Jide akiwa na zawadi toka kwa wadau wakimpongeza kwa kutimiza miaka 10 katika libeneke usiku wa kuamkia leo katika Mzalendo Pub Millenium Towers Kijitonyama jijini Dar.
Jide akimlisha keki ma hazbendi wake ambaye pia ni meneja wake huku rafiki yao wa karibu Joan Mwingereza akishangilia
Jide na Machozi band wakizindua albamu ya kwanza ya bendi hiyo ambayo ilimtambulisha mwanamuziki mpya Mao Santiago (wa pili shoto) aliyejiunga nao hivi karibuni kuongeza nguvu
Jide akiwa amevalia kama mwimbaji wa kiMisri akiwajibika na vijana wake
Chegge wa TMK Wanaume alikuwa mmoja wa nyota waliofika kumpa taffu Jide. Hapa wanaimba wimbo wao wa kolabo wa 'Mambo Bado'
Mwimbaji mtanashati Mwinyi kama kawaida yake alifurahisha kwa uimbaji na uchezaji
mcharaza kinanda cha pili mahiri
kinanda cha kwanza

mkaanga chipisi kazini

nyuzi bin nyuzi
wadau walifurika Mzalendo Pub hadi pakawa hapatoshi. Wengi walisikika wakilalamikia uongozi wa Millenium Towers kwa kukataa kutoa nafasi zaidi ambapo kwa kawaida kama kuna shughuli kubwa huruhusu sehemu ya kuegeshwa magari itumike. lakini wakagoma bila sababu za msingi
fundi mitambo kazini
Mlinzi binfasi wa Jide akiwa nje ya kichumba cha kubadilishia
Walinzi binfasi wa Jide hawakuwa wale mabaunsa tuliowazoea bali vijana wakakamavu wenye miili ya tizi tizi
Jide na Machozi band jukwaani
sehemu ya umati



































Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. jide anamwogopa mumewe kukatika au ni hawezi? manake wale wanaume wanakatika mpaka ninafikiria nikiwa na mmoja wao itakuwaje naona ni PATASHIKA tu, kwa kweli sina usemi naona watanikuna ndipo

    ReplyDelete
  2. ama kweli kama nywele si zako watu watajua tu manake huishi mtu kuangalia kulia na kushoto naona mziki ulifana

    ReplyDelete
  3. huyu jide angepata mkuu mmoja wa ulaya angemtia masopsop angetutangazia jina la bongo sio kama kina hashim thabit majidai mengi hata kikombe hana watu kama jide wanafanya kazi zao kwa mapenzi, huyu dada atakumbukwa sana sio kama hawa wengine wanapita njia.

    kazi njema jide na hongera kwa miaka 10

    ReplyDelete
  4. Michuzi umekosea uliposema kuwa Jide amevaa kama mwanamke wa kiIran , wanawake Iran hawavai nguo matumbo yakiwa njee (nusu uchi au mwili ndani kuonekana) utatafuta wanyongwe. ungesema amevaa kama belldancer wa ki Egpyt au mcheza nachi wa kihindi. hakiki habari kabla ya kupost.
    mdau Paka la jikoni.

    ReplyDelete
  5. tunarudi kulekule kwa wakongoman

    ReplyDelete
  6. Jide Hongera kwa kufikisha miaka 10 katika fani uipendayo ya Muziki.

    Mungu akutuangulie ufikishe miaka mingine 10 kwa mafanikio zaidi.

    Tanzania inadhamini mchango wako katika kuinua sanaa ya muziki na kuhamasisha wanamuziki wengine hasa Wanawake.

    Kila la Kheri.

    Soames,
    Reading, UK.

    ReplyDelete
  7. Huyo mlinzi binafsi anaweza kweli kusimama mkono !! mbona kama njaa!1

    ReplyDelete
  8. WE ANON 10:17 NDO MWEUPE KWANI KAANDIKAJE HAPO KIMISRI MAANAYAKE KI EGPYT IRAN HAIJATAJWA NAONA UNA VISUAL HALUSINASION

    ReplyDelete
  9. hongera sana mama gadner

    ReplyDelete
  10. Jamani mbona wamekosea kuandika neno anniversary kwenye hiyo picha ya kwanza? Si wangeandika basi kwa kiswahili tu...hiyo ni lifetime picture na inaweza kuingia kwenye kumbukumbu za miuseum zetu kwa vile huyu ni msanii kabambe mtu badala ya kuchukua tu dictionary na kuangalia hilo neno linaandikwaje...Jamani huyo aliyeitoa hiyo zawadi mbona anajiaibisha hivyo?. Tukipende basi kiswahili chetu

    ReplyDelete
  11. wee 1.53 ndio una visual hallucination kabisa ..kabla hujakurupuka basi fikiria watu si wajinga kutuma comment zao hivyo...hiyo ilikua imeandikwa hiyoa wali na sasa hivi imebadilishwa...

    kama huna la kuchangia basi usiandike kitu..

    ReplyDelete
  12. wewe fala anon wa 01:53:pm kabla ya kuandika na kuwakandia watu ujue unaandika nini na unasema nini. ukitazama anon wa 10:37 aliandika kukosoa maelezo yanayohusu kivazi cha Jide (kama kavaa kiIran ) asubuhi 10:37AM na mimi pia nilisoma nikaona makosa ya Ankal inaonyesha Ankal baada ya kukosolewa akabadilisha maelezo na wewe umeandika maelezo yako saa 1:53pm ukumbuke ni masaa zaidi ya matatu yamepita .inaonyesha wewe ndio kichwa maji na nyie ndio wale watu wa kujikomba komba sasa Michuzi asikosolewe au Michuzi yeye si binadamu na hakosei? pu&?~+ff.

    ReplyDelete
  13. Dear Jide,

    Hongera sana kwa hatua uliyo ifikia, nafikiri ni kutokana na mipango pamoja na dhamira uliyo kuwa nayo ndivyo vimekufikisha hapo, umeudhibitishia ulimwengu kuwa as a man thinks so he is, so what we are seeing are the products of your thoughts. Pili kuna kitu kimekuwa kikinitatiza siku za hivi karibuni. Huyo mwanamziki wako mpya mao santiago ananichanganya sana. Nakumbuka aliwika sana mwishoni mwa miaka ya 90 na mwanzoni mwa elfu mbili, lakini nakumbuka pia kuna ajali ilitokea hapo kona ya kawawa road na mwananyamala rd, ilihusisha gari ya landrover kama sikosei kati ya mwaka 2001 au 2003, na mmoja ya watu waliotajwa kufa kama sikosei alikuwa huyu Mao Santiago! Sasa naomba kueleweshwa, ni huyu alitajwa kimakosa, au nilielewa vibaya walimtaja mwingine(mkongo mwenzake)na kwa kipindi cha hapa kati alipotelea wapi? Nitafurahi nikifahamishwa. Zaidi ya yote nakutakia mafanikio mema katika shughuli zako. Mpenzi na shabiki wako mkuu, genius-Manchester, UK.

    ReplyDelete
  14. Nyie aliyewadanganya nani kuwa wa-iran hawachezi belly dancing? Watu wengine bwana. Tumieni google/youtube muone wanavyofanya.Mnadhani sababu ni nchi ya kiislamu basi mambo ya belly dancing hakuna.Fumbukeni macho.

    ReplyDelete
  15. 10th Anniversary ya JiDe ilifana lkn Da Jide mbona maadhi ni ya Kikongo? Wadau wanataka Machozi band iwe na taste tofauti na kina Ngwasuma, Twanga na wengineo...kila la kheri, we're lookinf forward kushereke miaka 20 ijayo panapo majaaliwa.

    ReplyDelete
  16. Hongera JIDE lakini Michuzi umekosea sana kuweene inamfanya ka hiyo clip kidogo tu ambayo wanacheza sebene la kikongo. inamfanya jide aonekana hana Identity wakati sisi tunaoenda Machozi tunajua huwa anaimba nyimbo zake pamoja na za ku copy ungetuweka niekuwa Teeeeeeeeeja ndio ungekuwa umemtendea haki, hapa anakuwa kama sio yeye kabisa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...