JK na Mama Salma Kikwete wakimjulia hali mtoto Khamis Bakari(14) mkazi wa Wawi aliyelazwa kwenye hospitali ya Chake Pemba baada ya kujeruhiwa alipokuwa akijaribu kuingia katika uwanja wa michezo wa Gombani kuhudhuria maadhimisho ya sherehe za miaka 46 ya mapinduzi ya Zanzibar.
Katika ajali hiyo mtu mmoja alipoteza maisha na wengine 18 kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali hiyo ya chake ambapo Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Amani Abeid Karume na Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha pamoja na viongozi wengine waliwatembelea majeruhi na kuwapa pole Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...