Marehemu Dr. Aaron D. Chiduo
(3 May 1933 – 13 April 2007)

1 Thessalonians 4:13-14
Sekunde, Dakika, Masaa, Siku, Wiki, Miezi na sasa ni miaka mitatu tangu Mungu wetu mwenye wingi wa rehema na upendo alipodhihirisha utukufu na mapenzi yake makubwa kwako hadi akaamua kukuchukua alfajiri ya siku ya Ijumaa terehe 13/04/2007.
Huzuni na majonzi bado vimebaki kuwa ni sehemu ya maisha yetu katika familia lakini tuna imani neno la Mungu litatimia na siku moja tutakutana tena; na hapo hatutatengana tena milele. Matendo yako mema yamebaki kuwa lulu na mwanga uiangaziayo familia yetu.
Maisha yako ya upendo, unyenyekevu, uadilifu, utu wema na bidii katika kazi ndiyo dira inayotuongoza sisi mke wako Mama Ahilai, watoto wako Sydney, Sarah, Oripa, Geofrey, Rodney, wakwe pamoja na wajukuu zako Dennis, Caren, David, Samantha na Jovin. Tutakukumbuka sana na kukulilia siku zote. Tunaendelea kukuombea ili upate pumziko la amani siku zote.

Ndugu zako wa uzaliwa wako na familia zao na ndugu wengine wote wa koo za Chiduo, Chitemo, Chigongo, Mheta, na Msele nao pia wanakukumbuka sana. Kwetu sote imebaki kumbukumbu ni jinsi gani ulikuwa mhimili wa familia.

Rafiki zako, Madaktari wenzako, Wanasiasia wenzio wachache na wengine bado wanakumbuka bidii yako na mchango wako mkubwa ulioutoa katika kulitumikia Taifa hili. Bado wanazungumzia hulka yako ya uaminifu, uadilifu, unyenyekevu na kupenda haki viliyokujengea heshima kubwa miongoni mwa jamii.

"The righteous perish, and no one ponders it in his heart;
devout men are taken away, and no one understands that the righteous are taken away to be spared from evil. Those who walk uprightly enter into peace; they find rest as they lie in death." Isaiah 57:1-2

Bwana alitoa na Bwana ametwaa.
Jina la Bwana Lihimidiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. We love you but God loves you more, rest in peace Dr Chiduo.

    ReplyDelete
  2. Ilikuwa sifahamu kama Dr. Chiduo amefariki. RIP DR. Chiduo

    ReplyDelete
  3. Mi mwenyewe imebidi nisome kbs mpk chini ili ni hakikishe kama ni yeye kweli au wanafanana

    aisee habar hz sikufanikiwa hata kuona kwenye habari aliyekuwa waziri wa afya mmh

    RIP Dr

    ReplyDelete
  4. Duh!!hata mimi sikujuaga

    ReplyDelete
  5. I knew him personally, he was a calm and a peaceful person.He was ahead of me in medical school. One day our professor of anatomy had given him 20 out of 20 in an exam, and said to us,you lot,you got to follow his example
    God bless him,and rest him in perpetual peace
    wakatabahu

    ReplyDelete
  6. Alikuwa Mbunge wangu
    So fun kwamba ndio nashtukia hapa kama alifariki
    POleni wana familia wooote

    ReplyDelete
  7. Me too, jamani ndo kwanza nashtukia!
    R.I.P Dr. Chiduo.
    Poleni sana Rodney, na wanafamilia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...