Wiki hii tunatimiza mwaka (kwa tarehe za kiarabu) tangu mzee wetu Haroub Othman atangulie mbele za haki. Wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki tutakua na kisomo (hitma) katika Msikiti Ngazija siku ya Alkhamis kuanzia saa 11 alasiri. Kwa kupitia blogu yako naomba kuwakaribisha wote watakaoweza kuhudhuria.
Kwa wale walio mbali nasi basi nawaomba msimsahau mzee wetu katika Du'a zenu. Kwa walioko Zanzibar hitma itasomwa tarehe 26 mwezi huu, taarifa za muda na msikiti zitatolewa baadae.
Natanguliza shukurani
zangu na nakutakieni wiki njema.
Tahir H. Othman
Ni Mwaka mmoja tangu ututoke majonzi na uchungu bado tunayo utadhani msiba ulikuwa jana tu.Inshaallah Mwenyezi Mungu atakupa maghfira na atajalia kaburi lako liwe bustani katika bustani za peponi.Amin.
ReplyDeleteI REALLY MISS U UNCLE!!
Unajua mimi sikufahamu kama Prof Haroub alikuwa Mwarabu kwa muda wa miaka minne yote niliyosoma pale UD. Nimejua leo pale mwanae alposema kuwa ni mwaka mmoja wa kiarabu tangu afariki ili tusome hitma. Mwenyezi Mungu aendelee kuipumzisha roho ya Prof pahala pema.
ReplyDeletemdau acha fitna kwenye mambo ya kuwa serius,wapi imeandikwa alikuwa muarabu,umeambiwa kwa mwaka wackiarabu,ambao waislam ndo wanafata,kama ilivyo kwa wakiristu kufata mwaka wa kizungu,na wachina wana mwaka wao,thailand na nchi nyingi pamoja na dini tofauti zinatofautiana mwaka.sasa unaposema hivyo tukuelewaje,think before u talk,rest in peace profesa.ammen
ReplyDeleteNi mwaka mmoja tangu TANZANIA Impoteze mwanazuoni wa hali ya juu kabisa.Tutakukumbuka daima profesa,mbele yetu nyuma yako profesa HAROUB OTHMAN,Wewe ulikua kisima cha elimu ambapo wengi wamechota,umetuachia urithi wa hekima na busara.
ReplyDeletekufuata tarehe ya kiarabu sio maana kwamba Prof alikuwa Mwarabu. Maana yake wanafuata kalenda ya kiislam.
ReplyDeleteKusema mwaka wa kiarabu haimainishi moja kwa moja kuwa Prof. Othman H. alikuwa mwarabu. Alivyoitoa ni reference tu ya kuhesabia na si lazima iwe kama unavyofikiria.
ReplyDeleteAngetumia tarehe ya kalenda ya kiislamu. Hivi Tanzania inamkakati gani wa kupika kizazi hiki ili tuweze kuwapata watu kama Marehemu Prof Haroub?
ReplyDeleteTunamuombea na inshallah Mwenyezi Mungu ampumzishe pema.
mtoa comments wapili, kusema tarehe za kiarabu hakumaanisaha ni muarabu , kawaida waislam tunatarehe zetu za kiislam sio hizi zinazotumika kawaida nasio kuitwa kwa kiarabu ni maandishi tu na kwa ilivyozoeleaka lakni ni kwaida huitwa ni tarehe ya kiislam. ndio maana kufunga kwa ramadhani na sikukuu za kiislam always zinachange kutoka na hizo tarehe.
ReplyDeleteNi kwa majonzi makubwa sana tunamkumbuka Prof wetu na kwa sisi tuliomjua kidogo alikuwa binadamu mwema sana, na kichwa cha kweli.
ReplyDeleteTahir hebu tusaidie hapa kwani Prof alikuwa Mwarabu...? Mi sidhani maana sikuwahi ona maumbile yoyote ya Kiarabu katika mwonekano wake. Au wewe Tahir ndio umependelea kuitoa hiyo kalenda kiarabu..?
Mungu amuweka pema peponi Mwanamapinduzi msomi wetu.
Mtume wa mwisho Muhammad S.A.W anasema anayeongea Kiarabu ni Mwarabu..uwe mweusi mweupe, na menginyo wewe ni Mwarabu.Ama kuhusu tarehe hizo zinazoitwa za Kiarabu ni Tarehe za Kiisilamu au Hijiria yaani mwaka kuanzia Mtume Muhammad(S.A.W) Alipohama Makkah kuelekea Madiinah ndio karne ya Kiisilamu ilipoanziana mwaka huu wa Kiisilamu huenda kwa mwendo wa Mwezi(mwezi mwandamo)kutofautisha na ule mwaka wa Kikiristo(Gregorian) ambao huendana na mwenendo wa Jua.
ReplyDeleteMasuala mengi ya Kiisilamu huendana na tarehe hizi za Kiisilamu, kama ilivyo Marehemu Prof.Haroub Othman alikuwa Muisilamu na Uisilamu hutangulia kwanza kabla ya weusi/Uafrika kwa mtu mwenye kuzingatia.
Khamis Hassan Batanyaga
We anonymous wa Mon Jun 14, 12:53:00 PM.
ReplyDeleteKwani wanatumia mwaka wa kizungu(kalenda ya kizungu)kama wewe, ni wazungu? kwa habari yako kuna kalenda nyingi sana duniani, inategenea umechagua ipi. Kila mtu ana uhuru wa kutumia kalenda anayotaka.
Nadhani mtoto wa Marehemu alikosea hapo juu kuandika, aliandika imefikia mwaka mmoja kwa tarehe za Kiarabu. ilipaswa kuandika kwa tarehe za Kiislamu, kama sijakosea huo ni mtizamo wangu. RIP Comrade.
ReplyDeletemdau Pakacha UK.
Brother Michuzi,
ReplyDeletenashukuru sana kwa kuniwekea hili tangazo. Kwa kuwa mimi ni mdau wa blogu yako nilitaraji huu mjadala ungetokea kwa kuwa ni kawaida ya mabandiko yote. Ifahamike kuwa mimi si mtaalamu wa lugha na dhumuni langu ni kuwatangazia marafiki kuhusu hitma ya mzee kwa njia nyepesi na ya haraka. Mjadala wa kama tarehe ni ya kiarabu au kiislamu (ingawa sina uhakika kama waarabu wakristo wanatumia tarehe tofauti) nitawaachia TUKI, Bakita na wadau.
tahir
Oh my God, hata sikujua kama Prof. Othman amefariki!!! Kila ninapokumbuka enzi zangu pale mlimani namuwaza pia, kumbe hata hayupo nasi tena maskini! Poleni sana kwa msiba wanafamilia, ndugu, marafiki na Watanzania wote kwa ujumla, huyu alikuwa msomi muhimu sana nchini na nje ya nchi! Mungu ailaze pema peponi roho yake, na awatie nguvu wote mlioumizwa na kifo chake moja kwa moja!
ReplyDeleteAllahuma firlahu, waarhamahu waaskanahul filjanna.
ReplyDelete(US Blogger)
Mchangiaji wa pili, Hapa duniani kuna KALENDA TANO KUU zinazoashiria MIEZI NA MIAKA: (1) Gregorian Calendar, yaani kalenda ya kizungu, ambayo inatumika zaidi na mwaka mmoja ni mzunguko wa sayari yetu (planet earth) kuizunguka jua (wastani wa siku 365 na robo). (2) Kalenda ya pili ni kalenda ya HIJRA ambayo ndiyo ya Kiislamu. Hii inafuata mzunguko wa mwezi kuuzunguka dunia. Ina miezi 12 na, kwa wastani, ina siku 12 chache zaidi ya mwaka wa kizungu. Waislamu hutumia kalenda hii katika funga ya Ramadhani, n.k. (3) Kalenda ya Kichina (4) Kalenda ya Bani Israil ambayo ilikuwa ni kama kalenda ya hijra hadi hapo walipoamua waufanye mwaka wao uwe na siku 365 hivyo wakaongeza siku 12 katika mwezi mmoja wa mwisho wa mwaka. Wahabeshi wa Ethiopia pia waliamua kuunda mwezi wa 13 ili mwaka wao uwe na siku 365. (5) Mwaka wa kiajemi (Persian) (siku hizi Iran) ambao unaanza na sherehe za Nauroz. Unguja na Pemba Washirazi wa pwani na vijijini bado huadhimisha siku hii kwa KUKOGA MWAKA. Baada ya maelezo haya, nachukua fursa hii kuwapa pole Auntie Saida, Tahir na familia yote ya Prof. Haroub na kumwomba Muumba amlaze mahali pema peponi. Amin.
ReplyDeleteMchangiaji wa pili. Wahenga wamesema, kuuliza si ujinga. Kama hujui kitu bora uulize uelimishwe. Nadhani hapa si forum ya wewe kuonyesha chuki na prejudices zako. Kama una principles zozote au heshima cha kufanya ni wewe kuomba msamaha (hii si zeutamu)kwa comments zako zisizokuwa na kichwa wala miguu. Profesa H Othman we will never forget you. Asante kwa kutuelimisha, uzalendo wako na utetezi wako wa wanyonge kupitia legal aid programme yako. You made a difference. RIP!
ReplyDelete