Abdul Dau (MJUMBE KAMATI KUU TAIFA), Desa Makoko (MWENYEKITI WA KIKAO KUTOKA TANZ UK TAIFA) NA Frida Kusamba (MJUMBE KAMATI KUU TAIFA).
Uongozi mpya toka shoto: Ali Omar Ali (MJUMBE), Khalid Kasim Ndagiye (MWEKA HAZINA), Khamis Sahal (KATIBU), Saleh Al-bahry (MAKAMU MWENYEKITI), Suwedi Yunus Abdallah (MWENYEKITI), Hamisi Kayugwa (KATIBU MWENEZI) na Moses Kusamba (MWEKA HAZINA MSAIDIZI).

Jumapili 4/7/2010 Jumuia ya Watanzania (TANZ UK)
tawi la mji wa Leicester ilifanya uchaguzi wa viongozi wake, huu ukiwa
ni uchaguzi wa kwanza kabisa kwa tawi hili.

Uchaguzi ulitanguliwa na zoezi la kuandikisha wanachama, ambapo Bw. Desa Mambo Makoko ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa kusimamia uchaguzi huo.
Waliochaguliwa kushika nafasi za uongozi ni hawa wafuatao:

Mwenyekiti: Suwedi Yunus Abdallah
Makamu Mwenyekiti: Saleh Hemed Al-Bahry
Katibu: Khamis Sahal
Katibu Mwenezi: Hamisi Kayugwa
Mweka Hazina: Khalid Kassim Ndagiye
Mweka Hazina Msaidizi: Moses Kusamba
Mjumbe: Ali Omar Ali
Mjumbe: Saleh Ali Juma

Pia tawi linao tayari wajumbe wawili
wanaoliwakilisha katika Kamati
Kuu ya TANZ UK taifa, ambao ni:
Frida Kusamba
Abdul Dau
Hatua ifuatayo ni kwa viongozi kufanya kikao cha mwanzo cha kugawana na kuelekezana majukumu, na kisha kuandaa Mkutano wa uhamasishaji, ambao utajumuisha wadau mbali mbali kutoka ndani na nje ya Leicester, utakaokuwa na lengo la kuitangaza TANZ UK na kufafanua malengo ya kuwepo kwake pamoja na faida za mwanachama.
Kuhusu uanachama,
katiba ya TANZ UK inasomeka hivi:
Aina za Uwanachama
Uanachama wa Jumuiya utakuwa katika aina zifuatazo:
I. Mwanachama kwa kuwa ni raia wa Tanzania aishie Uingereza .
II. Mwanachama wa Wakutunukiwa {heshima}, atakuwa ni mtu yeyote ambaye kwa wadhifa wake, utalamu wake, au mchango wake kwa jamii utatambulika anaweza kutunukiwa tuzo ya uwanachama na mkutano mkuu wa jumuiya. Uanachama wa aina . Uanachama wa aina hii utaamuliwa na Kamati ya Utendaji.
III. Wanachama wasio raia wa Tanzania, lakini wakubaliana na malengo na madhumuni, mila na desturi za Kitanzania, pamoja na katiba ya jumuiya.

Kwa maelezo zaidi juu ya kazi za TANZ UK Leicester pamoja na namna ya kujiunga uanachama, tafadhali wasiliana na:
Mwenyekiti: balozisuwedi@yahoo.com
simu: 07931204823
Katibu: ksahal@hotmail.com
simu: 07982124581

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 09, 2010

    Mkwe naona unazidi kuiva tu!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 09, 2010

    Mwenyekiti Suwedi umerudi lini?nilisikia unatengeneza vijisenti bongo!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 09, 2010

    Mbona majina ya Kiislamu mengi kwa hao viongozi?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 10, 2010

    na mbona majina ya kina JOHN mengi toka wilaya hadi TAIFA hulalami anon?!

    au ndo ile ya yenu nyie "DUH" ya wenzenu midomo juu?!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...