Ankal.....

Nakupongeza sana kwa kuendeleza libeneke
ukiwa kama mkuu wa wilaya ya nanihiii......

Kuna hili jambo moja la hii kitu inaitwa UTABIRI wa hali ya hewa huwa linanichanganya sana. Utamsikia mtangazaji wa utabiri huo akisema mfano "Maeneo ya kati mikoa ya Dodoma na Singida yatakuwa na mawingu kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache na vipindi vya jua"!!!
Au "hali ya bahari itakuwa na mawimbi madogo madogo hadi makubwa" Sasa swali ni je? katika utabiri huo ni kipi kilichoachwa hapo?? Maana possible outcomes zote zimesemwa!! yaani mawingu, mvua, jua, mawimbi madogo hadi makubwa!!
Ni hilo tu Ankal...naomba wadau wanielimishe kuhusu hilo.

Mdau wa kweli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. IMEACHWA SNOW NA UPEPO MKALI AU DHORUBA

    ReplyDelete
  2. Huu sasa ni UCHAWI. wewe unataka sisi na watoto wetu tukale wapi?? kama hutaki kudanganywa acha kusikiliza. macho makubwaa lione vile!!
    -Mfanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa!!

    ReplyDelete
  3. Hao jamaa tulishazoea huwa wanatabiri tsunami na masika ambayo hayatokea na hata bila aibu.

    Sasa sijui wanachanganywa na hiyo outdated radar ambayo waingereza wameamua kuturudishia pesa tulizotapeliwa?

    ReplyDelete
  4. Na Nambari wani wanapokwambia 'maisha bora kwa kila mtanzania' unafikiri wanamaanisha nini. ukipata jibu la maisha bora kwa kila mtanzania utakuwa umepata jibu la swali lako.

    ReplyDelete
  5. UTABIRI WA MAMLAKA YA HALI YA HEWA HUU HAUNA TOFAUTI NA NGUVU ZA GIZA!!

    ReplyDelete
  6. umenichekesha sana unajua mimi naonaga kama wazushi sijawahi kuwasikiliza kwa makini kumbe wanatajaga kila kitu ha ha ha sasa hapo umetabiri nini si kila kitu kinaweza kutokea asante kwa kunifumbua macho mdau hawa ni wasanii
    wewe ni jinias

    ReplyDelete
  7. Yaani wewe mdau una akili sana. Ni kweli hata mimi sijawahi kuona hii sentensi inabadilika hata siku moja. Kila siku ni kama ulivyosema. Ndurumo huwa ni ngurumo. Tangu huyu mtangazaji akariri hii sentensi hajawahi kubadilisha.

    Ngoja tuone mawazo ya wengi tuone mawazo ya wengi utapata jibu na mimi nikiwepo.

    ReplyDelete
  8. Mdau wa kweli: Ungekuwa jirani mimi ningekununulia hata soda au bia. Yaani imenichekesha ile mbaya. Uliyosema ni kweli, ila tu sema watu wengi huwa hatufuatilii sana kusikiliza kipindi cha hali ya hewa na kusikiliza nini wanatamka. Unajua si hapa bongo tu watu hawasikilizi vizuri utabiri wa hali ya hewa. Hata ulaya vile vile huwa hawasikilizi sana. Mpaka waandaji wa vipindi huwa wanaweka mamodo ili watangaze.

    ni hayo asante

    NakipendaKiswahili

    ReplyDelete
  9. BWAHUHUHUUU nimecheka in capitoli letazi maana kweli kichekesho herihata huwa siwasikilizi loh kwa maana hiyo mtu unabeba jacket mwamvuli na hendikachifu ya jua nacheka nafa hapa mwe mwe mwe

    ReplyDelete
  10. Hili wala halihitaji darubini kulishtukia, wewe uanitabirije eti kutakuwa na jua, mvua na ngurumo za hapa na pale! Kwani kuna mtu hajui kama Dar jua lipo kila siku? Kusema ukweli hawa waungwana wanatuongopea hivyo nashauri wapunguze wingi wa maneno na waiondoe ile ramani yao ya tangu niko St. Government primary school kwa kusema tu jua litakuwepo na usiku utawadia kama kawaida ila hali ya hewa tutajua kesho hiyo hiyo!

    ReplyDelete
  11. Hahahah that's funny Baada ya kuangalia super ball nimeamua kuingia kwenye ankal kabla sijalala.

    Nani kwakwambia ulaya watu hawasikilizi hali yahewa....Uzuri wa bongo ni kuwa hali yetu ya hewa inakaa week mbili the same. Huku usiposikiliza unaweza lala njia ukirudi nyumbani usiku. Asubuhi mvua mchana jua usiku snow.....Mtu halali bila kuangalia hali ya hewa ya kesho itakuaje na pia hundoki nyumbani asubuhi bila kuangalia tena weather na traffic.....

    Na huku meteorologists ni vichwa kikweli kweli. Hawadanganyi

    ReplyDelete
  12. Hilaliaz
    Nimecheka mbaya

    ReplyDelete
  13. HAPA KITU MUHIMU NI AJIRA TU IDARA HII INATOA AJIRA KWA JAMII LAKINI HAINA FAIDA YA ZIADA KWA JAMII KWANI UTABIRI WAKE NI FINYU SANA INGAWA TULIAMBIWA RADA INGESAIDIA KULETA USAHIHI, MATOKEO WANALIPUA KWA KUTUPA UTABIRI WA JUMLAJUMLA NCHI NZIMA; CHA KUSIKITISHA ZAIDI HAWAJUI HATA TOFAUTI ZA MAJIRA YA MVUA KATI YA MIKOA NDIO KINACHO SABABISHA KUWASHAURI WAKULIMA NCHI NZIMA KUANZA KUANDAA MASHAMBA INAPOTOKEA DAR IMENYESHA MVUA KUBWA!

    ReplyDelete
  14. Jamani tunashangaa hayo? Mbona hata hao wafadhili wa libeneke hili nao wanatangazo lao linasema

    PATA DAKIKA SITINI BUREEE KWA SHILINGI MIA TANO!!!

    Teh teh teh Bure kwa shilingi mia tano. Hiyo BURE nayo inauzwa shilingi mia tano. Hapa ndio Bongo bwana!!!


    K.O.R.

    ReplyDelete
  15. nimepaliwa na maziwa hapa

    hahahahaaaaaa uwiii kwi kwi kwi!!

    mweee,ntaaza kusikiliza sasa!

    ReplyDelete
  16. mdao ulosema ulaya hawasikilizi hali ya hewa sio kweli labda bongo,Kitu cha kwanza Ukiamka tu ulaya kabla ya hiyo news basi unasubiri hali ya hewa kujua kujipigilia au la,kwa sababu usafiri unaathirika vibaya mfano kipindi cha snow as well,kwa hilo umekosea ila narudia tena HAWAJATABIRI SNOW NA UPEPE MKALI HAPO

    ReplyDelete
  17. Mi nadhani tatizo linatokana na kichwa cha habari"UTABIRI WA HALI YA HEWA" ila kama ingekuwa ni hali ya hewa kwa kipindi cha saa fulani zijazo basi ingeweza ku-cover hizo outcomes zote.

    Mdau kichali

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...