya anauchungu wa nci wakati yeye halipi kodi? lipi kubwa kukopa na kutolipa on time au kukwepa kodi? kodi ni ya wananchi na mtu akikopa ni juu yake na mkopeshaji wake.
ReplyDeleteJamani..kama nimemuelewa vyema mheshimiwa RA ni kwamba kuna mafisadi wanafahamika sana lakini hawafichuliwi na wakubwa mpaka hapo watakapokuwa kwenye bad books zao.
ReplyDeleteMaana kweli kama RA na vyeo vyake vyote hivyo alikuwa anayafahamu maovu ya Mzee Mengi, alikuwa anangoja nini kuyafichua? Ni wangapi wengine anaojua maovu yao lakini anakaa kimya mpaka wamseme yeye? Wananchi wa Igunga...kazi kwenu....Mchele ni upi na pumba ni zipi?
Huyu R.Aziz mpuuzi yote aliyosema ni upuuzi mtupu. Hiyo mikopo ya R. Mengi ni documented loans zilizofata taratibu zote za mikopo ndiyo maana hata yeye ameweza kupata kumbukumbu zake sisi tonachotaka kujua ni yeye kwanini anaficha uhusika wake kwa hizo kampuni zilizotajwa na R.Mengi. Hayo maugonzi na watu hayatuhusu tunachotaka kujua kuhusu Richmond,Dowans na n.k.lakini hajajibu shutuma zake anaanza kutusomea wasifu wa Mengi kama tutakuwa na wasiwasi naye tutamtafuta Mengi ayaeleze mwenyewe.Wewe R. Aziz sisi tunataka maelezo kuhusu Richmond na Dowans na Kagoda.
ReplyDeleteMtanzania halisi
huyo rostam aziz ,manji,lowasa wanadeserve adhabu kali kabisa wanatufanya watanzania wote tuonekana wajinga,kufanya walioyafanya na wanaendelea kuyafanya bila kuchukuliwa hatua kali za kisheria ina confirm jinsi gani nchi hii yetu tulivyo passive na ndo mana maskini,huko marekani watu waliandamana door to door kwenye nyumba za executives kutoa hujumbe mkali just becouse of their poor leadership that lead to credit crunch,bongo watu wanakula rushwa plus utawala mbovu,afu bado wanakula anasa dar ktk nchi ambayo pato la mtu kwa mwaka alizidi 400 $,this shit can not go on
ReplyDeleteMambo yanazidi kunoga. Tumetajiwa mapapa ya ufisadi na nyangumi wa ufisadi.
ReplyDeleteEndeleeni kutajana tujue nani ni dagaa, kambare, sangara na kamongo wa ufisadi. Msiishie hapo, wadau tunataka kujua kama kuna pweza, ngadu nk wa ufisadi.
HAWA WEHINDI NI WAPUMBAVU TU. MAELEZO MENGI LAKINI HAJAJIBU ALICHOTUUMIWA NACHO. WATU WA UGANDA INABIDI WASHUKURU IDD AMINI KUWAANGAMIZIA MBALI HAWA MASHETANI WAKUBWA. WATANZANIA NASHANGAA MNAPOJIFANYA ETI MADUME WAWILI WAMEKUTANA WAKATI MNAJUA HAWA WATU HAWATUPENDI HATA KIDOGO. NENDA KWAO INDIA UKAFANYE KAMA WANAVYOWAFANYIA NYIE NDIO UTATAMBUA NINACHOKISEMA.
ReplyDeleteDAIMA TUSIENDELEZE UJINGA.
HAWA JAMAA NDIO CHANZO CHA MATATIZO TULIYONAYO MPAKA SASA HIVI.NAFAAMU WAO NDIO WATAKUWA WAMEJAZANA WANATUMA MAONI YAO HILI KUENDELEA KUTUMALIZA. MICHUZI NAJUA NAWEWE COMENTS ZA KULINDA TAIFA LETU UWEKI SIJUI INAKUWAJE BWANA?
BASICALLY WHAT RA IS SAYING IS THAT, HE IS NOT DENYING THAT HE IS FISADI BUT MENGI HAS NO MORAL AUTHORITY TO ACCUSE HIM, BECAUSE HE CONSIDER MENGI AS ONE OF FISADI`S. JUST LIKE RA
ReplyDeleteROSTAM HUYO JAMAA MPELEKE KWENYE VIOMBO VYA SHERIA ASIKUSUMBUE KWANZA UNAO USHAHIDI TOSHA.
ReplyDeleteHIVI KWANINI HAO WAHINDI KOKO SIJU ROTA NA WENZIE WASIRUDISHWE HUKU KWAO,YANI KWAO NI UMASIKINI WAKUFA MTU,WANAPAKIMBIA ALAFU WANAKUJA KUWANYANYASA WA TZ
ReplyDeleteJamani kumbe tajiri Mengi ndio fisadi kuliko wote! Hii kali. La maana ni kuwafilisi wote kudadadeki! Tupe vituuuz braza michuuuz
ReplyDeleteRostam made some really sensitive and credible attacks towards Mengi but also Mheshimiwa Rostam anajitamba kwamba "utajiri wake ameupata kihalali kutokana na familia yao kujituma vizuri kibiashara tangu miaka ya 1892 mkoani tabora" This is bullshit their sins can be traced back to when whites used Indians and some arabs to control african slaves to build railways mfano (reli ya tabora).I know i am supposed to forgive lakini Rostam unabidi ufahamu Watanzania wanaijua vizuri historia yao ya kuhuzunisha sana na hawajasahau mababu zao walivyoteseka.
ReplyDelete...hivi hawa mafisadi wanafikiri wanaongea na nani?ohoo!!mara papa wa ufisadi mara nyangumi wa ufisadi wote ni wezi tu,hizo habari wapeleke vijijini kuwadanganya!!!!!!
ReplyDeleteRA amesema kweli. Watanzania sasa hivi wamejua kutenganisha pumba na mchele. Tatizo walilo nalo wakishavitenganisha hivi vitu wanaacha mchele na kuchagua pumba.
ReplyDeleteData za Waziri MASHA hizo alizokuwa anataka kumuua nazo Mengi
ReplyDeleteKapata kwa kuziingiza amumalize
Mengi alipiga kelele wanataka wanikague wanifilisiiiiiiiiiiiiiiiiii
Kumbe alikuwa anajua what waz koming
RA kapewa aue
Mnalisaidia taifa kuogopa ufisadi
Toboaneni macho
acheni kudanganyka na press nyie,hana uzalendo wowote,na hzo document anazosema anawasilisha kwenye vyombo husika ni uzushi tu,huyo kijana ana inttelegence yakumchimba mengi.,by the way kesho ijumaa WANACHUO WOTE TUNAANDAMANA KUM BACK UP MZAWA, MENGI.ENOUGH IS ENOUGH
ReplyDeleteSwali dogo tu, hizi data/info zote za kibenki huyu Rostam amezipataje? Fisadi anasidiwa nwa watu wa ndani ya serikali huyu!
ReplyDeleteHII MIARABU KOKO NA MIHINDI NDIO INALETA MATATIZO NCHINI KWETU KUANZIA RUSHWA NA KUGOMBANISHA WATANZANIA KUANZIA BUNGENI MPAKA URAIANI. MUNGU IULIE MBALI HILI TAIFA LETU LIWEZE KUOKOKA. HATA KAMA MENGI ANAIBA LAKINI ANAIBA MALI ZA NCHI YAKE SIO KAMA HII MIGENI HAINA HATA URUMA NA INADIRIKI HATA KUJIFANYA INAUCHUNGU NA NCHI YETU.
ReplyDeleteBAADHI YA VIONGOZI WETU WALIO WAPUMBAVU SIJUI KWANINI WANAIKUMBATIA HII MIJITU WAKATI NDIO INAANGAMIZA NDUGU ZETU
Du kweli watanzania wengi ni mbumbumbu,hawa watu mnawajua jinsi gani wanavyowanyanyasa lakini bado mnadu=iliki kusema mengi kaumbuka wakati huyu ni mtanzania mwenzenu na hawa ni wageni. Kweli nchi yetu vichwa vya wendawazimu ndio vimejaa.
ReplyDeleteWAINGEREZA NDIO WALITULETEA MATATIZO KWA KUTULETEA HAWA WATU...HAWAFAI KABISA. ANGALIA HUKO KWAO INDIA, PAKISTAN, SRI LANKA..HAKUKALIKI!!!!
ReplyDeleteWAAMBIE WAENDE ULAYA/SCANDNAVIA, WATAKIMBIA MNO, KWASABABU HUKO WATU WAMESIMAMA, WAKO MACHO, HAWANA NAFASI YA KUWACHEZA SHERE VIONGOZI HUKO, WATU WENYE UCHUNGU NA NCHI ZAO.
Eeeeheee! Jamani mpambano mkali wa kukata na shoka ndani ya FISADISBOOK wale bingwa wa kurushiana mipasho hodari kabisa kati ya ROSTAM AZIZ a.k.a FISADI PAPA V/S REGINALD MENGI a.k.a FISADI NYANGUMI, Mpambano huu mkali watakapopanda jukwaani mahakamani kuonyeshana MIPESA YAO na UBABE WAO. Njooni mshuudie taarabu ya kichaga na kihindi. Ili kumpata mshindi kaeni mkao wakula....wenzetu wanasema stay tuned! hawa si lolote Rostam mbabaishaji nimefatilia kwa makini sana maswali aliyopigwa na waandishi wa habari jana alikua anatoka nje ya topic anazunguka maswali dhahiri anaonekana taperi, kubenea alimpiga maswali makali akajibu out of topic, huyu ni fisadi tena akae kimya kuliko kudangany umma watanzania, ametunyonya vyakutosha, wanajinufaisha jasho letu kwa manufaa yao na familia zao ENOUGH IS ENOUGH sasa imefika mwisho, makanisani, misikitini wazee wa matambiko tunafanya sala kubwa kuwaumbua wale wanene wanaotuumiza sisi walalahoi na mmoja baada ya mwingine wataumbuka, endeleeni kuumbuana hii chein si mchezo itawagusa mafisadi wengi sana wengine matumbo joto, magabachori watu wabaya sana huyu Rostam anajifanya nature ya ufanyabiashara amezaliwa nao ktk familia yao, Mengi amepata gafla.... nauchungu sana na hawa watu wanaotingisha nchi, tunapata shida na umeme bei juu pumbaaaaaavvvvvvvv, marabuk!!!! Hamna aibu ata kidogo, kwanza nampongeza mtukufu raisi kwa kutengeneza magereza wakapumzike kule hawa tumewachoka mtaani, na magabachori wengi nimafisadi kazi kukimbiza hela canada serikali inakaa kimya hawa wanasumbua nchi km nani? au ndio wenye nchi? sisi wapangaji? Anna Kilango nimwanamke wa shoka sana yule mama nammind sana anastahili tungepata wamama km hao 100 nchi ingekuwa bombastic mafisadi wangelipuka km mabomu ya mbagala. Haogopi huyu mama kabisa namsifu sana kujitoa muhanga kwa nchi yake HONGERA SANA MAMA YANGU MPENZA MUNGU AKULINDE. Sophia Simba inaelekea anahisa na wahindi ndio maana ananyoosha mdomo kumkemea mengi bora angekaa kimya. Rostam alivyopata kashfa alikaa kimya mengi alipomuhuku eti ndio anaamka kwakuwa kamgusa mbona asijitete na serikali wakati wa Richmond asikanushe? aibu mbunge gani si msafi? unawakilisha nini bungeni? nyie ndio mnaokula hela za bure km alivyosema slaa. Hustaili kabisa cjui ata km next time utapata kura. Lowassa nafkiri ndio fisadi namba 1 kwacc watu weusi huyu nitajiri tanzania nzima hakuna ukitoa wahindi, hatosheki mmasai huyu. Sumaye nae ni mwizi mwizi mali zake nyingi ametumia migongo yawatu km kina philbert Bai huyu ni fisadi hatari sana. na mengi yakuongea lakini nikipata nauli mjomba nitakuja kukuambia zaidi.
ReplyDeleteEeeeheee! Jamani mpambano mkali wa kukata na shoka ndani ya FISADISBOOK wale bingwa wa kurushiana mipasho hodari kabisa kati ya ROSTAM AZIZ a.k.a FISADI PAPA V/S REGINALD MENGI a.k.a FISADI NYANGUMI, Mpambano huu mkali watakapopanda jukwaani mahakamani kuonyeshana MIPESA YAO na UBABE WAO. Njooni mshuudie taarabu ya kichaga na kihindi. Ili kumpata mshindi kaeni mkao wakula....wenzetu wanasema stay tuned! hawa si lolote Rostam mbabaishaji nimefatilia kwa makini sana maswali aliyopigwa na waandishi wa habari jana alikua anatoka nje ya topic anazunguka maswali dhahiri anaonekana taperi, kubenea alimpiga maswali makali akajibu out of topic, huyu ni fisadi tena akae kimya kuliko kudangany umma watanzania, ametunyonya vyakutosha, wanajinufaisha jasho letu kwa manufaa yao na familia zao ENOUGH IS ENOUGH sasa imefika mwisho, makanisani, misikitini wazee wa matambiko tunafanya sala kubwa kuwaumbua wale wanene wanaotuumiza sisi walalahoi na mmoja baada ya mwingine wataumbuka, endeleeni kuumbuana hii chein si mchezo itawagusa mafisadi wengi sana wengine matumbo joto, magabachori watu wabaya sana huyu Rostam anajifanya nature ya ufanyabiashara amezaliwa nao ktk familia yao, Mengi amepata gafla.... nauchungu sana na hawa watu wanaotingisha nchi, tunapata shida na umeme bei juu pumbaaaaaavvvvvvvv, marabuk!!!! Hamna aibu ata kidogo, kwanza nampongeza mtukufu raisi kwa kutengeneza magereza wakapumzike kule hawa tumewachoka mtaani, na magabachori wengi nimafisadi kazi kukimbiza hela canada serikali inakaa kimya hawa wanasumbua nchi km nani? au ndio wenye nchi? sisi wapangaji? Anna Kilango nimwanamke wa shoka sana yule mama nammind sana anastahili tungepata wamama km hao 100 nchi ingekuwa bombastic mafisadi wangelipuka km mabomu ya mbagala. Haogopi huyu mama kabisa namsifu sana kujitoa muhanga kwa nchi yake HONGERA SANA MAMA YANGU MPENZA MUNGU AKULINDE. Sophia Simba inaelekea anahisa na wahindi ndio maana ananyoosha mdomo kumkemea mengi bora angekaa kimya. Rostam alivyopata kashfa alikaa kimya mengi alipomuhuku eti ndio anaamka kwakuwa kamgusa mbona asijitete na serikali wakati wa Richmond asikanushe? aibu mbunge gani si msafi? unawakilisha nini bungeni? nyie ndio mnaokula hela za bure km alivyosema slaa. Hustaili kabisa cjui ata km next time utapata kura. Lowassa nafkiri ndio fisadi namba 1 kwacc watu weusi huyu nitajiri tanzania nzima hakuna ukitoa wahindi, hatosheki mmasai huyu. Sumaye nae ni mwizi mwizi mali zake nyingi ametumia migongo yawatu km kina philbert Bai huyu ni fisadi hatari sana. na mengi yakuongea lakini nikipata nauli mjomba nitakuja kukuambia zaidi.
ReplyDeleteKWANINI HAYA YOTE YAMEKUJA SASA NA SIKU ZOTE YALIKUWA WAPI? HII INATISHA.
ReplyDeleteWATANZANIA KIKUBWA NI KUCHAGUA KIONGOZI WA MAANA MWAKANI MSIANGALIA CHAMA JAMANI NCHI INAKWENDA PABAYA.
MKITAKA RAISI WA MAANA SALUM AHMED AU WARIOBA HAWA NI WATOTO WA BABA WA TAIFA.
AMA WENGINE NI KUIBA NA KUENDELEZA FAMILIA ZAO KUANZIA JUU HADI CHINI.
''Kama unawadhulumu wananchi masikini kwa kutowapa ajira za kudumu na badala yake kuwaajiri kama vibarua wa siku ''
ReplyDeleteHapo umenena, manake haupiti mwaka ridandance, malipo njiwa....hapo umenena. Akane hili tumeone kweli anajali
watanzania hebu msiwe biased..ndomaana mnaambiwa 90 percent of u are ignorant.. dont judge a man by the colour of his skin but by the content of his character..sasa kama rostam is from the asian origin. do not condemn him by his race.. angalieni jinsi mambo yalivyo ndo mumjudge...na mnapumbazwa na misaada,misaada ndo inamsafisha mtu.. na mengi is using that as a facade to his blundders..acheni ushamba wa ukabila... tumieni akili zenu vizuri.
ReplyDeleteAt least we have known the other side of Reginard Abraham Mengi. He is also a fisadi and corrupt so to speak. Information is power bwana, just let these guys display their secrets of how they succeeded in businesses to our poor and vulnerable Tanzanians. But honestly, Laiti kama taarifa za maendeleo ya taifa letu na fursa kwa vijana wa Tanzania zingekuwa zinatolewa kwa msisimko namna hii nchi yetu ingekuwa mbali sana jamani. doh.
ReplyDeleteKwa kweli nashukuru sana kwa majibu ya Mhe. Rostam Aziz. Lakini naomba aelewe kuwa bado hajajibu hoja zinazomhusu. Alichofanya yeye ni kumshambulia Mzee Mengi na kueleza matukio mengi ya nyuma ya Mengi. Hayo kwa sasa hayatuhusu sana, kinachotuhusu ni yeye kujibu hoja ambazo zimeelekezwa kwake. Hoja hujibiwa kwa hoja. Sasa yeye Mhe Rostam kila kitu anakanusha kwa mdomo, hana data naona amezoea kudanganya. Tunaomba Rostam ajiweke bayana tujue ni Fisadi au sio fisadi na aacha kutapa tapa.
ReplyDeleteHivi mengi utaendelea kutafuta huruma ya watanzania mpaka lini? angalia sasa umeanikwa hadharani, kumbe ndiye uliyewasababishia watanzania wale waliokuwa wanafanya kazi NBC kupunguzwa kwa sababu ya benk kukosa ufanisi wa kutosha. ile ilikuwa benk yetu sote iweje mwenzetu ujichotee peke yako? rudisha mahela yetu bwana.
ReplyDeleteMengi mengine mengineo,na wewe rostam,roster,lost etc,ohhh mbona hivyo?Nyie si mnasaidia kwanza kwa kujuana?Siyo?.Japokuwa Mengi ana roho nzuri zaidi nafikiri,na wewe Rostam Lost men unamsaidia nani?Duuuuuuuuuu inatisha.Tunataka maendeleo TZ siyo kugombana.Asante
ReplyDeletewizi mtupu
ReplyDeleteMengi ni mtanzania wa damu na anakula mali za ndugu zake kuliko hii hawa wanaotoka nje na kula mali zetu bila uchungu.
ReplyDeleteMimi kama mtanzania , kwakweli siwapendi wahindi na waarabu. Wananyanyasa sana waafrika na isitoshe kwenye nchi yetu. mimi nataka wahindi na waarabu warudi kwao. Siwataki kabisa. Ni maselfish na hawalete maendeleo yoyote kwa masikini. RM bora amefungua makampuni na wametoa ajira. Mnaosema Mengi kawanyanyasa kazini, ndugu zangu watanzania ni wavivu na mnapenda dezo kufanya kazi kwa bidii hampendi. Na kama ungekuwa unafanya kazikwangu na unaleta uzembe kazini nitakufukuza tu. Go Mengi toa mafisadi wa kihindi bora tule wenyewe mali zetu.
ReplyDeleteMy friend Rostam, just get rid of that public nuisance called Mengi.
ReplyDeleteAmeiba $2m za wananchi na kununu akampuni iloyofilisika na kudai alichukua hatua ya ku resign. Ku resign kunasaidia nini wawekezezaji badala ya kurudisha hela zao zilizoingia kwenye mifuko ya familia.
Just finish him off atokomee. Anajifanya anajua siasa sasa mfundishe wewe ni nani.
Mdau-Witchita
Jamani watanzania tuamkeeee. Mi nawashangaa hawa wadau wanao mtetea Rostam eti kwa madai kuwa kawafumbua macho kwa kutaja ufisadi wa Mengi. Hebu jiulizeni yeye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa(NEC), kamati kuu ya CCM na mbunge wa bunge la jamhuri, alishindwa vipi kufichua uovu wa Mengi? Sasa leo anasema yote hayo kwa kuwa yake yamefichuliwa. Tena kama alivyosema mwenyewe huyu Mengi yeye hana wadhifa wowote wa kuchaguliwa kapata wapi ujasiri wa kuthubutu kuwanyooshea vidole wao? Ni kweli, hata kama nae Mengi ni fisadi basi bora yeye AMETHUBUTU kuwataja wenzake na wakati yeye hana wadhifa zaidi ya kuwa ni mfanyabiashara. Rostam ana wadhifa wa kisheria wa kukemea ufisadi kwanini hakufanya hivyo kabla? Hata kama Mengi nae ni fisadi haimfanyi yeye Rostam asiwe fisadi. Amemchambua vizuri Mengi, angetumia uchambuzi kama huo kubainisha kuwa yeye si fisadi, yaani angeweka data zake wazi kuwa madai dhidi yake sio ya kweli. Mengi ni SHUJAA hata kama amefanya hivyo kwa ajili ya sababu za wivu wa kibishara, bado ni SHUJAA.
ReplyDeleteUS BLOGGER
ReplyDeletemdau witchita mnafiki na ulegee na ushindwe na ukaliwe na fisadi papa!
US BLOGGER
NILIKUWA WA MWANZO KUMZUNGUMZA RM HATA KABLA ROSTAM HAJAJIBU TUHUMA ZAKE.
ReplyDeleteWENYE BLOG WAKAAMUA KUZIWEKA MESSAGE ZANGU MBILI KAPUNI.
HIYO IKANIFANYA NIJIULIZE, KUMBE NYIE WANAHABARI MNAOJIDAI KILA SIKU KUPIGANIA HAK NA KUTETEA WANYONGE NDIO NYINYI NYINYI MNAOVUTI UPANDE WENU, MKAIKANA HAKI.
RM NI MWENZENU, MNAAMUA KUIZIKA HAKI KWA AJILI YAKE.
TANZANIA ITAFIKA WAPI?
YIE HAMNA MPANGO WOWOTE KUSEMA KWELI, HAMWONI KAMA WATU KAMA RM NI HATARI KWA MAENDELEO YA TANZANIA NA RIA ZKE.
SIKU ZOTE MTU HUU YUKO TAYARI KUJIFANYA ANA UCHUNGU NANCHI, UKWELI WATU WENGI TU TENA MPAKA BAADHI YA VIONGOZI WA SERIKALI WANAJUA JUU CHINI NAMNA "NYANGUMI" MENGI ANAVYOFISIDI NCHI YETU.
MBONA BASI NYIE WANAHABARI AMBAO KWA KIASI TUNAWATEGEMEA MUITETEE JAMII MNAKUBALI MANYANGUMI WAENDELEE KUTUMALIZIA KIDOGO KILICHOPO KWA KUTIA KAPUNI MAONI YETU?
MNATUPELEKA WAPI?
KWANI ANAKUPENI NINI HUYU NYANGUMI?AU NDOO UBAGUZI WA RANGI WENYEWE HUO?
Mndengereko, Ukerewe
Watanzania tumelala usingizi mzito pakipambazuka habari itakuwa " KAFIA USINGIZINI, MAZIKO SAA KUMI" yaani tutakuwa tumeshazikwa! Mahakama inachunguza juu ya kesi iliyoko mezani kwake tayari, kesi zinazofunguliwa magazetini hazihusiki, au mnafikiri serikali haina macho?
ReplyDeleteHebu tulijenge na kulilinda taifa!
MUWE MAKINI NA MAMBO, MENGINE YANALETWA ILI MSHABIKIE NA KUSAHAU UKWELI!
GJK
Mimi Mzawa sina mengi ila natoa mchango wangu Kiduuuchu "KWA AIBU KUU NAJISIKIA VIBAYA KUITWA MTANZANIA,NITAWAAMBIA NINI WAJUKUU WANGU????
ReplyDeletehe is so cute!
ReplyDeleteRacial card ya Mengi haitamfikisha popote.
ReplyDeleteImekuwa vizuri kawasha moto na Rostam katuonesha Mengi ni nani.
ZEUTAMU UPO JUU ZAIDI YA MICHUZI KAZI KUWEKA PICHA ZAKE KWENYE BLOG YAKE, SURA KAMA PUA YA ROSTAM.
ReplyDeleteBIG UP ROSTAM HUYO MENGI MNAFIKI HATOI MPAKA CAMERA ZIWEPO ANAPENDA SANA MATANGAZO, BWANA MDOGO WANGU ROSTAM KULA NAE SAHANI MOJA ASIKULETEE ZA KULETA ANAJIFANYA MUNGU MTU YEYE MTOA RIZKI ZA WATU NA JK TULIA USIINGILIE FANYA KAZI ZA MAANA HAYO MAJUNGU YASIKUSTUE MENGI WEWE SIO MTOA RIZKI ZA WATU KWANI WEWE KAMA NANI WACHA SERKALI ITAFUTE MAFISADI YENYEWE USILETE CHOKO CHOKO
ReplyDeleteUkiwa katika nchi za nje haki zimepangwa kama ifuatavyo.
ReplyDeleteMzungu- tena wa nchi za magharibi blonde
Miksa wa kizungu
Hapa weka mifugo kama vile mbwa,paka n.k
Waarabu
Wachina
Walatin
Wahindi na makabila yake.
Sasa...tumechoshwa kuona hao wadosi na wenzao kujihusisha sana kwenye mambo ya siasa ya nchi yetu tena kwa mabaya tu.
Leo hii gabachori ndiyo anasiimamia maswala ya nani mwizi hii si noma jamani?
Jamamni watu wazima ndo wazungumzie swala la mengi na siyo huyo mhindi kwa sababu ni mwizi tu.
Mmeshaona Mtanzania anamuhukumu mtu yeyote INDIA?Nani atamsikiliza.
Hao wahindi wajenge Upendo kwa watu wenye nchi yao naa kujaribu kuchanganya damu.
Swala la wizi wao ndiyo wezi wakuu hapo.
MUNGU IBARIKI AFRIKA MUNGU IBARIKI TANZANIA
peace and love