Ankal akipongezwa na mgombea ubunge wa Kasulu Mashariki Bw. Jamal Abdallah walipokutana usiku huu mjini Kigoma. Bw. Abdallah, ambaye ni mdogo wake mchambuzi wa kandanda Dokta Liky Abdallah, alishinda kwa kishindo katika kura za maoni Ankal akiwa na kikosi kazi cha wapiganaji mjini mgara ambao wanaongozana
na JK kwenye msafara wa kampeni ambao wanasherehelea nae besdei yake ya kuzaliwa wakiwa ziarani
Ankal na mhariri wa Habari Leo Mgaya Kingoba ( wa pili shoto) wakiwa na wapiganaji wapiganaji wa Ngara.
Ankal anapenda kutoa shukrani za dhati kwa wadau wote wanaomtumia salamu kupitia Facebook na mitandao mingine. Anasema asanteni sana wadau kwa salamu hizo na hana cha kuwalipa zaidi ya kuwatakia maisha mema na fanaka katika shughuli zao.
-Michuzi



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. Happy birth day ankaliiiiiiiiiii......happy birth day to you.....nakutakia maisha marefu zaidi ya hapo

    ReplyDelete
  2. Happy b-day bro Michu a.k.a Ankal kama siyo mkuu wa wilaya ya kuzalisha nutrient mojawapo ya zege pale mjini Dar. Nakutakia maisha mema na yenye mafanikio. Mdau RJ.

    ReplyDelete
  3. Michuzi ulipokuwa kwetu ulipata kile vinywaji vyetu "umuramba" na "Gwagwa" kama hujaonja hivyo vitu hujafika Ngara.

    ReplyDelete
  4. Anko Miposi, mbona hamgeuki nyuma tuone majaketi yameandikwa nini mgongoni?

    ReplyDelete
  5. HEPI BESDE, MI NILIZALIWA JANA

    ReplyDelete
  6. Many Best Wishes and May Alimghty God bless you with many many more birthdays...

    ReplyDelete
  7. cha msingi anko hacha u-ccm we mwandishi wa habari unapotosha wapi kura sasa hapo hiyo njano yangu au sisi anko umezidi sasa kaka una danga jamaa husipotoshe jamani kwa tamaa zako binafsi tunajua unalipwa kufanya hizi lakini watu wanataka maendeleo ondoa uozo wako uchoki siku ccm wakishindwa utajuta watu wanakuangalia tu ndio utajua ushabiki sio dili shauri yako kua we mtu mzima sasa au hii blog sio yako tunashaanga inatoka na hela za EPA nini

    ReplyDelete
  8. Happy Brithday Ankal !Mzee wa Libeneke,tunakutakia maisha marefu,afya njema,mungu akuzidishie mafanikio Zaidi,
    Pia tunakuomba uzidi kuichunga Fulanazzzzzzzzzz!!!!!!
    Happy Brithday
    wadau
    FFU wa ughaibuni

    ReplyDelete
  9. HEI!!MIE NIMESHAONA KWAMBA HII BLOG NI YA CCM...MICHUZI UTAKOSA WATU KWENYE BLOG YAKO..ACHANA NA VYAMA FANYA KAZI YAKO YA UANDISHI

    ReplyDelete
  10. Hepibathidei ankal lakini acha ushamba kidogo.

    ReplyDelete
  11. Heri na baraka za kuzaliwa. Tunakutakia afya na mafanikio ya kikazi na kijamii.

    NB: hivyo vikoti nusu vyenye mifuko debe ni gov issued? Kazini kwangu kuna waajiriwa wenye haki ya kutumia pesa za muajiri kununua nguo za kazi. Kwa kua wananunua toka sites zifananazo, basi wote hutembea kama mapacha....
    Blackmpingo

    ReplyDelete
  12. Happy birthday to me and you as we have the same date and year, 28/08/1961. Ila mtu wangu unapendelea CCM hutaki kuweka mikutano ya vyama vingine, leo tunataka kuona picha za CHADEMA pale Jangwani, mtu wangu nadhani utasikia kilio changu hata mimi wa birthday moja kweli utanitupa kapuni?

    ReplyDelete
  13. Mbona hakuna picha za ufunguzi wa kampeni za CHADEMA?Sisi wengine tuko mbali tunapenda kuona na upinzani unafanya nini pia ndugu yetu?Kama huwezi toa tamko tujue kuwa huwezi kuweka habari za upinzani!

    ReplyDelete
  14. Hepi ya kuzaliwa, Michuzi!

    Lakini hiyo sare ya kisibau kwa "wapiganaji" iliamuliwa na nani ivaliwe?

    Hili swali niliwahi kuuliza hapo mapema; sikupata jibu kutoka kwako..! Swali lilihusu Ayoub Mzee wa BBC kuvaa hiyo sare akiwa Tanzania wakati mmoja!

    Au tunaiga wenzetu wa magharibi wenye kupenda kuvaa hivyo wakiwa nchi za joto?

    ReplyDelete
  15. Happy birth day ankal miaka mingapi umefikisha? kama sikosei umegonga 59!

    ReplyDelete
  16. Kama unaishi nchi za masikini, miaka 50 unaongeza 15, kwa hivyo Ankal anagonga 65 sasa.

    ReplyDelete
  17. Hongera ya Siku ya Kuzaliwa kaka, zimebaki dakika nane kabla sijachelewa siku!
    Maggid,
    Iringa.

    ReplyDelete
  18. Habari ankal, tafadhali sana uwe unauliza habari vizuri kabla ya kupost, maana hapo umepotosha watu JAMAL ABDALLAH TAMIMU ni mgombea Ubunge jimbo la MUHAMBWE KIBONDO na amemtoa Bwana KIJIKO nasio kama ulivyooandika tafadhali rekebisha ili usiendelee kupotosha watu. mimi ni mdogo wake Jamal na unaweza kuuliza kwa wahusika wakakuelewesha vizuri. narudia tena sio mbuge wa kasulu.

    ReplyDelete
  19. happy belated birth day babu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...