Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bwana Ludovick Utouh akimkabidhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ripoti za ukaguzi wa matumizi ya Fedha za Serikali na Taasisi zake Ikulu jijini Dar leo mchana. Kushoto ni Msaidizi wa mkaguzi mkuu Bwana Atanas Tarimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. CAG Kila mwaka anakabidhi riport kama hizi, ila mbona hakuna mabadiliko?. Au report ni kubwa sana kuimaliza kuisoma kwa mwaka mmoja? kabla haijaisha ingine imefika Duh! Kazi kweli!

    ReplyDelete
  2. sasa hapo wote wachagga....walipendelewa au merits

    ReplyDelete
  3. Kwa maoni yangu suala sio kupendelewa. lakini upo uwezekana kuwa wamependelewa ndio maana hata wewe umeuliza hilo swali la kizushi. Kwani mbona wapo wasomi wengi tu ndugu yangu acha ushamba! unaonekana ni limbukeni wa kazi za serikali, watu wamesoma na wanafanya kazi zao wenyewe... Amka Bwenge wewe!!

    ReplyDelete
  4. Anon, Mar 31,09:10Pm
    Umeniacha hoi, kinachofanyika ni kusoma utangulizi na walioshiriki kuandaa ripoti kwisha.Inasubiriwa ingine mwaka ujao

    Mdau

    ReplyDelete
  5. Jeetu Patel aomba kesi yake ya Epa isitishwe kusikilizwa

    Upande wa utetezi katika kesi ya wizi wa Sh. bilioni 3.9 za Benki Kuu Tanzania (BoT) katika Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa), inayomkabili Jayantkumar na wenzake, umeiomba mahakama kusitisha kusikiliza kesi hiyo hadi kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na washtakiwa itakapomalizika.

    Aidha, washtakiwa hao walifungua kesi ya kikatiba yenye namba 30, ya mwaka jana wakiiomba mahakama kuwafutia kesi hiyo baada ya kuandikwa katika vyombo vya habari na kuitwa mafisadi.

    Maombi hayo yalitolewa jana mbele ya jopo la mahakimu, wakiongozwa na Ignas Kitusi, John Mgeta.

    Wakili wa utetezi, Martin Matunda, alidai kuwa washtakiwa walifungua kesi ya kikatiba pamoja na maombi ya kufutiwa kesi hiyo, lakini Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, alirejesha shauri hilo Mahakama ya Kisutu.

    Aidha, Jaji Mfawidhi aliagiza maombi ya kusitisha kusikiliza kesi yafanyike kwenye Mahakama ya Kisutu huku kesi ya kikatiba ikisubiri kusikilizwa na kutolewa maamuzi.

    Hata hivyo, upande wa mashitaka uliomba muda wa siku moja kupitia nyaraka za kujibu pingamizi la utetezi ambapo watatoa hoja zao kesho.

    Kesi hiyo iliahirishwa hadi kesho itakapoendelea kusikilizwa.

    Mbali na Jeetu Patel, washtakiwa wengine ni Devendra Patel, Amit Nandy na Ketan Chohan.

    Katika kesi hiyo, washtakiwa wanadaiwa kughushi, kuwasilisha hati za kughushi, wizi na kujipatia ingizo za fedha katika akaunti zao Sh.3,924,992,009.25 kwa kutumia kampuni ya Bina Resorts ya Tanzania baada ya kudanganya kuwa imehamishiwa deni na Kampuni ya C. Itoh &Company Ltd ya Japan.

    CHANZO: NIPASHE

    ReplyDelete
  6. hivi hiyo ripoti ni yakufanyiwa kazi au ni zawadi...maana naona imefungwa kwenye gift paper kabisa...wabongo bwana..taaabu kweli kweli...yaani haya ni mambo ya aibu tu...bwana michuzi plz toa hii picha..haya mambo mengine ya aibu hivi tuyaache bongo kwetu tu..maana sielewi hiyo gift wrap inafanya nini kwenye such a serious report?

    ReplyDelete
  7. MAZINGAOMBWE YANAENDELEA..NEXT PLEASE!...HALAFU NA HUYO ASYEEELEWA MWINGINE ANAULIZA KAMA NI WACHAGA ILI IWEJE?KWAMBA WANA AKILI SANA? AU KWA VILE WAMEPELEKA RIPOTI KWA JK BASI NDIO NONGWA,UZUSHI MTUPU HAPO,MAZINGAOMBWE TU HAPO UNAWEKA KITAMBAA ANATOKA NJIWA TUENDELEE TUSIENDELEE PROFESA MATATA,ALITOA TOOOOAAAAA
    MZAZI CHOPANGA

    ReplyDelete
  8. anon,march31,09:10PM.

    unaishi nchi gani wewe?mijitu kama wewe ndo haitakiwi kwenye jamii .choka mbaya tu wewe.

    ReplyDelete
  9. anon wa Wed Mar 31, 09:10:00 PM naona unaongea mambo ya kupendelewa kama ukitaka kuelewa cheki CV zao kama hujazimia.Watu wameenda shule we utabaki ukiongea mambo ya upendeleo.

    ReplyDelete
  10. kumbe makabidhiano ya ripoti hizi yanahitaki mbwembwe za ribbon ties? mimi nilifikiri ni sehemu ya kazi za mtu za kawaida ambazo hazimuhitaji mpiga picha.

    ReplyDelete
  11. Anon Mar 31, 09:10 PM asishambuliwe yupo sawa kabisa.

    Mdau ana haki ya kuhoji. Kwa nini baadhi ya watu hawataki issue kama hizi ziguswe. Ukweli ni kwamba kuna watu walishaweka mtandao wa kujinufaisha wao kwa wao.

    Kama walio wengi hawalioni hilo leo basi wataliona kesho, ukweli waja.

    Nawasilisha.

    ReplyDelete
  12. we michuzi ng'ombe wahed!! umebana meseji yangu ili iweje? narudia tena huyo jamaa suruali imejikunja kama imeliwa na ng'ombe aibu sana

    ReplyDelete
  13. ukiona vyaelea vimeundwa na dua la kuku alimpati mwewe ukiona mwezio yuko atua tano mbele kuna kitu anafanya cha ziada ambacho wewe ufanyi sasa nenda kajifunze kwake kuanza majungu na vitisho sio suluhu in short know yourself accept yourself and better yourself na ujue mambo mazuri yanataka kusota kwanza wako ngazi kwa ngazi utafika sasa ukifika ukigeuka pembeni unamuona wa karibu yako ehe vp na wewe ni dar es salaaam manake itafika kipindi itakuwa sio ukabila watoto wa mjini mbona wako wengi wanapendelewa kila kitu kiko dar

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...