mkuu wa libeneke,ass.aleikum.naomba msaada,
mimi ni mkazi wa hapa dar,natafuta kausafiri ka bei nafuu kazuri na reasonable price.natafuta gari safi,nzuri ambayo haizidi 10 million cash.mwenye kuwa nayo anitumie picha na negotiable price kwa email yahya.simon@gmail.com,tel .
mimi ni mkazi wa hapa dar,natafuta kausafiri ka bei nafuu kazuri na reasonable price.natafuta gari safi,nzuri ambayo haizidi 10 million cash.mwenye kuwa nayo anitumie picha na negotiable price kwa email yahya.simon@gmail.com,tel .
0782 302164
workplace JMALL/Harbour View towers.
kama inawezekana ailete gari hapa JMALL anipigie au anibeep nitampigia tuonane tuongee tupatane na kumaliza biashara.Mkuu wa libeneke kutokana na umaarufu wako na kheri za mwezi huu utanisaidia na inshaallah sina cha kukulipa kikubwa ila mola atakulipa.Sifanyi mzaha kweli nahitaji usafiri soonest.
Sambamba na hilo pia mkuu nahitaji kununua plot/shamba hata nje kabisa ya mji-barabara ya morogoro-isizidi Kibamba,barabara ya bagamoyo-isizidi boko/bunju,barabara ya mbagala-isizidi mbagala,CAP price ni 10,000,000.ukubwa wa eneo walau eka moja(atleast one acre).
Nisaidie mkuu,
ndimi nduguyo Yahya.
unahitaji kutapeliwa weye...kah!
ReplyDeleteMwana naona unavyojipanga kuuchakachua ule mgao...teheheee,cheza kwa step.,kikinuka patakuwa hapatoshi
ReplyDeleteHakuna mashamba kabla ya Mbagala ama sivyo utauziwa eneo wazi la jeshi palee palipolipuka mabomu. Ni hapo peke yake pana eneo kubwa otherwise utauziwa bonde la mto mzinga wee ndugu yangu.
ReplyDeleteUkitaka shamba la eka moja inabidi utoke nje kidogo ya Mbagala. Mimi nina eka moja na zaidi Kigamboni Mikwambe liko ndani kidogo maana barabarani pamekwisha pimwa. Sasa hicho kishamba ninauza milioni 3 kwa eka, kwa hiyo kwa milioni 6 ninaweza kukukatia eka 2.Pako poa gari inafika mpaka shambani.
Nimeweka hapa wazi kwa sababu hizi ni kumbu kumbu siku yoyote mtu anaweza kusearch akazikuta kwenye archives.
Mdau wa Mwanerumango
gari utapata,lakini shamba 1 acre hutopata.Ukilipata ujue ni la utapeli!Hupati shamba wala kiwanja surveyed kwa bei hiyo may be kiwanja unsurveyed high density ndio utapata otherwise nenda Kongowe..
ReplyDeletekaka unafannya kazi wapi? Hivi kweli mtu mwenye milioni ishirini aliyezitafuta kwa jasho lake anaweza kuuliza anunue gari au kiwanja wapi.
ReplyDeleteNa nina imani unazo nyingi zaidi ya hizo.manake huwezi kumalizia zote kwenye gari au kiwanja.
`Ndugu, nadhani wewe kwa kufanikiwa kushika pesa nyingi hivyo kwanza ni lazima unahekima na unaelewa thamani yake.. kwa ushauri kama unataka kuendelea kutumia kwa hekima..kwanini usiende Wizara ya ARDHI ukapata kiwanja kwa bei ya serikali na kwa uhalali..kwani nyumbani ni nyumbani hata ukikaa BUNJU..ni KWAKO...Na Gari mbona siku hizi kuna direct contact na maagent unapata gari mpya au yenye hadhi.. au mwenzetu umetoka machimboni pesa zimekutia kiwewe kila mtu ajue unazo... TARATIBU BABA money made man MAD..na hiyo ni BONGO au ujambazi umekwishaaaaa
ReplyDeleteyahya assalaam.
ReplyDeletemimi nina eneo kinyerezi kifuru tayari limeingizwa katika mipango miji tunasubiri fidia na kugawiwa viwanja. kama huna haraka tuwasiliane 0713 211726
Acheni kumdanganya..Nyie manasema hawezi kupata kiwanja..Mimi nimenunua kiwanja kina hati na ni surveyed na lawyer kila kitu million tatu...Usikate tamaa utapata wabongo waongo sana wanaandika hapa tu maneno utazania wao wamenunua kwa hiyo bei...Kumbe ni kutaka kuengezeana bei tu na kutishia wengine na kuwafanya watu wakate tamaa. Nilikua kila siku nikisoma naona mahela huku watu wanaweka nikasema sitaweza kitu kwa mwendo huo lakini ukweli viwanja vya bei za kueleweka vipo sana tu ambavyo vipo na hati na kila kitu. Nilikwenda summer na nimepata kabisa kiwanja....Hapo hapo Dar sehemu nzuri tu (jina nalihifadhi)...
ReplyDeleteMimi ninacho kiwanja njia ya Bagamoyo nyuma kabisa ya Kituo cha daladala bondeni kipo kushoto kabla hujafika njia panda kwenda Kawe, kipo barabarani kabisa karibu na kituo cha daladala cha Lugalo nitakufanyia Million8 kina miti na vichaka vingi sana hivyo gharama za kukisafisha ni juu yako kinafaa kwa fremu za maduka. Nitakupigia/au piga tigo ya zamani 403016 ili tumalize biashara hati miliki ipo nakiuza kwasababu ya usumbufu ninao upata kwa kutokukiendeleza.
ReplyDeletenadhani unatania, kama hutanii basi pesa hizo hujazipata kwa jasho, umetapeli, dhuluma ama wizi. duh. unachezea shilingi chooni. mimi nina new model rav4 tukutane msitu wa pande ama gerezani mitaa ya saa tano usiku ndo nakuwa nimemaliza shughuli zangu
ReplyDeletendugu yangu umeshazivuna Njoo bar tuzinywe alafu utapata nyengine za kununua ndege sio gari manaeke utaongeza foleni tu sikushauri kununua gari kodisha texii tu pesa tunapombeka tu au vp karibu Bondeni bar hakuna wateja
ReplyDelete