JK akipanda ndege usiku wa kuamkia leo tayari kuelekea Jamaica kwa ziara rasmi ya siku mbili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Duuuuuuuuuuuuuuuh

    ReplyDelete
  2. Nafurahi sana kuona Rais Kikwete anakwenda Jamaica. Ni nchi ambako alizaliwa mama yangu mzazi na pia bado nina ndugu wengi sana huko upande wa mama.

    "Out of Many, One People."

    ReplyDelete
  3. michuzi umepost hii hapamkuchokoza watu. kwa post hii watu wakaage mkao wa comments zao kutupwa kapuni!! haya mi nisaidien tu hii ndege ni ndege ya shirika gani?? hii rangi siifahamu kbs. au ni ile ndege ya rais?

    ReplyDelete
  4. Jamani President wetu mbona anasafiri sana. Kila siku namuona yupo safarini. Kweli no comment

    ReplyDelete
  5. Wananchi tunajitizama wenyewe huku Mzee ndio kila siku Safari. Usisahau kutuletea "JANI" nitalia na UGALI hahahaha. Kijiweni Nje ya Ikulu. Mvuvi.

    ReplyDelete
  6. Mama Salma Kikwete yuko wapi?

    ReplyDelete
  7. mjomba huwa simwelewi msimamo wake kabisa, si ni juzi hapa alianguka mwanza wakadai ni kutokana na uchovu wa safari nyingi?

    ReplyDelete
  8. Marekani huenda kuomba sasa huko anaenda kufanya nini?
    Na wewe Chemi umekua sasa, unashangilia rais kuteketeza pesa yet kisa anaenda kuona ndugu zako

    ReplyDelete
  9. DUH MZARAMO AKIPATA BWANA NI HATARI SANA SASA HUKO JAMAICA KUNA NINI TENA JAMANI HEBU SEMENI UKWELI KAMA SI KUARIBU PESA ZA WATANZANIA BURE? DUH YAANI KIKWETE ANAPENDA KUPANDA NDEGE ILE KINOMA SIJAWAHI KOUNA.

    ReplyDelete
  10. Sio vibaya, ni pamoja na kuhudhuria mkutano wa kuadhimisha miaka 60 ya Nchi za Madola nchini Trinidad & Tobago.

    Viongozi wa Afrika wanaohudhuria Mkutano huo wangeendeleza safari yao kupitia Kuba ... angalau kuwapongeza kwa kazi kubwa waliyoitendea Afrika.

    Afrika inaisahau Kuba!!!!!!!!!!!! Ukombozi wa Afrika Kusini, Namibia na Angola!

    Na sisi Tanzania ingawa pengine hatuwezi kuwalipa wa-Kuba, ki-fedha, tunaweza kabisa (kwa muda wa miaka mitano) kuandaa mashindano nchini Kuba na washindi watano wakapewa nafasi ya kuja kutalii nchini Tanzania kila mwaka!

    BAP

    ReplyDelete
  11. Safi sana, Jah rastafari! Labda atarudi na akili mpya.

    ReplyDelete
  12. JK badala ya kukaa nchini angalie matatizo ya nchi na kuyatafutia uvumbuzi yeye kila siku yuko njiani na safari. Hata mzazi kama hakai nyumbani muda wa kutosha na kuangalia watoto na vitu vya nyumbani mwisho wa siku hatakuta watoto hawaendi shule lakini hana taarifa, nyumba imepata ufa karibu itaanguka, hata wakati mwingine mke au mume anatembea nje.

    Safari za nje nyingine amwachie Membe tu anatosha. Au JK bado anafikiri yeye bado ni waziri wa mambo ya nje nini?

    ReplyDelete
  13. mzee Jk msuba wa huko sio mchezo,
    jamaika wana mjani unaweza kubadilisha hotuba

    ReplyDelete
  14. kwa kweli huyu rais amazid yan nadhan sasa ameingia kwenye Guiness Book of World records kama rais aliyefanya ziara nyingi za nje ya nchi na zisizo na mpango...nadhan hii ilikuwa ndoto yake toka utotoni kuzunguka dunia!!!!HONGERA MKUU!!!!

    ReplyDelete
  15. Nadhani mjomba ameukumbuka wimbo wa JAMAICAN FAREWELL ulioimbwa na Harry Belafonte.

    ReplyDelete
  16. Waswahili hatuna maana hata kidogo ndio maana tukaitwa manyani.hiv kweli tunashindwa kujiendeleza,,,, kula bata mwana kichogo ww

    ReplyDelete
  17. Watz waondoe hofu ambazo hazina maana. Kwa hii Tanzania ya leo ziara za rais wetu nje ni za muhimu sana. JK ni mtu anayeelewa sana hawezi kuwa anafanya utalii kama ambavyo wengine wanafikiria.

    Ziara za nje zinai-promote nchi na kufungua masoko mapya. Anaimarisha uhusiano wetu na mataifa ya nje. Kutokana na kuimarika uhusiano watz wataweza kunufaika na fursa mbali mbali zinazoweza kujitokeza.

    Kwa maoni yangu mara rais anapokuwa amemaliza kufanya ziara katika nchi fulani ni juu yetu watz sasa kuangalia ni maeneo gani ya ushirikiano ambayo wamekubaliana kushirikiana na kuanza kufanya contacts na ofisi za ubalozi kule na huku kuona kuna vitu gani tunaweza kufanya.

    Jamaica wanafanya vizuri sana kwenye michezo kama riadha kwa kupitia JK chama cha riadha wanaweza kujifunza kutoka Jamaica. Hata masuala ya muziki jamaa wa bongo flava wanaweza kunufaika.

    Hayo ni mambo madogo madogo tu kubwa zaidi ni fursa mbali mbali za kibiashara ambazo tunaweza kuzitumia na kunufaika.

    Watz amkeni, tayari kumekucha.

    ReplyDelete
  18. ukipata kitimie ukikosa kijutie

    ReplyDelete
  19. Amezidi kusafiri jamani hivi kazi anafanya saa ngapi?? jamani Tanzania kuna matatizo mengiiiii, ni wakati muafaa sasa akae nyumbani apige mzigo na kutatua matatizo ya watanzania.
    Hata kama atasafiri kila siku kutafuta misaada then akirudi na hiyo misaada haisimamii vizuri misaada yoteeee inaibiwa faida yake ni nini?? watu wake huko serikalini ni wezi sana, hakuna anayejituma ni balaa tupu, kaa nyumbani raisi wetu tuijenge nchi yetu. Kwanza unajichoshaa bure ukirudi uanze tena kuanguka anguka bure majukwaani.

    Safari njema, ila usisafiri tena mwaka huu subiri 2010 tumechoka na safari zako, pesa za walipa kodi sasa zifanye kazi vijijini wapate maji safi, hospitali nk.

    ReplyDelete
  20. Atakuja awe katibu mkuu wa umoja wa mataifa! Ngojea akimaliza mda wake wa Urais muone. Mtakuja mniuliza eti nilijuaje:)

    ReplyDelete
  21. sasa ndege akiitumi watu wanasema eti anasafiri sana. Akiwa haitumii wanmpigia hesabu za maintenance wanasema kila siku tunatumia hela zote hizi kuimaintain hii ndege ambayo hata huwa haitumiwi na kwamba pesa za wananchi zinapotea. sasa nyie wanadamu mnataka yeye afanyeje? Au ndio wivu tu?

    ReplyDelete
  22. MHESHIMIWA KACHOKA NA KITU CHA ARUSHA SASA ANAKIFUATA KILE ORIGINAL CHA MZEE TOSH HAHAHAHAHA NILETEE JAPO KIPINCH MKUBWA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...