Kaka Michuzi
I was in the course of my duty at the Old military airport in Entebbe Uganda and later the head of state of Congo Brazaville arrived with massive cases for a three days meeting as you can see in the pictures . There was a fist fight with the Uganda security personnel who wanted to check the cases and these guys claimed diplomatic immunity. It led to a stand off . But the congolese later won because the luggage was not checked ! What do you think was in these cases?. Why do presidents travell with such massive cases ?
Maomba msaada tutani kwa wadau wa Blogu ya Jamii hii inakuwaje??
Mdau Ayoub mzee
The suit cases
Stand off



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 32 mpaka sasa

  1. Sifahamu mambo yalivyo Uganda ila ningeongelea juu ya misafara ya US VIPs abroad. CODEL au VIP visit yoyote (presidential kiboko zaidihivyo siiongelei) zinaanzwa kuandaliwa mapema mno hata miezi 3 mpaka 6 (Mama Clinton ndo anapenda ibuka ghafla kutokana na kazi zake). Balozi na consulate zote zina watu maalum wa Customs na Visit coordinators ambao kazi zao ni kuwasiliana na local authorities na kupanga mkakati ni kipi chaja na kitapita vipi.Pia kuna office ya RSO na RSO Investigators (jina zuri tu) ambao wanashughulikiana na wapokezi wao on legal side ya vitu kama silaha/bodyguards/motorcades etc. Pia kuna ma runners (senior military officers)wafikao mapema wakiwa na information yote ya mizigo including chewing gums etc. Ofcourse inawezekana kuwa wanakuwa na vitu wasivyo declare lakini haijawahi tokea kuwa locals wakaweka kifua kuvipiga chachi. Kwa mikataba ya kimataifa, kama sikosei diplomatic bags/liggage/pouch uwa hasisachiwi. Labda jamaa walinusa kuwa kuna unga au silaha....
    Blackmpingo

    ReplyDelete
  2. Watanzania tumezoea kuibua mambo ambayo hayana mantiki. He3bu tumuulize huyu bwana ameshindwa kutuma kitu ambacho ni habari? Inaonyesha wazi kwamba haelewewi maana ya Presidential delegation/entourage. Rais analindwa na sheria za kidiplomasia za kimataifa na kuna utaratibu unaeleweka wa kuheshimu heshima hiyo wanayopewa viongozi. Yeye ametumia maneno yanayoashiria masanduku mengi/makubwa kama vile Rais anasafiripeke yake. Mhe. Rais wa Congo anasafiri na masafara wake ambao una wasaidizi wake pamoja na watendaji wake hivyo si ajabu kuona picha kama hiyo wakati Rais wa Zanzibar wacha wa Muungano anaposafiri. Munaishi ulaya lakini munashangaza kwamba hamusomi vitabu na kujifunza na macho yenu yanayojiri katika misafara ya viongozi. Huko aliko mwandishi viongozi wetu hawajawahi kwenda na kuona watu wa itifaki wanashughulikia mizigo ya viongozi na msafara mzima. Tufungue macho na tutume taarifa zenye maana badala ya kujenga mazingira ya kufikiria uovu kwa wenzetu.

    ReplyDelete
  3. Diamonds hizo...tayari mzigo upo tayari kusafirishwa ng'ambo

    ReplyDelete
  4. Sio ajabu. Unaweza kukuta ana matatizo ya shingo au mgongo akaamua kujichukulia mito yake halafu kumbuka pia amesafiri na mamaa na baadhi ya wanafamilia.

    Masanduku mengine ni matupu ili ajazie kwa shopping atakayoifanya Uganda.

    Bwana mdogo najua wewe umezoea kubana vidude vyako vyote (cameras, viatu, viguo vya miguuni, viguo vya mwili kati, nguo za kawaida, vitabu, kalamu, writing pad, magazeti etc) kwenye sanduku kamoja.

    Ni kawaida tu, plz relax.

    ReplyDelete
  5. Huyu jamaa ni mshamba sijapata kuona. Has he ever heard of Presidential deligation? Hayo mabegi ni ya kiongozi na msafara wake kaka acha ushamba..Nenda shule ya diplomasia ili uache kuhumu watu ndivyo sivyo...Umenibora

    ReplyDelete
  6. mi mbona naona kuna kabinti na kilonga chake? au macho yangu haya oni vizuri

    ReplyDelete
  7. What do you think was in these cases?.

    Answer : Properties belonginging to president and his entourage.

    Not diplomatic luggage.! Presesident is not a diplomat , he is a again, a president and/or a head of state.

    Ni utovu wa adabu kufungua mizigo ya raisi..

    ReplyDelete
  8. Uliyetundika, define what you mean by the term, "cases".

    Anon wa Sat Aug 21, 05:33:00 PM: Hongera kwa kuyafamu hayo ya Amerika! (CHEKA)!

    ReplyDelete
  9. Ayoub Mzee, samahani!

    Pengine, si wewe uliyeandika kichwa cha habari. Ndio nimeona, "the suit cases"!

    ReplyDelete
  10. Mbona jamaa ameuliza freshi tu lakini mnajibu vibaya vibaya namna hiyo jamani? Sio poa, mtu akiuliza swali mjibu kistaarabu tu maana anahitaji kufahamishwa tu, hivyo kama wewe unafahamu fika basi mueleweshe kistaarabu tu, mashuleni hatufundishwi kila kitu ndugu zangu, pole pole.

    ReplyDelete
  11. wewe mdau wa pili huna akili kweli.hii ndio kazi ya mwandishi wa habari wewe siku tatu masanduku yote ya nini hayo? alafu ndio tunashangaa silaha zinawafikiaje magaidi.

    ReplyDelete
  12. Jamani mbona mna jazba sana wandugu. kaka Ayou ameuliza swali ili afahamishwe siku nyingine awe anajua nini kinaendelea katika misafara ya kidiplomasia. mhenga anasema " the most stupid question is the one not asked" sasa yeye anataka kuepuka upumbavu huo jamani... na nyie wenye jazba shule hamkufundishwa namna ya kuongea na watu vizuri ni akili yako tu baada ya shule. elimikeni kwanza kisha ndio muingie humu.... kaka ayubu rejea article 27 yaVienna Convention
    http://en.wikipedia.org/wiki/Vienna_Convention_on_Diplomatic_Relations


    mdau lesta.

    ReplyDelete
  13. Mimi sioni kama ni luggage nyingi kabisa ukifuatia watu alioandamana nao etc etc..

    Ila hiyo heading ndio nzito kweli ulikua una maana ya suitcases?
    English za dictionary ngumu kudigest. Why don't you make it simple for your readers?????

    ReplyDelete
  14. HAUJUI KWA NINI, NI KWA SABABU KUKITOKEA KASHESHE NCHINI KWAKE HARUDI. NCHI KAMA CONGO BRAZAVILLE SI UNAJUA HALI SIYO SHWARI SAAAANA. PIA KUMBUKA WAKONGO WANAPENDA KUVAA BRAND NA KUPENDEZA. WANABADILISHA NGUO KILA KUNAPOKUWA NA BREAK, KWA NINI WASIWE NA MABEGI MENGI. NI HULKA YA WAKONGO NA PIA KUTOKUWA NA UHAKIKA WA KURUDI KONGO.

    ReplyDelete
  15. KWANZA HILI SWALI LA RAIS WA CONGO AMEENDA UGANDA NA MABEGI MENGI LINATUHUSU NINI SISI WANABLOG AMBAO WENGI NI WATANZANIA.

    EMBU ULIUZA MAMBO YA MAANA BWANA

    ReplyDelete
  16. jamaa ana begi chache sana nadhani ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wa africa, Rais na msafara wake wanakuwa kama watu wanaenda mjini nakurudi?
    kaka kwa utaalam nilo kuwa nao hapo bado.
    Rais huwa anasafiri na ofisi mahali popote ni kazi kwa kwenda mbele hapo bado hajabeba usiogope huyo hana mambo kama unavyodhania

    ReplyDelete
  17. hili ndio tatizo wabongo hatuendelei mtu ukitaka kujua unaambiwa mjinga jamaa ameeleza vizurihata miminashangaa MIMI nafanya kazi HEATHROW AIRPORT TENA SEHEMU HIYO HIYO YA MIZIGO NA SIJAPATA KUONA HATA SIKU MOJA RAIS NA LORI ZIMA LA MABEGI-HUYU LABDA ALIKUA NA KIKOSI CHAKE KAMILI NA HIYO PIA INATIA WASI WASI KWA NINI TENA MABEGI YAWE SARE YOTE KAMA NI YA WATU TOFAUTI? PAMOJA NA YA WAKE ZAO?

    ReplyDelete
  18. wewe unayesema unafanya kwenye mizigo utawaona wapi maraisi wakipitisha mizigo yao kwenye sehemu za regular customers huku?

    Uganda ndio imechemsah inapitisha maraisi kwenye sehemu hizo hizo za abiria na kutaka kukagua mizigo yao...

    Wanaona ajabu kwa vile viongozi wa Africa wakienda kwenye nchi zingine wanaenda na kimkoba tu wakirudi kwao ndio wamebeba macontainer na kuyapitisha nyuma ya milango. Wanaona ajabu raisi akienda na vitu vyake kwao. Huyo amekwenda kufanya kazi kweli kweli wengine wanaenda nchi za watu kufanya shopping tu.

    Na angekua raisi wa nchi za ulaya au marekani kweli wangemkagua na mabegi yake? waache hizo...

    ReplyDelete
  19. Hee bwana wewe,come on..!! tusidanganyane hapa.!! This is the really news.Yaani dunia ya sasa, technologia ya leo, kweli mtu anatembea na shehena zima kama hili..?? It doesnt make sense..!!.
    This is the high level of abusing and exploitation of power.Full stop..!!. The misuse of tax payers and sweaters..!!.There is no alternative way you can express this situation right than this,this is it..!!

    ReplyDelete
  20. yaani bongo. wasiojua ndo wenye kutoa matusi na maneno ya kejeli. kwani nini maana ya elimu. acheni kujifanya mnajua.

    nadhani wadau wa hii blog tujifunze kuwa wastaarabu. kama hupendi post, hakuna haja ya kuchangia. kaa kimya.

    ReplyDelete
  21. THE GUY IS MOVING THE MONIES(TAX MONIES).
    Ayubu usiwe unapaki ukiona watu wanaji sevia.

    ReplyDelete
  22. Now i know why Tanzania will never develop. Because we ask this and we get that, the guy ask very polite indeed and what he get back is not answers but full of abuse.. LET STOP THIS AND SAY WHAT YOU THINK OR KNOWS... IF YOU KNOW NOTHING ... IT IS NOT NECESSARY TO PARTICIPATE ON THIS KIND OF DIALOGS...

    NOW back to the topic, and diplomatic or head of state and his or her delegates can not be inspected unless other wise, but international laws it’s not allowed. And when that thing needs any clarification of what is in it then head of the protocol will give that explanation if needed. In some countries where their airport are advanced they put scanners in VIP area and when the luggage’s are passing through they can check them, US do this so is UK. They will check them without your knowledge because u will be waiting the bags on the other side you can’t take them straight from the aircraft to cars. But this is liaison between head of the delegation and the protocol of the receiving countries.

    ReplyDelete
  23. Nilikuwa bongo mwezi wa 7. Security Officer wakati naondoka akaniambia kuwa nina cologne kubwa kuliko inayokubalika kusafiri katika begi la mkono lakini nikimpa shaving cream ataniruhusu kupita na perfume yangu ya bei mbaya (dola 150). Nikampa na mambo shwari. Nikasema kuwa kweli Bongo hakujabadilika, umasikini uko pale pale.

    ReplyDelete
  24. Hivi tujiulize kwa safari ya US ama UK mheshimiwa huyu angeruhusiwa kupitisha tani zote hizi za misanduku bila kuulizwa maswali? Mbona hawa viongozi wakisafiri kwenye nchi za watu wanakuwa makini na hawathubutu kusafiri staili hii? Waafrika tuko nyuma kweli! Eti masuali ya nini?

    ReplyDelete
  25. NIMECHUNGUZA AYOUB AKIPOST KITU HAPA HATA KAMA KIKIWA CHA MAANA WATU WEPESI KUMPONDA KAWAFANYA NINI KAKA WA WATU?UANDISHI WAKE TUMESHAUJUA HATA AKIFICHA JINA ANAJULIKANA TU, LABDA WALE WARUSHA MATUSI WANGESEMA TATIZO NINI?

    ReplyDelete
  26. Kila nchi inaruhusa ya kuuliza maswali kwenye mzigo wowote hata kama ni diplomatic bad pale wanapohisi kuna utata wa kilichomo ndani.
    Imeshaikumba hata misafara ya marais kibao pale maofisa wao waliposhindwa kufuata taratibu fulani. Mfano katika nchi fulani mmoja wa wajumbe wa Msafara wa Rais alikuwa na kiasi kikubwa cha fedha na hakutoa taarifa. Nchi husika ilimsachi kama kawa. Mbona wakubwa wetu kibao na mifuko yao inapoigwa screen sana huko nje mara inapoonekana kuna usanii.

    ReplyDelete
  27. i think there is no such thing as a wrong question. yuko sawa kuuliza kwa sababu hafahamu, na nina shukuru kuwa amejibiwa na watu wachache wastaarabu. labda kuongozea tu kidogo, niseme tu kuwa raisi ni "the number diplomat of the state." Kwa hiyo mizigo yake itakuwa labelled diplomatic luggage, na kwa hiyo haitakiwi kuchunguzwa na walinzi wa hapo kampala au port yoyote ile.

    ReplyDelete
  28. we mdau wa perfume una mashauzi sana, navyojua air port zote ulimwenguni huruhusiwi kubeba perfume kubwa kwenye begi la mkono inategemeana na ujazo, au labda uwe umenunua duty free, sasa wewe ulifanya makusudi au? nafikiri wakati unarudi bongo hukufanya huo upuuzi manake majuu hawana cha mswalie mtume unaicha hata kama ulinunua dola 500, punguzeni dharau na mashauzi ya kijinga watu kukaa majuu sio kwamba mko paradise na hukumkuta mnoko ungeiacha tu, sababu sheria zinaruhusu uliza wenzio

    ReplyDelete
  29. MNASHANGAAA YA WENZENU TU !! HAMUONI YA JK ???

    ReplyDelete
  30. hayatuhusu sisi sio ma-diplomats
    diaspora mna wazimu???ebu mchekini uyo wa "perfume ya dola 150 tu"

    ReplyDelete
  31. Mdau Aug 23 04:56. Nadhani kujafahamu pointi yangu. Sio mara yangu ya kwanza kusafiri na najua 50ML ni maximum kwa perfume kuchukuliwa katika begi la mkono.

    Pointi ni kuwa, Bongo, mambo ya sheria hamna. Jamaa kaniachilia nipite na perfume kubwa zaidi ya 50ML kama nikimpa shaving cream. That's my point. Ningekuwa Marekani hata Uarabuni wasingeiramba kwa kuwa kisheria watu wa ndege wangeichukua na kuirudisha katika begi langu kama ilivyonitokea Korea Kusini kabla sijafahamu mambo ya 50ML perfume. Kwa kifupi, njaa ndio iliyomfanya jamaa wa Airport kutaka shaving cream sio kuwa anafanya kazi yake.

    Kama anafanya kazi yake basi angewaita wafanyakazi wa British Airways ili warudishe perfume yangu katika begi. Kwa kuwa shaving cream ni dola mbili, nilimwachia nayo naye awaringie washikaji wake kijiweni. Umasikini mbaya sana.

    ReplyDelete
  32. Mashauzi ni nini? nadhani nimekaa sana ulaya nasahau Kiswahili sasa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...