Salaam Wadau,
Ninapenda kuwajulisha, kwa watakaohitaji, kuhusu Southern Highlands School iliyopo mji wa Mafinga mkoani Iringa, Tanzania.
Hii ni shule ya msingi ya bweni inayotumia kiingereza, yaani english medium boarding primary school, na ambayo tangu kuanzishwa kwake haijawahi kufelisha mtoto.

Hivi sasa Southern Highlands School inapokea
wanafunzi kwa madarasa karibia yote. Kwa walio USA, ukipenda kupata habari zaidi kuhusu hii shule na labda ungependa kumpeleka mtoto wako au kumfadhili ndugu yako yeyote hapo SHS, basi unaweza kuwasiliana na mkurugenzi wa shule hiyo, ambaye yupo hapa USA kwa muda mfupi,
kupitia namba 214-604-1726.
Ahsante.
Mdau Kitova
wanafunzi darasani

shule inavyoonekana kiubavu



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2009

    Inaonekana shule imetulia,ila waendeshaji ningewashauri muifungulie website ili watu wakitaka kupata more information wazipate kwa urahisi,haya mambo ya kutafutana kwenye simu kwa ajili ya details wazazi wengi hatuna imani nazo.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 17, 2009

    Hivi mbona mnakua malimbukeni jamani wenye shule. Mmeweka namba ya sim kwa wale waishio Marekani sasa sisi tuliopo hapa Bongo tupige Marekani? Anzeni na namba ya nyumbani then mseme walioko huko majuu wapige ... Plz tundikeni namba yenu ya sim hapa bongo tuwaendee hewani faster kabla nafasi hazijajaa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 17, 2009

    Weka basifull information, kama fees ni kiasi gani, mahali ilipo, matokeo ya taifa shule inakuwa ya ngapi! vitu kama hivyo!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 17, 2009

    Huyo mtu anayetaka watu wampigie simu yake bado hajagundua watu hupata more information about school from the website, naungana na anon no 1, we mwenye shule acha hiyo mambo, fungua hata kablogu.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 17, 2009

    Kwa walioko nyumbani namba ya simu ipo kwenye tangazo lao. 026-277266. Mpaka namba ya nukushi na anuani pepe wametoa.

    ReplyDelete
  6. Al MusomaJune 17, 2009

    Nafikiri kutumia au kutotumia Kingereza si muhimu (labda uwe na itikadi kama ya shangazi yangu). Ningependa kuona wasifu wa walimu waliopo hapo shuleni. Mwalimu mwenye sifa mwenye Kingereza alichojifunzia Chang'ombe ni bora kuliko mwalimu mwenye lafudhi ya Kimarekani (alozaliwa na kukulia US) na anaingia ualimu baada ya kazi ya miaka kadhaa ama ya kufanya kazi Posta au shirika la bima (AIG). Na kama alivyoomba mdau mmoja hapo juu, tunaomba na sisi namba za simu za hapa nyumbani ili tujaribu maana za Uganda na Kenya tushazichoka. Mwisho, mkurugenzi mkuu anafanya nini US?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 17, 2009

    bongo bwana sasa kiingereza ndo elimu hio si lugha tu km lugha nyengine,, mungeweka sifa za maana sio eng,,,kuna nchi duniani zimeendelea bila hata ya kutumia hicho kiingereza ktk elimu

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 17, 2009

    Mara nyingi malimbukeni huwaita wengine malimbukeni. Angalia kwenye hiyo picha ya kwanza info zote zipo hapo.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 18, 2009

    Mkuu KITOVA hii shule inaonekana si mchezo, naona vijana wakila internet kwa mbali. Sasa mimi ninaenda nyumbali karibuni nitaenda kuiangalia shule na kama ni mvuri sio kwa sura ni kwa ufundishaji basi nina vijana wako nyumbani wanatakiwa kuanza shule january itabidi niwapeleke huko ila kama nitarizika na ufundishaji na matokeo ya nyuma ya wanafunzi. Na nikikosa nafasi nitakusumbua uongee na huyo mkurugenzi anisaidie, shukrani kwa information.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 18, 2009

    Nyie ndugu zangu mnaoulizia namba za simu, mbona imewekwa hapo juu kabisa kwenye picha, kwaa jili ya watu wote walioko TZ na wasiokuwako TZ. Simu ya walioko US ni moja tu, nayo ni kwasababu mkurugenzi yuko US sasa. Lakini akisharudi, simu ya kuwasiliana ni moja tu kwa walio nje na walio ndani. Watu wakishasikia tu Marekani wanajisikia hasira kama wametengwa vile!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 18, 2009

    My God, Mafinga is growing fast so tremendously! Kwa uchumi hata wana Iringa town watakwama si mud mrefu. Na ukiacha vyuo vikuu vya Iringa, eneo la Mafinga/Mufindi, wana shule nzuri sana sasa.
    Mafinga Seminary..
    Donbosco Seminary...
    Consolata Seminary...
    Bethel Sabs Girls...
    Mafinga Sec School/J.J.Mungai
    Changarawe sec school...

    Ukiacha shule ya J.J.Mungai sec school, zote zilizobaki zinatamba kitaifa. Sijataja shule zingine za eneo hilo nyingi, ambazo ni za Kata, bado zinasuasua.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 18, 2009

    Mnaoomba Namba ya simu za TZ ipo kwenye Tangazo.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 18, 2009

    bela mwagito...kamwene na makasi

    sasa shule km iko bomba ivi email website sii ndo muhimu???yan tunataka full information ya shule yako yan huduma zipatikanazo apo,ada na michango mingineyo na wasifu wa walimu jamen...
    websites zooote zenye akili dunian wanaweka wasifu za kuanzia head of school/college na waalimu wote na administrator nk
    ili watu tuwe na imani na tufanye kasi si kupapasa siku izi kuna usanii mwiiingi sana izi english medium...uganda/kenya ukipeleka watoto wanarudi vyangu/mashoga.
    wee utapiga simu uongee masaa mangapi???na unaweza sahau maswali mengi tu,SO WEKA WEBSITES APO
    ila nakufagilia sana bela kufungua skuli IRINGA-MAFINGA kwetu kubooma

    ni hayo tu

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 18, 2009

    hao wote wanaolalamika kupata namba ya simu ya nyumbani lazma watakuwa alifeli kwa uzembe kwenye mitihani yao ya shule..hawako makini,contacts zote zipo kwenye picha ya tangazo lao hapo..yani wabongo zie kulalamika tu bila sababu..so disgusting!!

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 18, 2009

    Mafinga, mh????
    Too cold for my Dar-born kids!
    Asante. Au unasemaje my neighbour Rwegasira?

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 18, 2009

    Anony wa June 18, 2009 1:16 PM

    ETI, '..... TOO COLD FOR MY DAR-BORN KIDS!" HIVI WEWE MZAZI WA JINSI GANI? UMESOMA NA KUELIMIKA? WATOTO WAKO KUZALIWA DSM UNATOA TANGAZO AU UKO SERIOUS KUWA HAWATASOMA NJE YA DSM? WANGAPI WANASOMA ULAYA, USA NK. KWENYE BARIDI, TENA BARAFU NA WAMEZALIWA DSM?
    UNAONEKANA KAMA MZAZI UNA FIKRA ZENYE UPUNGUFU KIASI.... POLE.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...