Ndugu watanzania,
Kwa majonzi makubwa, na huzuni nyingi, naKwa niaba ya wanaopenda haki wote, ndugu jamaa na marafiki.Naomba nichukue fursa hii kuwafahamisha kuwa mpendwa wetu Jaji Mstaafu James Mwalusanya Alifariki dunia jana, nyumbani kwake Dodoma.
Mipango ya mazishi inaendelea kufanyika.Tutawajulisha zaidi baada ya mipango hiyo kukamilika. Hon. (rtd) Justice James Mwalusanya amefia Dodoma ambako alikuwa akiishi baada ya kustaafu kazi ya ujaji mwaka 1997.
Miongoni mwa Kesi alizowahi kuamua ni ili kesi maarufu na inayotuka sana katika nchi za jumuiya ya madola ya REPUBLIC v. MBUSHUU @ DOMINIC MNYAROJE AND ANOTHER , High Court of Tanzania at Dodoma, Criminal Sessions Case No.44 of 1991 .
Ni hukumu ya aina yake ambapo aliweza kutamka kwa aina yake kuwa adhabu ya kifo ni batili na inakinzana na Katiba ya Jamuhuri
Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake libarikiwe.
Wadau wa Mahakama,
Dodoma
The number one judge of Tanzania has passed away. Tanzania has lost the giants of the giants of the law, the legal luminary. His contribution to our legal system will be remembered forever.
ReplyDeleteMungu ametoa, Mungu ametwaa!
Poleni Mpoki,wadogo zako na familia kwa ujumla kwa kuondokewa na baba yetu.
ReplyDeleteThe only judge I know in this country who fought for the minority. RIP
ReplyDelete