Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wanaotoka Kikundi cha New Hope Family Street Children jijini Dar es Salaam, wakiandamana huku wakiwa na mabango yenye ujumbe unaoitaka Jamii na Serikali kuwajali kwa kuwapatia haki yao ya kupata elimu na maisha mazuri. Watoto hao ambao asilimia kubwa wanaishi mitaani katikati ya Jiji walifanya maandamano hayo kivyao baada ya kutoalikwa kwenye shughuli mbalimbali za maadhimisho ya Siku ya Mtoto Afrika leo.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Leoni Msimbe (kulia) akiangalia michoro ilichorwa kwenye kuta za jengo la Watoto Muhimbili kwa msaada wa OTIS. Kushoto ni Esther Micahael ambaye ni Mhandisi Mauzo wa OTIS
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Leoni Msimbe (kulia), akiwalisha keki watoto wanaopata matibabu kwenye Hospitali ya Muhimbili jijini Dar leo.
Watoto wanaopata matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam, wakipuliza kuzima mishumaa kwenye keki iliyoandaliwa wakati wa uzinduzi wa michoro iliyochorwa kwa msaada wa Kampuni inayotengeneza lifti ya Otis kwenye Jengo la Watoto la MNH, ikiwa ni moja ya shamrashamra ya maashimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika jijini leo





Mkurugenzi wa Kampuni ya OTIS, Justine Lyatuu
(kushoto) akigawa zawadi kwa watoto wakati wa hafla hiyo.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2010

    AIBU NA TUNASIKITISHA TANZANIA....DUH!
    WATOTO WAKIBONGO HUYO 'WINNIE THE POOH' KATUNI WANAMJUA? ANAHUSU NINI KWA MAADILI YAO?.... TUMESHINDWA KUWA NA KATUNI ZINAZOFANANA NA UTAMADUNI WA KWETU WENYEWE JAMANI?? AIBU TUPU.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...