Hey Joe

Jimi endrix

Mashabiki wa Jimi Hendrix,mpiga gitaa maarufu (electric guitar) ambaye anasemekana kuwa ndiye bora kuliko yeyote yule aliyewahi kutokea,watapata nafasi ya kusikia vitu vipya kutoka kwa mkali huyo hivi karibuni.

Familia yake kwa kushirikiana na Sony Commercial Music Group wanatarajiwa kutoa album “mpya” tarehe 8 mwezi Machi. Album hiyo imepewa jina la Valleys of Neptune imesheheni rekodi za Hendrix za kutokea mwaka 1969. Nyimbo zilizomo katika album hiyo ni zile ambazo hazijawahi kupatikana kibiashara sehemu yeyote ile duniani.
Jimi Hendrix alizaliwa tarehe 27 mwaka 1942 huko Seattle,Washington na kufariki jijini London nchini Uingereza akiwa mwaka 1967 akiwa na umri wa miaka 27 tu.Ukitaka kujua zaidi kuhusu maisha ya Jimi Hendrix ambayo yalikuwa na mikasa ya kila aina,bonyeza hapa.{ http://en.wikipedia.org/wiki/Jimi_Hendrix}
Written for Blog ya Jamii by
www. bongocelebrity.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Alifariki 1970 na sio 1967

    ReplyDelete
  2. hilo ndo falme la gitaa toka enzi hizo mpaka leo hakuna kama yeye

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...