Vodacom yamzawadia 13m/-
mshindi wa promosheni ya Samsung
Vodacom yamzawadia 13m/- mshindi wa promosheni ya Samsung
Vodacom Tanzania jana ilimkabidhi Shilingi milioni 13 mshindi wa promosheni ya Samsung Bi. Mariam Andwele (20) mkazi wa Uwanja wa Ndege, Jijini Dar
Vodacom yamzawadia 13m/- mshindi wa promosheni ya Samsung
Vodacom Tanzania jana ilimkabidhi Shilingi milioni 13 mshindi wa promosheni ya Samsung Bi. Mariam Andwele (20) mkazi wa Uwanja wa Ndege, Jijini Dar
Mariam aliibuka mshindi mwishoni mwa mwaka jana na aliwataka Watanzania kushiriki kwenye promosheni mbalimbali ili waweze kujishindia zawadi mbalimbali.
“Mwishoni mwa mwaka jana, nilipigiwa simu na kuelezwa kwamba nimeshinda shilingi milioni 13, kwa kweli nilifurahi sana,” alisema.
Alifafanua kwamba lengo lake ni kuzitumia fedha hizo vizuri kwa kujiendeleza kielimu na kwamba amepania kufika hadi Chuo Kikuu.
Mariam ambaye alimaliza kidato cha nne mwaka 2008, Jijini Mbeya na kisha kuhamia jijini Dar Salaam, alisema hakuna kiu kubwa ya maisha yake zaidi ya kujiendeleza kielimu . Aliishukuru Vodacom Tanzania kwa kubadili maisha yake na pia ya Watanzania wengine.
Meneja Uhusiano wa Vodacom, Nector Foya, alisema kampuni yake imekuwa ikiendesha promosheni mbalimbali kwa lengo la kuboresha maisha ya Watanzania.
“Promosheni hii na nyingine tunazoziendesha zinalenga kuboresha maisha ya wateja wetu na Watanzania kwa ujumla, hivyo tunawaomba wateja wetu wajitokeze kwa wingi kushiriki,” alisema.
Naye mwakilishi wa Kampuni ya Samsung Tanzania, kitengo cha Simu za Mkononi, Amina Iddy, aliwaomba wateja wa Samsung waendelee kutumia simu za kampuni yake kwani ni imara na bora.
“Tutaendelea kushirikiana na Vodacom kuendesha promosheni kama hii kwa lengo la kuyaboresha maisha ya wateja wetu,” alisema
Dada Mariam hongera sana kwa ushindi huu ushauri wa bure,k.m unatembelea blog,jua kwamba sasa utapata marafiki wa kila aina,kuwa macho,mshirikishe Mungu katika kupanga matumizi ya pesa yako na utapata mafanikio makubwa sana.
ReplyDelete