.jpg)
.jpg)
.jpg)
Uncle Michuzi,
Hebu naomba uturushie hii kwa wadau wanaohusika hasa hasa watu manispaa hapa junction ya karibu na Oysterbay Primary school , hivi vibao vilivyowekwa hapa bila utaratibu mzuri vimekuwa kero kubwa kwa watumiaji wa barabara kwa kusababisha ajali mara kwa mara karibu kila wiki tunashuhudia ajali.
Hivi ninavyoandika hii email ni punde ajali imetokea kama inavyoonekana kwenye hizo picha hapo.
Mfano hiki kibao cha vodacom uwekaji wake si mbaya sana kwa kuwa kipo juu lakini hivi vingine huwezi kuona gari linalokuja mpaka uingie kidogo barabarani kitu ambacho ni hatari. Tunaomba mamlaka husika ishughulikie uwekaji wa hivi vibao au kuweka taa au matuta pande zote nne za barabara kuwezesha kupunguza ajali za mara kwa mara kama walivyofanya junction ya migombani karibu na nyumbani kwa mheshimiwa.
Tunaomba Uncle utusaidie kuturushia hii kwa wadau husika.
Angalia hivyo vibao vilivyojaa bila mpangilio
Ndimi mdau Oysterbay
Hebu naomba uturushie hii kwa wadau wanaohusika hasa hasa watu manispaa hapa junction ya karibu na Oysterbay Primary school , hivi vibao vilivyowekwa hapa bila utaratibu mzuri vimekuwa kero kubwa kwa watumiaji wa barabara kwa kusababisha ajali mara kwa mara karibu kila wiki tunashuhudia ajali.
Hivi ninavyoandika hii email ni punde ajali imetokea kama inavyoonekana kwenye hizo picha hapo.
Mfano hiki kibao cha vodacom uwekaji wake si mbaya sana kwa kuwa kipo juu lakini hivi vingine huwezi kuona gari linalokuja mpaka uingie kidogo barabarani kitu ambacho ni hatari. Tunaomba mamlaka husika ishughulikie uwekaji wa hivi vibao au kuweka taa au matuta pande zote nne za barabara kuwezesha kupunguza ajali za mara kwa mara kama walivyofanya junction ya migombani karibu na nyumbani kwa mheshimiwa.
Tunaomba Uncle utusaidie kuturushia hii kwa wadau husika.
Angalia hivyo vibao vilivyojaa bila mpangilio
Ndimi mdau Oysterbay
Hii ajali unayozungumzia haina uhusiano wowote na hivi vibao. Hii rav 4 imetokea masaki kwenda st peters na huyu jamaa wa nissan anatokea msasani kuingia barabara kubwa alitakiwa asimame wa rav 4 anayetoka kushoto barabara kubwa apite. vibao vipo upande wa kulia ukitoka msasani. ni kweli vibao vingi barabara za dar es salaam vinazuia kuona barabara kwenye makutano ila kwa hii ajali kuna uzembe au tatizo lingine kwa dereva wa nissan.
ReplyDeletemizinga juction hiyo ya barabara ya Haile Sellasie na Karume eneo la O'bay primary school halijaanza leo, maana tangu mie nasoma hapo O'bay primary ktk miaka ya 1970s na 1980s, ingawa kulikuwa hakuna vibao vya matangazo kabisa, ajali zilikuwa nyingi tu.
ReplyDeleteHii inaonyesha kuwa suala kuu hapa ni uzembe wa madereva kutofuata sheria na hili la vibao ni kisingizio tu.
Sheria za barabarani zifuatwe na wote yaani madereva na pia halmashauri ya jiji kuhusu wapi panafaa kuweka mabango.
Pia Chuo Kikuu cha University of Dar-es-Salaam wafanye research kwa nini ajali hutokea eneo hilo hata wakati wa miaka ambayo mabango hayakuwepo na kutoa ripoti kwa kamanda wa polisi trafiki na umma kwa ujumla.
Mdau1
Vibao vya matangazo vinaweza kua pia ni sababu, lakini sababu ya msingi hapo ni mwenye gari aina ya Rav 4 ya blue. Huyu alipashwa kumwachia huyo mwenye pikup apite kwanza kwani ndiye aliye kulia kwake na sheria inasema hivyo sehemu yenye makutano isiyo na taa, basi sheria ya ile ile ya eneo la mzunguko "round about aka keep left" ndio inayopewa kipaumbele. Pole kwa mwenye Rav 4 maana hapo imekula kwake
ReplyDeleteni hapohapo mzee vijisenti alipokula mzinga uliompeleka mahakamani mpaka usawa huu...
ReplyDeletehivi kesi ya zombe iliishia wapi?
ReplyDeleteNdugu yangu uliaandika maoni yako 11:59:00 kama ungesoma maoni ya 11:32:00 ungekuwa umepata elimu nzuri ya usalama barabarani, mahali barabara zinapokutana sheria ya keep left haitumiki, inatumika tu mahali palipo na mzunguko, ila kwa udereva wa kujihami inashauriwa kuchukua tahadhari kila wakti unapoondesha chombo cha moto barabarani. Aliyekuwa barabara ya Haile Selassie analindwa na sheria ya kuwa barabara kuu ukilinganisha na hiyo nyingine ya kuelekea kushoto au kulia kwake. Yeye ndiye aliyeingiliwa katika eneo la njia yake kwa wakati huo. Lakini sitashangaa iwapo anaweza kunyimwa haki hiyo kwani wapindishaji wa mambo wana nguvu.
ReplyDeletehiyo ajali mimi niliishuhudia ni kwamba huyo mwenye nissan aliingia bila kuangalia magari yanayokuja kwenye main road (au aliangalia lakini hakuona) hiyo Rav4 ilikuwa inatokea masaki kuelekea saint peter ilijaribu kukwepa hiyo nissan lakini ikashindikana na kugongana papohapo hiyo nissan ilikuwa ikiendeshwa na m-mama wa makamo. cha msingi hapa kama mdau alivyoshauri yawekwe matuta pande zote kutoka masaki, kutoka saint peter na kutoka kwa makam wa rais na upande wa pili ili kupunguza mwendo wa magari yanayopita kwenye junction hiyo.lakini pia vibao hivyo vinachangia kutopata clear vision hasa ukiwa na gari ndogo (ya chini)
ReplyDeletehe! we! zombe alishaachiwa siku nyingi...alishinda ile kesi..we uko nchi gani vile?maana swali lako duh!
ReplyDelete... Pia na zile kelele za New Maisha Club zifuatiliwe.... Yule mama mpenda pesa ajifunze kuwa klubu imezungukwa na makazi ya watu yaani binadamu.... Kinamshinda nini kuweka sound proof???????? Michuzi safari hii usiibanie!
ReplyDeletekwenye juction zote zina hitajika matuta, speed zipunguwe.na unga mkono Ndimi mdau O BAY.
ReplyDeletekAMA HATUNA TRAFFIC LIGHTS AT LEAST KOKOTO NA LAMI TUNAWEZA KUIAGIZA china KWA AJILI YA MATUTA.lakini traffic watakula wapi jamani?
Hivo vibao bomu, pia vinaweza kusababisha ajali, sie tunafanya mambo kienyeji tu bila kujali usalama wetu hata siku moja.
ReplyDeletePia magari yetu, tumeamriwa kujaza stika za nenda kwa usalama, insurance n.k.n.k. mpaka dereva hujui kama kioo cha mbele ni cha ma traffic au cha gari!
Sie wabongo na usalama wetu na kama mbwa na paka kabisa!
Bure kabisa!
Hapa 'matrafiki' wa nje ya uwanja tutakuwa wengi, mimi naona kama barabara ya kutoka masaki kuelekea saint Peters ndio main road, kwa hiyo yoyote atokaye pembeni kuingia barabara hii lazima awe makini zaidi. Na kwa hapo naona rav 4 ilibidi isubiriwe ipite kwanza.
ReplyDeleteMara nyingi uzembe wa madereva ndio husababisha asilimia kubwa ya ajali za barabarani, kila mtu ana haraka, sasa haraka nyingine mwisho wake ndio huu.