Marehemu Mnomba Njaidi,wakati wa uhai wake.

Kwa niaba ya Familia ya Njaidi, mimi kaka wa marehemu Yusuf Njadi na mke wa marehemu Sarah Mirambo kwa moyo mkunjufu, tunapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru ndugu, jamaa, marafiki waliopo Tanzania, Jumuiya za Watanzania Cardiff, Cork, Leicester, Birmigham,Reading na London kwa kufanikisha shughuli zote za msiba wa Marehemu ndugu na rafiki yetu, Mnomba Njaidi.

Mnomba alifariki huko Cork City Ireland katika hospitali ya Cork University HospitaI tarehe 27/08/2010 na hatimaye kuzikwa tarehe 12/09/2010 kwenye makaburi ya Kisutu mjini Dar es salaam.

Asanteni kwa dua, maombi na kujitokeza kwenu katika kutufariji na kututia nguvu. Shukrani za pekee ziwaendee kamati nzima iliyoratibu na kufanikisha shughuli nzima ya kuusafirisha mwili wa Marehemu Mnomba kufika Tanzania.

Shukrani pia ziuendee Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Papa King na wanablogu wote waliolitoa tangazo la kifo kwenye Blogu zao.

Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru kila mtu kipekee,tunaomba shukrani hizi mzipokee wote mliohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha shughuli nzima ya msiba huu wa ndugu yetu Mnomba. Hatuna cha kuwalipa bali tunamwomba Mwenyezi Mungu awajalie na kuwazidishia katika shughuli zenu za kila siku.

Asanteni sana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Pole sana kaka Yusufu nasi pia tunasikitika saaana ila usijali sana tuko pamoja.

    ReplyDelete
  2. R.I.P OUR BROTHER, POLE KWA FAMILIA NA MARAFIKI

    ReplyDelete
  3. Poleni sana familia ya Njaidi popote mlipo...Oj kaka wa marehemu anatoka gerezani terehe 24/09/2010ni kweli? TEXAS

    ReplyDelete
  4. pole sana kaka Yusuph, Mungu azidi kukupa nguvu

    ReplyDelete
  5. pole kaka yusuph mi maka hapa nipe namba yako pse mpe pole pia adam

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...