bwawa la maini oye!
anko nanihii akifuturu na hadija mwanamboka, asia idarous na farida
anko akiwa na waandaaji wa keki, da'monica na mumewe jose mara pamoja na fina
shamim zeze akitayarisha mahali pa kuwekea keki
mamou (shoto) ambaye yuko vekesheni na wenzie wakijiunga kusherehekea hepi besdei ya kuzaliwa dad. kati ni maggid na kulia ni zahra
da'mishi (pili kulia) wa virago boutique na rafikize walikuwapo
sehemu ya waalikwa
da'monica na mgeni wetu toka ughaibuni wakifuturu kwa raha zao
wakala wa wachezaji anayetambulika na FIFA Saidi Tuli akimpa keki anko
bosi wa JamboLeo Juma Pinto akipatiwa kipande chake
anko nanihii akipata keki toka kwa mai sista wake mishi wa virago

lady jay dee akila konozzz huku akimpa keki anko
ben kisaka anajiandaa kumeza
auntie monica akiwasilisha keki ya Bwawa la maini kwa anko nanihii kwenye futari ya hepi besdei kwenye mgahawa wa Chef"s pride ya Mjini Dar Ijumaa hii.
keki ya bwawa la maini iliyoandaliwa na auntie monica kwa ajili ya futari maalumu kusherehekea miaka nanihii ya kuzaliwa anko nanihii Ijumaa jioni kwenye mgahawa maarfu wa Chef"s pride jijini dar.

Globu ya Jamii inapenda kutoa shukran kareem kwa wote waliohudhuria futari hii ya kusherehekea hepi besdei ya anko nanihii katika hafla iliyofana sana. Pia Globu ya Jamii inapenda kutoa asante za dhati kwa wadau wote waliotuma salamu za pongezi za siku hii ya kuzaliwa kupitia mitandao mbalimbali ikiwemo FaceBook.

Ni vigumu kutoa asante kwa mdau mmoja mmoja kwa vile ni wengi mno, hivyo anko nanihii anaomba shukrani hizi ziwe kama wakala wa shukrani zake za dhati kwa wooooote waliotoa salamu za pongezi. Anawapenda sana.

Shukrani za pekee ziwaendee Tanzania Mitindo House walioandaa hafla hii ya futari na kula keki na pia Jose Mara wa FM Academia na mai waifu wake kwa kuandaa keki maalumu hiyo hapo juu. Asanteni sana Jose, Monica na Hadija Mwanamboka pamoja na Asia Idarous kwa ukarimu wenu.

Anko nanihii pia anatoa shukrani kwa bintiye Mamou pamoja na dada yake Zahra na kaka yao Maggid kwa kuungana naye kwenye hafla hiyo iliyoandaliwa na ndugu, jamaa na marafiki bila kuwasahau Juma Pinto na Ben Kisaka wa Jambo Leo, Kim Tenga, Da'Kabula wa TBL, Mariam Mogella na wenzie wa TSN, Saidi Tuli, Da'Mboni, na Dada Mishi wa Virago Boutique ya Namanga pamoja wote waliohudhuria.

taswira zaidi zitakuja kukicha...

-Michuzi
Picha zingine
na

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 75 mpaka sasa

  1. Michuzi keki ilikuwa nzuri si siri

    ReplyDelete
  2. Hongera Kaka.
    Uwe na maisha mema na UELIMISHAJI MWEMA

    ReplyDelete
  3. Happy Birthday Bro. Mithupu, leo nilimpigia my Bro. Rodger kumpongeza kwa happy birthday naona mmezaliwa tarehe moja, next year nitamwambia akutafute ili msheherekee pamoja na ninafikiri itakuwa sio mwezi mtukufu!
    Happy birthday again.
    Mdau USA

    ReplyDelete
  4. Mbona sisi hatukualikwa kwenye hii happy besdei ya siku ya kuzaliwa kwako?

    ReplyDelete
  5. MBONA UNATUBANIA PICHA NYINGINE UNCLE MITHUPU? TUMA ZOTE BWANA..
    HAPPY BITHDAY KAKA, MAY YOU LIVE LONG TO BLOW OUT MILLIONS OF CANDLES..
    BE BLESSED

    ReplyDelete
  6. NI JAMBO ZURI KUSHEREHEKEA SIKU YA KUZALIWA. USHABIKI PIA NI JAMBO LA KUUTIA MOYO FURAHA. LAKINI FURAHA UWA ISIYO KIFANI IWAPO USHABIKI WETU UTAJALI UZALENDO. SASA HII KEKI INGEPENDEZA SANA KAMA INGECHORWA MLIMA KILIMANJARO, AU MAANDISHI YA SERENGETI BASI HATA KISIWA CHETU ZANZIBAR. LIVERPOOL WALINYONGWA WATUMWA WENGI WEUSI. KAMA NI MPIRA BASI TUWAPE MOYO YANGA AU SIMBA.
    KHERI KWA KUZALIWA KWAKO;TUMEFURAHI.

    MAINA A. OWINO

    ReplyDelete
  7. Hepi Besdei tu yu, Hepi besdei tu yuuuuuuuuuu. Hepi besdei, hepi besdei. Hepi besdei tu yuuuuuuuu, ukate keki tulee, kata keki tuleeeeee. Kata keki, kata keki. Kata keki tuleeeeeee. Nakutakia miaka mingi zaidi, Mungu akupe afya na nguvu uendelee kutupasha na kukutananisha watanzania. Hakika tunajivunia globu ya jamii, idumu milele!!!!

    ReplyDelete
  8. Happy Birthday Brother Michuzi!

    ReplyDelete
  9. Hongera zake huyo ailiyetengeneza hiyo keki ya bwawa la maini. Inavutia.

    ReplyDelete
  10. HAPPY BIRTHDAY 2UUUUU, HAPPY BIRTHDAY 2UUUUU, HAPPY BIRTHDAY DEAR MICHUZIIIIII, HAPPY BIRTHDAY 2UUUUUUUUU. HOW OLD RUUU 2DEIIIII HAPPY BIRTHDAY 2UUUUUUUUUUUUUUUUU... MAKE A WISH.... NAWASILISHA, MWITA, TARIME

    ReplyDelete
  11. happy birthday kaka michuzi. i bet you wish liverpool to be crowned the premiership this season. REMEMBER: A birthday is just the first day of another 365-day journey around the sun. Enjoy the trip!!! jim

    ReplyDelete
  12. Because time itself is like a spiral, something special happens on your birthday each year: The same energy that God invested in you at birth is present once again. happy birthday mkuu wa nihiii. mdau, uk

    ReplyDelete
  13. Growing old is mandatory; growing up is optional. happy birthday issa... mdau, bongo

    ReplyDelete
  14. oooh, happy birthday kaka michuzi. mbona umeifanya kimya-kimya au masjala ni tarehe nyingine?

    ReplyDelete
  15. In childhood, we yearn to be grown-ups. In old age, we yearn to be kids. It just seems that all would be wonderful if we didn't have to celebrate our birthdays in chronological order. HAPPY BIRTHDAY MI-TOP-LAYER. mdau, mzumbe uni

    ReplyDelete
  16. happy brthday kaka michizi. je wajua kwamba, the first sign of maturity is the discovery that the volume knob also turns to the left?

    ReplyDelete
  17. Hepibethdei Misupu pamoja Na Mfungo Mwema...Mie Hio Keki Nilijua Ni LIverpool Wanafanya sherehe Ya Vipigo??

    ReplyDelete
  18. dear michuzi happy birthday. When I was younger, I could remember anything, whether it had happened or not; but my faculties are decaying now and soon I shall be so I cannot remember any but the things that never happened. It is sad to go to pieces like this but we all have to do it.

    ReplyDelete
  19. kaka michuzi, happy birthday. You are only young once, but you can stay immature indefinitely.... remember this! mdau jim

    ReplyDelete
  20. They say that age is all in your mind. The trick is keeping it from creeping down into your body.

    ReplyDelete
  21. hEPI BESDEI YA KUZALIWA ANKO NANIHII! MAY YOU LIVE MIAKA 100 YEARS UKIWA NA STRENGTH YA NGUVU TELE YA KUENDELEZA LIBENEKE LA GLOBU YA JAMII NA MENGINE MENGI MAZURI KWA WANAJAMII !!!

    KT WA GONGO LA MBOTO

    ReplyDelete
  22. Hiyo keki ilikuwa haina michuzi?

    ReplyDelete
  23. happy b'day mkuu wa wilaya ya nanihii. vipi kichekecho cha jk kimekumuzea? ujumbe: Middle age is the time when a man is always thinking that in a week or two he will feel as good as ever. mdau720

    ReplyDelete
  24. Hivi anko nanihii kwani we hunaga my wife wako? Mbona hujamuonyesha?

    Kule kwa Michuzi Junia amewaonyesha my children wako tu! Kwa nini unatuficha my wife wako? Au kaenda Nakasero?

    ReplyDelete
  25. happy b/day kaka michuzi. Just remember, once you're over the hill you begin to pick up speed. take care & watch your back!

    ReplyDelete
  26. kaka michuzi, happy birthday kwa saana tu. ka-ujumbe kangu: First you forget names; then you forget faces; then you forget to zip up your fly; and then you forget to unzip your fly. mdau

    ReplyDelete
  27. Samahani anko,nina swali kidogo kabla ya kukupongeza kwa siku yako ya kuzaliwa.

    Swali langu ni hili:hivi anko huna mke? naona siku zote uko mwenyewe tuuu,hata siku moja hujawahi kusema hapa nilikuwa na mai waifu wangu,haya hata katika kutoa shukrani umewashukuru watu wote ndugu,jamaa,marafiki na watoto wako,mkeo yeye hastahili hizo shukrani?mpe haki yake bwana hata kama hutaki kumuonyesha lakini panapostahili pongezi zake mpatie,namuonea huruma maskini sijui anajiskiaje?

    Happy birthday anko.

    ReplyDelete
  28. A diplomat is a man who always remembers a woman's birthday but never remembers her age. Michuzi happy birthday. mimi hapa

    ReplyDelete
  29. Michuzi nakupa hongera sana kwakutimiza myaka...
    Pia nina swali tena naomba unijibu kama swali ulilo ulizwa na mdau anayekupenda na blog yako,swali lenyewe ni hili;wewe mheshimiwa michuzi umeowa?una familia?yaani watoto?Sasa kama una familia, kwanini huleti picha zako na ukiwa na mai waifu?na watoto?Kwa sababu nakumbuka kwenye hepibesdei ya wazili mkuu Pinda,baada yakukata keki alilisha maiwaifu wake,badae familia na wageni kwa ujumla.Sasa wewe!! Usituaibishe mtu wetu.Mwaga picha hapa mwanzo wa siku kuu mpaka mwisho wa siku kuu,,Ila samahani usikwazike nakupenda sana my brother,na usinitie ndani ya gunia.

    ReplyDelete
  30. Ukiona watu wanapata mida ya kusherekea besidei basi ujue ufisadi umelipa. Fisadi wewe michuzi! Ulishamwona mama yako au baba yako wakisheherekea? Kwanza hata hiyo tarehe yako ya kuzaliwa si ajabu umetunga tu! Haya basi badala ya hizo pesa ungepeleka zisaidie watoto yatima wewe unatanua tu. Ni busara hiyo? najua utaminyia hii comment lakini ujumbe utakufika wewe fisadi kadogo-dogo. sasa kuran inasema ufuturishe wasiojiweza au utanue mwezi huu wa Ramadhani?

    ReplyDelete
  31. duh! hii sasa too much

    ReplyDelete
  32. PETER NALITOLELAAugust 29, 2009

    michuzi vipi mnakuja kwenye mazishi ya Ted Kennedy? Mbona mmechelewa ama ndege ya mweshimiwa Jakaya iko kwenye mawe? maana siku hizi hata trip zako zimepungua ama utasingizia mwezi mtukufu nini?

    ReplyDelete
  33. Mama we, mama wee (machozi yababuika)
    Mbona mie sikukaribishwa
    Masikini ya Mungu mmenisahau
    Mama weeeee
    All the same happy birthday
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  34. Mh. mkuu wa nanihii ya nanihii, Mbona wapiga boksizzz hatukualikwa?
    Mpiga boksiiiiz mwandamizi!

    ReplyDelete
  35. UTABIRI WANGU NI KWAMBA UMRI WAKO UKICHUKUA NA UWEKE ALAMA HII(-)KATIKATI YA HIZO NAMBA MBILI HAYO NDIO MATOKEO YA GAME YA MAN UNITED NA ARSENAL.YANI KAMA UMETIMIZA MIAKA 51 MATOKEO YATAKUWA 5-1.UTANIMABIA HUMU BAADA YA GAME.

    ReplyDelete
  36. Aaaa jamani mbona mwenyewe hatumuoni akikulisha keki bwana!!! Kwani watuogopa yakhe tumuone anaekupaga hilo smile!! Woooooooooooote wamekulisha hayo maini ya keki lakini nguzo ya uncle nanihii hatujaiona.
    Hii sio kitanzania jamani...Twaitaka picha ya first lady wako au mafirst ladies kama wapo.
    Ama tupe maeleso ....sisi tuna hisa hapa.
    Acha kutubania hapa..
    Mzawa

    ReplyDelete
  37. hepi besidei michuzino mungu akujalie miaka mingine miingiuwe na full afya using'atwe hata na mbu ili libeneke lidumu luv you, hepi besidei

    ReplyDelete
  38. michuzi sio vizuri kujirusha na wanawake kibao huku mkeo akiwa sijui wapi loo mkeo unaweza ukakuta anaumia sana sema hana jinsi labda.

    ReplyDelete
  39. Misupu mamsup yuko wapi mbona hatumuoni? tuambie siye ma-single tujue kama nawe ni single!

    ReplyDelete
  40. Happy birthday aunko nanii!!!! and mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa. Ramadhani. Birthday inaonekana ilikua nzuri kweli, kwani ni kufunguria kwa kujichana,

    ReplyDelete
  41. MKEO SASA NI YUPI KATI YA HAWA MAANA NA WEWE KITAMBO SANA,tUONYESHE MAI WAIFU WAKO ZE MISUPU UNAFICHA NINI????.

    ReplyDelete
  42. Brother Michuzi ni kwa nini umeweka nembo ya liverpool kwenye keki yako? huu ni ukoloni mamboleo kwa nini usiweke ya SIMBA AU YANGA?
    Unafikiri hao wachezaji wa liverpool wanakufahamu?
    Tulitegemea nyinyi ndio muwe mfano kwa wengine !!!!!!

    ReplyDelete
  43. KEKI HIYO MJOMBA RANGI YA BIA INAKUWAJE TENA...HAPPY B.DAY FROM NY.

    ReplyDelete
  44. Happy Birthday Mkuu wa Blogu ya Jamii. Miaka mingi myema ingali mbele yako!

    ReplyDelete
  45. Anko Michuzi Hepi Besdei, lakini katika picha zote sikuona wala kusikia kuhusu Anti Michuzi, vipi hapo? wacha nivute subra pengine katika taswira zijazo kukicha.

    ReplyDelete
  46. Hepi basdei ya kuzaliwa Michu

    US Blogger

    ReplyDelete
  47. Mbona hatujamuona mkeo, naona wewe na wadada wengine tuu, yuwapi?

    ReplyDelete
  48. Nyie mnauliza picha ya mai waifu wake, nani uliona akaacha vitu vyake vya thamani anavyovipenda hadharani?.
    Ni kama kuatangaza namba ya siri ya benki(ATM pin)ndo maana wengine wanafunika ninja. Keep it that way!. michu umesoma sana. I like it.

    ReplyDelete
  49. Mbona hakuna picha ya mkeo kukulisha keki. Huna mke nn?

    ReplyDelete
  50. Mithupu my wife wako yupo wapi mbona unamtenga katika matukio mengi, alipaswa kukulisha keki yeye! Mimi hili swala linanikereketa sana, ila ninashukuru siku hizi umepunguza too much konozzz!Ujue sio vizuri inatakiwa mama Michuzi naye aonekane kama mama mlezi wa blog ya jamii!
    Mdau USA

    ReplyDelete
  51. Birthday hii wala haijafana kwani mama mlezi wa blog ya jamii hajashiriki you need to resume this party! sio vizuri kabisa kwani mama nanihii alitakiwa kuwa pembeni na awe wa kwanza kumlisha anko nanihii keki. Mimi ninaugomvi na ninyi ninawapa siku 2 kuweka picha ya mama michuzi la sivyo nita-suspend kuangalia blog hizi mbili kwa miezi 2 nitarudi kwa ippmedia! Mdau USA

    ReplyDelete
  52. Michuzi acha ushamba ndugu yangu. Hiyo ni siku muhimu lakini mtu ambaye ni muhimu zaidi kwako ni Mke wake au huyo aliyekuzalia watoto Hujamweka kwenye hizi picha, umewaweka wakina Khadija Mwanamboka na mashangingi mengine, Mke wako yupo wapi?

    ReplyDelete
  53. Michu wapi mai waifu wako????? plzzzzzzzzzzzz usitubanieeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  54. Happy B'day Baba Abdul wapi wake zako??? Naona wadau na watoto tu wapi mama Abdul?????????

    ReplyDelete
  55. hongera kaka michuzi tunakutakia maisha mema na yenye kheri

    ReplyDelete
  56. anko mithupu happy birthday,imefana sana ila sijamuona my wife wako akikulisha keki au ukimlisha,naona tu watu wengineeeeeee????????????????

    ReplyDelete
  57. Happy Birthday Michuzi....!
    Is good to get old,unakuwa more wise,asikuambie mtu.

    Sasa kuna mambo mawili yanayo nichanganya

    1.keki kwenye box yenye nembo ya Liverpool..mzee kulikoni? Ungeweka picha yako,au familia yako au nchi yako..lakini Liverpool who are loosers...nasikia kichefuchefu.

    2.Mzee kilasiku unashika mikono ya wakidada na kutuonyesha watoto wazuri..wapi mke wako?Unatuonyesha unalishwa keki na Jdee badala ya mke wako Kulikoni???

    Mzee tutaanza kukufanya uwe accountable with your own actions.Tunataka uwe mfano kwa watanzania wote, they look up to you.

    Mdau USA

    ReplyDelete
  58. IS MICHU SINGLLE, IF MARRIED ISN'T THIS SUPPOSE TO BE THE OCCASSION WHERE MAMSAP IS AROUND. KWA NINI ANAFICHA? ANABOA SASA

    ReplyDelete
  59. Yaani bwana michuzi mimi nimeumia sana kuona au kugundua kwamba wewe huna mke,,yaani inaumiza sana mtu kama wewe kwenye siku kuu kama hiyo unaonekana na mashangingi tu! baba mzima mwenye familia unaonekana na watoto tu bila mama watoto??aise kama ulimpa kadi nyekundu au talaka unatakiwa uowe mwingine si vizuli mtu mzee kama wewe uende kwenye maisha ya uzee bila mke.sorry usinipige mkwaju.

    ReplyDelete
  60. JAMANI WADAU WA BLOGU YA JAMII, ACHENI TEN MMKOME KABISA KAKA MICHU. OOOH ANTI MICHU YUKO WAPI, OOOH MAIWAIFU WAKE YUKO WAPI. UNAFIKI MTUPU. MKUU WA NANI HIIII NI MWENYE BUSARA SANA - HAKUONA NI BUSARA KUFANYA KAMA WADAU MLIVYOTEGEMEA - NI MAPENZI YAKE. KAMA SIO MMOJA JE - SASA NI YUPI ATAMLISHA HIYO KEKI AU KAMA JE HANA AFANYEJE. KUNYWA MAZIWA SIO LAZIMA UWE MFUGAJI ATI...... Mdau FAZA

    ReplyDelete
  61. Wadau labda mwenyewe ndio hapendi kuwekwa picha yake humu bloguni.....

    ReplyDelete
  62. HUKO NI KUMDHALILISHA MAMA WATOTO WAKE, AU ALISHAKUFA? AU WAKO WENGI? MBONA MZEE YUSUFU ANAO WENGI NA WOTE ANAWAWEKA MTANDAONI HADI EX WIFEY

    ReplyDelete
  63. Hepi belated besidei Anko Michuzi!

    ReplyDelete
  64. Asalam aleykum, mimi napenda kukukumbusha kuwa kushereheka Birthdays haramu, Allah s.w hapendi na pia hivyo unafanya hayo kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhan. wanawake na wanaume wamechanganyika pamoja, unajua dhambi zake? Jiepusheni na moto jamani. Moto wa Jahannam huwezi kuufananisha na chochote hapa dunia. Ukiataka shereheka kila siku unapoamka asubuhi sababu umejaaliwa kuamka mzima na bado wapumua. Kila la kheri

    ReplyDelete
  65. HATA MIMI NASHANGAA BIRTHDAY INASHEREHEKEWA MWEZI WA RAMADHANI. ANGEKUWA PAULO AU THOMAS NDO WANA BIRTHDAY SI MANENO YANGETOKA HUKO, OOH HAESHIMU MWEZI WA RAMADHAN, OH WAKIRISTO HIVI....ANYWAY HAPPY BIRTHDAY

    ReplyDelete
  66. Inawezekana mke wake halipi au mbaya ndio maana anaona haya kumuweka hapa.

    ReplyDelete
  67. michuzi jibu hoja,mke wako yuko wapi?naona wajuaji wajiji tu,usimbaniee,muweke hadharani.
    mdau wa Lusungo Ipinda Kyela.

    ReplyDelete
  68. MICHU UNANIOGOPESHA MKUBWA NAONA SURA ZA KITAPELITAPELI MJINI HAPO KIBAO,INA MAANA HAO NDIO TYPE ZA MA-BEST ZAKO NINI?KUNA HADI MAWAKALA WA SOKA KWELI NCHI HII HASARA TUPU

    ReplyDelete
  69. Bora amfiche tu au awafiche maana wabongo hatuna dogo, aku anko michu we wafiche tu kwani wake zao??? kwanza wanavyojifanya wanajali utafikiri wako siriasi...wafiche babu we humu ndani hakuna dogo wataanza kuwa nanihii mara vile vikaenda vikashuka ..wafiche babu we

    ReplyDelete
  70. NAFURAHI SANA KUONA KUWA WATANZANIA TUNAVYOHESHIMU NA KUTAMBUA NAFASI NA HESHIMA YA MWENZIO KATIKA FAMILIA. TENA PALE AMBAPO MNA WATOTO. UNCLE NANIHII KWA KWELI ATAKUWA ANAPOTEZA HESHIMA KUBWA KWA WADAU KWA KUTOJIBU HOJA HII ILIYOWAGUSA WENGI.
    SI JAMBO JEMA SISI KUONA TU WADADA WENGINE WANAKUSHANGILIA LAKINI MAMA WATOTO KAFICHWA.
    ILA PIA SI VYEMA KUITA WATU MAJINA YASIYO NA HESHIMA NA KWA KWELI BWANA UNCLE INABIDI UANGALIE JINSI UNAVYOWEKA HAYA MAONI MAANA UNARUHUSU WATU KUKEJELI WENZAO. KUITA WATU MASHANGINGI, MATAPELI SI TABIA NZURI NA IKEEMEWE.

    BWANA MICHU WEKA MAMBO WAZI MAANA WEWE NI PUBLIC FIGURE HIVYO WE ARE STAKEHOLDERS NA INABIDI UWE MFANO KWA JAMII!
    MZAWA.

    ReplyDelete
  71. like father like son...
    ze fulanazzz

    ao mabinti 2 ni wako??mh

    miaka mingapi umefikisha?

    ReplyDelete
  72. Happy beLated Birthday Michuzi; swali la msingi naomba unijibu mama mbona sijamwona kushereheka nawe?? pia jamani wadau Chef' Pride bado wana-operate kama kawaida mwezi huu mtukufu watu tutembelee?

    ReplyDelete
  73. Anon Tarehe Sun Aug 30, 11:20:00 AM,na anon Tarehe Sat Aug 29, 11:28:00 PM, nk. nashukuruni kwa kumuuliza kuhusu mke,

    Michuzi anamke nipo hapa. Mimi nashaaga ananibania!! Sijui vipi?? Sijui ninakasoro gani namuomba aweke bayana nijue...

    ReplyDelete
  74. Jamani nyinyi wadau anti Muchuzi mbona nipo.

    ReplyDelete
  75. Msimseme seme kipooza roho wangu, mkewe nipo nimejaa tele. Hadi nione wake wa wadau woote ndio mimi nitajitokeza.

    Mbona Osama hajajitokeza hamumtafuti kama mnavyonitafuta mimi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...